Header Ads

LightBlog

VYOMBO VICHACHE VYA HABARI VINAJARIBU

KAULI YA BALOZI WA MAREKANI

Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mark Green, amemwambia mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima (27 Sept. 2007), Peter Nyanje, kuwa kuibuliwa kwa tuhuma za ufisadi kumethibitissha ni jinsi gani vyombo vya habari vya Tanzania vilivyo na uwezo na uhuru wa kufuatilia na kuripoti masuala ya ubadhilifu wa mali ya umma kwa uwazi.

“Kuna baadhi ya nchi ambako vyombo vua habari haviwezi kuripoti kama ambavyo inafanyika hapa Tanzania sasa. Katika nchi kama hizo, unaweza ukadhani hakuna rushwa, wakati ukweli ni kwamba ipo, ingawa vyombo vya habari havifichui hali hiyo,” Balozi amenukuliwa akisema.

Amesema, “Hapa inaonekana kuwa vyombo vya habari na waandishi wa habari wana nguvu za kutosha kusema mambo haya…” amesema balozi.

Mwandishi amemnukuu balozi akisema kwamba tuhuma za ufisadi zisigeuzwe kuwa uhasama “kati ya waliozitoa na waliotuhumiwa.”

No comments

Powered by Blogger.