Header Ads

LightBlog

JINSI YA KUKUSANYA FEDHA ZA EPA

SITAKI Na Ndimara Tegambwage


Ukusanyaji fedha gizani, pakachani

SITAKI serikali iwanyime wananchi kile ambacho wanahitaji. Sitaki ikatae kutekeleza haki yao ya kujua kile wanachopaswa kujua.

Tangu Rais Jakaya Kikwete aunde Tume ya kushughulikia makampuni 22 yaiyojichotea au yaliyochotewa mabilioni ya shilingi kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kumekuwa na kilio kikubwa cha taarifa.

Wananchi wanataka kujua ni nani hasa hao waliochota au waliochotewa mabilioni ya shilingi. Hivi karibuni, baada ya Waziri wa Fedha, Mustapha Mkullo kutangaza kuwa wachotaji wamerejesha nusu ya kiasi walichokwapua, ndipo hamu ya wananchi ya kujua ilipoongezeka.

Ni nani hao waliorejesha bilioni 50 kati ya bilioni 133? Wako wapi? Wanafanya nini? Kuna waliolipa zote? Fedha hizi anakabidhiwa nani? Zimerejeshwa kweli au hiyo ni “fiksi?” Kuna maswali mengi.

Ili kutafuta jinsi ya kukidhi mahitaji ya habari muhimu kwa wananchi; na ili kutekeleza matakwa ya haki ya kimsingi na kikatiba ya wananchi kuhusu upatikanaji wa habari na uhuru wa kutoa maoni, hapa chini kuna jedwali ambalo limeandaliwa rasmi na asasi ya IDEA ili kuisaidia serikali kuondoa kiu ya habari.

Jedwali hili likijazwa ipasavyo, na maelezo ya jedwali yapo hapa chini kama ufunguo rasmi, basi angalau wananchi watakuwa wamepata taarifa za awali za kufanyia kazi: kuishauri na hata kuikosoa serikali yao.

Mwanasheria Mkuu wa serikali, ambaye ni mkuu wa Kamati ya Rais inayoshughulikia urejeshwaji wa fedha zilizoibwa kutoka Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya BoT, atumie mamlaka yake kutujazia fomu hii ili kuondoa uvumi unaoweza pia kudhoofisha shabaha nzima ya kazi aliyopewa.




A B C D E F G H I J K L M N O P
Na. jk ki tr bz ht kk tr zn ns zk zl mk km ko mn
1.
2.
3.
4.
5.
Endelea hadi makampuni 22.

Ufunguo:
A=Namba. B=Jina la kampuni iliyochota fedha. C=Kiasi kilichochukuliwa. D=Tarehe zilipochukuliwa. E=Benki zilimochukuliwa. F=Kwa hundi/taslimu. G=Kiasi kilichorejeshwa. H=Tarehe ya kurejesha. I=Zimerejeshwa kwa nani. J=Namba ya stakabadhi. K=Zimebaki kiasi gani. L=Zitalipwa lini. M=Mmiliki wa kampuni. N=Kazi za kampuni. O=Inalipa kodi. P=Maelezo mengine muhimu juu ya kampuni.

Sitaki kuwe na kiza katika suala la urejeshaji wa fedha zilizoibwa benki.


(Makala hii ilichapishwa katijka gazeti la tanzania Daina Jumapili, 9 Machi 2008. Mwandishi anapatikana kwa simu: 0713 614872; imeili: ndimara@yahoo.com)

No comments

Powered by Blogger.