Header Ads

LightBlog

MEMBE, LOWASSA & SITTA


Posted to forum: mabadilikotanzania@googlegroups.com,    Monday, 20 August 2012

Mjadala juu ya kauli za Lowassa, Membe na Sitta kuhusu vita na Malawi:


1. Tukubaliane na kujiridhisha kuwa Kikwete-Sitta-Lowassa-Membe walikuwa wamekubalinana. Matamshi yanalenga kutangaza vita kati ya Tanzania na Malawi. Wasingeweza kuyatoa hivyo kilevilevi. Kilichokuwa kinasubiriwa ni amri ya Amiri Jeshi kuamuru majeshi kusogea/kwenda uwanjani:

      (a) Wasingekuwa wamekubaliana, hivi sasa wasingekuwa na kazi kwa kujaribu kuingiza nchi vitani bila idhini ya Bunge na, au mkuu wa majeshi.
      (b) Membe ni mtu wa karibu sana na rais - "tarishi wa kidiplomasia" asiyetakiwa kwenda kinyume sana na mwajiri.
      (c) Lowassa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi - anashirikisha mhimili mwingine (Bunge) na hapaswi kuropoka kama hakuna mjadala nyuma ya pazia.
      (d) Sitta ni waziri wa mahusiano ya kimataifa ya Afrika Mashariki ambaye ana nafasi ileile ya Membe, uzito wa waziri wa muda mrefu na mwandani anayekaimu nafasi ya waziri mkuu bungeni.

2. hata hivyo, katika mazingira ya sasa ya utawala wa Kikwete, kuna ukimya hata pale ambapo maisha ya wananchi yako hatarini. Yawezekana pia walikuwa wanajaribu kina cha maji huku wakisema, kama hali itaonekana kutibuka, rais ambaye ni "mwenye kauli ya juu" (siyo ya mwisho), ndiye atatoa msimamo. Tayari ameutoa.

3. Yawezekana pia kauli ya Kikwete ikawa sahihi ingawa siyo kweli: Kwamba "ni kelele za wapinzani." Hakika Sitta, Lowassa na Membe wanatajwa kwenye orodha ya washindani wa tiketi ya urais kupitia CCM. Siyo wapinzani wa CCM, bali wanapingana wao kwa wao na wangependa kuonyesha nani mwenye msuli katika "kulinda nchi" pindi ikiingia mgogoro.

4. Ni ubabe wa kipuuzi unaopuuza kekima na historia na unaodharau ushauri na juhudi za amani. Hapa Mtoi ana pointi.

ndi.

No comments

Powered by Blogger.