Header Ads

LightBlog

Ndimara na CUF



Ijumaa, 28 Julai 2017
Kilichofanyika na kinachoendelea kufanyika CUF; na kwa CUF, ni kuasisi mfumo wa kuua uhuru na haki za watu; ni kujenga woga usiomithilika na ambao utafanya wengi waishi mithili ya msukule; ni kupanda mbegu za "uharamia wa kisiasa..."

Ijumaa, 28 Julai 2017

NANI awezaye kusema kwa uhakika au hata kutabiri, kwamba Prof. Lipumba hatapeleka kwa Spika, orodha nyingine ya wabunge wa chama chake - CUF ili watimuliwe bungeni? Nani awezaye kusema kwa uhakika kwamba, katika orodha hiyo, hakutakuwa na wabunge wa kuchaguliwa ambao watakuwa wanakabiliwa na tuhuma zilezile zilizowakumba wabunge wa viti maalum? Ikifika hapo, nani atazuia Tume ya Uchaguzi (NEC) - baada ya kuarifiwa na Spika kuwa wabunge wamefukuzwa na chama chao - kutangaza kuwa majimbo yako wazi, na hapo kuitisha uchaguzi mpya? Nani?

No comments

Powered by Blogger.