Header Ads

LightBlog

NIPIGE NIKUPIGE

Ni jana tu mjini Dodoma. Upigaji kura za "maruhani" ulishindikana. Msimamizi wa uchaguzi Kizota, Anna Makinda alikuja na utaratibu mpya. Kwanza, kila mkoa upigie katika sanduku lake peke yake. Pili, atakayeona karatasi ya kupigia kura imeharibika, aende kwake apate nyingine. Kumwondoa Kikwete uongozini kama Thabo Mbeki, kumekwama licha ya gharama za kikundi kimoja kudaiwa kupeleka vijana Afrika Kusini kujifunza jinsi ya "kumfungisha virago." Sasa wanaotaka kumwondoa watulie au wahamie chama kingine - kile chama cha washindi.

No comments

Powered by Blogger.