<?xml version='1.0' encoding='UTF-8'?><?xml-stylesheet href="http://www.blogger.com/styles/atom.css" type="text/css"?><feed xmlns='http://www.w3.org/2005/Atom' xmlns:openSearch='http://a9.com/-/spec/opensearchrss/1.0/' xmlns:georss='http://www.georss.org/georss' xmlns:gd='http://schemas.google.com/g/2005' xmlns:thr='http://purl.org/syndication/thread/1.0'><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839</id><updated>2012-01-06T06:41:43.624-08:00</updated><title type='text'>Uhuru Hauna Kikomo. Kikomo Kinawekwa Na Maadui Wa Uhuru</title><subtitle type='html'>Tunataka kuendelea kulinda uhuru wetu wa mawazo na uhuru wa kujieleza, kwani uhuru huo ni haki yetu. Na uhuru hauna kikomo, wala hakuna wakati tunapoweza kusema uhuru tulionao unatosha. Hapana. Kila hatua inazaa matakwa mapya ya uhuru wa binadamu.</subtitle><link rel='http://schemas.google.com/g/2005#feed' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/posts/default'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default?max-results=100'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/'/><link rel='hub' href='http://pubsubhubbub.appspot.com/'/><link rel='next' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default?start-index=101&amp;max-results=100'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><generator version='7.00' uri='http://www.blogger.com'>Blogger</generator><openSearch:totalResults>144</openSearch:totalResults><openSearch:startIndex>1</openSearch:startIndex><openSearch:itemsPerPage>100</openSearch:itemsPerPage><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-1270722877286208104</id><published>2010-12-23T11:00:00.000-08:00</published><updated>2010-12-23T11:14:23.105-08:00</updated><title type='text'>UTETEZI WA LUGHA ZA WATU NA HAKI ZAO</title><content type='html'>&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROeNwivN0I/AAAAAAAAAIU/y3g517yQ5R0/s1600/LewisMakame%2B2.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 250px;" src="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROeNwivN0I/AAAAAAAAAIU/y3g517yQ5R0/s320/LewisMakame%2B2.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5553956724684044098" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                        &lt;strong&gt;Lugha ya Tume ya Uchaguzi haisikiki&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                            &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt; Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI uamuzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wa kulazimisha matumizi ya Kiswahili peke yake katika kampeni za uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakumbuka ilikuwa hivyo mwaka 1995 wakati nagombea ubunge jimbo la Muleba Kaskazini. Bado ni hivyo hata leo. Safari hii matumizi ya lugha yamekuwa moja ya masharti ambayo vyama vimelazimishwa kusaini.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiswahili ni lugha ya taifa. Ni lugha kuu inayotumiwa na wengi ndani ya soko la ajira – serikali na makampuni yake, shuleni na baadhi ya vyuo; katika biashara za kati, ndogo na katika mawasiliano ya kawaida.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiswahili kimeenea mijini – miji mikubwa na midogo na katika baadhi ya vijiji ambako kimetumiwa kwa muda mrefu au wakazi wake wamekuwa na mwingiliano mkubwa na wale wanaozungumza lugha hii. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwingineko Kiswahili kimeenezwa na shule za msingi na sekondari ambako walimu na wanafunzi wameathiri matumizi ya lugha za asili, bila kusahau juhudi za makusudi za kupambana na ujinga kwa njia ya Elimu ya Watu Wazima (Kisomo Chenye Manufaa).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kampeni za kisiasa nazo zimekuwa na mchango mkubwa kwa uenezi wa lugha hii, zikiongezea kwa mipango ya awali, mara baada ya uhuru, ya kusambaza vipeperushi na filamu juu ya matakwa na mbinu za “maendeleo” katika Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na yote hayo, bado nchini Tanzania kuna maeneo ambako kuta za lugha za asili zingali imara; na hasa imara sana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni lugha hizi za asili ambazo zimeendelea kuwa chimbuko la misamiati na istilahi mbalimbali kwa matumizi ya sasa ya kukuza Kiswahili na hata kueleza maana halisi ya kile wanachosema wale wanaotumia lugha yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siyo bahati mbaya basi kwamba Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuna idara inayoshughulikia lugha za asili. Watafiti katika eneo hili hawafanyi kazi ya “kuzienzi” lugha hizi za asili – iwapo tutaazima vineno vya kisiasa – bali wanavuna maarifa ndani ya lugha hizo na kupitia lugha hizo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuwepo kwa lugha hizo kunakoweza kusaidia kuelewa jamii na utamaduni wake – kwa kudhamiria au kwa utuki tu – kumekuza na kunawirisha Kiswahili na hata lugha nyingine za asili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ndiyo maana kumekuwa na wanaharakati wa ngeli na ngeli wakitetea kuendelea kuwepo lugha za asili zilizohifadhi hekima na falsafa za jamii ambako zinatumika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, ni lugha hizi ambazo watafiti wanaoumba kamusi za Kiswahili na hata lugha nyingine zinazotumika katika maeneo haya, wanakimbilia kupata maneno halisi – hasa istilahi katika ufundi na teknolojia ya kale na sasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hizi basi siyo lugha za kuua hivihivi tu kisiasa. Bado zina nafasi muhimu katika jamii kama vile walivyo watu wanaozitumia; na wanaendelea kuwa Watanzania hata kama hawawezi kuongea Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa Tume ya Uchaguzi inasema wanasiasa wanaotafuta kura katika uchaguzi mkuu wasitumie lugha nyingine yoyote ile isipokuwa Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maagizo ya tume yanafanana na kanuni za Wizara ya Habari zinazolazimisha kila chombo cha habari kilichosajiliwa nchini, kutumia ama Kiswahili au Kiingereza – lugha mbili peke yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukichanganya haya ya maeneo mawili, utaona kuwa wasiojua Kiswahili hawapaswi kujua kinachotangazwa redioni au kinachoandikwa kwenye magazeti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni hivi: Kama hawajui lugha hizo – Kiingereza na, au Kiswahili – basi potelea mbali. Ndiyo tafsiri ya kile ambacho Tume inasema na ambacho serikali inasisitiza. Ndivyo wenye vyama walivyoweka saini kutetea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anayeomba kura, aingie Usukumani. Maeneo ambako Kiswahili hakitumiki kwa kiwango kikubwa. Pale ambako maneno ya Kiswahili yanatumika kwa ushabiki tu – ama kueleza kuwa anayeyajua ni “mkora” au “mwerevu” kutoka mjini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa, Tume inataka anayeomba kura atumie Kiswahili. Atatumia. Baada ya hotuba kuna kipindi cha maswali. Hakuna anayeuliza kwa kuwa hakuna aliyeelewa. Kuna haja gani basi ya kufanya kampeni katika “lugha ya kigeni?”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nendeni Loliondo vijijini, katika mkoa wa Arusha. Kuna shule za msingi. Wanafunzi na walimu wana akili nzuri. Wanajua kuwa Kiswahili na Kiingereza, zote ni lugha za ngeni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya walimu wanafundisha kwanza kwa Kimasai na baadaye kuweka katika Kiswahili. Njia bora kabisa. Ni kwa misingi sahihi kwamba lugha ya kufundishia iwe ile ambayo mwalimu na mwanafunzi wanaelewa. Mara hii ni Kimasai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wazazi katika eneo hili ambao ndio wapigakura, wanajua vema lugha yao moja – Kimasai. Wanaokwenda magulioni mara kwa mara ndio wameokoteza istitahi za kibiashara katika Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa aende mwanasiasa anayetafuta kura. Amwage hapa kampeni yake kwa Kiswahili. Ataondoka kama alivyokwenda. Mtupu. Bila kura hata moja. Kwa nini? Kwa kuwa hawakumwelewa; lakini pia kwa kuwa naye ni mpumbavu – anatumia lugha ambayo anajua vema kuwa anaowaambia hawaijui.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili lina tafsiri moja kuu. Kwamba kwa miaka 50 ya utawala wa chama kimoja, watawala wamekuwa wakiimba na kijipiga vifua kuwa wana “lugha ya taifa – Kiswahili.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe yamekuwa majigambo yasiyo na mashiko. Wameshindwa kueneza lugha hiyo hapa nchini kama walivyoshindwa kutumia wataalam wake kuigeuza kuwa “bidhaa” ya kuingiza fedha za kigeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wameshindwa kukuza Kiswahili; wameshindwa kukuza lugha za asili; wameshindwa kutoa ajira kwa wanaojua lugha hizo ili wawe wakalimani kwa wasiojua lugha za kigeni; wamebakia na amri – “Tumia Kiswahili!”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa amri na mantiki ya Tume, wasiojua Kiswahili “shauri yao.” Hii siyo haki. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi wanaojua lugha zao wanastahili kupelekewa kampeni katika lugha zao; na kama njia ya kueneza lugha kuu, wapiga kampeni waombwe kudondosha maneno ya Kiswahili hapa na pale kama kupanda mbegu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vinginevyo itafikiriwa kuwa serikali, na vyombo vyake, imeamua kuwatenga, kuwatelekeza, kuwasahau na kuwanyima haki ya kushiriki siasa za nchi yao, wale wote ambao hawajui Kiswahili au Kiingereza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria, kanuni na taratibu zinazoondoa haki ya mtu; kupoteza utashi wake, tena ndani ya nchi yake, hazistahili kuheshimiwa na haitakuwa mara ya kwanza kukataa kuzishemu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Njia bora ya kuzipinga ni kuongea na wananchi katika lugha yao. Wananchi ndio watakuwa watetezi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;em&gt;(Makala hii ilichapishwa Tanzania Daima mwanzoni mwa kampeni za uchaguzi, Agosti 2010)&lt;/em&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-1270722877286208104?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/1270722877286208104/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=1270722877286208104' title='11 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1270722877286208104'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1270722877286208104'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/12/utetezi-wa-lugha-za-watu-na-haki-zao.html' title='&lt;strong&gt;UTETEZI WA LUGHA ZA WATU NA HAKI ZAO&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROeNwivN0I/AAAAAAAAAIU/y3g517yQ5R0/s72-c/LewisMakame%2B2.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>11</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-6181289738618462421</id><published>2010-12-23T10:46:00.000-08:00</published><updated>2010-12-23T10:58:28.705-08:00</updated><title type='text'>BAADA YA KUONA WAMEZIDIWA KETE NA UMAARUFU WA DK. WILLIBROD SLAA</title><content type='html'>&lt;strong&gt;Wachovu wa CCM na umbeya wao: MWANZO WA UCHAKACHUAJI&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                    &lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI wananchi waingizwe kwenye ubishi wa kipuuzi unaopaliliwa na kunawirishwa na wachovu wa siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wiki hii tumesikia baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakidai kuwa watashitaki Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wamesema watapeleka malalamiko kwa Tume na Msajili wa Vyama vya Siasa kwamba Chadema imefanya kampeni kabla ya Tume kuruhusu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachotia kichefuchefu ni baadhi ya wanasiasa upande wa upinzani kuitikia kibwagizo cha CCM na wao kuimba kuwa Chadema na CCM wanaweza “kuchukuliwa hatua.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali iko hivi: Dk. Willibrod Slaa anateuliwa na chama chake kugombea urais. Chama kinaanua kufanya mikutano katika miji mikuu ya mikoa kadhaa. Kinambeba mteule wake. Hii ni kwa sababu kuu mbili:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, kumtambulisha kwa wanachama wake na wananchi. Pili, kuendeleza kazi yake ya kisiasa kama chama chochote kile kilichohai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama kilichohai, kikipata fursa, sharti kiitumie kuwafikia majaji wakuu katika taratibu za kidemokrasia; ambao ni wananchi wapigakura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chadema haikufanya hivyo juzi tu. Imekuwa ikifanya hivyo kila inapotaka kuwa karibu na wananchi; na wapigakura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo ndivyo CCM imefanya. Imetangaza wagombea wake, halafu ikawapeleka kwenye mikutano ya hadhara – kwa wapigakura – ili wanachama wenzao na wananchi wawafahamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama kingine chenye ushindani ni Chama cha Wananchi CUF. Hiki hakikuwa na kiongozi wa kutambulisha kwani mgombea urais wake mwaka huu, ni Profesa Ibrahim Lipumba ambaye tayari amepigiwa kura za urais mara tatu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, CUF muda mfupi baada ya kutangaza mgombea wake, iliweka wazi kwa mgombea, ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho kitaifa, atatembelea mkoa wa Dar es Salaam kwa madhumuni ya “kuangalia uhai wa chama.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiyo nayo ni fursa nyingine kwa chama makini kuwa karibu na wananchi na wanachama wake wakati muhimu wa kuelekea uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiangalia kwa makini, utaona kuwa kila chama kina njia zake za kufanya kazi za kisiasa – iwe asubuhi, adhuhuri, alasiri, mangharibi au usiku.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muda huu wa maandalizi ya kuingia kipindi maalum cha kampeni na uchaguzi mkuu, hautawaliwi na pingu za NEC. Ni muda na eneo huru la kuzidisha kazi za kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hasa ni kipindi maalum kwa vyama upande wa upinzani, kutekenya jamii, kuizindua, kuielimisha, kuishawishi na kuiandaa kuachana na ukale ulioizonga na kuipa kilema – kudumaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mfano, kwa upande wa Chadema, ni wakati wa kuendeleza na kuhitimisha kwa nguvu, kazi ya kisiasa inayoitwa “Operesheni Sangara” – iliyovuma na kuvuna nyoyo za wengi – kabla ya kuingia katika uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wa CUF, ni wakati mzuri wa kuendeleza na kuhitimisha kazi ya kisiasa iliyoitwa “Zinduka” – iliyozindua wengi – kabla ya kuingia katika uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, kinachoipa kiwewe CCM, siyo Chadema “kufanya kampeni” kabla ya muda uliopangwa na Tume, bali umaarufu wa mgombea wa Chadema anapolinganishwa na yule wa chama chao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiwewe kinatokana na mgombea mpya anayefahamu vema serikali na nyendo zake. Anayejua serikali ilivyokwama kwenye tope la ufisadi, ukosefu wa ubunifu; ukame wa mbinu mpya na ahadi tuputupu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kelele za CCM zinalenga kufanya mwendelezo wa ghiliba kwa wananchi. Chama hiki, kama ilivyo serikali yake, kina midomo mingi na uwezo wa kupakazia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kina vyombo vya habari vya serikali (wanadai ni vya umma), ambavyo vinatawaliwa na makada wake. Humu hupitishwa kampeni na propaganda angamizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CCM ina “marafiki” wenye vyombo vya habari ambao huipendelea kwa kila hali kuliko hata gazeti lake la UHURU.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kutumia midomo yake mingi; laghai wake wengi; ujuzi na uzoefu wa kutunga ghiliba na kupakazia, chama hiki kinaweza kuanzisha mjadala finyu, kikaupa mvumo, ukapandikiza mitafaruku na kupotosha wananchi wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama hikihiki kinaweza kutumia kauli za nguvu kuyumbisha watendaji serikalini; kutishia walioko madarakani katika sehemu muhimu kama Tume ya uchaguzi na kuogofya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haitakuwa mara kwanza kwangu kujenga hoja kwamba watawala wetu wamekuwa wakitegemea sana ujinga, woga na umasikini wa wananchi (vilivyosimikwa na chama kinachopanga ikulu), kama mitaji yake mikuu katika juhudi za kubaki madarakani kwa nusu karne sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama hiki kina watu wenye ujasiri wa kukataa ukweli; wakaidi wa kutaka kila mmoja aone, kwa mfano, kuwa hili ni chungwa wakati ni kiazi kikuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CCM isingekuwa hivyo, kama ilivyofafanuliwa hapo juu, viongozi wake wasingejitokeza kupandikiza uzushi kwamba Chadema imefanya kampeni kabla ya NEC kutangaza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani kampeni za kuwaelimisha wananchi kujua kuwa diwani, mbunge au rais huyu hafai; anayefaa ni fulani kutoka chama kingine, hazisubiri uchaguzi mkuu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni kazi ya Oktoba hadi Oktoba, kwa kipindi chote cha miaka mitano ya wanaokuwa madarakani na wanaokuwa wakisubiri kuingia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi chote hiki NEC inajiandaa kusimamia uchaguzi lakini wanasiasa wanakata mbuga kuandaa wananchi kwa “mavuno.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa hakuna udhibiti hadi unapoingia rasmi kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu. Kazi za kisiasa za chama chochote, haziruhusiwi wala hazipaswi kuzuiwa na Tume. Na pasito zuio kuna uhuru kamili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mfano huu: Katika mazingira ambako hakuna sheria inayolazimisha kila mmoja kuvaa tai shingoni, hakuna anayeweza kukamatwa na kushitakiwa kwa kutovaa tai. Hakuna sheria inayombana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiyo ndiyo hali iliyopo katika kipindi ambapo wachezaji watarajiwa wa mchezo wa siasa hawajajifunga kushiriki; na mchezo wenyewe haujaanza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huwezi kuwabana. Huwezi kusema aliye nje ya uwanja ameharibu kanuni na taratibu za mchezo. Kudai hivyo ni kupanda mbegu ya uhasama ambao CCM na serikali yake, havina uwezo wa kuzima ndimi zake pale zitakapokuwa zimechomoza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi sasa, CCM ni chama kinachokwenda kwa mazoea tu. Hakina jipya ingawa kinataka kubaki ikulu, kwa “gharama yoyote ile.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na hili la kubaki madarakani kwa gharama yoyote ile, ndilo liwezalo kuleta maafa kwa nchi na watu wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani wanajua kuwa kuondoka kwao kutaweka wazi mengi machafu ambayo yamekuwa yakitendeka.  Hili, viongozi wake hawataki kuliona wala kulisikia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wako tayari kuua mbegu mpya na bora kwa kupitia madai yasiyo kichwa wala miguu, alimradi wamebaki ikulu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini katika hili la kupakazia kufanya kampeni mapema, tundu limezibwa. Hata kwa mgongo wa “tu-vyama twingine” kwenye upande wa upinzani, kama vile Tanzania Labour Party (TLP) ka Augustine Mrema, CCM itaendelea kukaliwa kooni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tayari kuibuka kwa Dk. Slaa kumebadili mwelekeo wa siasa nchini na kuleta uwezekano wa kuifinyaza CCM na mikonga yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali wananchi wanataka umoja wa vyama; kwa maana ya ushirikiano katika uchaguzi huu ili mradi wa kuadabisha CCM uweze kufanikiwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umbeya na ghiliba ya CCM vyaweza kuzimwa. Je, hili la ushirikiano laweza kufikiwa? Tusubiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii ilichapishwa katika Tanzania Daima, Novemba 2010 katikati ya vuguvugu la uchaguzi na CCM ilipoanza kuhaha)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-6181289738618462421?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/6181289738618462421/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=6181289738618462421' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6181289738618462421'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6181289738618462421'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/12/baada-ya-kuona-wamezidiwa-kete-na.html' title='&lt;strong&gt;BAADA YA KUONA WAMEZIDIWA KETE NA UMAARUFU WA DK. WILLIBROD SLAA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-4897024250486108350</id><published>2010-12-23T10:22:00.003-08:00</published><updated>2010-12-23T10:33:14.376-08:00</updated><title type='text'>USHINDI 'CHAKUPEWA' WA CHAMA CHA MAPINDUZI</title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROVGtxdwcI/AAAAAAAAAIM/IgT7TNXcWbg/s1600/jAKAYA%2B4.jpg"&gt;&lt;img style="float:right; margin:0 0 10px 10px;cursor:pointer; cursor:hand;width: 247px; height: 314px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROVGtxdwcI/AAAAAAAAAIM/IgT7TNXcWbg/s320/jAKAYA%2B4.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5553946708076773826" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;              &lt;strong&gt;MADAI YA WIZI WA KURA YATAWALA MIJADALA &lt;br /&gt;          MAJUMBANI, SHULENI, VYUONI, SOKONI, MAOFISINI &lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                          &lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kuwaudhi wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwaambia kuwa aliyeshinda katika uchaguzi mkuu siyo Jakaya Kikwete bali Dk. Willibrod Slaa na kambi ya upinzani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kutotaka kuwaudhi, sitaki pia kuandika kwa urefu kwa kuwa matukio ya hivi karibuni, yanayohusu uchaguzi, yangali mabichi na wananchi wanahitaji kuyajadili, kuyatafakari na kuyafanyia kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niseme tu kwamba waliokuwa bado na shaka juu ya uwezekano wa CCM kuwekwa kando, kufungiwa virago na kuondoshwa ikulu, sasa waanze kufikiri upya. Inawezekana!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho kinatangazwa kuwa ushindi wa CCM wa asilimia 61 katika uchaguzi mkuu ndicho hasa kinaonyesha mporomoko wa chama hicho na uwezekano wa kuenguka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lini Tanu na CCM viliwahi kufikia asilimia 60 za kinachoitwa “ushindi” hata katika mazingira ya “ushindani wa mwendawazimu” anayekimbia peke yake na hatimaye kudai ameshinda?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lini, tangu kurejeshwa kwa maneno ndani ya katiba “mfumo wa vyama vingi vya siasa,” lakini kubakia chama kimoja kifikra na kiutendaji, CCM imewahi kupewa asilimia 60?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani, miongoni mwa viongzi wa CCM, akiwemo mwenyekiti Jakaya Kikwete, aliwahi kuota Tume inawapa asilimia 60 au kupata kiwango hicho kwa njia zao za abrakadabra?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata Kikwete alipokuwa anaanza na kufunga kampeni, alitangaza kuwa atashinda kwa “kishindo kuliko hata ilivyokuwa katika uchaguzi uliopita” – 2005. Yako wapi? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, ni mtindo wa watawala wa Uingereza wakati wa Vita Vikuu vya Pili? Walikuwa wakitangaza kuwa tayari vita vimeisha; Wajerumani wamesambaratika na wengine wamejisalimisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nia ilikuwa kuamsha na kujenga morali ya wapiganaji wao na kuzamisha na kufisha morali ya Wajerumani na waliowaunga mkono.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yawezekana CCM imefikia viwango hivyo? Propaganda za “kyakutinisa kitakulye” – kinachoogopesha lakini kina madhara kidogo au hakina madhara kabisa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mfano mmoja. Kwa maamuzi ya haraka na ya dakika ya mwisho, kwamba Dk. Slaa ndiye awe mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), chama cha zamani CCM kimetikisika hadi mizizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa miezi mitatu tu ya kuwafikia wananchi, hata mahali ambapo chama cha Dk. Slaa hakikuwahi kusikika, elimu ya uraia kwa njia ya mikutano ya hadhara imepenya kwa kasi.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kwa miezi mitatu tu ya kuwafumbua macho wananchi na kuwasaidia kuchambua matatizo yao, wameelewa kuwa kumbe watawala wao wamekuwa sehemu ya matatizo yao. Hivyo hawana msaada kwao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yote hii ni kwa vile kwa miaka mingi wameishi kama wafungwa; wana utulivu ya magereza lakini bila amani. Sasa wameona anayewasaidia kutafakari maisha yao na kwa kiasi fulani kukata baadhi ya minyororo kwa kauli chambuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mzunguko wa miezi mitatu, ulioongozwa na Dk. Slaa, kwa hoja nzito na kauli za matumaini mapya, CCM imeporomoka kutoka “ushindi wa kishindo” hadi asilimia 61 ilizopewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika baadhi ya maeneo, na hasa kule ambako CCM iliishakuwa serikali, polisi, mahakama na bwana jela, ujumbe wa Chadema na Dk. Slaa umefanya baadhi ya wananchi waone kuwa “kumbe CCM ni chui wa karatasi.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miezi mitatu ya kutafuta kuwaamsha wananchi kuchukua serikali yao kutoka kwa waliochoka na walioshindwa kuleta, siyo tu mabadiliko bali hata matumaini, imezaa uelewa mpana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukichukua asilimia 61 za wanaotamba kubakia ikulu na kulinganisha na maarifa – uelewa, ung’amuzi, mwamko, matumaini mapya na utayari wa wananchi kushiriki katika kuleta mabadiliko katika maisha yao, ndipo utagundua kuwa CCM “wameliwa” au “wamejila wenye.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mfano mwingine. Profesa Kulikoyela Kahigi alishinda katika kura za maoni ndani ya CCM; jimbo la Bukombe. Akafanyiziwa. Rufaa yake ikazimwa. Vijana na wazee wakasema, “…nenda kule tutakupigia kura hukohuko.” Leo ni Mbunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Juhudi za Yusuf Makamba, katibu mkuu wa CCM, kujaribu kugeuza mkondo, zilikwama. Alifikia hatua ya kutukana wanachama na viongozi wake kuwa wamrejeshee mashati yake ya kijani, kama wanakuwa wanachama mchana tu na usiku wanakwenda upinzani. Kyakutinisa kitakulye!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfano huohuo unahusika Maswa Magharibi ambako ghiliba na husuda vilikuwa sehemu ya sala ya viongozi wa CCM kwa shabaha ya kumzima John Shibuda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Shibuda alihama CCM baada ya kuenguliwa. Naye akasema hakuna chama pale na kwamba kilikuwa kinaishi kwa pumzi ya rushwa. Wananchi wamemlinda. Wamemchagua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miezi mitatu ya kazi ya Dk. Slaa na chama chake; juu ya kazi ya awali ya sauti ya mageuzi; vimejenga ujasiri usiomithilika nyoyoni mwa umma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kila mahali ambako uelewa na maarifa vimesambazwa na kuzama vichwani na nyoyoni mwa wananchi, CCM imedaiwa kuvuna sifuri au kujichukulia “kwa mbinu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wala Dk. Slaa hana sababu ya kusononeka na kulia. Hapana! Ameshinda. Mara hii ushindi wa kishindo; tena ulio halali na tofauti na vungavunga ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiwewe kilichotembelea CCM kutokana na wimbi kubwa la upinzani na nguvu ya mgombea wa Chadema, vimefanya chama hicho kilichopanga ikulu kiweweseke, kiishiwe nguvu na hata kuwa butu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kiwewe kilichofanya viongozi wa CCM wajiingize katika kujadili uchumba, ushenga na ndoa ya Dk. Slaa. Ni hichohicho kilichofanya waanzishe mtandao wa vineno vya kashfa na kuvisambaza nchi nzima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiwewe hichohicho ndicho kilifanya CCM wabuni uwongo juu ya Dk. Slaa kuwa ni mbishi, kaidi na anayegombana na vyombo vya ulinzi na usalama na anayetaka kuleta vita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Walilenga kuwa wananchi wakisikia Dk. Slaa “anagombana na askari,” basi watamkimbia na CCM itakuwa imepona upele ulioletwa na upupu wa ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Eti wananchi waogope vita vya kujikomboa lakini wasijali mafisadi wanaowaibia na kufanya maisha yao yatoweke haraka kuliko kama kungekuwa na vita! Kyakutinisa kitakulye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni CCM waliopenyeza katika hotuba zao, madai ya vita na kumbukumbu za vita vya Burundi na Rwanda ili wananchi wakatae mpiganaji wa Chadema. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni chama hicho chenye kupanga ikulu, ambacho kilianzisha na kuvumisha kuwa kuna “udini” kikilenga kuzamisha sauti za wapenda mabadiliko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati askofu wa katoliki anasema, mwaka 2005 kuwa Kikwete, ambaye ni mwislam, ni “Changuo la Mungu,” CCM walikaa kimya. Leo, Kikwete anachuana na mkristo mwenye rekodi nzuri na ambaye hashikiki kwa hoja, CCM inaibua madai ya udini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chadema imetumia uchaguzi mkuu huu kuandaa mtaji kwa ajili ya uchaguzi ujao. Kile ilichobakiziwa kwa njia ya idadi ya kura na asilimia, ni ushahidi tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wekezo kuu la Chadema katika uchaguzi ni elimu iliyowaacha wananchi na maarifa mapana; ujasiri wa kusema “hapana” na utashi wa kuchagua chenye thamani na endelevu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kutumia mizani hiyo, mbegu ya mabadiliko imepandwa nyoyoni mwa wananchi wengi; haiharibiki kwa ukame wala mafuriko ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndiyo maana ni halali kusema Chadema imevuna; ukitaka – imeshinda. Si kwa asilimia peke yake ambazo zaweza kutiliwa shaka, bali hasa kwa wekezo la maarifa na ujasiri ambavyo ni muhimu kesho, kuanzia ngazi ya kaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;em&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii ilichapishwa katika gazeti la Tanzania Daima mara baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu, Novemba 2010)&lt;/strong&gt;&lt;/em&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-4897024250486108350?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/4897024250486108350/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=4897024250486108350' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/4897024250486108350'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/4897024250486108350'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/12/ushindi-chakupewa-wa-chama-cha.html' title='&lt;strong&gt;USHINDI &apos;CHAKUPEWA&apos; WA CHAMA CHA MAPINDUZI&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROVGtxdwcI/AAAAAAAAAIM/IgT7TNXcWbg/s72-c/jAKAYA%2B4.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-5277058704279954754</id><published>2010-12-23T10:12:00.000-08:00</published><updated>2010-12-23T10:20:24.574-08:00</updated><title type='text'>MUNGU, WACHAWI NA UCHAGUZI TANZANIA</title><content type='html'>&lt;strong&gt;Baadhi ya imani zinazoathiri fikra za &lt;br /&gt;             wengi katika siasa na maisha ya kawaida&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NI mahojiano ya chapuchapu, kwenye kaunta ya M.S. Hotel jijini Mwanza, Jumatano 27 Oktoba 2010. &lt;strong&gt;Ndimara Tegambwage &lt;/strong&gt;aliyeko hapa kwa ushauriano na waandishi wa habari wa kanda ya Ziwa Viktoria, anakutana na Fikiri Mabula na kwa muda mfupi anapata “fikra” za binti mdogo juu ya Mungu, uchawi na uchaguzi mkuu wa 31 Oktoba. Fuatilia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Wewe unaonekana mdogo. Unafanya kazi hapa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Hapana. Nimemfuata dada yangu. Kwa nini unauliza hivyo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali:  Niliona kama mwenyeji vile; halafu nikaona kwa umri huo usingekuwa mfanyakazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Siyo mfanyakazi hapa lakini natafuta kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Una umri gani?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Mimi? Miaka mingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Miaka mingi mingapi? Kama yangu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Ehee! Miaka 22.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Una watoto wangapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Mimi? Mmoja tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Ungetaka kuwa na wangapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Wengi ni wangapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Watano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Wote hao utaweza kuwatunza na kuwasomesha shule?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Eee, wewe vipi? Hivyohivyo tu. Sasa nikizaa…kwani wewe ungetaka nizae wawili au watatu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Unaniuliza mimi tena? Naona ungekuwa na watatu tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Watatu? Watatu tu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Si ndiyo? Halafu urudishe mwili; utulie na kutafuta njia za kuwalea na kuwasomesha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Mimi naona nizae watoto watano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Wote hao wa nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Sikiliza. Nikizaa watano, Mungu atachukua mmoja; dunia itachukua mmoja na wachawi watachukua mmoja. Nitakuwa nimebakia na hutu tuwili (akionyesha kwenye vidole).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Kwani Mungu anahitaji mtoto wako?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Eee! Imeandikwa. Yeye akitaka anachukua wakati wowote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Aache kuchukua mtu mzima kama mimi hapa achukue kifaranga chako?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Eee! Hata akichukua mtu mzima; atakuwa amechukua mtoto wangu. Yeye anaamua lini anataka kumchukua; uwe mdogo au mkubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Na wachawi je? Wana sababu gani ya kuchukua mtoto wako?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Wewe! Wenye roho mbaya; hawapendi kuona mtu akipata kitoto chake kizuri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Mbona watoto wazuri wako pote duniani. Hivi wachawi hawajawaona au wameelemewa kwa kuwa dunia ni kubwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Labda huko kwingine hakuna wachawi; lakini katika maeneo yetu haya, wapo na wana roho mbaya kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Au dini ndiyo imepunguza wachawi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Inaonekana wewe hujui mambo mengi. Hao wanaoonekana waumini wakuu ndio wanakamatwa kila siku wakifanya uchawi makaburini; lakini Jumapili au Ijumaa ndio wako mbele karibu na mchungaji au sheikh. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Wewe ni mwislamu au mkristo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Mimi mwislamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Lakini kwa ulivyoelezea waumini wachawi, ina maana kuwa huendi msikitini kusali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Naenda. Mimi ni mwislamu lakini dada zangu wawili na baba, ni wakristo. Kila mmoja na madhehebu yake. Mimi nimekaa upande wa mama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Hapo nyumbani hamgombani kwa kuwa na imani tofauti?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Tugombanie nini? Kila mtu anaamini vyake. Kuna mambo yanayofahamika kuwa ni mabaya, kama wizi, uchawi, hayo mmoja wetu akiyafanya lazima tutagombana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Je, kama mnatofautiana kisiasa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Kisiasa? Hayo si mambo ya wanasiasa? Sisi kazi yetu kupiga kura tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Si mnaweza kugombania nani awe diwani, mbunge au rais?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Wewe unachekesha. Tugombanie chakula cha wengine? Kwa nini? Mimi kwa mfano, nitapiga kura kwa mara ya kwanza. Nitampigia Kikwete. Wengine wote pale nyumbani wanasema watampigia Dk. Slaa. Sasa ugomvi utatoka wapi? Kila mtu na chaguo lake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Kwa nini unataka kumpigia Kikwete?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Wewe unataka niseme mengi. Kwanza nimeishatoa siri yangu ya nani nitampigia; na sasa unataka sababu za kumpigia kura ninayependa. Au wewe mwandishi wa habari?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Nadhani sababu za kupenda mgombea siyo siri. Kila  mmoja anasema… na hakuna siri, au vipi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Mimi sina sababu kubwa. Ni kama wasemavyo “zimwi likujualo...” Kwa kuwa amekuwepo, basi naona aendelee huyohuyo. Halafu kuna maneno yanapita…mh, hayo tuyaache. Nitachagua huyo. Kwani wewe utachagua nani?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Unataka nami nitoe siri? Nitachagua mmoja wa wagombea (kicheko).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Sawa, lakini nimekuuliza, wewe ni mwandishi wa habari?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Napenda kuwa mwandishi wa habari. Kwani wewe unaona nafanana mwandishi wa habari?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Huwa wanasema waandishi wa habari huuliza maswali mengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Kwani polisi hawaulizi maswali mengi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu:  Sijawahi kuhojiwa na polisi. Sijui (kicheko).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;em&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii ilichapishwa katika toleo maalum la gazeti la MwanaHALISI,20 Oktoba 2010 kwa lengo la kuhamasisha wapigakura)&lt;/strong&gt;&lt;/em&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-5277058704279954754?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/5277058704279954754/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=5277058704279954754' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5277058704279954754'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5277058704279954754'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/12/mungu-wachawi-na-uchaguzi-tanzania.html' title='&lt;strong&gt;MUNGU, WACHAWI NA UCHAGUZI TANZANIA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-8926844374778421305</id><published>2010-12-23T09:55:00.000-08:00</published><updated>2010-12-23T10:11:04.239-08:00</updated><title type='text'>CHILIGATI: WAZIRI HATARI, ANATETEA UBABE, ANAPINGA DEMOKRASI, ANACHOCHEA VURUGU</title><content type='html'>&lt;a href="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROPbRnj5sI/AAAAAAAAAIE/4I13qbN93Hs/s1600/john-chiligati.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 250px; height: 218px;" src="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROPbRnj5sI/AAAAAAAAAIE/4I13qbN93Hs/s320/john-chiligati.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5553940464226526914" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;               &lt;strong&gt;Chiligati, CCM wanaandaa maafa&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                    &lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kusikia Rais Jakaya Kikwete akifikiria kumteua John Chiligati kuwa mmoja wa mawaziri au washauri wake wa karibu. Amwache.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya Chiligati kuhusiana na wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukataa kumsikiliza rais akihutubia Bunge la 10, zinaonyesha ni mtu wa shari asiyemwelewa hata rais ambaye anadai kumtetea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfano Na. 1: Chiligati anasema bunge linaweza kuandaa azimio la kuwaondoa wabunge wa Chadema waliotoka nje ya bunge wakati Rais Kikwete ameanza kuhutubia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yaani katibu mwenezi taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) – bila woga wala aibu – anajenga hoja ya kula njama ya kufukuza wawakilishi wa wananchi wa chama kingine – Chadema, kutoka bungeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwamba wabunge wengi wa CCM, ambao hujigamba kuwa wanajua demokrasia; watumike kufukuza wawakilishi wenzao wa chama kingine kwa madai ya kutomsikiliza rais akiongea bungeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chiligati ni hatari. Ana lake jambo. Anajenga woga miongoni mwa wabunge. Anajenga wasiwasi, chuki na uhasama miongoni mwa wananchi. Anafanya uchokozi na kutukana wapigakura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katibu mwenezi wa CCM anataka kuzua mtafaruku mchafu, wa aina yake, ambao hauwezi kuishia kwenye kauli tupu na ambao Chiligati na waliomtuma hawawezi kuuzima. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfano Na. 2: Chiligati anataka watu wakae kimya. Wasitoe neno. Wasilalamike. Wasikemee. Wasisute. Wasilie. Wasilaani. Wasinune. Wasipinge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiona kiongozi ana akili ya aina hiyo, ujue ni mbegu ya udikiteta, ukatili, lakini pia ni mtu asiye na chembe ya fikra juu ya matokeo ya kauli na matendo yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Asiyetoa kauli ya wazi kutokana na vitisho vya watawala, anajenga hazina ya hasira na chuki. Kauli, hasira na chuki ambavyo havikutoka leo kutokana na ubabe wa watawala, vitatoka kesho lakini kama bomu la maangamizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chiligati hajui hayo au anayajua lakini anayapuuza. Anaongea kwa jazba. Anafoka. Aanaunda bomu la maangamizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msemaji huyo wa CCM anajua kuwa Chadema hawajafanya lolote baya kwa kukataa kumsikiliza rais. Hakuna sheria wala kanuni inayoweza kuwabana wabunge kwa kutomsikiliza rais. Haipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna sheria wala kanuni inayozuia wabunge au hata chama kusema. “…wewe umeniibia kura. Sitambui ulivyopata ushindi.” Haipo!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chiligati ataleta balaa. Chiligati ataleta maafa. Chiligati anatamka hadharani kuwa wabunge wa Chadema, waliochaguliwa na wananchi, wafukuzwe na wabunge wenzao wa CCM wakishirikiana na wale wa vyama vingine vidogo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya wananchi na hasa wanachama wa CCM wameanza kuamini kuwa hilo linaweza kutendeka. Haliwezekani! Chiligati anachezea akili za wananchi wapigakura. Ataleta balaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyu bwana anajaribu kudharau, kuchezea na kusimanga kura za wananchi zipatazo milioni mbili na nusu zilizosema kuwa zimeichoka CCM na zinataka mabadiliko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbona Kikwete mwenyewe anajua haya? Chiligati amekwama wapi? Siyo lazima aseme, lakini Kikwete anajua vema kuwa ana katiba yenye makengeza; inayotumika kuminya uhuru na haki za wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbona anajua kuwa ana katiba na sheria vinavyowazuia wananchi anaotawala kudai haki zao? Hatasema lakini anajua vema kuwa chombo kama vile Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ni “mali yake” na chama chake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anapokuja mtu wa saizi na viwango vya Chiligati na kusema wabunge wa chama kikuu cha upinzani wafukuzwe bungeni, anamtakia mema Kikwete na utawala wake? Bado anataka kazi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itakuwa wapi amani anayohubiri? Utakuwa wapi umoja anaopeperusha midomoni kwake? Utakuwa wapi utulivu anaodai anataka iwapo atatukana na kuvunja uhuru na haki za wapigakura?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chiligati anaonekana kuwa na tatizo la “kulipua kauli” bila kufikiria matokeo yake. Kwamba anaweza kusema sehemu ya “bunge la CCM” ifukuze sehemu kubwa ya “bunge la upinzani,” ni kutokuwa makini; ni kutumia jazba badala ya fikra ang’avu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani anaweza kusema mtu huyu anamwakilisha rais ambaye angetaka kufikia mwisho wa kipindi chake kwa furaha na hata kupata mahali pa kuishi baada ya urais bila kusumbuliwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nasema Kikwete hakubaliani na Chiligati kwa kuwa huyu Kikwete amekuwa katika nchi nyingi duniani akiwa waziri wa mambo ya nje. Ameona na kushuhudia makubwa zaidi ya kumwacha rais akihutubia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kikwete ameona marais wanaotupiwa viatu, mayai viza, mawe, mchanga; wanaosusiwa wanapokwenda kwenye majimbo ya baadhi ya wabunge na wanaopingwa moja kwa moja kwa kauli kali na katili. Kitu gani Chadema kumwacha apumue bila presha!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Chadema wana haki ya kuchukia. Walisema hawatambui matokeo yaliyotangazwa na Tume. Hawakwenda kwenye sherehe za matokeo. Hawakwenda kwenye kuapishwa kwa rais. Hawakuwa kwenye kuapishwa kwa waziri mkuu. Na juzi walifunga kazi kwa kutomsikiliza Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Basi. Inatosha. Wapigakura wao wamesikia; wanasubiri ufafanuzi tu wakati wa mikutano ya kuwashukuru kwa kuwapa kura ambazo hazijawahi kwenda kwa upinzani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wale ambao hawakuwapigia kura nao wamesikia. Wanaoitwa washindi wamesikia. Tume imesikia. Mataifa yamesikia. Kila hatua ina fundo lake. Baada ya hapa wanaanza kazi yao ya uwakilishi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua zote hizi ambazo Chadema wamechukua, zina maana kwao wakiwa chama; zina maana kisiasa na katika kushamirisha hoja nzito za kuwa na Tume huru ya uchaguzi na katiba mpya inayokidhi matakwa ya sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anatoka wapi Chiligati kudai kuwa hatua hizi za Chadema ni usaliti? Usaliti upi na kwa nani? Yeye aliwatuma wafanye nini na yeye ni nani kwa chama hiki?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni Chiligati anayepandikiza chuki. Hataki kuonwa kama anavyoonekana. Anataka kurembwa kwa marashi, poda na hariri. Azivae basi zionekane nje na ndani ya roho yake. Hana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chadema wameonyesha jambo moja kubwa na la kuigwa. Wamekomaa katika kufikiria na kutumia mbinu sahihi kufikisha ujumbe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Enzi za kuviziana kwa mawe, mchanga na mayai viza zimepitwa na wakati; hasa unapokuwa una uhakika kuwa unachosema ndicho kile ambacho wananchi wengi wanapenda na kusimamia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Labda kwa kumsaidia Rais Kikwete hapa ni kwamba, hakika watatoka na kuingia, lakini siyo kwa kuibembeleza serikali kutekeleza miradi katika majimbo yao. La hasha!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi ni walipakodi. Kukataa kupeleka miradi ya maendeleo katika majimbo ya upinzani ni aina nyingine ya rushwa miongoni mwa rushwa kubwa. Ni uhalifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo anayetarajia kupigiwa magoti ili apeleke miradi ya maendeleo katika jimbo la upinzani, ajue anamwita budi kulilia mlangoni mwa chama chake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira ya sasa, hasa kwa mwamko wa wananchi, acha uchaguzi uje, kiongozi wa namna hiyo atatupwa nje, hata kama amekuwa madarakani mwa miaka 50.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali kauli za Chiligati hazinabudi kuogopwa na kukataliwa; njama zake kuvunjwa na yeye kuzomewa. Kwani mbegu yake ikiruhusiwa kumea, ndiyo hatari kuliko hatari zote tulizowahi kutamka nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chiligati anataka kuua uhuru wetu na haki zetu kama zilivyojitokeza kupitia hatua za Chadema katika wiki mbili hizi. Hatukubaliani na mpango wake; heri ufe mapema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bila shaka Chiligati siyo mmoja wa wachapakazi ambao Kikwete anahitaji. Kama ni uchapakazi, basi ni ule wa kuleta maangamizi. Tunayachukia. Tunayakataa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;em&gt;&lt;strong&gt;MREJESHO:&lt;/strong&gt; Rais Kikwete hakumchagua Chiligati.&lt;/em&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii ilichapishwa katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili, Novemba 2010)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-8926844374778421305?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/8926844374778421305/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=8926844374778421305' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8926844374778421305'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8926844374778421305'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/12/chiligati-waziri-hatari-anatetea-ubabe.html' title='&lt;strong&gt;CHILIGATI: WAZIRI HATARI, ANATETEA UBABE, ANAPINGA DEMOKRASI, ANACHOCHEA VURUGU&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROPbRnj5sI/AAAAAAAAAIE/4I13qbN93Hs/s72-c/john-chiligati.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-9066354918655097989</id><published>2010-12-23T09:29:00.000-08:00</published><updated>2010-12-23T09:52:30.421-08:00</updated><title type='text'>KATIBA MPYA! KATIBA MPYA TANZANIA</title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROKwz04ZyI/AAAAAAAAAH8/AKaQUez4gkM/s1600/Kikwete%2B2.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 130px; height: 87px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROKwz04ZyI/AAAAAAAAAH8/AKaQUez4gkM/s320/Kikwete%2B2.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5553935336628315938" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                    &lt;strong&gt;WANANCHI WAANZA KUDAI KATIBA MPYA&lt;br /&gt;                            SERIKALI YA KIKWETE YAWEWESEKA&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                    &lt;strong&gt;Katiba mpya ndilo jibu pekee&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                              Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;BAADA ya wabunge wa Chadema kumwacha Rais Jakaya Kikwete bungeni, kwa shabaha ya kusisitiza umuhimu wa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, watawala wameweweseka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyu anadai Chadema wanataka kuvunja umoja, amani na utulivu wa Tanzania. Yule anafura mithili ya kufutu akidai Chadema “wahaini.” Mwingine analoloma kuwa Chadema ni wasanii; na mwingine anasema wafukuzwe bungeni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kila watawala wanapobanwa hukimbilia kauli zenye utata au uwongo wa moja kwa moja: kuwa wanaodai haki yao au ya jamii au taifa zima, wanataka kuleta vita na kuondosha amani na utulivu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo ndivyo wananchi wamezoeshwa. Watawala hawataki wananchi wafikiri zaidi ya hapo. Kauli za “wanaotaka kuleta vita na kuondoa amani,” ni silaha kuu za watawala katika kunyamazisha umma na hata kuufanya usifikiri tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa miaka 18 sasa kumekuwa na madai ya wazi kwenye majukwaa ya siasa kuwa nchi inahitaji katiba mpya na tume huru ya uchaguzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watawala ama wametoa majibu ya kejeli au wamekaa kimya. Walichoona kwenye marekebisho ya katiba ni kutamka tu kwamba nchi ni ya mfumo wa vyama vingi vya siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kamba, minyororo, pingu na magereza, vilivyomo ndani ya Katiba ya nchi na sheria za uchaguzi, vimebaki vilevile. Siyo kwamba watawala havioni. Wanaviona kuwa ni vya ubabe na katili, lakini wanaviacha viendelee kuwemo kwa kuwa vinawasaidia kubaki madarakani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tuchukue mfano halisi wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Jielekeze kwenye Ibara 41 (7). Inasema hivi:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chini ya utawala wa mfumo wa chama kimoja, lilikuwa kosa kumpinga rais. Kwanza, rais alikimbia peke yake kama mwendawazimu na hatimaye kijitangaza kuwa ameshinda. Alikuwa anashindana na nani?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa kuna “Ndiyo” na hapa kuna “Hapana.” Ukiandika ndiyo ina maana kuwa ni yuleyule. Ukiandika hapana, ina maana kuwa hapana mwingine isipokuwa huyohuyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yule ambaye chama tawala kimetaka awe rais, hata akipata “Hapana” nyingi, lazima ziwe au zionekane, au zisomeke au zionyeshwe kuwa ni “Ndiyo.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuelewa kuwa hatimaye taarifa zitavuja, kwamba “hapana” zimefanywa “ndiyo,” ibara ikasukwa ndani ya katiba, kwamba pale mtu atakapokuwa ametangazwa kuwa rais, isiwepo mahakama yoyote ile “itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtu aweza kujiuliza: Kwa nini kuwe na katiba inayoruhusu mwanya wa kutenda uhalifu? Kwa nini kuwe na katiba inayotilia mashaka nguzo muhimu ya dola – mahakama – katika usimamizi wa haki?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inawezekana watawala wanajua kuwa siyo wasafi? Kwamba hawana sifa isipokuwa ghiliba? Kwamba hawakubaliki isipokuwa kwa shinikizo? Kwamba hawawezi kumudu kushindanishwa na wengine mpaka kuwepo mwanya wa kukiuka taratibu, kanuni na sheria?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kwamba hilo halitoshi, maandalizi ya uchaguzi yanakabidhiwa kwa tume iliyiochaguliwa kwa utashi binafsi wa rais. Ni tume hii inayopewa mamlaka kisheria ya kuandaa, kusimamia uchaguzi na kutangaza mshindi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili tuliangalie hivi: Msimamizi wa uchaguzi ni mteule wa rais. Yule ambaye mteule wa rais atatamka kuwa ndiye mshindi, basi ndiye huyo. Huyo aliyetangazwa hapaswi kupingwa mahakamani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii maana yake ni nini? Ni kwamba tume ya uchaguzi imepewa madaraka makubwa sana kiasi kwamba inaweza “kuchagua” nani awe rais; na ikiishatamka, basi aliyetangazwa hawezi kulalamikiwa mahakamani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna mwanya mdogo. Mlalamikaji aweza kulalamikia tume kwa kutofuata kanuni, taratibu na sheria; au kwa watendaji wake kukiuka sheria. Mahakama yaweza kutolea maamuzi malalamiko hayo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini hakuna uwezekano wowote kwa maamuzi hayo kumwondoa madarakani rais aliyepatikana kwa rushwa, wizi wa moja kwa moja; kwa fedha za mafisadi au kwa udanganyifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Faida pekee ya njia hiyo ni kuweka wazi kilichotendeka; nani walitenda nini na uhusiano kati ya yaliyotendekake na aliyetangazwa kuwa rais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kila baada ya uchaguzi mkuu, waliochaguliwa wamekuwa wakiapa kulinda katiba hiihii yenye upogo; ambayo ina uwezekano wa kuleta viongozi waliopatikana kwa njia chafu lakini hawawezi kuhojiwa mbele ya mahakama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si hayo tu, katiba ya Tanzania imejaa vipengele ambavyo havilingani na mazingira ya sasa ya mfumo wa vyama vingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Moja ya mifano inayotajwa mara kwa mara ni pamoja na ule wa katiba kutaja kuwa hii ni nchi ya “kidemokrasi na ya kijamaa.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja zinajengwa: Iko wapi demokrasi katika mazingira ya kukatalia mahakama kusikiliza malalamiko kuhusu aliyetangazwa kuwa mkuu wa nchi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujamaa ni itikadi. Uko wapi utekelezaji wa itikati ya ujamaa chini ya utawala wa CCM? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunachoona ni uwezeshaji, kwa kauli, taratibu, kanuni na sheria wa makampuni na mataifa ya nje, kuingia nchini na kuvuna kana kwamba ni “shamba la bibi.” Hakuna ujamaa hapa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa msingi huo, Chadema wanapojaribu kuweka wazi, kilio chao na cha wananchi kuhusu umuhimu wa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, hakika wanastahili kusikilizwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wasiposikilizwa wanatafuta njia mwafaka, kama ile ya juzi bungeni, ambako rais, watawala wenzake, wageni rasmi walipata ujumbe wa moja kwa moja; bila kuchujwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali bahati mbaya, wenye fikra za John Chiligati, Katibu mwenezi wa CCM, wanajitokeza na kudai kuwa Chadema wanataka kuleta “uvunjifu wa amani.” Kwa kudai katiba mpya na tume huru?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani hapa anatishia uhuru, umoja, amani na utulivu wa nchi, kama siyo yule anayelinda katiba iliyopitwa na wakati na ambayo wananchi wana kiu ya kuibadilisha lakini bila mafanikio.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni halali kusema hapa, kwamba kuendelea kuwa na katiba kama hiyo na sheria kandamizi, ndiyo kuvunja umoja, kuangamiza amani na kupoteza utulivu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni sahihi kabisa kuanza sasa kuandika majina ya wote wanaong’anga’ania hali hii ya hatari – ya kuendelea kuwa na katiba iliyopitwa na wakati na isiyokidhi matakwa ya wengi – na kuyawasilisha mahakama za kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni kwa kuwa ikitokea amani ikavunjika, wawe wa kwanza kuhojiwa kwa kusababisha hali hiyo. Kwa leo, tuanze kwa kufikiria kupeleka jina la John Chiligati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;(Makala hii ilichapishwa katika gazeti la MwanaHALISI toleo la tarehe 8 - 14 Desemba 2010)&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-9066354918655097989?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/9066354918655097989/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=9066354918655097989' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/9066354918655097989'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/9066354918655097989'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/12/katiba-mpya-katiba-mpya-tanzania.html' title='&lt;strong&gt;KATIBA MPYA! KATIBA MPYA TANZANIA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROKwz04ZyI/AAAAAAAAAH8/AKaQUez4gkM/s72-c/Kikwete%2B2.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-188275327330481554</id><published>2010-12-23T09:22:00.000-08:00</published><updated>2010-12-23T09:26:41.036-08:00</updated><title type='text'>TCRA YAAMKA NA KUTUNISHA MSULI</title><content type='html'>&lt;strong&gt;JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA&lt;br /&gt;MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAI&lt;br /&gt;Hivi karibuni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imegundua kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunzaji wa siri za mawasiliano binafsi ya watumiaji wa huduma za mawasiliano ya simu za mkononi. Mawasiliano hayo yamefikia hatua ya kuchapishwa katika vyombo vya habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mamlaka ya Mawasiliano inapenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha wenye makampuni ya Simu na wananchi kwa ujumla kuwa, kutoa taarifa za mawasiliano binafsi ya simu bainA ya watumiaji wa huduma hiyo, ni uvunjaji wa Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta Na. 3 ya mwaka 2010 na Kanuni za Mawasiliano (Kulinda Wateja) za mwaka 2005.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu cha 98 ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kinasema;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;(1) “Mtu yeyote ambaye ni mfanyakazi wa kampuni yenye leseni ya kutoa huduma za mawasiliano, au mwakilishi wake, ana wajibu wa kutunza siri za mawasiliano binafsi na taarifa zozote za siri za wateja kwa mujibu wa sheria hii”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;(2) “Mtu yeyote haruhusiwi kutoa taarifa binafsi za mteja yeyote alizopokea au kusikia kwa mujibu wa sheria hii isipokuwa tu mtu huyo ameruhusiwa kwa mujibu wa sheria”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu cha 123 (1) kinasema:-&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtu yeyote ambae bila sababu za msingi atasababisha kuingilia au kuzuia kupokewa kwa mawasiliano yeyote ya kielektroniki anafanya kosa and akipatikana na makosa atatakiwa kulipa faini ya shilingi za kitanzania zisizopungua milioni tano au kwenda jela kwa muda wa usiopungua miaka miwili au adhabu zote kwa pamoja”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kanuni ya 12 ya Kanuni za Mawasiliano za mwaka 2005 za Tanzania (Kulinda Wateja) inasema:-&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Mtoa huduma za Mawasiliano haruhusiwa kuingilia kati, kusikiliza au kutoa taarifa zozote za mazungumzo ya mteja yeyote yaliyopitia kwenye mtandao wa mtoa huduma, isipokuwa kwa ruhusa kulingana na mahitaji maalumu kwa mujibu wa sheria zilizopo”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutolewa kwa taarifa za mawasiliano binafsi ya watumiaji wa simu za mkononi ni lazima kunafanywa na mtu mwenye ujuzi na uelewa wa jinsi ya kupata taarifa hizo na wenye ruhusa ya kufanya hivyo katika mtandao wa Kampuni husika ya kutoa huduma ya mawasiliano; ama peke yake au kwa kushirikiana na wenzake kwa kuingia kwenye mtandao kwa makusudi kwa lengo la kuingilia mawasiliano binafsi ya watu, ambayo ni uvunjaji na kinyume na matakwa ya kifungu cha 123 cha Sheria Na. 3 ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mamlaka ya Mawasiliano inayakumbusha Makampuni ya simu kuweka uzuizi na kuhakikisha siri za mazungumzo binafsi ya wateja zinahifadhiwa na hazitolewi kwa yeyote isipokuwa kwa mujibu wa sheria na; kuhakikisha yanafanya uchunguzi kugundua walioiningilia mazungumzo binafsi ya wateja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi wanapewa tahadhari kuhusu kutafuta au kutaka kupata taarifa za mawasiliano ya siri kutoka kwa watoa huduma na kuzitumia taarifa hizo binafsi za mawasiliano pasipo kufuata utaratibu ulioruhusiwa kisheria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa taarifa ambazo zimechapishwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari hivi karibuni, Mamlaka ya Mawasiliano inafanya uchunguzi wa uvunjwaji huo wa sheria kwa kutoa taarifa binafsi za wateja kinyume na sheria. Baada ya kuwabaini wahusika, Mamlaka itachukua hatua za sheria kwa yeyote atakayebainika kuvunja sheria hiyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Imetolewa na&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkurugenzi Mkuu&lt;br /&gt;Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)&lt;br /&gt;22 Desemba 2010&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-188275327330481554?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/188275327330481554/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=188275327330481554' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/188275327330481554'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/188275327330481554'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/12/tcra-yaamka-na-kutunisha-msuli.html' title='&lt;strong&gt;TCRA YAAMKA NA KUTUNISHA MSULI&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-1394505113301269944</id><published>2010-12-23T08:59:00.001-08:00</published><updated>2010-12-23T09:11:40.589-08:00</updated><title type='text'>MSUKUMO WA KATIBA MPYA WAONGEZEKA</title><content type='html'>&lt;a href="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROBDQgwZiI/AAAAAAAAAH0/eFGKdyDwmts/s1600/kIKWETE%2BNA%2BcLINTON"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 320px;" src="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROBDQgwZiI/AAAAAAAAAH0/eFGKdyDwmts/s320/kIKWETE%2BNA%2BcLINTON" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5553924658449901090" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Katiba mpya siyo kwa hisani&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;             &lt;strong&gt; Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;KATIBA mpya ya nchi ambayo wananchi wanataka, si mali ya rais. Si mali ya waziri mkuu. Wala katiba hii haipatikani kwa hisani ya mtawala yeyote. Hapana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi wanataka kuandaa makubaliano juu ya mamlaka ya usimamizi na utawala; na misingi inayoweka udhibiti wa mamlaka katika mahusiano ya watawala na watawaliwa na miongoni mwa vyombo vingine vya dola.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ufupi, wananchi wanataka kushiriki kuandaa taratibu, kanuni na misingi itakayokuwa mwongozo mwafaka wa jinsi wanavyotaka kujitawala; na siyo katiba ya kuviziana ya mfumo wa chama kimoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa unaweza kusema wananchi wanataka kuandika mkataba kati yao na watawala, wa sasa na wa baadaye, jinsi nchi yao inavyopaswa kuendeshwa katika nyanja zote za maisha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itakuwa historia. Sharti iwe. Wananchi wote – kwa kuulizwa au kwa utaratibu wowote ule wa kushirikisha maoni yao, akiwemo mtawala mkuu – watakuwa wamepata fursa ya aina yake ya kukubaliana jinsi wanavyotaka kujitawala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wiki iliyopita, kwenye ukurasa huu, tulieleza jinsi watawala wanavyojua vema jinsi katiba iliyopo ilivyo na kasoro nyingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ufupi tulisema wanajua kuwa rais anaweza kupata kura zisizo halali; lakini hawezi kulalamikiwa mahakamani. Katiba inaziba fursa hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tulionyesha pia kuwa katiba ya sasa inazuia mtu kugombea nafasi yoyote ya kisiasa iwapo si mwanachama wa chama cha siasa. Ni ubaguzi mchafu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rafiki yangu anasema huo ni “ukabila wa kichama;” wa kuziba haki ya mtu kwa sababu dhalili lakini za uchu wa kunyanganya haki ya mwingine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watawala wanaelewa vema kuwa kuna raia wenye akili nzuri, elimu ya kutosha na uwezo wa kufikiri na kutenda kuliko baadhi ya wanachama wa chama chao waliopachikwa madaraka; lakini kwa “ubaguzi wa kichama,” wanaziba fursa zao za kutumikia taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haya yote Rais Kikwete anayajua. Pinda anayajua. Wanajua kuwa siyo sahihi. Siyo haki. Lakini wanayaendeleza. Wanayapakata kwa kuwa yanawawezesha, wao na chama chao, kukaa kileleni. Yanawachafua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mfano mwingine. Watawala wanajua kuwa kazi kama zile za mkuu wa wilaya (DC) na mkuu wa mkoa (RC), zingekuwa zinachukuliwa na watu waliopatikana kwa kupanda ngazi kikazi katika maeneo ya utawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa wafanyakazi wenye elimu na uzoefu wanaachwa; badala yake wanachukuliwa “wowote wale,” wakiwemo maaskari wastaafu ambao hawana ujuzi wala uzoefu katika kazi hizo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inagharimu serikali muda na mabilioni ya shilingi ya kodi za wananchi, kufundisha, bila mafanikio, watu wazima ambao hata siku moja maishani mwao hawakuota kuwa kwenye utawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkono wa kuteua unafika hata kwa wakurugenzi wa halmashauri na manispaa kwa sababu moja kuu: Kuongeza idadi ya wafuasi na watendaji kisiasa kwa niaba ya chama kilichoko ikulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mteule wa rais anakuwaje kiranja katika utawala wa wananchi katika halmashauri, badala ya madiwani kutafuta na kuajiri mtendaji ambaye wanaona ana sifa za kuwatumikia?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni baadhi ya wateule hawa ngazi ya wilaya (wanaokuwa wasimamizi wa uchaguzi), ambao wamekuwa chanzo cha migogoro wakati wa uchaguzi kwa vile wamekuwa wakitishiwa kuwa, kama chama tawala hakikushinda watapoteza kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haya yanaweza kupatikana katika mazingira ya katiba ya sasa na safu hii itaendelea kufafanua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, anasema serikali iko tayari “kufanya marekebisho” ya katiba ya nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alikuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake Ijumaa iliyopita na kunukuliwa akisema atamshauri rais ili marekebisho hayo yafanyike katika kipindi cha “miaka mitatu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hauhitajiki uchunguzi wowote kujua kuwa Pinda tayari aliishakutana na Kikwete na kujadili hoja hii kabla hajatangaza kuwa atakwenda kumwona.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri mkuu hatangazi kila anapotaka kumshauri rais. Aidha, siyo lazima rais akubaliane na uamuzi wa waziri mkuu. Kwa hiyo, hatua ya kutangaza kuwa anakwenda kumshauri rais inaweza kutafsiriwa kuwa ameagizwa na rais kutoa kauli hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, hiyo siyo hatua mbaya wala ndogo. Ni hatua inayoonyesha kuwa, angalau mara hii, masikio ya watawala yamefunguka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatizo lipo kwenye hatua ya Pinda kumshauri Kikwete. Kama ilivyoelezwa hapo awali, katiba haiji kwa hisani ya rais. Rais anahitaji katiba mpya. Itakuwa yake kama ilivyo kwa raia yeyote wa nchi hii. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais anahitaji katiba itakayomwondolea uwezekano wa kushutumiwa na kutuhumiwa kutenda visivyo; kuwa anaminya, ananyang’anya au anavunja haki za raia na haki za binadamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais anataka katiba nzuri, kuliko hii iliyopo, ili huko tuendako, watawala wapya wasije kumgeuzia kibao na kuitumia kumminya kama Frederick Chiluba alivyomtendea rais mstaafu Kenneth Kaunda huko Zambia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais aliyeko madarakani anahitaji katiba inayotabasamu kwa wote; isiyojenga kinyongo wala kuminya haki ya mwingine. Hii italeta mazingira bora ya utawala ambapo kila aliyeko madarakani atajisikia kuwa huru hata pale anapokuwa amestaafu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katiba mpya itamfanya rais na watawala wenzake, kutembea bila kujishuku; na wasipotenda haki, ama watasahihishwa waziwazi, bila woga wala aibu; au watatemwa kabla muda wao wa utawala kumalizika kwani kutakuwepo utaratibu mwafaka na mwepesi wa kufanya hivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katiba isiyo na nia mbaya, inamhakikishia rais anayemaliza muda wake, utulivu kwa maisha yake yote, akila chake, akifurahia shahada zake za heshima alizopewa na vyuo vikuu ambazo zitakuwa zikipamba kuta za nyumba zake maridadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais Kikwete hana cha kupoteza kwa kuanzisha sasa mchakato wa katiba mpya. Kama kipo cha kupoteza ni woga usio na msingi. Bali kwa hili, aweza kunyakua sifa ambazo zimewashinda marais wote waliomtangulia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, nimekuwa nikipata ujumbe wa simu (sms) kutoka kwa baadhi ya wasomaji kuwa wananchi wengi hawajui katiba ya sasa inasema nini na kwamba wanahitaji kuelimishwa kwa “muda mrefu” kabla katiba mpya haijapatikana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimewajibu kuwa wananchi wanajua kuwa utawala bora ni ule unaotambua, kuheshimu na kulinda haki zao binafsi za kuzaliwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni utawala unaopaswa kusimamia na kuhakikisha kuwa haki zao za kiuchumi, kisiasa, kiimani na nyingine zote zinafurahiwa na wote. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini wanapoona kuwa haki zao hizo zinakanyangwa, unakuwa ujumbe wa kutosha kuwa hakuna katiba; kama ipo basi si “katiba nzuri” au hakika sio yao. Wanataka katiba tofauti; mpya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanajua hakuna makubaliano kati ya watawala na watawaliwa; kama yalikuwepo basi yamefutwa au watawala wameasi; na hivyo kuna umuhimu wa kuwa na “kitu kipya.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni muhimu kweli kusoma katiba, lakini haina maana kuwa ambao hawajaisoma hawajui kuwa, ama katiba haipo au iliyopo ni katili. Wanataka katiba mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;(Wiki ijayo: Mifano ya uhusiano kati ya katiba na maisha ya kawaida ya wananchi)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii ilichapishwa katika gazeti la MwanaHALISI toleo la 22-29 Desemba 2010) &lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-1394505113301269944?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/1394505113301269944/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=1394505113301269944' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1394505113301269944'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1394505113301269944'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/12/msukumo-wa-katiba-mpya-waongezeka.html' title='MSUKUMO WA KATIBA MPYA WAONGEZEKA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TROBDQgwZiI/AAAAAAAAAH0/eFGKdyDwmts/s72-c/kIKWETE%2BNA%2BcLINTON' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-465629422513420381</id><published>2010-12-23T07:58:00.000-08:00</published><updated>2010-12-23T09:17:59.772-08:00</updated><title type='text'>KUMEKUCHA: WANANCHI WATAKA KATIBA MPYA</title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TRN_BNdv19I/AAAAAAAAAHs/Rz4_cIfBptA/s1600/Celina.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 88px; height: 107px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TRN_BNdv19I/AAAAAAAAAHs/Rz4_cIfBptA/s320/Celina.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5553922424248981458" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Waziri Kombani ametukana wananchi&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CELINA Kombani – Waziri wa Sheria na Katiba, ametukana Watanzania. Hata akiomba radhi hatakubaliwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania wenye nia nzuri wanasema tuwe na Katiba mpya inayoondoa uwezekano wa wananchi kuchinjana pale watakapokuwa wameshindwa kuelewana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini Kombani anawajibu kuwa Katiba mpya haina maslahi kwa serikali wala taifa. Kwamba serikali haina fedha za kuanzisha mchakato wa kuandika katiba. Kwamba wanaodai katiba hawajampelekea madai yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenye nia njema kwa taifa lao wanasema kuwepo mkataba mpya (katiba), kati ya watawala na wataliwa; ule unaolingana na matakwa ya sasa; wenye kwenda na wakati tuliomo na siyo wakati wa ukoloni na utawala wa kikiritimba wa chama kimoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini waziri Kombani anawajibu kuwa wale wanaodai kuwepo katiba mpya ni watu wa barabarani na wasiokuwa na uelewa juu ya masuala ya katiba na utawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenye uchungu na nchi hii wanasema kuwepo katiba inayoruhusu kila mmoja kushiriki siasa za nchi yake – kuchagua na kuchaguliwa – na siyo ubaguzi uliowekwa ndani ya andiko kuwa ili uchaguliwe sharti uwe mwanachama wa chama chochote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini Kombani anasema serikali yake inaridhika na katiba iliyopo na kwamba itaendeleza utaratibu wake kuiwekea viraka kila itakapoona inafaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania wenye shauku ya kuona ustawi wa nchi yao wanasema kuwepo katiba mpya, itakayokuwa mwongozo katika kila kitu ili kuepusha migogoro kwa kujenga misingi ya haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanasema ukasuku wa “umoja, amani na utulivu” si lolote si chochote, mahali ambapo hakuna katiba inayounganisha fikra za watu wote na kusimamia haki ya kila mmoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini Kombani anasema serikali anayotumikia hailazimiki kuwa na katiba mpya kwa vile kuwa na katiba mpya siyo sera ya Chama Cha Mapinduzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni bahati mbaya kwamba tunatukanwa na mtu mdogo sana aliyeibuliwa mvunguni na kuitwa waziri. Lakini ni bahati mbaya zaidi, kwamba Kombani amemtukana na kumtukanisha Rais Jakaya Kikwete ambaye amempa kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Celina Kombani, kwa kauli zake, andhalilisha umma wa Tanzania; anajenga ghadhabu mioyoni mwa wengi; anaelekeza watu watupe chini matumaini yao; wakate tamaa na kuamua kuishi utumwani milele.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenye nia nje na nchi hii wanasema kuwepo tume huru ya uchaguzi. Tume isiyo ya rais. Tume isiyo na madaraka ya kuteua rais, bali yenye majukumu ya kusimamia uchaguzi ili wananchi wapate matokeo ya uchaguzi wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Celina anasema, tena kwa jeuri, kuwa hayo hayamo katika ilani ya uchaguzi wa chama chake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kipofu huyu; kipofu na siyo asiyeona; hawezi kutambua haki ya wananchi kumrudi mbunge au rais wao. Hawezi kuheshimu uhuru wa wananchi kuchagua watu safi na siyo wezi wakuu na majambazi yaliyokubuhu kwa kuliibia taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Celina Kombani hawezi kuona umuhimu wa fursa kadha wa kadhaa za wananchi kukataa kutawaliwa na wezi ambao wamethibitika kwa ushahidi wa mahakama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyu ni waziri wa sheria anayekataa kuwa na katiba mpya inayotoa fursa zote hizo ambazo zinakuza uhuru wa mtu binafsi; kunawirisha fikra za jamii na kuwapa wananchi madaraka ya kujitawala kwa kusimamia uongozi safi uliochaguliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa jeuri au kutojua, Celina Kombani anasema wanaodai katiba hawajampelekea madai yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa akili yake, anaona kuwa ana uwezo wa kushika utumwani taifa hili kama anavyopenda; na hadi atakapoamua kulifungulia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri huyu anafikiri kuwa mabadiliko ya katiba huanza kama madai ya wastaafu wa iliyokuwa jumuia ya Afrika Mashariki. Anataka orodha. Anadhani ni jambo la binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ina maana yake. Kwamba akiwa mtawala, Celina hawezi kuona mambo yanayoweza kuleta hatari ya baadaye hadi atakapoandikiwa kwenye karatasi na kukabidhiwa mkononi. Kipofu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Celina Kombani ametukosea, lakini kuna aliyetukosea zaidi kama taifa. Ni Rais Kikwete. Amemtoa wapi mtu wa aina hii ambaye anajenga mazingira ya mifarakano katika jamii?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Orodha ya watakaoitwa mbele ya mahakama ya kimataifa kueleza kushiriki kwao katika kuleta machafuko nchini Tanzania, sasa inaendelea kukua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tulianza na John Chiligati. Wasomaji wa makala zangu wakaleta majina mengine: Yusuf Makamba na John Tendwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mmoja wa wasomaji aliandika kwa ukali. Soma aliyoandika: “Kwa nini humtaji rais? Unamwogopa?” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa Kombani amejiunga na orodha ya wasiopenda nchi yao. Watu wenye shari. Wasiopenda amani. Waliotayari kuona taifa linaagamia alimradi wao wako madarakani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna Mkenya awezaye kujivuna sana kwamba ana katiba. Ipi? Iliyokuja baada ya kukatana mapanga; kuuana na kuwa wakimbizi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katiba iliyochelewa, inayokuja kuzika, kukausha majeraha na kuandika kumbukumbu za maafa? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania inahitaji katiba mpya leo. Benjamin Mkapa, rais mstaafu amesikika, ingawa kwa kupitia sauti ya mwingine na katika nchi ya jirani ya Burundi. Amefumbuka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni maneno yake kuwa Katiba ndiyo “moyo wa nchi; moyo wa binadamu unaofanya mwili mzima ufanye kazi.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais Kikwete, Celina Kombani atafanya nini pale kama siyo kukuumbua na kukuletea uadui zaidi na Watanzania wenye nia njema kwa taifa lao?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tisifike anakotaka Kombani. Waziri binafsi aweza kukimbia; lakini kuna sisi ambao tuliapa hatutatoka hapa, ije mvua lije jua. Kuna umma usiong’oka kwao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii ilichapishwa katika gazeti la MwanaHALISI toleo la 8 - 14 Desemba 2010)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-465629422513420381?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/465629422513420381/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=465629422513420381' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/465629422513420381'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/465629422513420381'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/12/kumekucha-wananchi-wataka-katiba-mpya.html' title='&lt;strong&gt;KUMEKUCHA: WANANCHI WATAKA KATIBA MPYA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TRN_BNdv19I/AAAAAAAAAHs/Rz4_cIfBptA/s72-c/Celina.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-2690348797757869833</id><published>2010-10-10T10:56:00.000-07:00</published><updated>2010-10-10T10:59:27.672-07:00</updated><title type='text'>CCM YABANWA MBAVU, YABAKIA KUJITETEA</title><content type='html'>SITAKI&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Waliozoea kubana upinzani nao wabanwa&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kuwa mtovu wa shukrani kwa waliosoma makala yangu ya wiki iliyopita juu ya ahadi za mgombea urais Jakaya Kikwete alizotoa mkoani Kagera na ambao wamenipelekea maoni; hasa wakazi wa Bukoba, Ukerewe na Kigoma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kilio kitupu. Tuanze na aliyesahihisha tukio la kihistoria. Huyu alisema meli ya mv Viktoria iliingia ziwani Viktoria mwaka 1963 (siyo 1965) baada ya kukata maji kwa “kipindi kirefu”  katika mto Thames nchini Uingereza. Namshukuru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwingine akasema nilionekana kuonyesha kuwa mv Viktoria bado inafanya kazi. Ameniuliza, “Watu wangapi wanapanda meli yako hiyo? Siku hizi watu hawana imani nalo. Wanapanda mabasi. Kutoka Bukoba saa 12 asubuhi unakuwa Mwanza kabla ya saa sita mchana siku hiyohiyo. Nani atapanda mzoga. Limebaki kubeba mikungu ya ndizi.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyo naye amejitambulisha kuwa anatoka Bukoba. Sasa huyu mwingine anatoka Ukerewe. Anasema mv Serengeti iliyokuwa ikienda kisiwani humo imeegeshwa gatini. Hawana huduma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Amesema “ka-meli kengine kanakoitwa Butiana, miezi mine au mitano iliyopita, kalizimikia ziwani” ambako walikwama na hatimaye kukokotwa saa sita baadaye. Hakuna usafiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nacho kivuko cha Clarias, ambacho kina umri mkubwa kuliko mbao zilizokiunda, kimeanza kuwa na mwendo usioweza kukifanya kishinde iwapo kitashindanishwa na kinyonga. Ukerewe wanalia. Si leo. Si jana. Si juzi. Kilio cha miaka mingi kama kile cha Bukoba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwingine huyu hapa. Anatoka Bunazi. Anajadili mambo mawili; tena kwa ufupi. Kwanza, anasema mkuu wa wilaya amesema hawezi kushiriki kugawa eneo la ranchi ya Kakunyu ambalo mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (rais) aliagiza likatwe na kugawiwa wananchi wenye uhaba wa ardhi, badala ya kuwafukuza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anasema mkuu wa wilaya amesema kauli ya mgombea haitoshi. Kwamba kilichopatikana kwa karatasi (hati ya kisheria), sharti kuondolewe katika hadhi hiyo kwa karatasi pia. Shaka imejengeka hasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, anasema mgombea aliahidi uwanja wa ndege wa kimataifa lakini wananchi wana shaka kubwa. Anasema, makao makuu ya nchi, Dodoma hayana uwanja wa ndege wa kimataifa; Mwanza mji wa pili kwa ukubwa nchini hauna uwanja wa kimataifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anasema uwanja wa Songwe, Mbeya ambao “wanatwambia utakuwa wa kimataifa, haujakamilika. Tunajiuliza kuna kitu gani kikubwa Misenyi (Bunazi) ambacho kinaweza kufanya serikali ijenge haraka uwanja wa ndege wa kimataifa, kilometa 40 au 50 kutoka mjini Bukoba.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini mkazi wa Kigoma/Ujiji ndiye ametoa mpya. Anaandika, “…acha haya ya kununuliwa meli mpya Bk; sisi Kigoma amesema anataka iwe kama Dubai, wakati umeme tu ni mtihani huku tuna maporomoko ya mto Maragalasi.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ahadi hizi zote Bukoba na mkoani Kagera kwa jumla, ni kama ahadi nyingine zilizotolewa na zinazoendelea kutolewa na mgombea wa CCM na baadhi ya wagombea wengine wa urais na ubunge wa chama hicho na vyama vingine nchi nzima. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinacholeta tofauti kati ya mgombea wa CCM na wagombea wa avyama vingine, ni kwamba Kikwete hawezi kujitofautisha na urais. Mara nyingi pia, anaongea kwa mamlaka ya rais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mfano, anapoagiza wananchi wakatiwe vipande vya ardhi kutoka kwenye ranchi, anaongea kwa kofia ya mwenye mamlaka juu ya ardhi, kwa mujibu wa sheria – rais – hata kama kauli yake itapingwa na kupinduliwa na wateule wake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini wingi wa ahadi, hasa zinazohusisha hata ujenzi wa viwanja vya ndege, Dubai ya Kigoma, meli, vivuko, bajaji kwa wajawazito (ahadi ya zamani); ahadi za kulipa mishahara ya wafanyakazi wa mgodi wa mkaa wa mawe Kiwira na kufufua mgodi huo, zinaonekana wazi kuwa zinatoka kwa kiwewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndiyo maana mmoja wa wasomaji ameandika, “Kikwete si anajua kuwa ni awamu ya mwisho. Hata  akiahidi yasiyotekelezeka, alimradi anamalizia muda wake ikulu; atakayemrithi aweza kusema ‘siyo mimi niliyeahidi.’”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli hii ya msomaji inaleta mazingira ambamo anayetoa ahadi na amri, atakuwa ameshinda. Haingalii upande mwingine. Bali hiyo siyo hoja ya msingi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja kuu ni kinachomsukuma Jakaya Kikwete kutoa ahadi nyingi na kwa wingi mara hii. Hiki kinaweza kupatikana katika kuchunguza mazingira ya kisiasa ya wakati tuliomo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara ya kwanza, tangu kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi, serikali imewambwa msalabani katika kampeni za uchaguzi mkuu wa rais na wabunge. Nayo imekiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja za vyama vya upinzani zimelenga kuonyesha udhaifu katika sera na mipango ya serikali ya CCM. Zimeibua vitendo vya wizi na ufisadi chini ya serikali ya chama cha umri mkubwa. Zimeweka wazi uongo, uzemba na usanii wa viongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara hii hoja siyo za maneno matupu. Zimesheheni takwimu na vielelezo juu ya kilichotendeka; alitenda nani, lini, wapi na katika mazingira yapi. Ni hivi: Hoja zimepangwa na kila hoja ina ushahidi mwanana ambao haupingiki. Ambao hauwezi kupuuzwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais mtaafu Benjamin William Mkapa, waziri mkuu mstaafu Frederick Sumaye na Rais Amani Abeid Karume, wamenukuliwa wakijadili mazingira ya sasa katika kampeni kuelekea uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwenye sherehe ya harusi ya mtoto wa Karume, mjini Zanzibar, kama miezi miwili iliyopita, viongozi hao walinukuliwa wakijadili “uimara” wa hoja za upinzani na umakini wa Dk. Willibrod Slaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yalikuwa mazingira ya sherehe lakini mmoja wa viongozi hao alinukuliwa akisema kuwa chama chao kimezoea kutoa takwimu bila ufafanuzi; lakini safari hii kuna mahiri (Dk. Slaa) wa kutafsiri na kutoa takwimu nyingine zenye fafanuzi ambazo zitakuwa kisiki kwa mgombea wa CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kauli hizo, alikuwa amepatikana wa kuvunja pingu za takwimu ambazo watawala walizoea kumwagwa mbele ya wananchi bila fafanuzi au walizitumia kujikweza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mfano, kutaja wingi wa vyumba vya madarasa kama maendeleo wakati havina madawati, walimu, vitabu, chaki, maabara, maktaba na vifaa vingine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hizi ni takwimu zilizopeperushwa na watawala – ghiliba ya wazi kabisa – na kujikinga nyuma yake wakisubiri kupigiwa makofi na kupewa kura. Mifano ya takwimu hizi ni mingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni takwimu zinazokidhi mahitaji ya mitaji mikuu mitatu ya watawala walioko madarakani kwa miaka 50 sasa. Mitaji hiyo imekuwa ujinga, umasikini na woga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujio wa mageuzi uliondoa woga mkubwa uliokuwa umetanda na kwa kiwango kikubwa kupandikiza ujasiri wa kuuliza maswali na kudai majibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujinga na umasikini viliendelea kushamirishwa na takwimu malaya zilizopewa tafsiri yoyote ile kukidhi mahitaji ya wakati uliopo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuibuka kwa tafsiri ya takwimu basi, na kutolewa takwimu zinazokinzana na zile zilizokuwa zikighubika akili za wengi, kumekuwa njia muwafaka ya kuongea na umma na kuuondoa katika kiza nene.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, kuibuka kwa uchanganuzi mwanana kunafuatia pia kudhihirika kwa vitendo vya wizi mkubwa na ufisadi wa mabilioni ya shilingi unaodaiwa kufanywa na, au kwa baraka za watawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mazingira haya ndiyo yanasaidia kujenga hoja nzito kuhusu mustakbali wa taifa – lakini siyo chini ya uongozi na utawala wa sasa unaotuhumniwa kutenda au kushiriki au kunyamazia yale ambayo yamekuza ujinga na kuongeza umasikini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakika hoja za aina hiyo ni ngumu sana kukabili. Watawala wa sasa, wakiongozwa na anayegombea urais kwa chama kilichoko ikulu, hawana majibu. Hawana!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanachoweza kufanya ni kuambaa nchi nzima; wakitoa kila ahadi kwa kubakiza moja tu wasiloweza kuahidi – ufalme wa mbiguni. Basi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hilo ndilo chimbuko la ahadi nyingi za Kikwete. Zitakuwa zaidi ya tulizosikia. Hata hivyo, ahadi hazijibu hoja. Zitabaki ahadi na maelezo yake na wakati mwingine amri na maelekezo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CCM itakiri, leo au kesho – na siyo suala la ushabiki bali uchambuzi sahihi – kuwa hoja za sasa za upinzani hazijibiki. Kama kuchaguliwa itakuwa ni kwa mazoea tu yaliyodumishwa na mitaji yake miwili iliyobakia: ujinga na umasikini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani kinachofanyika hivi sasa na ambacho hakijawahi kufanywa, ni kwamba CCM na serikali vimechukua upande ule ambako vimekuwa vikisukumiza wapinzani na wananchi – ule wa kujitetea; wa kujihami.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa chama kilichoko ikulu kuwa katika nafasi ya kujikinga, kujihami na kujitetea wakati wote; kuna maana kuwa “yamewafika.” Kuwa mabadiliko yaja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-2690348797757869833?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/2690348797757869833/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=2690348797757869833' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2690348797757869833'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2690348797757869833'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/10/ccm-yabanwa-mbavu-yabakia-kujitetea.html' title='&lt;strong&gt;CCM YABANWA MBAVU, YABAKIA KUJITETEA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-976179151391980669</id><published>2010-10-10T10:31:00.000-07:00</published><updated>2010-10-10T10:40:23.601-07:00</updated><title type='text'>UJINGA ULIOPATA DIGRII, UPROFESA</title><content type='html'>&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TLH6ONXEdmI/AAAAAAAAAHk/bNSfWpuWiVo/s1600/maghembe.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 281px; height: 320px;" src="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TLH6ONXEdmI/AAAAAAAAAHk/bNSfWpuWiVo/s320/maghembe.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5526473339771844194" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Prof. Maghembe anavyokana siasa&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI Profesa Jumanne Maghembe awe mfano wa jinsi usomi unavyoweza kuota kutu, kuwa butu na hata kuwa sumu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa huyu ndiye waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi; mbunge anayejaribu kutetea kiti chake, lakini kiongozi ambaye wizara yake ina ndimi mbili juu ya haki ya wanafunzi kupiga kura mwaka huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maelfu ya wanafunzi wa vyuo vikuu vya serikali walijiandikisha kupiga kura pale vyuoni kwao. Wizara ilijua hilo. Tume ya Uchaguzi ilijua na kupanga hivyo. Wanafunzi walijua watakuwa vyuoni. Serikali kwa jumla ilijua hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ghafla serikali ikasema muhula mpya wa masomo katika vyuo vyake utaanza mapema Novemba na siyo mwishoni mwa Oktoba – tofauti ya siku kumi tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maana ya maamuzi hayo ni kwamba wanafunzi hawatakuwa kwenye maeneo walikojiandikisha kupiga kura. Hawatapiga kura. Hapa ndipo zimetokea kauli mbili za serikali zinazoleta utata.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya kwanza ni kwamba maandalizi ya malipo kwa wanafunzi wanaoomba mikopo hayatakuwa yamekamilika mwishoni mwa Oktoba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya pili na iliyotolewa na waziri wiki iliyopita ni kwamba, vyuo vitafunguliwa mapema Novemba kwa sababu kumekuwa na mabadiliko katika mfumo wa udahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri anataka kila mmoja amwamini, yeye na serikali yake, kuwa katika siku 10 (kumi tu), ambazo ni tofauti kati ya tarehe ya awali ya kufungua vyuo na tarehe mpya, maandalizi ya malipo yatakuwa tayari na tofauti ya muda wa udahili itakuwa imetoweka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi ni visingizio. Ni njia ya kuwapora wanafunzi fursa na haki yao ya kupiga kura, hasa wale ambao wazazi wao hawana uwezo wa kuwawezesha kwenda vyuoni mapema; au kuwa karibu na vyuo ili wapige kura na siku 10 baadaye waingie vyuoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika baadhi ya nchi duniani, kuna mifumo ya kuhakikisha raia wake waishio ughaibuni, wanashiriki zoezi la uchaguzi huko watokako. Serikali huhakikisha kila kura inakusanywa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Walioko katika ofisi za kibalozi nje ya nchi, wafanyabiashara, wanafunzi na hata walioko katika majeshi, huwezeshwa kupiga kura makwao kutoka pale walipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania, hapahapa, humuhumu, maelfu ya kura yanaachwa hivihivi, njenje. Kuna tatizo. Siyo rahisi kufikiri kuwa siyo njama za kuzika utashi wa maelfu ya wanafunzi. Kwa kadri hali ilivyo, kuna uwezekano mdogo sana kwa serikali kubadili mwelekeo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa ndipo kuna mtihani wa nyongeza kwa wanafunzi vyuoni: Kufanya vyovyote iwavyo, kuwa maeneo walikojiandikisha – bila kusikiliza waziri wala tume – ili waweze kupiga kura. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua hiyo, inayoweza kufanywa na wanafunzi wachache, wengi au wote, yaweza kuwa ushahidi wa kudumu wa kupigania haki na kichocheo kwa vijana wengi katika kuthamini na kupigania haki zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni hatua hii pia itakayoweza kumrudisha darasani Prof. Maghembe, mara hii akifundishwa na wanafunzi wa umri mdogo, juu ya haki ya raia ya kupiga kura kuchagua yule anayeona anafaa kumwongoza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani ni Maghembe aliyekaririwa wiki iliyopita akisema kuwa anawashangaa wanafunzi kuweka shinikizo la kuwa vyuoni mapema ili waweze kupiga kura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Amenukuliwa pia akisema vyuo vya elimu ya juu siyo taasisi za kuendesha siasa bali ni “…maeneo yanayotumika kufundishia wataalamu wa kada mbalimbali.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tayari wanafunzi wamemjibu profesa. Wamemuuliza: Kama vyuo ni mahali pa kazi pekee ambayo waziri ametaja, kwa nini chuo kiliruhusu uandikishaji wanafunzi, tena hapo vyuoni?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Prof. Maghembe hawezi kupata jibu kwa swali hili kama ambavyo hawezi kupata majibu kwa maswali mengine kuhusiana nalo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mfano, profesa anasema nini kuhusu siasa kuwa moja ya masomo muhimu na kwamba chuo kikuu ni eneo la kuoka wataalamu katika sayansi ya siasa? Na hilo linafanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hajui hilo, basi kuna kila sababu ya kutilia mashaka nia, shabaha, uwezo wake wa uelewa na elimu yake, kwani kupiga kura siyo zoezi la ndimu mchangani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kuoka na kuipua wataalamu katika sayansi ya siasa, elimu ya kiwango cha chuo kikuu inapaswa kuwa ufunguo wa akili katika nyanja mbalimbali za maisha, ikiwemo siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, siyo lazima uwe katika idara au kitivo kinachohusiana na siasa ndipo ujue mazingira yako ya kisiasa na jinsi zinavyokuathiri – wewe na jamii yako.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni kwa kuwa kila eneo la jamii linahusika na kuathiriwa – vizuri au vibaya – na siasa za wakati uliopo. Ndivyo ilivyo pia katika vyuo vikuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maamuzi yanayotumiwa na watendaji na kufanya nchi hii iendelee kuwa makazi ya watu wengi, woga, masikini na wajinga, ni ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taratibu na mazingira yanayosababisha watoto wamalize madarasa saba bila kujua kusoma na kuandika; yanayolea wizi mkuu na ufisadi usiomithilika; ama zimetokana  au zimeathiriwa na maamuzi ya kisiasa ya wakati huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfumo wa maisha unaofanya waliohitimu chuo kikuu, hata maprofesa, wapauke haraka na wengine hatimaye kupoteza uwezo wa kufanya maamuzi na hata kusoma na kuandika; umeathiriwa kwa kiwango kikubwa na siasa za nyakati tulizomo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wahitimu vyuo vikuu, wanaokwenda kuwa walimu, wanasheria – mawakili na mahakimu – madaktari, mainjinia, mabwana na mabibi shamba na mifugo, wana-mipango na wengine, hawanabudi kujua mwelekezaji ni siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfumo wa utawala wa wanafunzi vyuoni, unaoamuliwa kwa njia ya uchaguzi wa viongozi wao na kushirikisha kila mmoja bila kujali anasomea nini, ndilo rejeo la haraka kwamba wasomi vyuoni wanapaswa kuwa hai juu ya kinachotendeka katika jamii na hasa kinachogusa haki zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama Profesa Maghembe anafikia hatua ya kusema siasa haziwahusu walioko vyuo vikuu, ama amesahau, amepotoka au amepauka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siyo rahisi kuzungumzia elimu ya juu bila kugusa mustakbali wake kwa jamii, kupitia mipango iliyowekwa au kuathiriwa na siasa zilizopo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, kudai kuwa vyuo siyo mahali pa siasa na kuweka vikwazo kwa wanafunzi ili wasifurahie haki yao ya kuchagua viongozi wanaotaka, ni kuendeleza ujuha ambao uliishafukuliwa na kutupwa nje ya vyuo na hata shule nyingi nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maghembe hasononeki kwa wanafunzi kushindwa kupiga kura. Serikali yake pia  haisoneneki. Labda walishajua kuwa wanafunzi hawatapigia kura chama chao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini walijuaje? Hiyo si kama kufyatua risasi gizani ambako waweza kukuta unaumiza au unaua mkeo, baba au mwanao?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zimebaki siku 21 kupiga kura katika uchaguzi mkuu. Wanafunzi wa vyuo vikuu bado wanasubiri serikali itende maajabu.&lt;br /&gt;Hayapo. Hayaji aua hayaji haraka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna kazi moja ambayo wanafunzi wanaweza kufanya iwapo serikali haitabadili msimamo. Wabaki walipo. Wahimize wananchi kuamka mapema na kupiga kura. Wafanye uwakala kwa vyama vyao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufanya hivi siyo kudhalilika. Njia hii ina faida mbili kuu. Kwanza, kuanzia hapo, wataelewa hila na husuda walizonazo watawala na kwamba haziondoki kamwe kwa sala kanisani wala msikitini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, watajifunza kuchukia na kuchukua hatua – mwanzo na mwisho wa lelemama – kwa njia ya kujiunga na wanaharakati kupigania haki zao na wote, ambao wakati wowote, waweza kunyang’anywa haki zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;br /&gt;(Imechapishwa katika Tanzania Daima Jumapili ya 10/10/2010)&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-976179151391980669?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/976179151391980669/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=976179151391980669' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/976179151391980669'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/976179151391980669'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/10/ujinga-uliopata-digrii-uprofesa.html' title='&lt;strong&gt;UJINGA ULIOPATA DIGRII, UPROFESA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TLH6ONXEdmI/AAAAAAAAAHk/bNSfWpuWiVo/s72-c/maghembe.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-2658002544344698079</id><published>2010-10-02T03:42:00.000-07:00</published><updated>2010-10-02T03:53:58.815-07:00</updated><title type='text'>OMBAOMBA YA KIKWETE INANUFAISHA NANI?</title><content type='html'>&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TKcOR2sjxRI/AAAAAAAAAHc/2L24GXfHGW4/s1600/Kikwete+marekani.bmp"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 212px;" src="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TKcOR2sjxRI/AAAAAAAAAHc/2L24GXfHGW4/s320/Kikwete+marekani.bmp" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5523399167896175890" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Safari za nje na ombaomba ya JK&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kusikia Jakaya Kikwete akisema kuwa asigefanya safari zake nyingi nje ya nchi, basi wananchi wangekufa njaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyu rais aliyemaliza muda wake anataka kusema kuwa alikuwa anakwenda kuhemea; kuomba kishika-roho ili Watanzania wasife njaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndivyo alivyonukuliwa akisema kwenye mikutano ya hadhara ya kuomba kura katika majimbo mawili ya uchaguzi ya Urambo – Mashariki na Magharibi mkoani Tabora. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati mgombea urais akisema hayo, Bolozi wa Ujerumani nchini, Guido Herz anawaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa nchi yake inashangazwa na umasikini ulioko nchini, tena katikati ya “raslimali nyingi.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Balozi anarudia yale ambayo yamesemwa kwa miaka nendarudi kuwa nchi hii, pamoja na raslimali nyingine, ina mito, maziwa, bahari, ardhi nzuri kwa kilimo na  vivutio vya utalii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Balozi anasema, “Kwa hakika siwezi kutaja sababu ya kuifanya Tanzania isipige hatua ya maendeleo,” bila shaka na kuondokana na umasikini wa kipato (ajira), chakula, elimu, mavazi, usafiri, maji, umeme na mahitaji mengine ya jamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni njaa ipi ya Watanzania anayosema Jakaya Kikwete ambayo imekuwa ikimpeleka nje ya nchi?  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa ndipo tunaweza kushona alichowahi kusema Mwalimu Julius Nyerere kuwa, ni upumbavu kufa kwa njaa wakati unaishi katika bonde lenye rutuba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira haya, ni vigumu kumruhusu mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutumia kampeni za uchaguzi mkuu kujidhalilisha, yeye na watawala waliomtangulia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakika hapa Jakaya Kikwete anajianika, kwamba ameshindwa kazi; na kwa njia ya ushauri wa bure, asijaribu kurudia kauli ile mbele ya wakulima masikini anaowaomba kura. Watamnyima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakulima wamejilisha kwa ndizi, muhogo, mahindi, viazi, mtama, uwele, ulezi, karanga, maharage na mazao mengine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wamejipatia matumizi kwa kuuza mazao yaliyotajwa hapo juu, pamoja na pamba, miwa, korosho, nazi, alizeti, karafuu na kahawa. Wafugaji wamelinda maisha yao kwa mifugo – mbuzi, kondoo na hasa ng’ombe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi masikini wamevua samaki kutoka mito na maziwa ambayo husema kila siku kuwa wamejaliwa na Mwenyezi Mungu; wamekula na kuendelea na maisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengine wamefukua dhahabu, almasi, tanzanite na madini mengine “tuliyojaliwa na Mwenyezi Mungu” kwa kutumia vijiti, majembe na koleo – alimradi wamepata vipande vya kuuza, kupata fedha na kusogeza miaka mbele.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kilimo, ufugaji, uvuvi na uchokonoaji madini kwa njia za kale, wananchi wengi wamebaki masikini. Wanatumia nyenzo duni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi wana mashamba madogo. Maeneo madoyo ya kulima na kuchungia. Wanapata mazao kidogo. Wanakula kidogo. Wanauza kidogo. Wanabakia na kidogo. Wanajiviringisha katika udogo-udogo ambao ni umasikini usioisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili ni somo pana lisoloweza kuenea kwenye kipande hiki cha ukurasa. Bali ni somo linaloeleweka vema kwa wakulima, wafugaji, warinaasali na wakusanya matunda porini; wafanyakazi na wasio na kazi, kwa kuwa ndio wanaishi maisha hayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukichunguza utaona udogo unaojadiliwa unatokana na “ubongo mdogo wa watawala,” kwa maana tatu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, kukosa uwezo wa kufikiri. Pili, kukosa utashi katika kutumikia wananchi. Tatu, uroho wa kijuha – wizi, matumizi ya kutanua na ushirika na watu wa nje katika kuibia nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huwezi kusema unakwenda kuhemea nje ya nchi kwa ajili ya mtu ambaye umemnyang’anya ziwa ambalo limekuwa chanzo cha mapato yake (samaki na fedha) na kiungo cha uhai wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi wanalia – nyavu zao na mitumbwi vimechomwa moto; wamekamatwa, kupigwa viboko na kuchomewa nyumba ili mwekezaji ziwani apate usalama wa kukomba “samaki wa mungu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hilo bakuli la ombaomba wa kitaifa, limemletea nini huyu aliyeachwa utupu na ambaye watawala hawataki kusikiliza kilio chake?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haiingii akilini kudai unakwenda kuhemea nje ya nchi kwa ajili ya mfugaji wa Kilosa ambaye watawala wamenyang’anya ng’ombe 600 au 1,000 na hata 2,000. Kuna nini lake ndani ya pochi ya mhemeaji aliyeacha amemfukarisha?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna mtawala awezaye kwenda kuhemea kwa ajili ya wafugaji ambao ng’ombe wao wameswagwa na kupotea porini, nyumba zao kuchomwa moto na wao kuamriwa, kwa mtutu wa bunduki, kuhamia wasikojua – kwa kauli za “rudi kwenu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anayekwenda kuhemea atawakuta wapi watu hawa ili awape alichopata? Kama siyo mzaha basi ni ukatili usiomithilika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua wachimbaji wadogo – wale wa vijiti, majembe na koleo. Wameswagwa kutoka walikoishi uhai wao wote. Wametengwa na chanzo cha “uchumi” na maisha yao. Sasa ni jinai kukutwa na madini “waliyopewa na Mwenyezi Mungu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani ataamini kuwa hata makombo kutoka kapu la mhemeaji Jakaya Kikwete, yataweza kuwafikia watu hawa, licha ya madai kuwa anakwenda nje kuhemea ili wasife njaa? Yatawakuta wapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nenda Rukwa, Ruvuma, Mbeya na Iringa – mikoa inayozalisha mahindi kwa wingi mpaka ikaitwa “Wababe Wanne.” Mazao wanayo. Hayana soko la ndani. Wanazuiwa kuuza kokote wanakotaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndivyo ilivyo kwa wakulima wa kahawa Kagera na wakulima wa karafuu Unguja na Pemba. Bado kuna ukiritimba ambao hauendani na siasa za watawala za soko huria. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna mwenye haki wala wajibu wa kuhemea kwa niaba ya wakulima hawa. Wana uwezo wa kijilisha; bali serikali imekuwa ikiwanyang’anya uwezo huo ili iweze kuwatawala kwa urahisi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali imekataa kufanya hata jambo dogo na kununua nafaka kutoka kwa wakulima, kwa bei nzuri kwa ajili ya kutunisha mfuko wa akiba (GSR). Kwa njia hii yaweza kuchochea mashindano katika kilimo na hivyo wananchi kulima zaidi na chakula kuwa kingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali ikishindwa kujenga mazingira ya kutumia mabonde, ardhi yenye rutuba, mito, maziwa, bahari, madini, misitu na mbuga za wanyama; badala yake ikadai rais wake anakwenda kuomba chakula nje ya nchi, ijue imeshindwa kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna awezaye kuelewa mantiki ya kuwa ombaomba katikati ya utajiri wa aina hii wa raslimali; wala hakuna atakayehusudu ombaomba katika mazingira ambamo watawala wenyewe ndio, ama chanzo au kichocheo cha njaa na umasikini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa nini basi tusikubaliane kuwa, watawala wetu wanakwenda nje ya nchi kutafuta utumwa; kwani hawataki kuishi kwa uhuru unaotokana na rasliamli lukuki zinazopaswa kuendelezwa kwa manufaa ya watu, ndani na nje ya nchi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-2658002544344698079?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/2658002544344698079/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=2658002544344698079' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2658002544344698079'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2658002544344698079'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/10/ombaomba-ya-kikwete-inanufaisha-nani.html' title='&lt;strong&gt;OMBAOMBA YA KIKWETE INANUFAISHA NANI?&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TKcOR2sjxRI/AAAAAAAAAHc/2L24GXfHGW4/s72-c/Kikwete+marekani.bmp' height='72' width='72'/><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-3341080422715461900</id><published>2010-09-23T23:27:00.000-07:00</published><updated>2010-09-23T23:33:16.660-07:00</updated><title type='text'>MARUHANI WALINDA IKULU DAR</title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TJxGIFL2rrI/AAAAAAAAAHU/sqZsDT3jsw4/s1600/sheikh-yahyabc.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 230px; height: 320px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TJxGIFL2rrI/AAAAAAAAAHU/sqZsDT3jsw4/s320/sheikh-yahyabc.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5520364347894181554" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Kikwete anayelindwa na mashetani&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;  &lt;strong&gt;    Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kusikia na kuamini kuwa vyombo vya ulinzi nchini vimeshindwa kazi – Polisi, Jeshi la Wananchi (JWTZ) na Usalama wa Taifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kuamini kuwa tayari walinzi wanakaa tu; lakini wanalipwa mishahara na marupurupu mengine – wanatumbukiza mifukoni na matumboni – bila kufanya  kazi yoyote ya kumlinda “Rais wa Jamhuri ya Muungano.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kuamini kuwa nadharia za kisasa za ulinzi, silaha za kisasa na uvumbuzi unaoendelea katika medani ya ulinzi, vinaweza kutupwa chini na badala yake akatafutwa mtu, watu au vikundi vya kumlinda rais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kukubali wawepo watu binafsi, vikundi na makampuni ya ulinzi; tena ya kumlinda rais – na huenda na wananchi na mali zao – ambavyo havitambuliki kikatiba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kuamini kuwa walinzi – waliosomea kazi hiyo na hata waliopendelewa kuwa katika nafasi hiyo muhimu – wanaweza kukubali “kuwekeana mikataba” na watu binafsi, makampuni na mataifa ili kulinda nchi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kuamini pia kuwa walinzi – wataalam wa zana na wenye maarifa makuu – wanaweza kujisalimisha kwa Sheikh Yahya Hussein ambaye anaona ulinzi wa rais na ikulu sharti uwe mikononi mwake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kuamini kuwa rais wa Jamhuri ana taarifa kuwa walinzi wake hawatoshi kumlinda; hawawezi kumlinda na kwamba zana zao na maarifa yao vimeshindwa kumwekea usalama unaostahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kuamini kuwa rais anaamini kuwa hana ulinzi wa kutosha; kwamba majeshi yake yamechoka na kuchakaa na sasa sharti atake, apewe au atafutiwe ulinzi wa nyongeza nje ya silaha na maarifa yanayotambuliwa kitaifa na kikatiba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kuambiwa kuwa rais anaweza kukubali kulindwa na vyombo vingine nje ya vile tunavyofahamu kitaifa na kikatiba. Atakuwa amedharau nchi yake, watu wake, majeshi yake na katiba ya nchi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini mnajimu Sheikh Yahya Hussein anasema, bila woga wala aibu kuwa “sasa atamlinda Rais Jakaya Mrisho Kikwete” kwa ulinzi maalum ambao hauonekani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mnajimu huyo wa Magomeni, Dar es Salaam, alisambaza waraka katikati ya wiki hii akielezea jinsi Rais Kikwete alivyoandamwa na wabaya na kwamba kuishiwa nguvu uwanjani Jangwani tarehe 21 mwezi uliopita, kulitokana na uchawi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haijafahamika iwapo Sheikh Yahya ndiye alitangua uchawi uliomwangusha Kikwete; ulikuwa uchawi wa kiwango gani; uliolenga nini na uliotoka kwa nani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kauli ya mnajimu, haikufahamika “amemwokoa” mara ngapi, amemkinga mara ngapi na anaaminika kwa kiwango gani kwa mkuu wa nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka jana alipotabiri kuwa atakayejitokeza kushindana na Kikwete, ndani ya chama chake, atakufa kifo cha ghafla, ndipo wengi walianza kumhusisha Yahya na wapangaji wa ofisi kuu ya nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa nia njema na labda kwa kutambua kazi yake nzuri, msemaji wa ikulu alipoulizwa juu ya kauli ya Yahya, alisema kuna haja ya “kuheshimu kauli” ya kila mmoja. Lakini Jakaya Kikwete hakusikika akisema lolote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haikufahamika iwapo kwa “kuheshimu kauli” msemaji wa ikulu alikuwa na maana ya kila mmoja kuwa na haki ya kutoa kauli au alikuwa anasisitiza umuhimu wa kutambua na kuzingatia utabiri wa Sheikh Yahya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati huo, Sheikh Yahya hakusema iwapo amemwekea kinga Rais Kikwete. Hakusema kifo cha ghafla kitaletwa na nani na nini – nyota, mwezi, mizimu katika mzunguko wa kinga-nikukinge au ua-nikuue.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali vyovyote iwavyo, kuibuka tena kwa mnajimu zikiwa zimebakia siku 51 kufanya uchaguzi mkuu, kumechukuliwa na wengi kuwa njia ya kuimarisha utabiri wake; kuongeza nguvu za “kinga” yake na hata kuonyesha “mteja wake” kuwa hajamtupa mkono; pamoja na yote yanayojitokeza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni mara ya kwanza kwa Sheikh Yahya kusema analinda rais aliye ikulu. Uhusiano huu kati ya mtu binafsi na ofisi kuu hauwezi kuwa umejitokeza ghafla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yawezekana pia uhusiano huu umekuwepo kati ya mganga huyu mwenye “ulinzi” (unaozidi ule wa maaskari na mashushushu) na marais waliotangulia; bali hapa hatuna uwezo wa kuwasemea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali la haraka ambalo kila mmoja anaweza kujiuliza ni: Mlinzi huyu wa majeshi yasiyoonekana, analipwa posho au mshahara? Analipwa kiasi gani?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani anamlipa mlinzi huyu? Fedha hizo zinatoka kwenye kodi za wananchi au yule ambaye anajisikia amelindwa na kufanikisha matakwa na malengo yake?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nikiwa bungeni pale Dodoma, mwaka 1997, mbunge mmoja wa CCM aliyekuwa akifurahia hoja zangu, alinitambulisha kwa wageni kutoka jimboni mwake ambao ambao pia walitambulishwa kwa wawakilishi bungeni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alitambulisha wageni saba; wakiwa wanawake watatu na wanaume wanne. Alinieleza kuwa aliyemtambulisha mwishoni “ndiye mtu wangu muhimu” – mganga/mlinzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uganga na kinga ndani ya nyumba za watu binafsi. Uganga ndani ya ofisi za serikali. Uganga ndani ya bunge. Uganga ndani ya ikulu – kwa kuombwa au kwa kujipendekeza. Uganga!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimekumbuka ikulu ya Banjul, Gambia ambako tuliambiwa mapema mwaka jana kuwa Rais Sheikh Profesa Alhaj Dk. Yahya Abdul-Aziz Jemus Junkung Jammeh, naye ni mganga wa aina yake; pamoja na “kutibu ukimwi.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katikati ya ulofa huu unaoitwa kinga, watoto wa kike wa hata umri wa miaka 12, wanabakwa na wazungu – katika mahoteli na mabaa yaliyotapakaa mjini Banjul; kufanywa wajawazito na kutupwa mitaani wakilia na kusaga meno. Umasikini wa kutaga mayai!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Imani za “kukinga” zimedumaza akili; zimekwamisha uwezo wa kufikiri; zimezamisha matumaini ya wengi huku zikifanya watawala washughulikie kitu kimoja tu: kujikinga. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bila shaka hapa Sheikh Yahya alikuwa anajitangaza ili wagombea nafasi mbalimbali wapate kumkumbuka na kumwendea, hasa wakizingatia kuwa ndiye mtoa kinga kwa rais badala ya vyombo vya dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wale askari wasioonekana; zile silaha zisizoonekana; ule utaalam usiosomewa vyuoni wala kufundishwa majumbani; ni  mashetani ambao mnajimu anataka yamlinde Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunasubiri mgombea urais wa CCM kukubali kwa faragha au hadharani kupata ulinzi huo; jambo ambalo litakuwa na maana moja tu: kwamba amefukuza kazi majeshi yote nchini na kuajiri mashetani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haitakuwa ajabu kuona hata walinzi wake kwenye msafara wake wa sasa wakiondolewa na yeye kubaki na wapiga debe wa umoja wa vijana wa chama chake. Tunasubiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-3341080422715461900?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/3341080422715461900/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=3341080422715461900' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3341080422715461900'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3341080422715461900'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/09/maruhani-walinda-ikulu-dar.html' title='MARUHANI WALINDA IKULU DAR'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TJxGIFL2rrI/AAAAAAAAAHU/sqZsDT3jsw4/s72-c/sheikh-yahyabc.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-7868415649140703178</id><published>2010-09-23T23:10:00.000-07:00</published><updated>2010-09-23T23:24:55.584-07:00</updated><title type='text'>SHERIA YA MABWEGE HII HAPA</title><content type='html'>&lt;a href="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TJxEI1-tpsI/AAAAAAAAAHE/DacMaai4ANM/s1600/Jaji+Lewis+Makame-4.JPG"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 180px; height: 320px;" src="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TJxEI1-tpsI/AAAAAAAAAHE/DacMaai4ANM/s320/Jaji+Lewis+Makame-4.JPG" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5520362161969145538" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI       &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Lugha ya Tume ya Uchaguzi Haieleweki&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI uamuzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wa kulazimisha matumizi ya Kiswahili peke yake katika kampeni za uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakumbuka ilikuwa hivyo mwaka 1995 wakati nagombea ubunge jimbo la Muleba Kaskazini. Bado ni hivyo hata leo. Safari hii matumizi ya lugha yamekuwa moja ya masharti ambayo vyama vimelazimishwa kusaini.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiswahili ni lugha ya taifa. Ni lugha kuu inayotumiwa na wengi ndani ya soko la ajira – serikali na makampuni yake, shuleni na baadhi ya vyuo; katika biashara za kati, ndogo na katika mawasiliano ya kawaida.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiswahili kimeenea mijini – miji mikubwa na midogo na katika baadhi ya vijiji ambako kimetumiwa kwa muda mrefu au wakazi wake wamekuwa na mwingiliano mkubwa na wale wanaozungumza lugha hii. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwingineko Kiswahili kimeenezwa na shule za msingi na sekondari ambako walimu na wanafunzi wameathiri matumizi ya lugha za asili, bila kusahau juhudi za makusudi za kupambana na ujinga kwa njia ya Elimu ya Watu Wazima (Kisomo Chenye Manufaa).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kampeni za kisiasa nazo zimekuwa na mchango mkubwa kwa uenezi wa lugha hii, zikiongezea kwa mipango ya awali, mara baada ya uhuru, ya kusambaza vipeperushi na filamu juu ya matakwa na mbinu za “maendeleo” katika Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na yote hayo, bado nchini Tanzania kuna maeneo ambako kuta za lugha za asili zingali imara; na hasa imara sana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni lugha hizi za asili ambazo zimeendelea kuwa chimbuko la misamiati na istilahi mbalimbali kwa matumizi ya sasa ya kukuza Kiswahili na hata kueleza maana halisi ya kile wanachosema wale wanaotumia lugha yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siyo bahati mbaya basi kwamba Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuna idara inayoshughulikia lugha za asili. Watafiti katika eneo hili hawafanyi kazi ya “kuzienzi” lugha hizi za asili – iwapo tutaazima vineno vya kisiasa – bali wanavuna maarifa ndani ya lugha hizo na kupitia lugha hizo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuwepo kwa lugha hizo kunakoweza kusaidia kuelewa jamii na utamaduni wake – kwa kudhamiria au kwa utuki tu – kumekuza na kunawirisha Kiswahili na hata lugha nyingine za asili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ndiyo maana kumekuwa na wanaharakati wa ngeli na ngeli wakitetea kuendelea kuwepo lugha za asili zilizohifadhi hekima na falsafa za jamii ambako zinatumika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, ni lugha hizi ambazo watafiti wanaoumba kamusi za Kiswahili na hata lugha nyingine zinazotumika katika maeneo haya, wanakimbilia kupata maneno halisi – hasa istilahi katika ufundi na teknolojia ya kale na sasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hizi basi siyo lugha za kuua hivihivi tu kisiasa. Bado zina nafasi muhimu katika jamii kama vile walivyo watu wanaozitumia; na wanaendelea kuwa Watanzania hata kama hawawezi kuongea Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa Tume ya Uchaguzi inasema wanasiasa wanaotafuta kura katika uchaguzi mkuu wasitumie lugha nyingine yoyote ile isipokuwa Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maagizo ya tume yanafanana na kanuni za Wizara ya Habari zinazolazimisha kila chombo cha habari kilichosajiliwa nchini, kutumia ama Kiswahili au Kiingereza – lugha mbili peke yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukichanganya haya ya maeneo mawili, utaona kuwa wasiojua Kiswahili hawapaswi kujua kinachotangazwa redioni au kinachoandikwa kwenye magazeti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni hivi: Kama hawajui lugha hizo – Kiingereza na, au Kiswahili – basi potelea mbali. Ndiyo tafsiri ya kile ambacho Tume inasema na ambacho serikali inasisitiza. Ndivyo wenye vyama walivyoweka saini kutetea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anayeomba kura, aingie Usukumani. Maeneo ambako Kiswahili hakitumiki kwa kiwango kikubwa. Pale ambako maneno ya Kiswahili yanatumika kwa ushabiki tu – ama kueleza kuwa anayeyajua ni “mkora” au “mwerevu” kutoka mjini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa, Tume inataka anayeomba kura atumie Kiswahili. Atatumia. Baada ya hotuba kuna kipindi cha maswali. Hakuna anayeuliza kwa kuwa hakuna aliyeelewa. Kuna haja gani basi ya kufanya kampeni katika “lugha ya kigeni?”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nendeni Loliondo vijijini, katika mkoa wa Arusha. Kuna shule za msingi. Wanafunzi na walimu wana akili nzuri. Wanajua kuwa Kiswahili na Kiingereza, zote ni lugha za ngeni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya walimu wanafundisha kwanza kwa Kimasai na baadaye kuweka katika Kiswahili. Njia bora kabisa. Ni kwa misingi sahihi kwamba lugha ya kufundishia iwe ile ambayo mwalimu na mwanafunzi wanaelewa. Mara hii ni Kimasai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wazazi katika eneo hili ambao ndio wapigakura, wanajua vema lugha yao moja – Kimasai. Wanaokwenda magulioni mara kwa mara ndio wameokoteza istitahi za kibiashara katika Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa aende mwanasiasa anayetafuta kura. Amwage hapa kampeni yake kwa Kiswahili. Ataondoka kama alivyokwenda. Mtupu. Bila kura hata moja. Kwa nini? Kwa kuwa hawakumwelewa; lakini pia kwa kuwa naye ni mpumbavu – anatumia lugha ambayo anajua vema kuwa anaowaambia hawaijui.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili lina tafsiri moja kuu. Kwamba kwa miaka 50 ya utawala wa chama kimoja, watawala wamekuwa wakiimba na kijipiga vifua kuwa wana “lugha ya taifa – Kiswahili.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe yamekuwa majigambo yasiyo na mashiko. Wameshindwa kueneza lugha hiyo hapa nchini kama walivyoshindwa kutumia wataalam wake kuigeuza kuwa “bidhaa” ya kuingiza fedha za kigeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wameshindwa kukuza Kiswahili; wameshindwa kukuza lugha za asili; wameshindwa kutoa ajira kwa wanaojua lugha hizo ili wawe wakalimani kwa wasiojua lugha za kigeni; wamebakia na amri – “Tumia Kiswahili!”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa amri na mantiki ya Tume, wasiojua Kiswahili “shauri yao.” Hii siyo haki. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi wanaojua lugha zao wanastahili kupelekewa kampeni katika lugha zao; na kama njia ya kueneza lugha kuu, wapiga kampeni waombwe kudondosha maneno ya Kiswahili hapa na pale kama kupanda mbegu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vinginevyo itafikiriwa kuwa serikali, na vyombo vyake, imeamua kuwatenga, kuwatelekeza, kuwasahau na kuwanyima haki ya kushiriki siasa za nchi yao, wale wote ambao hawajui Kiswahili au Kiingereza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria, kanuni na taratibu zinazoondoa haki ya mtu; kupoteza utashi wake, tena ndani ya nchi yake, hazistahili kuheshimiwa na haitakuwa mara ya kwanza kukataa kuzishemu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Njia bora ya kuzipinga ni kuongea na wananchi katika lugha yao. Wananchi ndio watakuwa watetezi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-7868415649140703178?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/7868415649140703178/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=7868415649140703178' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/7868415649140703178'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/7868415649140703178'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/09/sheria-ya-mabwege-hii-hapa.html' title='&lt;strong&gt;SHERIA YA MABWEGE HII HAPA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TJxEI1-tpsI/AAAAAAAAAHE/DacMaai4ANM/s72-c/Jaji+Lewis+Makame-4.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-1708881639976915476</id><published>2010-09-23T22:53:00.000-07:00</published><updated>2010-09-23T23:08:00.052-07:00</updated><title type='text'>UNYANYASAJI WANAWAKE WAENDELEA</title><content type='html'>SITAKI &lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Makongoro anavyonyanyasa shemeji yake&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;          &lt;strong&gt;  Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI Makongoro Nyerere aanzishe mgogoro kati yake na Leticia Nyerere, mke wa zamani wa ndugu yake, Madaraka Nyerere.&lt;br /&gt;Vyombo vya habari vimemnukuu Makongoro akisema, kwenye mkutano wa hadhara jimboni Kwimba, kwamba Leticia asijaribu kujihusisha na ukoo wa Nyerere kwa kuwa tayari aliishachika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siyo rahisi kujua iwapo Makongoro ameagizwa na Madaraka kusema aliyoyasema; kwani hakusema hivyo. Haijafahamika iwapo kulikuwa na kikao cha ukoo kuamua juu ya matumizi ya jina la Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini muhimu zaidi ni kwamba, haijafahamika kuwa kila anayejitambulisha kuwa wa ukoo wa Nyerere anapendwa zaidi, anaaminika na kupewa kura. &lt;br /&gt;Hapa kuna upogo katika jamii ambao umefanya wanawake watupilie mbali majina ya wazazi wao na badala yake kujibandika majina ya waume zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni upogo uliogeuka mtindo, hasa mume anapokuwa mtu wa kujiweza na mke anapenda kuitwa Mrs. Fulani – mwenye mali, nyumba nzuri, magari na fedha zisizokauka mfukoni.&lt;br /&gt;Bali ni kupoteza utambulisho. Kipi bora, kujitambulisha kama mtoto wa Fulani au mke wa Fulani? Tukiwa sekondari kulikuwa na mwanafunzi mmoja aliyeitwa Festo Kokugonza. Mwendelezo mwingine huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwamba siyo lazima kuwa na ubini wa baba. Waweza pia kuwa na ubini wa mama na maisha yakasonga mbele bila kelele wala mikwaruzo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini hebu turudi kwa Leticia Nyerere. Je, haijulikani kweli kwamba alikuwa ameolewa katika ukoo wa Nyerere? Si taarifa hizi ziko wazi kwa kila mmoja kujua, hasa wakati huu wa kutafuta ufalme wa kisiasa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, ni lazima kufuta jina la mume pale mwanamke anapomwacha mume au anapoachika? Je, kuendelea kulitumia kuna  maana kwamba unataka kurudi au hutaki kuharibu utambulisho uliokuwa tayari umejengeka?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, kuendelea kulitumia jina hilo kwa utambulisho tu kuna maana kuwa unalithamini sana au sasa ni lebo maalum ambayo kuibadili kunaweza kukugharimu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, kujigamba tu kwamba mtu anatoka katika ukoo fulani kunaweza kuleta manufaa yoyote wakati anaowaambia wanajua kuwa sivyo ilivyo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, hata kama mtu atajidai na kujinadi kuwa ni wa ukoo fulani, ukoo huo una kitu gani cha ajabu na cha manufaa kwa jamii kiasi kwamba kujitambulisha nao tu wewe utakuwa umenufaika?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyerere alionyesha mfano mmoja mkubwa ambao mabwege wengi huutumia kumlaumu. Alijua watoto wake ni watoto kama watoto wa watu wengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuwapendelea kwa kuwapeleka shule zenye majina makuu au kuwapeleka Ulaya na kuwaficha huko na ujinga wao, ili warejee hapa kwa mbwembwe wakati hawana akili; kama viongozi wengine wanavyofanya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna lolote katika ukoo wa Nyerere ni kwamba ulimzaa Julius Kambarage Nyerere; aliyetokea kuwa jasiri, mwenye uwezo wa kiakili na aliyeongoza harakati za kuleta uhuru wa Tanganyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna lolote katika ukoo huu ni kwamba, hatuhitaji kutafuta zaidi, bali kwa ufupi tu, ulitoa Nyerere kama tulivyomwona, tulivyomfahamu na tulivyomwelewa. Basi. &lt;br /&gt;Waliobaki – mke wake, watoto wake na wengine katika ukoo – sharti wajisimamie na hawawezi kwenda kwa sifa ya ukoo wa Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jamii itawaona na kuwaelewa kama mtu mmojammoja, mwenye sifa yake binafsi, udhaifu wake binafsi, ubora wake binafsi; kwani hakuna kitu maalum kinachoweza kuitwa alama ya ukoo wa Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ndio maana, pale Butiama na katika ukoo, hakuna kinachomwakilisha Nyerere kama Nyerere – akili yake, uwezo wake, siasa zake, visheni yake, utashi wake na mengine mengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alichokumbuka Makongoro – ng’ombe 30 – ambao baba yake alitoa ili Madaraka amwoe Leticia, ni historia isiyofutika na ambayo inamwingiza mama huyo katika familia mpya, ukoo mpya hata usingekuwa wa Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Isipokuwa siyo siri, kwamba akili na uwezo wa Nyerere havikuwa mali ya ukoo; vilikuwa mali yake binafsi, lakini kwa uchambuzi mpana – hazina ya taifa. &lt;br /&gt;Bahati mbaya hakuvirithisha kwa yeyote – awe mke wake, watoto au ukoo wake. Ukitaka waweza kusema hivi; kwamba wanaovitambua, kuviheshimu na kuvienzi, ni watu wengine, wakiwemo wa mataifa na wala siyo hata chama chake alichoanzisha – CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna mamia kwa maelfu ya watu ambao wanaweza kumtetea Nyerere; kutaka asichafuliwe kwa hoja kubwa na nzito kwa kuangalia aliyoyafanya kuliko kung’ang’ania ukoo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyovyote itakavyokuwa, kwa kuwa Leticia ameingia ulingoni, ataulizwa anatoka wapi; hilo jina la Nyerere alilipataje; huyo Nyerere ni yupi na yuko wapi? Atajieleza.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Watakaopenda kumshangilia kuwa aliishaonja maisha katika moja ya nyumba ya watoto wa Julius Nyerere, acha waseme. Watakaosema “unyerere” wake hauna uzito, acha wapuuze. &lt;br /&gt;Bali kwa Makongoro kufunga safari kutoka Musoma hadi Kwimba kumwambia shemeji yake asijitambulishe na ukoo wa Nyerere, hakika ni njia nyingine ya udhalilishaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Julius Kambarage Nyerere hakuwahi kuwa, na siyo mali ya ukoo. Inawezekana Leticia anamtaja leo baada ya kuingia katika siasa, kama wengine wanavyomtaja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huwezi kukaa na Nyerere, kwa mfano, akichimba mtaro wa mabomba ya maji wa Ntomoko; akijenga nyumba za wanakijiji Kibondo kwa wiki mbili; halafu ukamsahau, wakati una rais anayewekewa mkeka na kuvalishwa glovu mikononi ndipo apande mti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huwezi kusoma vitabu na maandishi mengine ya Nyerere; ukaelewa fikra zake halafu ukashindwa kumuunga mkono au kumpinga na hata kumsema mara kwa mara kufuatana na jinsi ulivyomwelewa; hasa unapokuwa na rais asiye na hoja za kutoa changamoto kwa ubongo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huwezi kuwa na Nyerere anayeanzisha chama cha siasa na baadaye kusema kinanuka rushwa na kutishia kukikimbia akisema “siyo baba, siyo mama;” wakati una utawala ambao unachefua kwa rushwa, wizi na ufisadi usiomithilika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushauri wangu kwa rafiki yangu Makongoro Nyerere ni kwamba, siyo tu amwache shemeji yake Leticia achanje mbuga na kutafuta ubunge kwa uhusiano wowote ule; bali awaache wote wanaomtaja Nyerere, kwa wema au ubaya na kwa sababu yoyote iwayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyerere siyo mali ya mtu mmoja, familia au ukoo. Na Nyerere hahitaji utetezi; bado anajiweza, hata baada ya kuaga dunia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, tusisahau kuwa upogo uliogeuka mtindo, utaendelea kutumiwa na wanaume wengi kudhalilisha wanawake, wakidhani kuwa hata wanapokuwa hawawagharamii tena, bado wananufaika kwa majina yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu siyo tu uongo, bali ujinga ulioambatana na ubabe wa miaka mingi na unaoendelezwa na ulimbukeni miongoni mwa wanaume, wakifikiri au kudhani tu kwamba majina yao yana ulimbo wa maisha bora.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-1708881639976915476?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/1708881639976915476/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=1708881639976915476' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1708881639976915476'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1708881639976915476'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/09/unyanyasaji-wanawake-waendelea.html' title='&lt;strong&gt;UNYANYASAJI WANAWAKE WAENDELEA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-6450999730445786700</id><published>2010-09-23T22:49:00.000-07:00</published><updated>2010-09-23T22:52:14.328-07:00</updated><title type='text'>AHADI LUKUKI ZA CCM</title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TJw8YE22amI/AAAAAAAAAG0/luFnT-o-75I/s1600/kikwete-msanii.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TJw8YE22amI/AAAAAAAAAG0/luFnT-o-75I/s320/kikwete-msanii.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5520353627567712866" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Ahadi nyingi za kiwewe za mgombea urais &lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kampeni zilizosheheni ahadi kebekebe na zisizokuwa na ukomo; hasa zinapokuwa zinatolewa na mgombea anayetaka kubaki ikulu kwa miaka mingine mitano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akihutubia mkutano wa kampeni mjini Bukoba mapema wiki hii, mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Mrisho Kikwete alinukuliwa akisema serikali itanunua meli kubwa na mpya itakayofanya kazi katika ziwa Viktoria na kupunguza kero ya usafiri kwa bandari za ziwa hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi sasa, meli ya mv Viktoria ndiyo kubwa inayofanya safari ziwani humo, baada ya mv Bukoba kupinduka na kuua zaidi ya watu 1000 Mei 1996.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kikwete ametonesha vidonda hai. Tangu mwaka 1996 serikali imekaa kimya. Benjamin William Mkapa alimrithisha Kikwete kimya hicho. Kikwete amekuwa kimya kwa miaka mitano. Bila shaka kuna sababu ya Kikwete kuahidi ununuzi wa meli. Tutaona.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakumbuka mama yangu alizimia muda mfupi baada ya kuambiwa kuwa meli imezama na kuua watu wengi. Siku ya tatu baadaye aliaga dunia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ilikuwa hivi: Kaka yangu alimwambia mama yetu kuwa meli imezama na kuua watu wengi. Alimwambia kuwa yeye alikuwa asafiri kwa meli hiyo, lakini alipoona imejaa, akaamua kubaki pale bandari ya Kemondo ili asafiri siku nyingine. Hiyo ndiyo ilikuwa safari ya mwisho ya mv Bukoba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndani ya meli hiyo aliteketea mke wa kaka yangu na watoto wake wawili. Aliteketea mpwa wangu Evelyn, mtoto wake na binti mmoja ambaye alikuwa amemchukua kutoka kijijini kwetu Bushumba ili amsaidie shughuli za nyumbani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nasimulia. Ilikuwa hivi: Baada ya kaka kumwambia mama yetu kuwa meli imezama na kuua wengi, mama aliuliza, “…na Ndimara alikuwemo?” Kaka alijibu, “Hapana. Ndimara yuko nje ya nchi.” Mama alijibu, “…hivyo ndivyo wamezoea kunidanganya…” Alikaa kimya hadi alipoaga dunia, siku ya tatu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakika nilikuwa nje ya nchi. Nilikuwa mji wa Kariba kwenye bwawa la Kariba lililoko mpakani mwa Zambia na Zimbabwe. Tulikuwa kwenye mkutano wa waandishi wa habari tukijadili “Sheria, Demokrasi na Vyombo vya Habari.” Nilipata taarifa kwenye televisheni iliyoonesha meli ilivyozama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niliomba gari kutoka ubalozi wa Sweden nchini Zambia. Nilipewa. Ni kilometa 249 kutoka Kariba hadi Lusaka. Kesho yake niliunganisha na ndege, wakati huo Shirika la Ndege Tanzania (ATC) iliyokuwa inapitia Harare na kurudi Dar es Salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilifika Dar es Salaam jioni ya saa 12. Niliondoka Dar es Salaam kwenda Bukoba kesho yake asubuhi. Nilifika kijijini Bushumba siku hiyohiyo saa 10.30 na kukuta wananawa mikono – wamemaliza kumzika mama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mjini Mwanza nilikuwa nimemwacha kaka yangu, Gration Tegambwage akichuruzika machozi yasiyoisha – amepoteza mke na watoto wawili. Nilimwachia andishi lililokuwa limeandikwa kwa njia ya shairi awe analisoma na kuona iwapo lingemsaidia kutuliza roho; lakini siyo kusahau.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Asingeweza kusahau haraka au polepole kwani kila baada ya muda, maiti zilizoopolewa ziliwekwa uwanjani Nyamagana na alilazimika kufunua kila maiti kuona iwapo atamwona mpenzi wake – mkewe au angalau mmoja wa watoto wake. Ni majuto. Ni machozi yasiyokauka. Hakuona yeyote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vilio hivi vimeendelea ndani ya mitima ya wengi. Serikali imekaa kimya. Miaka mitano imepita. Rais akaomba kura tena. Akapata. Akatulia ikulu. Akasahau. Miaka ikapita. Akaondoka. Akaja mwingine – Jakaya Mrisho Kikwete.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naye Kikwete amekaa miaka mitano. Sasa anaomba kura ili aendelee kupanga ikulu kwa miaka mingine mitano. Ndipo anaahidi meli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kumbukumbu zangu mv Viktoria iliingia ziwani Viktoria mwaka 1965. Tunaambiwa haikuwa mpya. Huenda ni kweli. Tangu hapo imekata maji usiku na mchana hadi ikazeeka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Meli hii imezimika mara kadhaa ikiwa safarini. Imeshindwa kuendelea na safari na kuwekwa ghatini kwa vipindi vingi. Imekarabatiwa na kukarabatiwa. Baadhi ya wafanyakazi melini humo wamesikika wakisema, “...nalo hili limeoza.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ina maana gani? Kwamba abiria wanasafiri kwenye mgongo wa mauti. Kwamba lolote laweza kutokea. Lolote lipi? Bila kutabiri majanga, lakini linajulikana: kuzama, kupinduka na kuua abiria mithili ya mv Bukoba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachouma ni kwamba mgombea wa CCM alipotoa ahadi ya meli, wananchi wa Bukoba walishangilia. Wachache walitikisa vichwa kwa masikitiko. Wachache au hakuna waliojiuliza kwa nini mgombea atoe ahadi siku hiyo na siyo miaka kadhaa iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niliwahi kuhutubia mkutano wa hadhara mjini Bukoba, miaka mingi iliyopita nilipokuwa mwakilishi wa Muleba Kaskazini. Niliwaambia wananchi, pamoja na mambo mengine kuwa, “…nimushekelela olufu nk’omunyima.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Omunyima ni mnyama ndogo mweusi ambaye, hata anapofukuzwa na kupigwa, kwa nia ya kumuua, bado anaendelea kutoa sauti kama anayecheka. Ndipo wenye lugha yao wakasema “unachekea mauti kama mnyima.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakazi wa Magharibi mwa Ziwa Viktoria wamekuwa wakichekea mauti kama mnyima. Kuna majanga mengi yaliyowakumba na serikali ikakaa kimya; lakini wao waliendelea kuonyesha tabasamu. Ni mengi na yanajumuisha vita vya Uganda na hata ukimwi uliokingiwa magego hadi watu walipoanza kupukutika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilitoka Bukoba siku ya Jumatano ambayo mgombea wa CCM alikuwa ahutubie mjini hapo. Nilikutana na wanaume wawili na mwanamke mmoja – wote wa makamo –  kwenye hoteli ya Victorius Perch.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni mwanamke aliyekuwa wa kwanza kueleza kuwa kuna mkutano wa mgombea urais wa CCM siku hiyo. Maneno yake yalidakwa na mmoja wa wanaume, na kama kawaida katika lugha yao. “Nani? Ekikwanga okyanga” – anayekukataa nawe huna budi kumkataa!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ujumbe mkataa. Inaonekana hao hawachekei mnyima tena. Wanajadili mengi ambayo serikali imefanya lakini imesahau au imedharau wasafiri kwenye ziwa Viktoria wanahitaji na hakika wanastahili chombo imara cha usafiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mmoja anang’aka, “Naona wanafikiri kuwa sisi tuna uzoefu wa kufa.” Mwingine anaorodhesha yale ambayo serikali imefanya na kutaja uwanja mpya wa taifa jijini Dar es Salaam kuwa ndio watawala wameona ni muhimu kuliko meli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kikwete atakuwa amebanwa sana katika kampeni za sasa za kutafuta urais hadi kufikia hatua ya kuahidi meli ziwani Viktoria ambayo hajawahi kutamka katika mipango yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kama alivyofanya kwa wakazi wa Misenyi mkoani Kagera ambao wamekuwa wakifukuzwa kutoka maeneo yao ya asili kwa madai kuwa ni eneo la ranchi iliyobinafsishwa. Sasa anasema wapimiwe viwanja ndani ya ranchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mgombea urais wa CCM anajua kuwa nani walinunua na wanamiliki ranchi ya Misenyi. Tumeambiwa ni baadhi ya marafiki zake. Alikuwa wapi hadi juzi ndipo aseme hilo? Mbona hakusikia vilio vya wananchi pale mkuu wa mkoa alipokuwa akiwakomalia kuwa wataweza kuhamishwa “hata kwa mtutu wa bunduki?”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ahadi za Kikwete zitakuwa nyingi mwaka huu. Anayejua sababu ni yeye mwenyewe na chama chake. Kinachoonekana ni kwamba katika maeneo mengi, kama Bukoba na Misenyi, anajichongea. &lt;br /&gt;Huenda kura zisitimie.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-6450999730445786700?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/6450999730445786700/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=6450999730445786700' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6450999730445786700'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6450999730445786700'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/09/ahadi-lukuki-za-ccm.html' title='&lt;strong&gt;AHADI LUKUKI ZA CCM&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/TJw8YE22amI/AAAAAAAAAG0/luFnT-o-75I/s72-c/kikwete-msanii.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-8568577618882783268</id><published>2010-09-23T21:28:00.000-07:00</published><updated>2010-09-23T21:31:24.926-07:00</updated><title type='text'>UCHOVU NA UMBEYA WA WAKUBWA</title><content type='html'>SITAKI    &lt;br /&gt;&lt;strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wachovu wa CCM na umbeya wao&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI wananchi waingizwe kwenye ubishi wa kipuuzi unaopaliliwa na kunawirishwa na wachovu wa siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wiki hii tumesikia baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakidai kuwa watashitaki Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wamesema watapeleka malalamiko kwa Tume na Msajili wa Vyama vya Siasa kwamba Chadema imefanya kampeni kabla ya Tume kuruhusu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachotia kichefuchefu ni baadhi ya wanasiasa upande wa upinzani kuitikia kibwagizo cha CCM na wao kuimba kuwa Chadema na CCM wanaweza “kuchukuliwa hatua.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali iko hivi: Dk. Willibrod Slaa anateuliwa na chama chake kugombea urais. Chama kinaanua kufanya mikutano katika miji mikuu ya mikoa kadhaa. Kinambeba mteule wake. Hii ni kwa sababu kuu mbili:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, kumtambulisha kwa wanachama wake na wananchi. Pili, kuendeleza kazi yake ya kisiasa kama chama chochote kile kilichohai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama kilichohai, kikipata fursa, sharti kiitumie kuwafikia majaji wakuu katika taratibu za kidemokrasia; ambao ni wananchi wapigakura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chadema haikufanya hivyo juzi tu. Imekuwa ikifanya hivyo kila inapotaka kuwa karibu na wananchi; na wapigakura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo ndivyo CCM imefanya. Imetangaza wagombea wake, halafu ikawapeleka kwenye mikutano ya hadhara – kwa wapigakura – ili wanachama wenzao na wananchi wawafahamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama kingine chenye ushindani ni Chama cha Wananchi CUF. Hiki hakikuwa na kiongozi wa kutambulisha kwani mgombea urais wake mwaka huu, ni Profesa Ibrahim Lipumba ambaye tayari amepigiwa kura za urais mara tatu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, CUF muda mfupi baada ya kutangaza mgombea wake, iliweka wazi kwa mgombea, ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho kitaifa, atatembelea mkoa wa Dar es Salaam kwa madhumuni ya “kuangalia uhai wa chama.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiyo nayo ni fursa nyingine kwa chama makini kuwa karibu na wananchi na wanachama wake wakati muhimu wa kuelekea uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiangalia kwa makini, utaona kuwa kila chama kina njia zake za kufanya kazi za kisiasa – iwe asubuhi, adhuhuri, alasiri, mangharibi au usiku.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muda huu wa maandalizi ya kuingia kipindi maalum cha kampeni na uchaguzi mkuu, hautawaliwi na pingu za NEC. Ni muda na eneo huru la kuzidisha kazi za kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hasa ni kipindi maalum kwa vyama upande wa upinzani, kutekenya jamii, kuizindua, kuielimisha, kuishawishi na kuiandaa kuachana na ukale ulioizonga na kuipa kilema – kudumaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mfano, kwa upande wa Chadema, ni wakati wa kuendeleza na kuhitimisha kwa nguvu, kazi ya kisiasa inayoitwa “Operesheni Sangara” – iliyovuma na kuvuna nyoyo za wengi – kabla ya kuingia katika uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wa CUF, ni wakati mzuri wa kuendeleza na kuhitimisha kazi ya kisiasa iliyoitwa “Zinduka” – iliyozindua wengi – kabla ya kuingia katika uchaguzi mkuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, kinachoipa kiwewe CCM, siyo Chadema “kufanya kampeni” kabla ya muda uliopangwa na Tume, bali umaarufu wa mgombea wa Chadema anapolinganishwa na yule wa chama chao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiwewe kinatokana na mgombea mpya anayefahamu vema serikali na nyendo zake. Anayejua serikali ilivyokwama kwenye tope la ufisadi, ukosefu wa ubunifu; ukame wa mbinu mpya na ahadi tuputupu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kelele za CCM zinalenga kufanya mwendelezo wa ghiliba kwa wananchi. Chama hiki, kama ilivyo serikali yake, kina midomo mingi na uwezo wa kupakazia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kina vyombo vya habari vya serikali (wanadai ni vya umma), ambavyo vinatawaliwa na makada wake. Humu hupitishwa kampeni na propaganda angamizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CCM ina “marafiki” wenye vyombo vya habari ambao huipendelea kwa kila hali kuliko hata gazeti lake la UHURU.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kutumia midomo yake mingi; laghai wake wengi; ujuzi na uzoefu wa kutunga ghiliba na kupakazia, chama hiki kinaweza kuanzisha mjadala finyu, kikaupa mvumo, ukapandikiza mitafaruku na kupotosha wananchi wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama hikihiki kinaweza kutumia kauli za nguvu kuyumbisha watendaji serikalini; kutishia walioko madarakani katika sehemu muhimu kama Tume ya uchaguzi na kuogofya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haitakuwa mara kwanza kwangu kujenga hoja kwamba watawala wetu wamekuwa wakitegemea sana ujinga, woga na umasikini wa wananchi (vilivyosimikwa na chama kinachopanga ikulu), kama mitaji yake mikuu katika juhudi za kubaki madarakani kwa nusu karne sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama hiki kina watu wenye ujasiri wa kukataa ukweli; wakaidi wa kutaka kila mmoja aone, kwa mfano, kuwa hili ni chungwa wakati ni kiazi kikuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CCM isingekuwa hivyo, kama ilivyofafanuliwa hapo juu, viongozi wake wasingejitokeza kupandikiza uzushi kwamba Chadema imefanya kampeni kabla ya NEC kutangaza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani kampeni za kuwaelimisha wananchi kujua kuwa diwani, mbunge au rais huyu hafai; anayefaa ni fulani kutoka chama kingine, hazisubiri uchaguzi mkuu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni kazi ya Oktoba hadi Oktoba, kwa kipindi chote cha miaka mitano ya wanaokuwa madarakani na wanaokuwa wakisubiri kuingia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi chote hiki NEC inajiandaa kusimamia uchaguzi lakini wanasiasa wanakata mbuga kuandaa wananchi kwa “mavuno.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa hakuna udhibiti hadi unapoingia rasmi kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu. Kazi za kisiasa za chama chochote, haziruhusiwi wala hazipaswi kuzuiwa na Tume. Na pasito zuio kuna uhuru kamili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mfano huu: Katika mazingira ambako hakuna sheria inayolazimisha kila mmoja kuvaa tai shingoni, hakuna anayeweza kukamatwa na kushitakiwa kwa kutovaa tai. Hakuna sheria inayombana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiyo ndiyo hali iliyopo katika kipindi ambapo wachezaji watarajiwa wa mchezo wa siasa hawajajifunga kushiriki; na mchezo wenyewe haujaanza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huwezi kuwabana. Huwezi kusema aliye nje ya uwanja ameharibu kanuni na taratibu za mchezo. Kudai hivyo ni kupanda mbegu ya uhasama ambao CCM na serikali yake, havina uwezo wa kuzima ndimi zake pale zitakapokuwa zimechomoza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi sasa, CCM ni chama kinachokwenda kwa mazoea tu. Hakina jipya ingawa kinataka kubaki ikulu, kwa “gharama yoyote ile.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na hili la kubaki madarakani kwa gharama yoyote ile, ndilo liwezalo kuleta maafa kwa nchi na watu wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani wanajua kuwa kuondoka kwao kutaweka wazi mengi machafu ambayo yamekuwa yakitendeka.  Hili, viongozi wake hawataki kuliona wala kulisikia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wako tayari kuua mbegu mpya na bora kwa kupitia madai yasiyo kichwa wala miguu, alimradi wamebaki ikulu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini katika hili la kupakazia kufanya kampeni mapema, tundu limezibwa. Hata kwa mgongo wa “tu-vyama twingine” kwenye upande wa upinzani, kama vile Tanzania Labour Party (TLP) ka Augustine Mrema, CCM itaendelea kukaliwa kooni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tayari kuibuka kwa Dk. Slaa kumebadili mwelekeo wa siasa nchini na kuleta uwezekano wa kuifinyaza CCM na mikonga yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali wananchi wanataka umoja wa vyama; kwa maana ya ushirikiano katika uchaguzi huu ili mradi wa kuadabisha CCM uweze kufanikiwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umbeya na ghiliba ya CCM vyaweza kuzimwa. Je, hili la ushirikiano laweza kufikiwa? Tusubiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com &lt;br /&gt;&lt;strong&gt;&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-8568577618882783268?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/8568577618882783268/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=8568577618882783268' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8568577618882783268'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8568577618882783268'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/09/uchovu-na-umbeya-wa-wakubwa.html' title='&lt;strong&gt;UCHOVU NA UMBEYA WA WAKUBWA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-9184667297229371036</id><published>2010-05-21T02:08:00.000-07:00</published><updated>2010-05-21T02:10:11.759-07:00</updated><title type='text'>TATIZO LA SHERIA KUHUSU HABARI NA MAWASILIANO</title><content type='html'>SITAKI             &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Wasioona tatizo la Mkuchika, sheria &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na  Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kuwa mchoyo. Someni wanavyosema baadhi tu ya wasomaji wa uchambuzi wangu juu ya hatua ya serikali ya kufungia gazeti la KuliKoni iliyochapishwa kwenye ukurasa huu Jumapili iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hadi jana saa tatu asubuhi, jumla ya wasomaji 127 walikuwa wameandika ujumbe mfupi wa simu na 39 wamepiga simu. Asilimia 99.7 wanapinga serikali kwa hatua iliyochukua. Someni kwa furaha:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naungana na mada yako leo. Mimi nilidhani wanaposikia habari mbaya zinazoliletea taifa aibu, basi ni wakati mzuri wa kufundisha jamii juu  ya kuishi kwa maadili mazuri, siyo kumfungia mtoa taarifa. Hii ni aibu kwa kiongozi aliyepewa dhamana – 0712-752595.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pole na hongera kwa kuchagua kuelimisha jamii juu ya kufungiwa kwa KuliKoni – 0717-664685.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kweli. Jeshi walikanusha asubuhi ileile habari ilipotoka hata bila kufanya uchunguzi wala kuomba undani wa habari ili wafanyie kazi (usianike namba yangu). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hongera kwa article yako. Hivi waziri (George Mkuchika, wa Habari, Utamaduni na Michezo) anajua mavazi ya watoto wa kike vyuo vikuu? Majumbani nako amefika? – 0713-243231.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mashaka yangu ni pengine waziri hajui istlahi uchi ina maana gani; uchi kwa mujibu wa nani, tatizo picha za uchi au uchi wenyewe? Kama watembea uchi wamo katika ibada je, picha za uchi magazetini ndio kero kuu ya wananchi Tanzania? – 0713-326376.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatizo kuu kabisa la wanaoitwa viongozi wetu, ni UNAFIKI. Kujikataa ndiyo uswahili wenyewe na utamaduni wa taifa. Inasikitisha. Inafedhehesha. Inadharaulisha. Reason na logical thinking havipewi nafasi kuchanua. Nakuomba endelea kuandika akina Mkuchika wapungue – 0754-532797.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dawa ya kufungia gazeti ni kumpa kibano aliyelifungia kama ilivyokuwa kwa MwanaHALISI. Mbona safari hii kama hamumwoni? Mwasubiri nini? Kazi njema – 0787- 155882.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimesoma uchambuzi wako. Umenifurahisha kwa kuwa umeongea ukweli – 0716-455073.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mungu akupe nguvu na hekima zaidi. Waandishi kama wewe mnapigwa vita lakini Mungu yupo upande wetu; amekushika kwa mkono wake wa kuume; hautatetereka. Songa mbele. A luta continua – 0715-808283.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimekusoma. Viongozi wetu hawakai hata siku moja wakasoma magazeti na kuchambua. Magazeti yanajaribu kuwakumbusha wakuu wetu kuwa taifa maadili hakuna…lakini leo gazeti la kurekebisha uozo waziri analifungia. Kisa? Limesema mitihani imeibwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunakwenda wapi? Wanataka magazeti yaandike kibaka kaiba kuku; lakini wakiandika wakubwa wamechota mabilioni ya shilingi, huo ni uchochezi…Tunaenda kubaya sana – 0765-938181.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimesoma makala yao. Umenikuna. Endelea hivyo. Tutafika. Gerald wa Kyela – 0767-481431.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndugu mwandishi, nakuombea kwa Mwenyezi Mungu uendelee na karama yako uliopewa na Mungu. By Masunga kutoka kijiji cha Mwasayi wilayani Maswa – 0787-229774.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Una kila sababu ya kuungwa mkono. Endelea. Wewe ni mpiganaji, una kila sababu ya kuungwa mkono – 0652-411969.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyombo vya habari vipo kwa ajili ya kuwajulisha wananchi habari za ukweli halisi ambazo wao ni vigumu kuzipata. Je, kuna ubaya gani wananchi kujua nchi yao inaelekea wapi? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufungiwa kwa KuliKoni na kufutwa kwa gazeti la Leo Tena ni kuvitisha vyombo…wakubwa wameamua kuhamishia hasira zao kwa wanyonge…Mkuchika amekurupuka. Mimi kama mwananchi sikubali – 0712-703631.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umesema magazeti kama Leo Tena huwa yanajifuta yenyewe. Tukisubiri yajifute yenyewe yatakuwa yameshaharibu sana. Nina wasiwasi kama uliliona gazeti hilo – 0755-923565.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sijui kama hujui kama yeye (Mkuchika) ni waziri mwenye dhamana…na majukumu yake ni “kuoversee” sekta ya habari. Naamini kwa uzoefu ulionao unajua kuwa ana kila mamlaka kufanya alichokifanya kwa mujibu wa sheria. Kwamba hukubaliani na sheria hiyo hakuna ubaya ni haki yako – 0655-280400.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa inabidi ianzishwe wizara ya ufisadi na utamaduni wa mikataba; pia wizara ya kufuta magazeti na vyombo vyote vya habari -0713-442524.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimesoma makala yako. Mbona sioni mshikamano wenu wa hadhara wa kupinga kufungiwa magazeti? Wananchi twataka mtuongoze – 0713-280002. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimekupata (Mkuchika na sheria yake). Zamani Bushiri alimwambia Chakubanga alipoona anaficha bagi baada ya kuona polisi: Uliyokwishavuta vitendo vyake utavificha wapi? – 0713-234722.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naungana na wewe 100% juu ya sheria na Mkuchika hasa aya ya 28: Huwezi kutumikia umma ambao umeufunga mdomo… – 0777-722382.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanahabari unganeni, msiandike habari zake hadi upite uchaguzi mkuu, Oktoba 2010 – 0714-768588.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bravo. Hapo umempasha Mkuchika. Laiti na wanahabari wengine wangekuwa na ujasiri huo (usianike namba yangu).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wamelifungia gazeti la KuliKoni lakini lengo lao ni MwanaHALISI, RAIA Mwema na Tanzania Daima. Je, kuna uhuru wa habari – 0718-122081.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maoni ni mengi. Kila mmoja ana lake la kusema kadri anavyoguswa. Tujiulize: Je, waziri mmoja akijiuzulu, siyo kwa kashfa za ukwapuaji mabilioni ya shilingi benki kuu, bali kwa kukataa kutumikia sheria katili, itakuwaje?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itakuwa hivi: Serikali itakumbushwa kuwa fimbo yake, iliyoweka ili kupigia nyoka pindi akitokea, sasa inatumika kupigia mume, mke na watoto. Itupwe. Hapana. Ivunjwevunjwe na kuwa kuni. Inanyang’anya haki. Inafedhehesha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 ni kitanzi shingoni mwa hata mawaziri wenyewe pindi watokapo kwenye “utukufu” wa wizara hiyo au wa serikali. Ina tabia ya kuwasubiri wastaafu au wastaafishwe ndipo waone kuwa ni katili kupindukia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachosikitisha ni vipi watawala wameona utamu – tangu mwaka 1976 – wa kuendelea kuwafunga midomo na akili – wazazi wao, watoto wao, ndugu zao na jamii nzima ya Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna haja kwa Watanzania kufanya maamuzi: Kama    hakuchi tufungue milango – alfajiri itukute nje katikati ya maandalizi mapya ya kutafuta haki. Na wewe umo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;O713-614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-9184667297229371036?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/9184667297229371036/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=9184667297229371036' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/9184667297229371036'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/9184667297229371036'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/05/tatizo-la-sheria-kuhusu-habari-na.html' title='TATIZO LA SHERIA KUHUSU HABARI NA MAWASILIANO'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-5841600113190606321</id><published>2010-05-21T02:02:00.000-07:00</published><updated>2010-05-21T02:07:57.948-07:00</updated><title type='text'>POROJO ZA SERIKALI NA MISHAHARA YA WAFANYAKAZI</title><content type='html'>SITAKI          &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Porojo za serikali kuhusu mishahara&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI waziri anayejifariji kwa kauli ndogo na rejareja hasa katika masuala yanayohitaji busara na hekima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anachokifanya Profesa Juma Kapuya, waziri wa kazi, ama kwa utashi binafsi au kwa kuagizwa na serikali, kinamuumbua na hata kuumbua serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafanyakazi wamesema watafanya mgomo kuanzia 5 Mei mwaka huu kushinikiza serikali kushughulikia maslahi yao. Wamesema pia kwamba hawamwaliki rais kwenye sherehe zao za Mei Mosi mwaka huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa Kapuya, kwa mizaha yake, akijua kuwa madai ya wafanyakazi ni nyongeza ya mishahara, amekurupuka na kusema mishahara katika sekta binafsi imeongezwa kwa asilimia 100.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliwaambia waandishi wa habari Jumanne iliyopita kwamba Mwanasheria Mkuu wa serikali atatangaza hivi karibuni, katika gazeti la serikali, ongezeko la asilimia 100 kwa mishahara katika sekta binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali au Kapuya wanapata wapi ujasiri wa kuongeza mishahara ya sekta binafsi lakini wanashindwa kuongeza mishahara kwa watumishi wake? Wana uhakika gani kwa viwango hivyo vitalipwa na vinakubalika?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama Kapuya anasema nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa serikali inahitaji majadiliano zaidi, kwa nini majadiliano hayo ya kina yasihitajike katika sekta binafsi inayolipa kodi serikalini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri wa kazi anasema mwanasheria “atatangaza hivi karibuni” nyongeza ya mishahara. Hivi karibuni ni lini hasa? Baada ya Mei Mosi? Kabla ya mgomo wa 5 Mei? Baada ya mgomo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama serikali ina uwezo wa kuahidi kitu “hivi karibuni,” ilishindwa vipi kuchukua hatua muda wote tangu wafanyakazi wadai mafao na kufikia hatua ya kutaka kufanya mgomo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili ndilo linafanya wengi wajenge mashaka juu ya nia na shabaha ya serikali. Au, kwa vile serikali inasema haishughulikii mishahara ya watumishi wake, basi itumie sekta binafsi kuepusha songombindo hili?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi nani amemwambia Kapuya na serikali yake kwamba wafanyakazi wanataka “tangazo la mwanasheria mkuu” wa serikali? Tangazo ni la nini hasa? Mbona katika madai ya wafanyakazi hakuna tangazo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, tangazo la mwasheria wa serikali linaloahidiwa “hivi karibuni,” likija kweli hivi karibuni na kusema mishahara itaongezwa lakini itakuwa mwaka kesho, litakuwa limekidhi haja ipi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kapuya na, au serikali, wameongea lini na wafanyabiashara, wenye viwanda na wakuu wa maeneo mbalimbali ya sekta binafsi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lini na wapi serikali ilikubaliana na watawala wa sekta binafsi kuwa kuanzia sasa walipe asilimia 100 ya mishahara ya wafanyakazi wake?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lini serikali ilikutana na wafanyakazi au viongozi wake; kujadili kwa kina na kukubaliana kuwa hicho ndicho kiasi wanachotaka – siyo zaidi wala pungufu – na hivyo kuanzisha mijadala na waajiri?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani ameidanganya serikali kuwa inaweza kutoka usingizini wakati wowote; au inaweza kuchomoka katika fukuto la woga wa migomo ya wafanyakazi na kuamuru waajiri kutoa viwango vya mishahara kama inavyotaka?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa baadhi ya waajiri katika sekta binafsi wameanza kusema kuwa hawataongeza mishahara. Wengine wanasema wanaweza kuongeza mishahara lakini itabidi wapunguze wafanyakazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), kikiongea kupitia msemaji wao Aggrey Mlimuka kilieleza kidiplomasia juzi Ijumaa kuwa kinaangalia mwenendo huu na kuchunguza la kufanya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa vyovyote vile, sasa serikali imechokoza nyuki. Kwanza imeleta ubaguzi kwa kusema itatangaza mishahara kwa wafanyakazi wa sekta binafsi na kuwataka watumishi wake “kusubiri.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi hao watumishi wa serikali watasubiri hadi lini ili wapate angalao tangazo la kupandishiwa mishahara kinadharia kupitia mwanasheria mkuu wa serikali; achilia mbali kulipwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, serikali imeingiza waajiri katika mgogoro wake. Nao wameanza kuitilia mashaka na kupinga hatua yake; siyo kwa kauli rejareja bali kwa vitendo vya kupunguza idadi ya wafanyakazi – jambo ambalo serikali haikutegemea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu, imekuza mapambano dhidi yake kwani wafanyakazi sasa wanaona kuwa serikali inataka kutumia mbinu ya kuwagawa kwa misingi ya sekta – binafsi na umma – ili kuwadhoofisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa Kapuya na serikali wanakumbuka  kuwa wakati fulani walitangaza nyongeza ya mishahara bila kushirikisha waajiri na waajiri, hasa wenye viwanda, wakakataa mapendekezo na amri za serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya wenye viwanda walikuja na mapendekezo yao wakitaka serikali ikubaliane nao kwa mujibu wa maelezo kuhusu mapato, matumizi na matarajio ya viwanda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna wakati serikali iliumbuka na kudhalilika, basi ni wakati huo. Ilibidi waziri wa kazi afanye kazi ya ofisa wa uhusiano wa makampuni hayo – akieleza jinsi ambavyo viwanda havitamudu kulipa mishahara hiyo – na kufikia hatua ya kuweka viwango vipya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yote haya yamekuwa yakifanywa kwa kasi na bila kuwa makini kwa vile kwa kipindi kirefu serikali inadharau matakwa, wito na madai ya wafanyakazi. Hivyo inakurupuka hatua za lalasalama na kulazimika kutumia hata viinimacho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa kauli iliyofanana na kuwaangukia wafanyakazi, bado hakuna hatua za haraka zilizochukuliwa kukutana nao na kuwasikiliza kwa makini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatizo kubwa ni kwamba watawala Tanzania, baada ya kurithishana madaraka kwa miaka yote hii – nusu karne – wamekuwa na tabia ya kuamini kuwa yanayosikika nchi za nje; ya wafanyakazi kugomea rais na serikali yake, hayawezi kufanyika hapa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna wafanyakazi wenye musuli la vyuma. Hakuna wenye damu ya kijani. Kote duniani wafanyakazi wamekomazwa na mazingira yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mahala pengi wamekomazwa na tabia na vitendo vya watawala. Bila kukohoa, kupaza sauti, kukemea, kukemea, kupanga na kupangua, kuandamana na kugoma, basi haki haipatikani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hilo ndilo linaunganisha wafanyakazi kote duniani: Kwamba kazi wanafanya lakini wananyonywa, wananyanyaswa na hawasikilizwi. Bila kuungana hawafiki popote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa njia hii huwezi kusema wafanyakazi wa Tanzania wana damu ya kijani na hivyo watakuwa na upole wa kondoo. Hapana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Acha wasimame imara kudai chao. Wasipokipata leo watakipata kesho, mradi hawalazi msuli. Na kama serikali haitasikia leo, bila shaka itasikia kesho, na huenda katika mazingira tofauti na leo. Kapuya upoo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-5841600113190606321?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/5841600113190606321/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=5841600113190606321' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5841600113190606321'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5841600113190606321'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/05/porojo-za-serikali-na-mishahara-ya.html' title='POROJO ZA SERIKALI NA MISHAHARA YA WAFANYAKAZI'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-6487128183655386625</id><published>2010-05-21T02:00:00.000-07:00</published><updated>2010-05-21T02:02:49.728-07:00</updated><title type='text'>KAWAWA NA 'USIMBA' WAKE</title><content type='html'>SITAKI           &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Wanaotaka kuzika ‘ujasiri’ wa Kawawa&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI Watanzania wasahau Rashid Mfaume Kawawa; ingawa hakika watamsahau. Kama wamesahau Julius Kambarage Nyerere, sembuse “kibarua” wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kawawa – Waziri Mkuu, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Makamu wa Pili wa Rais na wakati huohuo Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, aliaga dunia juzi, Alhamisi akiuza uyoga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tusemezane. Tuambizane ukweli. Wakati aliyewahi kuwa na madaraka, nyakati hizo, ya kuumba na kuumbua anakufa akiuza uyoga, karani mmoja wa Benki Kuu (BoT) anajengewa nyumba kwa Sh. 1.4 bilioni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msanii wa viwango vyake, Kipanya, amefafanua nyumba ya karani wa BoT kama ifuatavyo: “Tumetumia bilioni moja point four tu kujenga my haus…Vere spesho haus. Ukija moto inajizima, yakija mafuriko inapaa.” Utaongeza nini hapa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na vyeo vyote alivyokuwa navyo, Kawawa hakuweza kujichotea mabilioni ya shilingi au kutumia nafasi yake kulainisha wahusika ili apate fedha za kufanyia biashara, kujenga nyumba za kifahari au kulalia katika mto (takia) au mfaliso. Wanasema kwa kejeli, “Yule alikuwa mjinga kama Nyerere kaka yake, au alimwogopa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo katika mazingira haya, Kawawa aweza kusahaulika haraka. Hapana. Tuseme  ukweli. Aliishasahaulika. Jina lake limerejeshwa na kifo chake; misururu ya kumuaga, kumzika na kutandaza unafiki wa kisiasa wa kutoa sifa kemkem kwa mtu ambaye uwezekano wake wa kuwakemea haupo tena.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na atafutika haraka kweli. Hii ni kwa sababu Kawawa hakuandika vitabu. Hotuba zake hazikuhifadhiwa na kutungwa uzi na kuwa vitabu. Hakuandikwa sana na kufanyiwa utafiti kama  Nyerere. Yeye hakuandika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Juhudi za msomi mmoja ambaye hivi karibuni alitembelewa na busara za kuandika kitabu juu ya Kawawa, ni miongoni mwa watu wachache sana ambao wamehifadhi tunda la kichwa na mikono ya Kawawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vinginevyo, Kawawa alikuwa mtekelezaji zaidi kuliko mwana-nadharia. Nyerere, ambaye aliamini na kuheshimu akiishasema, basi. Fikra au agizo linalotoka katika kichwa kinachoaminika kuwa sahihi, linapaswa kutekelezwa kuliko kufanyiwa porojo. Huyo ndiye Kawawa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kawawa hakuzalisha mawazo kwa njia ya nadharia. Alitenda. Alitekeleza kilichoamuliwa. Hakuwa na nia, sababu wala muda wa kurudia miito. Vyombo vya habari vilinukuu amri zake. Havikumchabua. Ama viliogopa, hasa wakati wa mfumo wa chama kimoja; au vilikuwa na ukame wa waandishi wenye upeo mkubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuishia kudonoa na, au kuchambua maamuzi, sera, kanuni na taratibu; bila kujadili, kuchambua na kutafiti vitendo vya Kawawa, kumefanya mwanasiasa muhimu katika Tanzania kuwa na ukame wa fikra. Kumbe wenye ukame ni wale walioshindwa kutafsiri utendaji wake na kuupa nadharia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rashid Mfaume Kawawa hakutaka mjadala juu ya kilichoamuliwa. Alitaka utekelezaji. Hata pale Mwalimu Nyerere alipoonyesha kutoelewa au kutoafikiana na jambo fulani, yeye alikuwa wa kwanza kutenda, kwa njia ya kurekebisha, ili lifanane na Mwalimu alivyotaka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika nyakati za mfumo wa chama kimoja na magazeti mawili – la serikali na la chama (TANU), ambako watawala walikuwa wakitumia kauli, “kama nchi tumeamua;” Kawawa, kama wanasiasa wengine, alisema chochote alichokuwa nacho huku akijiaminisha kuwa “vijana wetu” – waandishi wa habari – “watayaweka sawa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni nyakati hizo waandishi wa habari walitakiwa kujua viongozi wanataka kusema nini. Hata pale walipokosea kuelezea sera au siasa za nchi, mwandishi alitakiwa kuwa makini na kufafanua, kana kwamba ni yeye aliyekuwa anahutubia, msimamo na utashi wa serikali na kuweka wazi kuwa ndiyo hayo yaliyoelezwa na kiongozi, au Kawawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mifano hii. Nyerere aliongelea unyonyaji unaofanywa na wenye maduka na kueleza kuwa hali ingekuwa tofauti iwapo kungekuwa na maduka ya ujirani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Palepale Kawawa alianza kwa kuamuru maduka ya watu binafsi yafungwe kwa kuwa yalikuwa ya “kinyonyaji.” Nchi ilitikisika chini ya kilichoitwa “Operesheni Maduka.” Bidhaa zikakosekana karibu na walipo wananchi. Haraka ya kutenda ambayo ilikuwa sura kamili ya Rashid Mfaume Kawawa. Ilichukua muda kurekebisha hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfano wa pili. Waliokuwepo watakumbuka Kawawa alivyoamuru Umoja wa Vijana wa TANU kusimamia operesheni ya kuvaa nguo za heshima. Vijana wa kike waliovaa nguo fupi walikamatwa na baadhi yao kushikiliwa katika mazingira ya kutatabishwa yaliyoitwa “udhalilishaji.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama siyo Nyerere kuingilia kati na kusema mavazi ni “fasheni tu” – zinakuja na kupotea, maisha mijini, na hasa Dar es Salaam, yalikuwa yameanza kuwa magumu kwa vijana wa kike. Lakini ni utekelezaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mfano mwingine wa kuhamia vijijini. Kawawa akiwa mtendaji mkuu, alitaka kila mmoja ahamie kwenye vijiji vilivyopimwa na alisisitiza sera hiyo kama ilivyoelezwa, kufafanuliwa na kuelekezwa na TANU na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninajua vema kilichotendeka. Nilikuwa mwandishi niliyeshuhudia uhamishaji katika wilaya ya Kahama. Nyumba na maboma ya mifugo vilichomwa moto. Mifugo ilisambaa. Watu walisombwa kwa malori hadi “vijiji vilivyoandaliwa” ambako hakukuwa na nyumba bali kusanyiko la wengine waliosombwa kama mizigo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukiwa katika ziara na Mwalimu Nyerere, mikoani Shinyanga na Mwanza, wananchi walijitokeza na kumwambia Mwalimu kuwa walitoka kwenye neema na kupelekwa kwenye majuto. Mzee mmoja aliyesimamisha msafara wa rais alisema, “Kuku wangu akitoka nje, tayari ameingia kwa jirani; sasa hapa ni kijiji kweli. Tunaishi kwa kugombana.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata matatizo ya kuku, maji, nyumba alitwishwa Kawawa. Wakati Nyerere aliyezalisha mawazo alibaki shujaa wa kufikiri, msimamizi wa utekelezaji alivuna lawama na laana: Rashid Mfaume Kawawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Karibu sera zote za TANU na baadaye CCM, zilizojaa fikra fikirishi – kuanzia Azimio la Arusha – hazikuwa na mipango mkakati wala mipango ya utekelezaji. Ndiyo maana hata sera nzuri kama “Elimu ya Kujitegemea” ilikosa mwelekeo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 20 baada ya Azimio la Arusha, kwenye kongamano la walimu wa siasa katika vyuo vya TANU, lililofanyika Chuo cha Kivukoni, Dar es Salaam, walimu walipoombwa kutoa maana ya elimu ya kujitegemea zilitokea tafsiri saba (7). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Walitofautiana juu ya utekelezaji kwa vile hawakuwa na mpango mkakati wala mpango wa utekelezaji. Yote haya alilundikiwa Kawawa. Mwalimu alifikiri, Kawawa alisimamia utekelezaji na kuvuna lawama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini Kawawa, kama Mwalimu Nyerere hawakukimbia matunda ya kazi zao. Nyerere ndiye alianzisha utaratibu wa kukiri makosa, hata kabla hajaulizwa, na kupendekeza masahihisho. Kwa njia hii alimnusuru “mpiganaji mwenzake” mara nyingi kabla hajalaumiwa, kushutumiwa na kulaaniwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini Kawawa anakumbukwa kwa kile wengi wanaita “uaminifu.” Historia haionyeshi mahali popote ambapo Kawawa alionyesha jeuri kwa Nyerere; kupingana naye waziwazi au kumhujumu. Inaonyesha tumshikamano, kukubaliana na kutenda “bila swali.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ulikuwa woga au utii? Kuna majibu mengi kwa swali hili. Lakini kinachoonekana wazi na haraka ni kwamba kulikuwa na mshikamano wa kikomredi, kati ya Nyerere na Kawawa – kila mmoja akisema na kuapa kuwa “tunachofanya ni kitu chetu hadi mwisho.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa Kawawa hayupo nasi tena. Alazwe mahali pema anapostahili. Katika hili hatuna uamuzi. Bali kwa nini tusimkumbuke kwa haya machache – ujasiri wa kutenda hata pasipo na mpango kazi; urafiki na ukomredi usio na unafiki; na kutopenda makuu. Hivi havijafa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-6487128183655386625?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/6487128183655386625/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=6487128183655386625' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6487128183655386625'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6487128183655386625'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/05/kawawa-na-usimba-wake.html' title='KAWAWA NA &apos;USIMBA&apos; WAKE'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-3556280560275334455</id><published>2010-05-21T01:54:00.000-07:00</published><updated>2010-05-21T02:00:04.475-07:00</updated><title type='text'>SERIKALI NA SHERIA ZA KISHETANI</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/S_ZLPbpQK5I/AAAAAAAAAGc/xXvLwDC8sGc/s1600/MKUCHIKA.JPG"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 235px; height: 300px;" src="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/S_ZLPbpQK5I/AAAAAAAAAGc/xXvLwDC8sGc/s320/MKUCHIKA.JPG" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5473645125606321042" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI             &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Sheria ya kishetani ya Waziri Mkuchika&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kuamini kwamba Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika anafanya kazi ya serikali. Hii ni kwa kuwa serikali nzima haiwezi kuwa na fikra finyu kiasi hiki. Haiwezekani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ijumaa iliyopita Mkuchika alitangaza kufungia gazeti la KuliKoni kwa siku 90. Waziri anadai gazeti limekiuka Sheria ya Usalama wa Taifa kwa kuandika “habari za jeshi.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri anasema “kosa” lilitendeka 27 Novemba 2009 pale gazeti lilipoandika juu ya kuvuja kwa mitihani ya jeshi na kuwepo  uwezekano wa upendeleo kwa wasiostahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkuchika, kama Sheria ya Magazeti ya 1976 inavyosema, ana mahakama yake binafsi. Iko akilini mwake. Iko mikononi mwake. Iko mdomoni mwake. Anatamka kuwa habari iliyoandikwa na KuliKoni “ni ya uwongo.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushetani wa Sheria ya Magazeti ni kwamba inasema anachosema waziri ndicho. Sheria iliyotungwa na binadamu mwenye kasoro na walakini kadha wa kadhaa, inampa waziri mamlaka ya kuumba na kuumbua, bila kupitia mahakamani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa Mkuchika anasema gazeti limesema uwongo. Hiyo ni katika mahakama ya akilini mwake kama alivyopewa mamlaka na sheria ya magazeti ambayo inamruhusu pia kufungia na hata kufuta gazeti bila kutoa sababu yoyote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna nchi ambako serikali zinaweza kuja na kupita na wakati huohuo kujiviringisha katika mazingaombwe na kuyarithisha kwa serikali zinazofuata, basi ni Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani kuwa na sheria ambayo inampa waziri uwezo wa kuamua anavyotaka, ni kufanya taifa kuwa la wanasesere wanaochezeshwa kwa vidolegumba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukweli ni kwamba wengine – sisi – siyo wansesere. Hata kabla ya Tume ya Jaji Nyalali (1992) tulikuwa tumepaza sauti na kusema Sheria ya Magazeti ni ya kishetani; ni ya kishenzi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ripoti ya Tume ya Nyalali ilipokuja, ikaleta hoja kuwa sheria hiyo ama ifutwe au ifanyiwe marekebisho makubwa. Watawala wamekaa kimya. Wanaipenda. Wanaipakata. Wanampa Mkuchika aitumie atakavyo. Mkuchika anataka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiona watawala wanapenda sana sheria chafu, ujue kuwa roho, nia na shabaha  zao ni chafu. Huwezi kulinda chema kwa kutumia sheria chafu. Huwezi kulinda kitakatifu kwa kutumia sheria ya kishetani. Utatumia sheria chafu kulinda kichafu. Huo ndio muwafaka. Mkuchika anataka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sisi, katika tasnia ya habari, tulianza kupaza zaidi sauti za kutaka sheria ya magazeti ifutwe tangu zaidi ya miaka 30 iliyopita. Ushahidi upo. Kila tulipopaza sauti ndivyo watawala walivyoweka sheria hiyo mbelekoni; kipenzi chao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo KuliKoni imekumbwa na mkasa ulioikumba MwanaHALISI. Imefungiwa na Mkuchika kwa siku 90 kwa uamuzi wa waziri asiyependa kwenda mahakamani wala asiyeshawishi wahusika kwenda Baraza la Habari Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;KuliKoni imekumbwa na sheria inayoruhusu waziri kutumia utashi binafsi, mapenzi, chuki na hata husuda kufungia gazeti – mdomo wa umma. Mkuchika anataka sana. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkuchika anasema amelalamikiwa na jeshi. Jeshi lina uwezo wa kwenda kwenye Baraza la Habari na kulalamika. Jeshi linaweza pia kwenda mahakamani. Kwani jeshi ni nini kama siyo Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa? Waweza kulalamika popote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri Mkuchika hataki jeshi lihangaike. Hataki hata jeshi liunde Tume ya kuchunguza kama lilivyopendekezewa. Anakaa kitini na kusema gazeti limesema uwongo kwa kuwa sheria inamruhusu kuumba na kuumbua. Mkuchika anataka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa ya gazeti, inayosema mfumo wa utungaji na ufanyaji mitihani ya kijeshi unawapa nafasi maofisa wasiostahili, inawezaje kuwa kitu cha kubomoa “usalama wa taifa?” Tangu lini usalama wa taifa umekuwa mweroro kiasi hicho?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Gazeti limetoka leo na malalamiko ya wahusika yanatoka siku hiyohiyo, hata kabla ya kuulizia wala kufanya uchunguzi. Kanusho la aina hiyo lina uzito gani? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msajili ya Magazeti ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari Tanzania (MAELEZO). Huyu anaamuru tu: “Jieleze kwa nini usichukuliwe hatua.” Basi. Yeye hafanyi uchunguzi angalu kupata mwanga na kusaidia walalamikaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anaposema hakuridhika na kauli au majibu uliyotoa, ina maana kuwa ni suala la binafsi linalotokana na kutojua kinachoendelea au ni la kushinikizwa na aliyemlalamikia au woga tu kwamba jeshi limetajwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira haya, waziri anadai kuwa taarifa ya gazeti imefedhehesha “jeshi letu na kulipaka matope.” Mkuchika amepata wapi fedheha? Amepata wapi matope wakati hata aliyelalamika hajaweka ushahidi wake hadharani mbele ya chombo chenye hadhi ya kutoa maamuzi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata katika suala la kujieleza; waziri anataka maelezo yenye ushahidi ili ayatumie wapi wakati yeye hafanyi uchunguzi wala hana chombo cha haki cha kutoa maamuzi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Gazeti la MwanaHALISI bado lina kesi na serikali inayotokana na hatua ya Mkuchika kulifungia kwa siku 90 bila sababu ya msingi. Hapana, ni zaidi ya hapo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna kesi mahakamani, inayotafuta kufutwa kwa sheria ya magazeti. Haijaamuliwa. Ilichochewa na kufungiwa kwa MwanaHALISI na ndio walalamikaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kabla kesi hiyo haijatolewa maamuzi, Mkuchika anaendeleza ubabe wake. Anaita taarifa za gazeti juu ya mitihani ya jeshi kuwa ni za “uchochezi” na analifungia kwa siku 90. Wako wapi wanasheria wa KuliKoni?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huyo ndiye Mkuchika chini ya mwavuli wa serikali. Sheria ipo. Watawala wanaipenda. Mawaziri wanaoteuliwa huipenda, kuitii na kuinyenyekea kwa kuwa tatizo lao kuu ni “mlo.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hajapatikana waziri wa kukataa kutumia na kutumikia sheria chafu; angekuwa ametoa funzo. Hajapatikana wa kuasi utumwa wa sheria hii kwa kuwa wengi wanatafuta mlo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huwezi kutumikia umma ambao umeufunga mdomo. Basi huutumikii bali unausulubu katika utumwa wa mawazo na hatimaye katika vitendo. Utapataje mawazo yake? Utapataje malalamiko yake? Utapataje ushauri wake?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni heshima na halali, kwa waziri, msajili wa magazeti, maofisa wa habari serikalini, waandishi wa habari, wadau wengine wa habari na wananchi, kuasi sheria katili.&lt;br /&gt;Kwa pamoja tunaweza kuvunja mikatale hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713-614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-3556280560275334455?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/3556280560275334455/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=3556280560275334455' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3556280560275334455'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3556280560275334455'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/05/serikali-na-sheria-za-kishetani.html' title='SERIKALI NA SHERIA ZA KISHETANI'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/S_ZLPbpQK5I/AAAAAAAAAGc/xXvLwDC8sGc/s72-c/MKUCHIKA.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-6894208771395095558</id><published>2010-05-21T01:43:00.000-07:00</published><updated>2010-05-21T01:46:17.488-07:00</updated><title type='text'>HAKUNA ADHABU YA KIFO: MUUAJI NI MUUAJI KAMA YULE WA KWANZA</title><content type='html'>SITAKI       &lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Kunyonga siyo adhabu, ni kuua tu&lt;br /&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;SITAKI kuona wananchi na watawala wakishabikia hukumu ya kunyonga, hata kama kuna sheria ya nchi inayoruhusu mtu “kunyongwa hadi kufa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria iliyopo ni katili, chovu, inayopaliliwa na kuendelea kurutubishwa na mfumo unaoendeshwa na watu ambao wamekuwa wagumu kuelewa mantiki ya thamani ya maisha na umuhimu wa adhabu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iwapo hawatakata rufaa, au wakikata rufaa na kushindwa, Masumbuko Madata, Emmanuel Masangwa na Charles Kalamuji, waweza kuuawa kutokana na hukumu iliyotolewa na Jaji Gabriel Rwakibalila.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jumatano iliyopita, mjini Kahama, Jaji Rwakibalila aliwakuta vijana hao watatu na hatia ya jinai ya kuua Masumbuko Dunia, mtoto wa shule, umri wa miaka 13 na mwenye ulemavu wa ngozi (albino). Sasa kuna wanaoshangilia hukumu ya kifo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifo cha Masumbuko kiliuma na kuumiza wengi, hata kama hawakuwa na uhusiano wowote naye. Umri wake mdogo; nafasi yake katika jamii iliyosababisha kuitwa majina ya kumtelekeza; utu wake ambao ulikuwa na bado ni sehemu ya utu wa kila mtu; ni sehemu tu ya chimbuko la uchungu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uchungu unakuwa mkubwa pale jamii inaposhuhudia mauaji yakilenga watu wenye ulemavu wa ngozi; wadogo kwa wakubwa, kwa sababu dhaifu, za kijinga na potofu – eti kupata viungo vya kuwawezesha “kuwa matajiri.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uchungu huu usio na udhibiti, unapokutana na sheria ambayo hata Jaji Mkuu Augustino Ramadhani amewahi kusema kuwa hafurahii kuitumia, ndipo unazaliwa ukatili mpya; ule wa kuondoa uhai wa aliyepatikana na hatia ya kuua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mahakama Kuu nchini Tanzania iliishawahi kutamka kuwa adhabu ya kifo ni ya kikatili na ya kudhalilisha na kutaka ifutwe. Pamoja na maeneo mengine, maneno “katili” na “kudhalilisha” ni ya msingi sana katika kuchambua hukumu ya kifo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katiba ya Jamhuri ya Muungano inakataza ukatili na udhalilishaji. Kwa hiyo kuwepo sheria inayoruhusu kuua; hivyo kuendesha “ukatili” na “udhalilishaji,”  ni kuvunja katiba ya nchi. Lakini Mahakama ya Rufaa haikuafiki. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna ubishi kwamba vijana watatu wa Kahama, kwa kupatikana na hatia ya kumuua Masumbuko, walivunja haki za binadamu. Bali “haki za binadamu” haziwekwi na watu; zipo na zinahusu kila mmoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watawala, sheria na hata Katiba za nchi, haziweki haki za binadamu. Ngazi zote hizo hazina uwezo wa “kugawia” watu haki za binadamu. Kinachofanyika ni kwa watawala, sheria na Katiba kutambua kuwepo kwa haki hizo na kutafuta jinsi ya kuzilinda na kuziendeleza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, hapa siyo mahali pa hoja za jino kwa jino. Hoja ni kutovunja haki za binadamu. Kutoua. Kutofanya ukatili. Kutodhalilisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja hii inaleta maana zaidi pale tunapojadili “thamani” ya adhabu anayopewa mkosaji. Watatu wa Kahama wamepatikana na hatia. Wamevunja haki za binadamu kwa kumuua Masumbuko. Wanastahili adhabu na ikiwezekana iwe adhabu kali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tujiulize. Je, hukumu inayoruhusu kifo ni adhabu? Je, kifo kinaweza kuwa adhabu? Je, adhabu hufanywa na aliyekufa? Kama sababu ya kuadhibu ni kutaka mtu ajirudi na kurejea katika utu wa jamii yake je, aliyeuawa anajirudi vipi, lini na wapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hizi zinaonekana hoja ndogo kwa waliovimba vichwa na vifua, kwa hasira na uchungu wa kweli wa kupoteza watoto, ndugu, jamaa, rafiki au wenzao katika tabaka au kundi tambulishi kama walivyo albino.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali hasira zilizokaba koo za wafiwa; chuki zilizotunisha misuli ya shingo za ndugu wa aliyeuawa; na woga uliokumba nyoyo za wahusika; vyote vinaziba mifereji ya fikra kuhusu uhai wa mtu mwingine na nafasi ya muuaji mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vijana watatu wamepatikana na hatia ya kuua. Sheria inaruhusu wauaji kuuawa. Jaji, kwa mujibu wa sheria hajakosea kutamka hukumu hiyo kwa shabaha ya kulinda sheria na kazi yake. Bali Jaji aweza kuwa anaasi “shangazi wa mtima” wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majaji wengi duniani wameeleza jinsi wanavyosutwa na dhamira zao pale wanapotamka hukumu ya kifo. Wameeleza jinsi kunavyokuwa na mapambano makali “rohoni” mwao na hatimaye kuanguka na kuwa mateka wa sheria na mfumo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo kuna vijana watatu wa Kahama. Wanakabiliwa na mauti na siyo adhabu. Atakayeua vijana hao ni nani kama siyo muuaji? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna tofauti gani kati ya aliyeua albino kwa panga na anayeua muuaji wa albino kwa kamba ya shingoni? Haipo. Wote ni wauaji. Mmoja anakanwa na sheria na mwingine anaruhusiwa na sheria. Wote wanatoa uhai wa watu wenye thamani ileile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninaelewa ugumu wa wafiwa kuzingatia hoja hii haraka. Lakini malezi ya jamii hayawezi kwenda kwa misingi ya walioko madarakani kujipa fursa ya kuua na kujikinga na sheria walizotunga wenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niliishawahi kuuliza katika safu hii wakati wa kujadili somo hilihili: “Kama serikali inaua, nani ataua serikali – ambayo sasa ni muuaji?” Sikupewa majibu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna haja ya kufikiri upya kuhusu sheria inayoruhusu kunyonga watu. Kunyonga ni kuangamiza maisha; siyo adhabu ya kurejesha mtu kwenye mstari wa maandili na utu wa wote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kunyonga ni kunyima aliyepatikana na hatia fursa ya mabadiliko katika maisha. Ni mabadiliko haya ambayo huweza kuwa mfano mkuu kwa jamii na kufanya watu wengi kukiri udhaifu wao na kuwa wanyoofu maishani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuua hakuleti nafuu kwa mfiwa. Hakuna mafao kwa serikali. Hakuleti faida kwa jamii. Kunaendeleza vilio. Kunasimika hasira na chuki mpya. Kunafanya jamii ishindwe kuelewa nani anaweza kuikinga na ukatili huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria zinazoruhusu mauaji kwa njia ya kunyonga ni za kuviziana; za kumalizana na mara nyingi, kama siyo mara zote, zinawaelemea wa tabaka la chini katika jamii. “Wakubwa” wana kila njia ya kuzipinda na hata kuzikatakata.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria za kunyonga zinafanya jamii ianze kuona kuwa maisha hayana thamani. Zinafundisha usugu na kutothamini uhai binafsi na ule wa mtu mwingine. Zinazaa tabia ya “nitakuua hata kama wataniua.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria zinazoruhusu mauaji zinakomaza chuki na ghadhabu na zinafuta msamaha na tabia ya kujirudi ambayo ni nguzo kuu katika kupata suluhisho na muwafaka. Zinainyang’anya jamii ujasiri wa kufunza waliopogoka na kuikosesha jukumu la kufunza vizazi na vizazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Adhabu ilenge kurekebisha muhusika; kumfanya ajutie tendo lake na kutamani kurejea katika utu wake wa asili. Aliyekufa hajutii makosa yake; harekebiki pia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Natamani kuona hukumu ya kifo ikifutwa na nafasi yake kwa sasa kichukuliwa na adhabu ya kifungo cha maisha. Aliyeua akiuawa, aliyeua muuaji anakuwa amekamilisha ukoo wa wauaji. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika ukoo huu, mauaji hayataisha. Hayataogopwa. Hayatapingwa kwa kuwa hayatachukiwa. Natamani yaishe. Jamii ivunje kimya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-6894208771395095558?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/6894208771395095558/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=6894208771395095558' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6894208771395095558'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6894208771395095558'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/05/hakuna-adhabu-ya-kifo-muuaji-ni-muuaji.html' title='HAKUNA ADHABU YA KIFO: MUUAJI NI MUUAJI KAMA YULE WA KWANZA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-1492575217035552940</id><published>2010-05-21T01:40:00.000-07:00</published><updated>2010-05-21T01:42:15.706-07:00</updated><title type='text'>POLISI NA MAUAJI YA SHELABELA YA WATUHUMIWA</title><content type='html'>SITAKI              Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Polisi wanaoua vyanzo vya taarifa&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI mauaji ya kila siku. Kila wiki. Kila mwezi na wauaji wakiondoka tu bila kukamatwa. Bila kuhojiwa. Bila kusutwa. Bila kukemewa. Bila kuchunguzwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ndiyo wanaita tuumachi! Polisi wanachukua bunduki. Wanaangamiza roho ya mtu mmoja, wa pili, wa tatu, wa nne, wa tano. Wanakunja sime. Wanaondoka. Nisikilizie: Tumeua majambazi. Halafu? Kimya. Utadhani hakuna kilichotokea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa za magazeti zimeeleza kuwa saa nane na nusu mchana; kweupe kabisa kwa tarehe 29 Novemba – wiki iliyopita tu – watu watano waliuawa katika kijiji cha Park Nyigoti wilayani Serengeti, katika mkoa wa Mara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Eti polisi wakishirikiana na askari wa hifadhi ya mbuga ya Serengeti, waliwapiga risasi na kuwaua watu watano “wanaosadikiwa kuwa majambazi.” Ama walipiga mmojammoja au kwa risasi zilizotoka kwa mpigo; waliwateketeza wote fyuu!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kawaida, polisi wakaondoka tu bila kujikamata. Bila kujihoji. Bila kujisuta. Bila kujikemea. Bila kujichunguza. Lakini pia bila kuhojiwa, kusutwa, kukemewa wala kuchunguzwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ilikuwa 19 Novemba, wiki mbili na nusu zilizopita, watu sita waliuawa na polisi mkoani Dodoma. Hao pia “walisadikiwa kuwa majambazi.” Gun! Gun! Gun! Hadi sita. Polisi wakaondoka. Hawakujikamata, hawakujihoji, hawakujisuta wala kujichunguza. Vijana wanasema “imetoka hiyooo!”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama unataka maelezo juu ya ilivyotokea, sharti uwe unajua lugha na mwepesi wa kuchambua. Maneno yanayotumika ni istilahi maalum ya kipolisi: “Waliuawa wakati wa kujibizana kwa silaha na polisi.” Hayo ndiyo mazingira ambamo wanakufa wale wanaoshukiwa, wanaodhaniwa na, au wanaosadikiwa kuwa majambazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku sita baadaye, ilikuwa 25 Novemba, polisi waliripotiwa kuua kwa kupiga risasi, “majambazi” sita huko Biharamulo mkoani Kagera. Gun! Gun! Gun! Wote sita, chini. Taarifa zinasema walikutwa na silaha za moto.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kawaida, hakuna polisi aliyekamata polisi kwa kuua. Hakuna aliyemhoji mwenzake. Hakuna aliyemsuta mwenzie. Hakuna mwenye nia ya kumchunguza mwenzake. Kimya. Utadhani umo kwenye tumbo la papa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumekuwa na taarifa za kutupiana risasi, kati ya polisi na “majambazi” lakini kama ilivyo kwa sinema za Chuck Norris, mara zote hizi polisi ndio washindi – hawafi na kama wameumia sana, basi ni michubuko. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtindo huu wa polisi kuua “majambazi” au “wanaosadikiwa” kuwa majambazi au “wanaoshukiwa” kuwa majambazi hautalifikisha taifa hili popote katika vita dhidi ya ujambazi. Hatimaye polisi wataitwa wauaji tu. Ikitokea hivyo, hawataweza kujitetea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Polisi aliyekabidhiwa bunduki ni yule aliyejifunza jinsi ya kuitumia kitaalam. Anapotumwa kwenye kazi ya kusaka majambazi, haendi au hapaswi kwenda kwa nia moja tu; kuua. Hapana. Kuna mambo mengi yanatarajiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Polisi amefunzwa kulenga shabaha. Amefunzwa jinsi ya kutokuwa na kiwewe na harara katika mazingira ya “uwindaji” wa aina hiyo. Amefunzwa jinsi ya kurudi na ushahidi unaoongea ambao ni muhimu sana kwa mipango na operesheni za baadaye. Polisi hapelekwi tu kuua na kurejea na maiti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tena wajuzi wa kutumia silaha – wale wenye shabaha ya kuonea wivu – ndio wanahitajika sana; siyo kwa kupasua ubongo au moyo; bali kwa kupiga mguuni na takoni ili waweze kulegeza muhusika, kumkamata na kumhoji kwa manufaa ya kazi zao za baadaye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kweli polisi waliotumwa kazi waweza kujaa kiwewe na woga uliopindukia na kuanza kufyatua risasi hata bila kutumia utaalam waliopata vyuoni. Ni kutokana na uwezekano huo kunakuwa na haja ya kutaka kujua jinsi operesheni zinavyoendeshwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndio maana hata kwa upande wa polisi kuna haja ya kuulizana: Mbona mmeua wote? Mbona hamkuleta hata mateka mmoja? Mazingira yalikuwa vipi hadi mkaishia kuua tu? Ndio maana kuna haja ya kujikamata, kujihoji, kujisuta, kujikemea, kujichunguza na hata kujiadhibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi ni kweli kwamba polisi wa Tanzania wanatumwa kuua tu? Hawataki mateka? Kama hawarudi na mateka watapata vipi taarifa za majambazi au wanaotuhumiwa kufanya ujambazi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Gun! Gun! Gun! Watu 17 katika siku 20; ambao ni wastani wa kuua mtu mmopja kila siku; hakika hii haiwezi kuwa kazi bora ya polisi na hata ikilazimishwa kuwa, haiwezi kuwa na tija. Hii ni kwa kuwa hakuna maghala ya majambazi kiasi cha kufikiri kuwa jinsi wanavyouawa, ndivyo wanavyopungua katika maghala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uhalifu unamea katika ngazi mbalimbali katika jamii kwa vishawishi na motisha kadha wa kadhaa. Hapa umekomaa na kuwa wa matumizi ya kalamu ndani ya mabenki na serikali; pale umekomaa na kuwa wa matumizi ya silaha; pengine bado haujafumuka na labda kwingine ungali unasuasua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, kuua raia kwa kuwa umemshuku au kwa kuwa amekutwa na silaha, hakusaidii polisi wala serikali. Moja ya kazi kubwa za heshima ambazo zinapaswa kufanywa na polisi, ni upelelezi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupeleleza kunahitaji vyanzo vya taarifa. Vyanzo vizuri vya taarifa, hata kama itabidi taarifa hizo kuchambuliwa kwa makini sana, ni mateka na siyo wafu. Ukiua vyanzo vya taarifa na kurudi unajipiga kifua, utashindwa kumaliza uhalifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuua kunaweza kuwa na shabaha nyingine. Shabaha ya kuficha ushahidi muhimu. Ili waliouawa wasijulikane wana uhusiano na nani katika polisi, katika biashara au katika utawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mauaji yakiendelea kwa miaka mingi yanakuwa njia ya kuondosha watu wasiokubaliana na polisi, watu mashuhuri au serikali. Katika baadhi ya nchi mauaji ya aina hiyo yamewakumba wapinzani wa watawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapo kuua huwa kunazoeleka na yeyote aweza kuokotwa kokote, kupelekwa Serengeti, Ngorongoro au hata Loliondo, kuuawa hukohuko na taarifa zikasambazwa kuwa “alikuwa mmoja wa majangili sita bali wengine aliokuwa nao wamekimbia.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuruhusu polisi kuendelea kuua watuhumiwa wa ujambazi, kunaweza  kuleta madhara zaidi kwa taifa. Kunajenga unyama usiomithilika nyoyoni mwa wauaji na woga miongoni mwa wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kunadumaza utaalam katika idara ya upelelezi ambayo sasa inabakia kutegemea uvumi. Kwani, upelelezi hukomaa zaidi katika mazingira ya uhalifu na huimarisha nyanja mbalimbali za sheria ambako mbongo huchuana na kuweka misingi mipya ya kutafsiri sheria zilizopo na hata kutunga nyingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuendelea kuua watuhumiwa kunaharibu jina, sura na tabia ya nchi na wananchi – kwamba nchi na watu wake wanaitwa wauaji; lakini pia kunajenga mazingira ya kuviziana na hata mafisadi kutumia mwanya huo kuangamiza wasiowaabudu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuua siyo njia bora ya kukabiliana na uhalifu. Hakika kuua kunaweza hata kuchochea uhalifu zaidi. Siku zote polisi waende kukamata, kupata vyanzo vya taarifa vya kuwasaidia katika uchunguzi na baadaye katika hatua za kukabiliana na ujambazi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Penye mfumo mzuri wa matumizi ya polisi, mauaji ya watu watano, watano na baadaye sita, katika siku 20 tu, hayawezi kufumbiwa macho. Kama ndani ya jeshi la polisi na serikali hawaulizani “kulikoni,” basi wananchi wana kila sababu ya kuuliza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-1492575217035552940?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/1492575217035552940/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=1492575217035552940' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1492575217035552940'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1492575217035552940'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/05/polisi-na-mauaji-ya-shelabela-ya.html' title='POLISI NA MAUAJI YA SHELABELA YA WATUHUMIWA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-454534354166682858</id><published>2010-04-23T06:59:00.000-07:00</published><updated>2010-04-23T07:01:20.403-07:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>Kwa miezi mitatu mfululizo, blogu yangu ilikuwa na matatizo ya kupokea makala na stori zangu. Sijajni nini hasa. Leo imekubali. Kesho naanza kazi ya kupakulia humu. Karibu. Edelea kuwa nami katika kujenga hoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;ndimara &lt;br /&gt;32 Aprili 2010&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-454534354166682858?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/454534354166682858/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=454534354166682858' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/454534354166682858'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/454534354166682858'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2010/04/kwa-miezi-mitatu-mfululizo-blogu-yangu.html' title=''/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-4747402304120422664</id><published>2009-11-08T00:03:00.000-08:00</published><updated>2009-11-08T00:18:21.833-08:00</updated><title type='text'>SERIKALI IKIKIRI KUSHINDWA 'IPUMZIKE'</title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SvZ-xaAfkzI/AAAAAAAAAGU/ZBxJV5LyVyQ/s1600-h/kIKWETE.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 122px; height: 124px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SvZ-xaAfkzI/AAAAAAAAAGU/ZBxJV5LyVyQ/s320/kIKWETE.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5401644190337569586" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                    &lt;strong&gt;RAIS APUMZIKIA KARIBU NA MIZOGA YA &lt;br /&gt;                    MIFUGO NA WAKULIMA WENYE NJAA&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;                      &lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;SERIKALI imesema isilaumiwe kwa ukame au vifo vya mifugo nchini. Rais Jakaya Kikwete amesema, "Wapo …wanaoichukia serikali kutokana na ukame; jamani hata sisi tunaomba Mungu hali iwe nzuri…"&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kauli za aina hii ambazo vijana wa mjini hupenda kuita, “funga kazi.” Tatizo la vijana hao ni kwamba hawaoni kuwa kazi haijafanyika. Ukweli ni kwamba hizo ni kauli za mwisho wa mwanzo wa kukata tamaa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tujadili. Kisiasa, kauli ya rais ilitolewa muda na mahali pasipofaa. Ilitolewa katika kijiji cha Olbalbal wilayani Ngorongoro. Taarifa za awali zilikuwa zimeeleza kuwa rais yuko likizo ndogo katika mbuga za wanyama za Ngorongoro.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ngorongoro ni moja ya wilaya ambazo zimekumbwa na ukame wa aina yake. Mifugo inakufa. Mizoga imetapakaa huku na kule. Wafugaji hawana maji. Niliwahi kuandika kuwa hata wao wanaweza kuitwa “mizoga inayotembea.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni huko rais alikwenda kufanya mapumziko. Nasema siyo sahihi kisiasa kwa kuwa rais kaenda “kujinyolosa” baada ya mahangaiko; pale – jirani tu – hata kama kwa umbali wa kilometa 80; lakini ndani ya wilaya hiyohiyo ambamo maafa ndiyo maisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama siyo kwa diplomasia – ule unafiki wa kicheko na mgonganisho wa bilauri za mvinyo huku watu wakiteketea – na hilo hufunzwa vyuoni – basi rais angekemewa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa rais amewahi. Amewaambia wananchi wanaoishi katika wilaya ambamo uoza wa Loliondo umefunika harufu kali ya ubani, kuwa hana la kufanya kuhusu ukame na vifo vya mifugo yao.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwamba wafuge kisasa; kwamba yeye ana ng’ombe 600 lakini hahitaji kuzungukazunguka nao kutafuta malisho; kwamba wajifunze kutoka wafugaji wa Uganda; kwamba hata serikali inaomba mvua zije.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukitaka waweza kuita hayo kuwa ni kejeli. Ukitaka waweza kuita kauli za kutojali kilio cha wafugaji. Ukitaka pia waweza kuita mizaha kwenye msiba. Mkuu wa nchi akisema hayo, wanasiasa wa viwango vya Yusuph Makamba watasema nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uko wapi mpango wa serikali wa kushirikisha wananchi – wafugaji – katika kutatua matatizo yao? Kwa mfano, uongozi wa wilaya au mkoa kukaa na wafugaji; kujadili jinsi ya kuchanga ng’ombe, kuwauza, kupata fedha za kununulia mabomba ili kuvuta maji kutoka mbali. Uko wapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uko wapi mpango wa serikali wa kutafuta vilipo vyanzo vya maji wilaya nzima; kuvilea, kuvihifadhi na kujenga malambo yenye uwezo mkubwa wa kulinda maisha ya mifugo na wafugaji?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna mfano mzuri Uganda, wafugaji wa huko walianza vipi? Walitoka usingizini wakajikuta wameanza kufuga kisasa; au kuna waelekezaji – wataalam wenye moyo wa kutumikia jamii – ambao waliacha umangimeza; wakajitosha kwenye maeneo ya wafugaji na kuanza kushawishi, kufundisha na kuonyesha mifano?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafugaji wa wilaya ya Ngorongoro siyo ombaomba. Hutozwa kodi, yao na ya mifugo. Wanahitaji utaalam wa wale wanaojali na wasiosingizia Mungu kwa kila janga, pamoja na janga la ukame. Wanahitaji uongozi wenye akili na unaowathamini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umbali uliopo kutoka yalipo maji hadi walipo wafugaji na mifugo yao inayokufa, hauzidi kilometa 80. Pengine ni kilometa tano. Pengine kilometa 15. pengine kilometa 40. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vilevile kuna maji yaliyofungiwa na wanaoitwa wawekezaji – wale waliojipa uwezo wa ki-Mungu wa kuamua huyu na mifugo yake hata wafe, potelea mbali, lakini hawawezi kuchota maji kwenye kisima kilichoko wilaya ya Ngorongoro, mkoa wa Arusha, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ushenzi uliopitiliza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanaoitwa viongozi wa wilaya wamefumba au wamefumbwa midomo. Viongozi wa mikoa yenye ukame wamejikinga nyuma ya pazia la “sheria.” Waziri wa mifugo anahangaika kukanusha ukweli usiokanushika. Leo rais anasema hana la kufanya labda kumwomba Mungu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Picha za mizoga ya mifugo – ng’ombe, mbuzi na kondoo, ni ushahidi wa serikali isiyotenda. Sauti za wafugaji, zinazotetereka na kupotelea mbugani bila kusikilizwa na watawala, ni ushahidi wa ukatili unaoendeshwa na wale wanaoishia kutukana, kukejeli na kufukuza wafugaji kutoka makazi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais ana ardhi. Ana maji. Ana fedha za kutunzia bustani za vyakula vya mifugo. Ana fedha za kununulia dawa. Ana maji ya kunywesha mifugo na kumwagilia bustani za vyakula vyake. Ana madaraka – maji hayakatiki. Yakikatika akikohoa yanarudishwa. Haombi Mungu mvua inyeshe ili mifugo isife.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais alipewa ushauri na wataalam. Anakofugia paliandaliwa na wataalam. Panakaguliwa na wataalam; na ng’ombe ni ng’ombe tu; awe wa rais au wa Masaai. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini mfugaji, mwenye elimu ya asili tu ya kujishughulisha na mifugo; kwa mfano kujua dawa za miti shamba za kuiponya na mahali pa kuilaza; anahitaji kufikiwa na mbinu za kisasa ili afuge kama rais au kama Jakaya Kikwete. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafugaji wengine, pamoja na kuishi mbali na miji, na hiyo ni faida kwao, wana ng’ombe wengi kuliko rais. Wengine wana hata zaidi ya 2,000. Kuwapa wananchi hawa wazo la kuchangia kupatikana kwa maji katika maeneo yao, hakuwezi kuwa mzigo. Watahiari. Lakini hakuna uongozi wa kufanya hivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili ni la kuwashirikisha – wao na utajiri wao wa mifugo. Haliwaondolei haki yao ya kufaidi matunda ya kodi walipazo. Hapa ndipo tungetaka kuona watawala wakiwajibika kwa walipakodi na siyo kuwaambia wamwombe Mungu ili mvua inyeshe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dunia nzima inatambua kazi ya kodi na mapato ya nchi kwa ujumla. Mfano wa Libya huwa unanijia mara kwa mara. Ni Kanali Muamar Ghadaffi, kiongozi wa nchi hiyo aliyesukuma maji kwa njia ya mabomba kwa umbali wa zaidi ya kilometa 1,700 ndani ya jangwa la nchi hiyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu wakanywa maji. Wakaonga. Wakafua. Wakatunza bustani ndani ya jangwa. Jangwa likakoma kuwa jangwa pale maji yalipotiririkia. Tanzania hakuna jangwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais Kikwete amekoleza kilio cha wananchi wafugaji wa wilaya ya Ngorongoro. Alikwenda kupumzikia kwao wakati wao hawana mapumziko. Wengi wanalala nje. Wamechomewa nyumba na maboma ya mifugo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais alikwenda kupumzikia kwa wale ambao wanaswagwa na watawala wilayani kwa msaada wa “wageni” waliokabidhiwa vipande vya ardhi ya nchi hii kwa ajili ya kuua raslimali wanyama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kubwa kuliko yote ni kwamba rais amewaambia wakazi wa Ngorongoro kuwa wachague Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika uchaguzi wa serikali za mitaa, kwa kuwa ndicho chenye “uhakika wa kuwaletea maendeleo.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uko wapi uwezo alioahidi rais? Uuliyeyuka palepale aliposema hana uwezo wa kumaliza ukame na kusitisha vifo vya mifugo katika nchi yenye mito mikubwa isiyokauka; maziwa makubwa, marefu, yenye kina kirefu; na maeneo mengi yenye unyevu kunakoweza kuchimbwa mabwawa na malambo kwa ajili ya huduma kwa watu na mifugo yao.&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii ilichapishwa katika gazeti la MwanaHALISI toleo Na. 160 la 28 October 2009)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-4747402304120422664?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/4747402304120422664/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=4747402304120422664' title='5 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/4747402304120422664'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/4747402304120422664'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/11/serikali-ikikiri-kushindwa-ipumzike.html' title='&lt;strong&gt;SERIKALI IKIKIRI KUSHINDWA &apos;IPUMZIKE&apos;&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SvZ-xaAfkzI/AAAAAAAAAGU/ZBxJV5LyVyQ/s72-c/kIKWETE.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>5</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-2589457239507853092</id><published>2009-10-17T01:23:00.000-07:00</published><updated>2009-10-17T01:37:44.016-07:00</updated><title type='text'>KUENZI NYERERE KWA ULEVI, USINGIZI</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/StmBhR8uEQI/AAAAAAAAAGM/e1TKt2SgiNA/s1600-h/Julius+Nyerere.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 103px; height: 137px;" src="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/StmBhR8uEQI/AAAAAAAAAGM/e1TKt2SgiNA/s320/Julius+Nyerere.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5393484437506625794" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;          &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;WANANCHI WANAAMBIWA WALALE NA HUKO WATAMSAHAU &lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                     &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;  Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kumkumbuka Mwalimu Julius Nyerere kwa njia ambayo haifanani kabisa na matendo na fikra zake pale alipokuwa kiongozi wa nchi hii. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kushiriki uchovu wa watawala unaoelekeza taifa kuwa kumkumbuka Mwalimu ni kuwa na siku ya mapumziko; siku ya kulala na kukoroma. Wengine wanaongeza hapo: kula na kuvimbiwa na kunywa na kulewa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyerere aliyemaliza zaidi ya wiki mbili akichimba mtaro wa mabomba ya maji wa Ntomoko, mkoani Dodoma, hawezi kukumbukwa kwa usingizi wa pono unaotokana na ulevi wa siku nzima isiyo na shughuli ya maana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa kuna Nyerere aliyemaliza wiki nzima katika kijiji cha Muyama, wilayani Kasulu, mkoa wa Kigoma akijenga nyumba za wanakijiji. Tulikamilisha nyumba 15. Huwezi kukumbuka kiongozi wa aina hii kwa kile watawala wa sasa wanaita “mapumziko.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwenyekiti wa kijiji atakwenda kwa Nyerere na kumwambia, “Mwalimu, unaona jua limekwenda; afadhali upumzike.” Nyerere atamwangalia kwa sekunde kadhaa, kumtolea macho na hatimaye kumwambia huku akicheka; kile kicheko chake cha mpasuko:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Hah, ha, ha! Mwenyekiti, hayo si maneno yako. Umetumwa na wale paleee. Watu wa mjini wale. Naona vitambi vyao vinaanza kuporomoka. Hapana. Siyo maneno yako. Mwenyekiti, siyo maneno yako. Njoo tufanye kazi.” Ataendelea kufanya kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyerere mchapakazi; aliye karibu na wananchi, hastahili kukumbukwa kwa kulala, kuamka, kula, kunywa, kulewa na kulala. Hapana. Nyerere asiyepumzika anaenziwa kwa mapumziko; tena ya nchi nzima? Kama siyo kejeli ni kashfa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuanzia saa 12 au saa moja asubuhi, Nyerere anakata mbuga na viongozi akikagua “miradi ya maendeleo,” ya kweli na uwongo. Hapa anakuta usiku wa kuamkia siku anayofika, ndipo wamesimika miche ya kabichi udongoni. Wanamwambia, “Mzee tunajitahidi kutekeleza siasa ya kujitegemea.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunazunguka bustani. Anaona. Hatimaye anachukua kifimbo chake na kusukuma mche mmoja, unaanguka. Anasukuma wa pili, unaanguka. Anasukuma wa tatu, unaanguka. Anasonya na kuondoka. Ataongea na viongozi wa wilaya au mkoa baadaye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni mwenye kutambua haraka. Ni mwenye kutonywa haraka na wale wanaomwamini. Ni mwepesi wa kusikia kilichonong’onwa na kuuliza, “Kuna nini? Maana yake nini?” Huyo ndiye taifa linaongozwa kukumbuka kwa usingizi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Twende kwenye chumba cha mkutano. Harufu. Ni harufu ya rangi iliyopakwa jana. Mwalimu anashika pua. Anaifinyanga. Anatoa kitambaa mfukoni; anaipangusapangusa kama anayetaka kupiga chafya. Anarudisha kitambaa mfukoni na kusema, “Hata kupiga rangi ni mpaka niwe ninakuja hapa?” Meseji delivadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anafundisha kila aendapo. Anasema mkoa wa Shinyanga umezidi kwa ukame; sasa unageuka jangwa. Anaagiza wapande miti. Mkuu wa mkoa katika mkutano wa viongozi anasimama na kusema, “Mheshimiwa rais, tunaomba mradi wa kupanda miti  uwe wa kitaifa.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyerere anag’aka, “Nasema Shinyanga inageuka jangwa. Panda miti.” Lakini angalia Nyerere katika kijiji cha Mwamihanza ambako anaambiwa kuwa mzeee mmoja analima bangi. “Mimi, mimi sina tatizo kana hafanyi biashara. Wengine wanatumia majani hayo kwa dawa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anawafikia wananchi wengi. Anatumia muda mwingi ndani ya nchi yake. Anasikiliza na kusikia matatizo mengi. Mwaka 2005, baadhi ya wafugaji waliokutwa Msata, mkoani Pwani, walipoulizwa wanataka kumpigia nani kura, kila mmoja alisema, “Nyerere.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyerere huyo bado amegota vichwani mwao. Hakuwaibia wala kuwaswaga kama mifugo kutoka kwenye makazi yao. Leo wanahitaji njia bora ya kumuenzi mchapakazi. Siyo kupumzika. Siyo kulala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyerere mwenye ujasiri wa kutunga maadili ya uongozi kwa viongozi – watu wazima na siyo watoto wa shule, akilenga uadilifu katika utawala; kiongozi wa kutangaza Azimio la Arusha na kutaifisha mashamba, majumba na mabenki, kwa nia njema kwa kadri ya uelewa wake na nia yake; leo anakumbukwa kwa kupiga usingizi? Ama ni mzaha au kashfa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais aliyepeleka nchi vitani na ikarudi na ushindi – kwa sababu zozote zile za kuwepo kwa vita dhidi ya dikiteta Idi Amin Dada wa Uganda; aliyekuwa jemedari wa vita vya ukombozi Kusini mwa Afrika akifundisha wananchi kujitolea damu na uhai wao; akumbukwe kwa kula, kunywa na kulala?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiongozi wa nchi ambaye wakati wake elimu ya watu wazima ilifikia kiwango cha asilimia 90; aliyethamini elimu na aliyesoma wakati wote hata baada ya siku nzima ya kuongea na wakulima, kufokoeana na wataalamu wa kilimo, wakuu wa wilaya na mikoa, aenziwe kwa “mapumziko,” tena ya nchi nzima?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwalimu Nyerere – kile “kitabu” cha rejea juu ya fikra na maoni mbalimbali duniani; mpambanishaji hoja hadi kuitwa kaidi; aliyeandika vitabu vingi akiwa madarakani na aliyethamini elimu; sasa anakumbukwa kwa mapumziko. Ili iweje?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiongozi wa nchi ambaye hakupora fedha wala mali ya taifa; hakujilimbikizia mali wala kutumia vibaya kile alichopangiwa; yule ambaye alilinda utajiri wa ardhini, misitu na wanyama hadi anatoka madarakani; anakumbukwa kwa kulala usingizi wa pono.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyerere alikuwa binadamu. Alitokeza kwa wakati wake na kufanya mengi ya wakati wake, hasa taifa lilipokuwa linamea na kukua kuelekea tulipo sasa. Alisisitiza uzalendo – mapenzi kwa nchi, watu wake na raslimali zake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili lina maana kubwa katika maisha ya taifa. Lina maana ya kutaka matumizi ya raslimali za nchi kwa manufaa ya wengi, kama siyo wote; lina maana ya kutumia raslimali za nchi kwa kiwango kikubwa ili kuepuka kuwa tegemezi. Kiini cha kujitegemea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa zitaandikwa. Makala zitaandikwa. Vitabu vitaandikwa juu ya Nyerere na mijadala juu yake haitaisha leo wala kesho. Kiongozi aliyetetea na kuishi maisha ya aina anayofundisha – ya uadilifu; hakustahili kuenziwa kwa mapumziko, bali kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hili halieleweki kwa watawala ambao aliwaacha madarakani, wanataka nani aje kuwafundisha kuwa hata kama alikuwa TANU na CCM, Nyerere alikuwa mtu kabla ya kuwa mwansiasa na mtawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku ya kumkumbuka Nyerere watawala wanatutangazia mapumziko ili tule na kuvimbiwa, tunywe na kulewa na kulala usingizi wa pono ili kujisahaulisha aliyotenda au kumzika na mema aliyoyatenda? Naomba kutoa hoja: Mapumziko haya yafutwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii itachapishwa katika&lt;/span&gt; &lt;span style="font-style:italic;"&gt;Tanzania Daima Jumapili&lt;/span&gt;, &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;toleo la 18 Oktoba 2009 katika safu ya SITAKI)&lt;br /&gt;&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-2589457239507853092?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/2589457239507853092/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=2589457239507853092' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2589457239507853092'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2589457239507853092'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/10/kuenzi-nyerere-kwa-ulevi-usingizi.html' title='KUENZI NYERERE KWA ULEVI, USINGIZI'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/StmBhR8uEQI/AAAAAAAAAGM/e1TKt2SgiNA/s72-c/Julius+Nyerere.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-1020985657202281093</id><published>2009-10-11T20:47:00.000-07:00</published><updated>2009-10-11T21:02:19.146-07:00</updated><title type='text'>WATU NA MIFUGO YAO WATAKUFA</title><content type='html'>&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/StKqQHjXwTI/AAAAAAAAAGE/QjssWxmPkKY/s1600-h/images.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 89px; height: 124px;" src="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/StKqQHjXwTI/AAAAAAAAAGE/QjssWxmPkKY/s320/images.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5391558897797939506" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;             &lt;br /&gt;&lt;strong&gt;SERIKALI IMEKWENDA WAPI LOLIONDO?&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                   &lt;strong&gt;     Na Ndimara Tegambwage &lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kuambiwa kuwa kuna serikali. Haipo. Kama ipo imelala, tena usingizi wa pono? Imezimia? Waliolala hawaamki? Waliozimia hawazinduki? Haipo!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafugaji wilayani Ngorongoro wanasema, tena kwa sauti kubwa kuwa kuna ukame. Kuwa mifugo yao – ng’ombe, mbuzi na kondoo haina chakula. Hakuna malisho. Hakuna maji. Mifugo inakufa. Serikali haipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi kutoka Loliondo anapaza sauti, kwa simulizi na takwimu: Hakuna maji. Hakuna nyasi. Mifugo inakufa. Ng’ombe sasa anauzwa kwa Sh. 2,000 hadi 20,000. Serikali kimya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfugaji anapaza sauti. Anadhani serikali haijasikia. Anasema maji yapo; wamekuwa wakiyatumia. Lakini maeneo yenye maji yamefungiwa kwenye mipaka ya vitalu vya uwindaji ambavyo serikali imegawa kwa watu wa nje – “wawekezwaji” – wale waliowekezwa badala ya kuwekeza. Serikali tebilimu! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna vilio, kwamba ng’ombe wawili wameuzwa kwa debe moja la mahindi. Kwamba bei ya debe la mahindi ni kati ya Sh. 8,000 na 10,000/=. Kwamba lazima ng’ombe auzwe haraka, hata kama ni kwa hasara, kabla hajafa. Serikali haipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sikilizeni sauti zao, hao wafugaji. Kwangu ng’ombe wamekufa watano. Kwangu wamekufa 20. Kwangu wamekufa 50. Elias Kagili wa kitongoji cha Kirtalo anasema: Kwangu wamekufa 100. Ni hatari tupu. Vifo. Vifo. Mwandishi kaona. Kasikiliza waathirika. Kaona na kupiga picha za mizoga. Serikali haipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sikilizeni kilio cha Ole Taki Saile wa kitongoji cha Ilichooroi. Ng’ombe wake 60 wamekufa. Wengine walio karibu kuwa taabani kawauza kwa bei ya kati ya Sh. 2,000 na 5,000. Naye Lekaneti Shekuti wa kitongoji cha Sekunya anasema karibu kila siku wanakufa ng’ombe wake 10. Serikali kimya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya Shekuti hii hapa. “Maji yapo pale. Nyasi zipo pale, lakini ng’ombe wetu wanakufa. Kampuni ya Thomson Safari inatuzuia kunywesha mifugo yetu pale,” anaonyesha sehemu husika kwa fimbo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maji yako Ngorika – mwekezwaji hataki. Maji yako Polelete; mwekezwaji hataki. Maji yako Sukenya, mwekezwaji hataki. Maji yako Olkimbai, mwekezwaji hataki. Maji yako Walaasaye, nako mwekezwaji hataki yanywewe. Kote huko ni visima na vijito vilivyoko katika ardhi waliyopewa wawekezwaji ili wafanyie “utalii wa uwindaji,” au ujangili ulioruhusiwa kisheria, ndani ya nchi ya wafugaji wanaotaabika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Teremka kijitoni au kisimani wakukute; utakiona cha moto. Sukuma mifugo yako kijitoni na wakukute; ndipo utajuta kwa nini ulizaliwa. Huu ndio ukatili unaosababisha vifo vya mifugo. Serikali haipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira ya Ngorongoro na Loliondo, vifo vya ng’ombe, mbuzi na kondoo maana yake ni vifo vya watu. Wanaohangaika kutafuta chakula na maji kwa ajili ya mifugo, wao hawana chakula. Ni mizoga inayotembea; inahangaikia mifugo yake. Siku moja itadondoka njiani. Serikali tebilimu!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali imetoa ardhi ya wananchi kwa makampuni  kutoka nchi za nje, iwe sehemu ya kuwindia kwa ajili ya kujifurahisha. Katika mazingira ya sasa, nyasi na maji vinapatikana katika maeneo ambako wawekezwaji hawaruhusu mifugo kuingia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, kuanzia Aprili mwaka huu, nyumba na maboma ya wafugaji yamekuwa yakichomwa moto kwa nia ya kuwafukuza wafugaji kutoka makazi yao ili wawindaji wa wanyamapori wapate kustarehe. Ni starehe ya wawekezwaji na adha kwa wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukatili. Ni unyama usiomithilika. Haustahili kusimamiwa au kuvumiliwa na wanaojigamba asubuhi, mchana na jioni kuwa wao ni walinda haki na watetezi wa demokrasi na haki za binadamu. Haiwezekani. Ni kwa kuwa serikali haipo. Serikali tebilimu!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama serikali ipo inasubiri nini? Inasubiri mifugo ife na kumalizika? Ili iweje? Ili wafugaji wawe masikini? Ili wawe ombaomba? Au ili wafe kama mifugo yao, huku wawekezwaji kutoka nje wakimeremeta; wakitweta kwa shibe na kunenepeana kwa faida na ziada ya uwindaji Loliondo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wawekezaji hutegemewa kuleta fedha. Wawekezaji hutegemewa kuongeza ajira. Je, wawekezwaji wanaleta nini kama siyo adha; wanaongeza shida na dhiki. Wanasababisha roho mbaya. Wanafungia maji na nyasi “kabatini;” ili mifugo ife; ili wenye mifugo wafe au wahame.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki kuamini kuwa kuna serikali. Ipo? Inamlinda nani? Inalinda wawekezwaji ili watanue, huku ng’ombe wa wafugaji wakifa? Huku mbuzi na kondoo wanakufa? Huku wafugaji wakisubiri kufa  pia?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kungekuwa na serikali ingeona mahangaiko ya wafugaji wa Kimaasai. Tuseme ipo lakini haioni? Ingekuwepo ingesikia kilio cha wafugaji, waandishi wa habari, wanaharakati na wafanyabiashara wanaonunua ng’ombe mmoja kwa Sh. 2,000. Tuseme haina masikio au yameziba?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kungekuwa na serikali, kwa maana ya watawala, ingekumbuka kuwa iliapa kutumikia watu, kuwalinda na kuwatendea haki; na iliapa kwa Mungu kuwa aisaidie kuyatenda kwa ukamilifu. Tuseme imesahau kiapo? Au wafugaji na maeneo yao siyo sehemu ya Tanzania? Au kiapo kimelainika? Nani amelainisha kiapo cha serikali?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kama mambo haya yangekuwa yanatendeka Nigeria au Kongo; huwezi kukaa kimya juu ya unyama wanaotendewa binadamu wa Ngorongoro. Risasi za moto zinatafuta nini katika makazi ya Wamaasai na mifugo yao?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Alikuwa Desmond Tutu aliyesema, “Ukiona mguu mnene wa tembo umekanyaga mkia wa panya, na ukaangalia pembeni na kusema hayakuhusu na wewe huna upande; panya hataelewa msimamo wako wa kutokuwa na upande katika ukatili huu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna kila sababu ya kuwa na upande katika kutetea haki. Na haki ya wananchi kuishi kwao na kufurahia matunda ya ardhi yao, haiwezi kupitwa na ujanjaujanja wa wawekezwaji hata kama wanamwaga mabilioni ya shilingi kwa yeyote yule.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;(&lt;strong&gt;Makala hii ilichapishwa katika gazeti la&lt;/strong&gt; &lt;em&gt;Tanzania Daima Jumapili&lt;/em&gt;, &lt;strong&gt;toleo la tarehe 11 Oktoba 2009 chini ya safu ya SITAKI&lt;/strong&gt;)&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-1020985657202281093?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/1020985657202281093/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=1020985657202281093' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1020985657202281093'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1020985657202281093'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/10/watu-na-mifugo-yao-watakufa.html' title='&lt;strong&gt;WATU NA MIFUGO YAO WATAKUFA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/StKqQHjXwTI/AAAAAAAAAGE/QjssWxmPkKY/s72-c/images.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-327584507619805803</id><published>2009-09-26T02:18:00.000-07:00</published><updated>2009-09-26T02:26:24.390-07:00</updated><title type='text'>ADHABU YA KIFO IMEPITWA NA WAKATI</title><content type='html'>&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/Sr3eNVvjsOI/AAAAAAAAAF8/YxVhZ8JsVEw/s1600-h/Chief+Justice+Augustino+Ramadhani.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 83px; height: 127px;" src="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/Sr3eNVvjsOI/AAAAAAAAAF8/YxVhZ8JsVEw/s320/Chief+Justice+Augustino+Ramadhani.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5385705050161262818" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Kunyonga siyo adhabu, ni kuua tu&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kuona wananchi na watawala wakishabikia hukumu ya kunyonga, hata kama kuna sheria ya nchi inayoruhusu mtu “kunyongwa hadi kufa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria iliyopo ni katili, chovu, inayopaliliwa na kuendelea kurutubishwa na mfumo unaoendeshwa na watu ambao wamekuwa wagumu kuelewa mantiki ya thamani ya maisha na umuhimu wa adhabu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iwapo hawatakata rufaa, au wakikata rufaa na kushindwa, Masumbuko Madata, Emmanuel Masangwa na Charles Kalamuji, waweza kuuawa kutokana na hukumu iliyotolewa na Jaji Gabriel Rwakibalila.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jumatano iliyopita, mjini Kahama, Jaji Rwakibalila aliwakuta vijana hao watatu na hatia ya jinai ya kuua Masumbuko Dunia, mtoto wa shule, umri wa miaka 13 na mwenye ulemavu wa ngozi (albino). Sasa kuna wanaoshangilia hukumu ya kifo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifo cha Masumbuko kiliuma na kuumiza wengi, hata kama hawakuwa na uhusiano wowote naye. Umri wake mdogo; nafasi yake katika jamii iliyosababisha kuitwa majina ya kumtelekeza; utu wake ambao ulikuwa na bado ni sehemu ya utu wa kila mtu; ni sehemu tu ya chimbuko la uchungu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uchungu unakuwa mkubwa pale jamii inaposhuhudia mauaji yakilenga watu wenye ulemavu wa ngozi; wadogo kwa wakubwa, kwa sababu dhaifu, za kijinga na potofu – eti kupata viungo vya kuwawezesha “kuwa matajiri.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uchungu huu usio na udhibiti, unapokutana na sheria ambayo hata Jaji Mkuu Augustino Ramadhani amewahi kusema kuwa hafurahii kuitumia, ndipo unazaliwa ukatili mpya; ule wa kuondoa uhai wa aliyepatikana na hatia ya kuua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mahakama Kuu nchini Tanzania iliishawahi kutamka kuwa adhabu ya kifo ni ya kikatili na ya kudhalilisha na kutaka ifutwe. Pamoja na maeneo mengine, maneno “katili” na “kudhalilisha” ni ya msingi sana katika kuchambua hukumu ya kifo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katiba ya Jamhuri ya Muungano inakataza ukatili na udhalilishaji. Kwa hiyo kuwepo sheria inayoruhusu kuua; hivyo kuendesha “ukatili” na “udhalilishaji,”  ni kuvunja katiba ya nchi. Lakini Mahakama ya Rufaa haikuafiki. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna ubishi kwamba vijana watatu wa Kahama, kwa kupatikana na hatia ya kumuua Masumbuko, walivunja haki za binadamu. Bali “haki za binadamu” haziwekwi na watu; zipo na zinahusu kila mmoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watawala, sheria na hata Katiba za nchi, haziweki haki za binadamu. Ngazi zote hizo hazina uwezo wa “kugawia” watu haki za binadamu. Kinachofanyika ni kwa watawala, sheria na Katiba kutambua kuwepo kwa haki hizo na kutafuta jinsi ya kuzilinda na kuziendeleza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, hapa siyo mahali pa hoja za jino kwa jino. Hoja ni kutovunja haki za binadamu. Kutoua. Kutofanya ukatili. Kutodhalilisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja hii inaleta maana zaidi pale tunapojadili “thamani” ya adhabu anayopewa mkosaji. Watatu wa Kahama wamepatikana na hatia. Wamevunja haki za binadamu kwa kumuua Masumbuko. Wanastahili adhabu na ikiwezekana iwe adhabu kali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tujiulize. Je, hukumu inayoruhusu kifo ni adhabu? Je, kifo kinaweza kuwa adhabu? Je, adhabu hufanywa na aliyekufa? Kama sababu ya kuadhibu ni kutaka mtu ajirudi na kurejea katika utu wa jamii yake je, aliyeuawa anajirudi vipi, lini na wapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hizi zinaonekana hoja ndogo kwa waliovimba vichwa na vifua, kwa hasira na uchungu wa kweli wa kupoteza watoto, ndugu, jamaa, rafiki au wenzao katika tabaka au kundi tambulishi kama walivyo albino.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali hasira zilizokaba koo za wafiwa; chuki zilizotunisha misuli ya shingo za ndugu wa aliyeuawa; na woga uliokumba nyoyo za wahusika; vyote vinaziba mifereji ya fikra kuhusu uhai wa mtu mwingine na nafasi ya muuaji mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vijana watatu wamepatikana na hatia ya kuua. Sheria inaruhusu wauaji kuuawa. Jaji, kwa mujibu wa sheria hajakosea kutamka hukumu hiyo kwa shabaha ya kulinda sheria na kazi yake. Bali Jaji aweza kuwa anaasi “shangazi wa mtima” wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majaji wengi duniani wameeleza jinsi wanavyosutwa na dhamira zao pale wanapotamka hukumu ya kifo. Wameeleza jinsi kunavyokuwa na mapambano makali “rohoni” mwao na hatimaye kuanguka na kuwa mateka wa sheria na mfumo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo kuna vijana watatu wa Kahama. Wanakabiliwa na mauti na siyo adhabu. Atakayeua vijana hao ni nani kama siyo muuaji? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna tofauti gani kati ya aliyeua albino kwa panga na anayeua muuaji wa albino kwa kamba ya shingoni? Haipo. Wote ni wauaji. Mmoja anakanwa na sheria na mwingine anaruhusiwa na sheria. Wote wanatoa uhai wa watu wenye thamani ileile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninaelewa ugumu wa wafiwa kuzingatia hoja hii haraka. Lakini malezi ya jamii hayawezi kwenda kwa misingi ya walioko madarakani kujipa fursa ya kuua na kujikinga na sheria walizotunga wenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niliishawahi kuuliza katika safu hii wakati wa kujadili somo hilihili: “Kama serikali inaua, nani ataua serikali – ambayo sasa ni muuaji?” Sikupewa majibu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna haja ya kufikiri upya kuhusu sheria inayoruhusu kunyonga watu. Kunyonga ni kuangamiza maisha; siyo adhabu ya kurejesha mtu kwenye mstari wa maandili na utu wa wote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kunyonga ni kunyima aliyepatikana na hatia fursa ya mabadiliko katika maisha. Ni mabadiliko haya ambayo huweza kuwa mfano mkuu kwa jamii na kufanya watu wengi kukiri udhaifu wao na kuwa wanyoofu maishani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuua hakuleti nafuu kwa mfiwa. Hakuna mafao kwa serikali. Hakuleti faida kwa jamii. Kunaendeleza vilio. Kunasimika hasira na chuki mpya. Kunafanya jamii ishindwe kuelewa nani anaweza kuikinga na ukatili huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria zinazoruhusu mauaji kwa njia ya kunyonga ni za kuviziana; za kumalizana na mara nyingi, kama siyo mara zote, zinawaelemea wa tabaka la chini katika jamii. “Wakubwa” wana kila njia ya kuzipinda na hata kuzikatakata.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria za kunyonga zinafanya jamii ianze kuona kuwa maisha hayana thamani. Zinafundisha usugu na kutothamini uhai binafsi na ule wa mtu mwingine. Zinazaa tabia ya “nitakuua hata kama wataniua.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria zinazoruhusu mauaji zinakomaza chuki na ghadhabu na zinafuta msamaha na tabia ya kujirudi ambayo ni nguzo kuu katika kupata suluhisho na muwafaka. Zinainyang’anya jamii ujasiri wa kufunza waliopogoka na kuikosesha jukumu la kufunza vizazi na vizazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Adhabu ilenge kurekebisha muhusika; kumfanya ajutie tendo lake na kutamani kurejea katika utu wake wa asili. Aliyekufa hajutii makosa yake; harekebiki pia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Natamani kuona hukumu ya kifo ikifutwa na nafasi yake kwa sasa kichukuliwa na adhabu ya kifungo cha maisha. Aliyeua akiuawa, aliyeua muuaji anakuwa amekamilisha ukoo wa wauaji. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika ukoo huu, mauaji hayataisha. Hayataogopwa. Hayatapingwa kwa kuwa hayatachukiwa. Natamani yaishe. Jamii ivunje kimya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;(&lt;strong&gt;Makala hii itachapishwa katika gazeti la&lt;/strong&gt; &lt;em&gt;Tanzania Daima Jumapili &lt;/em&gt;&lt;strong&gt;toleo la 26 Septemba 2009 chini ya safu ya SITAKI)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-327584507619805803?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/327584507619805803/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=327584507619805803' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/327584507619805803'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/327584507619805803'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/09/adhabu-ya-kifo-imepitwa-na-wakati.html' title='&lt;strong&gt;ADHABU YA KIFO IMEPITWA NA WAKATI&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/Sr3eNVvjsOI/AAAAAAAAAF8/YxVhZ8JsVEw/s72-c/Chief+Justice+Augustino+Ramadhani.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-5622940344170205915</id><published>2009-09-19T05:05:00.000-07:00</published><updated>2009-09-26T02:31:10.379-07:00</updated><title type='text'>NGUVU ZA UNAFIKI NA SIASA ZA NJIAPANDA</title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SrTLgx33KKI/AAAAAAAAAF0/oQgXdkj3h4I/s1600-h/Yusuf+Makamba.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 124px; height: 93px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SrTLgx33KKI/AAAAAAAAAF0/oQgXdkj3h4I/s320/Yusuf+Makamba.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5383151218618476706" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;           &lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Yusuf Makamba: Mara joto, mara baridi… &lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;SITAKI tabia ya Yusuf Makamba, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kuwa mara baridi, mara joto, mara vuguvugu na mara baridi, tena katika muda mfupi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mbunge, mteule wa rais, kiongozi mkuu wa utendaji katika chama kinachopanga ikulu, kuwa na tabia ya kubadilika kila kukicha au pale kipenga kinapopulizwa; siyo ishara ya kuwa makini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Joto lilipokuja – kwa msukumo wa chama au makundi au mtu binafsi – Makamba alifura kwa hasira na kutangaza ubabe. Alifanya hivyo baada ya vikao vya CCM vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu jijini Dodoma hivi karibuni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alimwakia spika Samuel Sitta na wajumbe wa chama chake kumkaripia, kumtishia, kumpa onyo na kutaka kumlegeza. Ni Makamba aliyesimama na kusema, “Kama siyo CCM, Samwel Sitta ahojiwe na nani?”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndani ya vikao vya CCM, Samwel Sitta alikuwa anakabiliwa na tuhuma nyingi zilizopelekwa kwa njia ya mjadala juu ya hali ya hewa ndani ya chama na serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwamba spika amejitwisha jukumu lisilo lake la “kupambana na mafisadi.” Kwamba ana upendeleo – anatoa nafasi mara nyingi kwa wenye “kupinga serikali” na hata wapinzani, kuhutubia bunge kuliko wale wanaotetea chama na serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ofisa mdogo katika ofisi ya Makamba, John Chilligati, kwa ushirikiano na Makamba au kwa kutumwa na chama chake, aliwawakia wale ambao wanadaiwa kupewa muda mwingi na spika “kukemea ufisadi,” akihoji nani aliwapa wajibu huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikaja asubuhi, ikaja jioni, siku zikapita. Makamba yuleyule, wiki iliyopita, akaenda jimbo la Urambo, mkoani Tabora. Huko ndiko nyumbani kwa spika Samwel Sitta. Akachukua sura ileile ya kuumbika na kuumbuka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliwaambia viongozi wa chama chake vikaoni na wananchi kwenye mkutano wa hadhara, kwamba CCM inatambua kuwa Spika Samwel Sitta anafanya “kazi yake vizuri” na hasa anafanya kazi ya chama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Makamba wa leo siyo wa jana, wa kesho wala keshokutwa. Anaumbika na kuumbuka au kuumbuliwa. Anafura kwa hasira, lakini dakika chache zifuatazo, anatoa kicheko – cha kweli au cha unafiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyombo vya habari vimemnukuu Makamba akisema kuwa Sitta ni mbunge wao imara na kazi anayofanya bungeni ni kazi nzuri ya chama chake; na kuwataka wamuunge mkono hata katika uchaguzi ujao. Hata walokole hawafikii hatua hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Joto la ndani ya vikao vya CCM ndilo lilifanya Makamba awe mkali, jeuri na aongee kwa kujiamini. Wajumbe walioongea kwa kukandia Sitta, tena mbele ya mwenyekiti wa chama na rais wa Jamhuri, Jakaya Kikwete, huku wakipendekeza afukuzwe uanachama, ndio walikuwa msukumo wa Makamba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msukumo mwingine ulikuwa “Kamati ya Mwinyi” iliyoundwa rasmi kuchunguza “msuguano” kati na baina ya spika, bunge na serikali. Kamati iliundwa katika kikao cha Halmashauri Kuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maandalizi ya vikao hivyo vya Dodoma; kwa taarifa kwamba wajumbe kutoka Zanzibar walikuwa wameandaliwa rasmi kumkabili Sitta na hivyo ndivyo ilivyojitokeza; na kwa wingi wa wajumbe walioongea kutaka “Sitta amalizwe,” hakika Makamba asingekuwa na mtu wa kutembelea Urambo anayeitwa Samwel Sitta – spika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tabia ya Makamba ya kubadilika haraka – kutoka joto sana hadi baridi na huenda kesho atakuwa vuguvugu – huenda ndiyo inamfaa yeyote anayetaka kuwa katibu mkuu wa CCM ya sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akiombwa na kundi moja linalopingana na lingine kuwa aandae mazingira ya uhasama na mashambulizi, basi afanye hivyo. Akiambiwa sasa apoe, ananyamaza kama aliyekwenda safari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini akitekenywa kwamba amwakie fulani, kwa sababu zozote zile, atafanya hivyo. Vilevile akiambiwa kurejesha amani, atawaangukia aliokorofishana nao na kukumbuka walivyopeana pipi wakiwa darasa la pili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Makamba anakuwa mkuu wa maabara isiyofuzu – CCM. Hawaamini kuwa waliishamaliza utafiti juu ya utengenezaji hewa ya oksijeni. Kwao utafiti ni utafiti tu usioisha hata kama waliishapata matokeo; ili mradi waonekana wako kazini, wanalipwa na wanatumiwa na waajiri wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Safari ya Makamba nyumbani kwa Sitta imekuja baada ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa kubanwa na wananchi na balozi za nchi za kigeni zilizoko Dar es Salaam, kuhusu vitisho alivyofanyiwa spika na nia mbaya ya kumdhoofisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kwamba Rais Kikwete alijua kuwa hali hiyo ingedhoofisha uhusiano kati ya serikali yake na wananchi, asasi za kijamii zinazopigania haki za binadamu na hata nchi wahisani, akatafuta jinsi ya kulegeza msimamo kwa kutoa “maelezo ya nyongeza” kwa yale yaliyotolewa na Makamba na Chilligati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais Kikwete alisema wiki iliyopita, katika kujibu “maswali ya wananchi ya papo kwa papo” katika televisheni kwamba, halmashauri kuu iliyokemea wabunge “wenye msimamo mkali,” ililenga tu kuleta nidhamu na siyo kuwatishia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alisema wabunge walikuwa wanatakiwa kujadili mambo ya chama chao ndani ya vikao vya chama na siyo hadharani; na kwamba kwa hatua hiyo, chama kamwe hakikulenga kuwanyamazisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kauli ya Kikwete ilikuwa ndiyo kauli ya halmashauri kuu ya CCM, basi Makamba na Chilligati hawajui kuripoti na kuwasilisha taarifa za chama chao kwa wananchama, wananchi na dunia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini kama taarifa zao, na hasa Makamba, ziliwakilisha yaliyojiri ndani ya vikao vya chama chake; na kauli za Kikwete ni tofauti na zilizolenga kupoza wanachama na kurejesha “amani” ndani ya CCM, basi kuna mgogoro ndani ya chama hiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali kinacholeta nuru juu ya yaliyotendeka ndani ya vikao na iwapo yalilengwa; ni kwamba hakuna hatua yoyote waliyochukuliwa Makamba na Chilligati kwa kutoa taarifa tofauti na zile za chama na tofauti na kauli za mkuu wa kaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dunia ya nje isiyotafiti wala kuchokonoa, yaweza kuamini kuwa aliyosema Kikwete ni sahihi na yale ya Makamba na Chilligati ni kauli binafsi au taarifa za chama zilizotiwa hamila. Kumbe sivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Makamba ni mchekeshaji wa kweli. Aweza kutumika kwenye sherehe na kwenye misiba. Si yumo katika vikao vya kumsulubu Sitta? Leo kapewa ngwe ya kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hadithi zatufundisha: Lini sungura anakuwa rafiki wa simba? Ni pale tu simba anapokuwa ameshiba au anapokuwa na swala upandeni. Bali ni urafiki wa muda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii &lt;strong&gt;haikuchapishwa&lt;/strong&gt; katika toleo la&lt;/strong&gt; &lt;em&gt;Tanzania Daima Jumapili,&lt;/em&gt; &lt;strong&gt;20 Septemba 2009 katika safu ya SITAKI kwa sababu ambazo mhariri aliniambia kwa simu kuwa ni "matatizo ya kiufundi.)&lt;/strong&gt; &lt;em&gt;Badala yake makala ilichapishwa katika gazeti la MwanaHALISI toleo la Jumatano 23 Septemba 2009).&lt;/em&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-5622940344170205915?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/5622940344170205915/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=5622940344170205915' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5622940344170205915'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5622940344170205915'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/09/nguvu-za-unafiki-na-siasa-za-njiapanda.html' title='&lt;strong&gt;NGUVU ZA UNAFIKI NA SIASA ZA NJIAPANDA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SrTLgx33KKI/AAAAAAAAAF0/oQgXdkj3h4I/s72-c/Yusuf+Makamba.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-743653637318984916</id><published>2009-09-13T01:40:00.000-07:00</published><updated>2009-09-13T01:48:15.808-07:00</updated><title type='text'>DC AKISHINDWA SERIKALI IMESHINDWA</title><content type='html'>&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;DC Tarime anapokiri kushindwa&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;br /&gt;                 Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kauli na mipango ya mkuu wa wilaya (DC) ya Tarime, Frank Uhahula aliyoitoa hivi karibuni. Inatishia maisha ya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Gazeti hili lilichapisha habari kuwa mkuu huyo ametishia “kufuta shughuli za ufugaji wa ng’ombe mkoani Mara, endapo wenyeji wa mkoa huo wataendelea kuibiana mifugo, hali ambayo inachangia vitendo vya mauaji.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuwa hakuna taarifa zozote za kukanusha taarifa hiyo tangu ichapishwe, 7 Septemba mwaka huu, inaweza kuchukuliwa kuwa ni kweli alitoa kauli hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hali ya kawaida, kauli hiyo haiwezi kutolewa na mkuu wa wilaya aliyepata mafunzo ya uongozi; aliyekulia katika mfumo wa uongozi au mwenye maarifa juu ya taaluma ya uongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni muhimu kurudia, kurudia na kurudia kusema kuwa uongozi ni menejimenti na menejimenti haiji tu kwa kuteuliwa kuwa mkuu wa mahali fulani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ama umesomea shuleni, umepata mafunzo kwa njia mbalimbali, umeelekezwa ukiwa kazini na umetenda kwa kutumia misingi husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika baadhi ya nchi, ukuu wa wilaya na mkoa ni vyeo vinavyojazwa na watumishi ambao wamefikia ngazi fulani katika mpangilio wa madaraka serikalini. Hachomolewi mtu kutoka popote kule na kufanywa DC. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mahali pengine vyeo hivi hupewa wale waliopata mafunzo na wenye maarifa ya uongozi na wamethibitika kuelewa jinsi ya kutumia taaluma hiyo ya menejimenti ya watu na raslimali zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haikutarajiwa basi, kusikia mkuu wa wilaya ya Tarime akitishia “kufuta ufugaji” ng’ombe mkoani Mara. Amekerwa sana? Hana njia ya kukabili tatizo la wizi? Ameshindwa kazi? Anakiri kwa niaba ya serikali kwamba utawala wa nchi umeshindwa kudhibiti wizi wa mifugo Tarime?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama mkuu wa wilaya ameshindwa kazi, si amwambie aliyemteua, tena kimyakimya, “Mzee hapa sipawezi,” ili atafutiwe pengine au aachwe njiapanda? Si kauli ya DC inadhalilisha hata serikali nzima? Na serikali ikishindwa, wananchi wafanyeje?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hiyo kauli ya DC ilitolewa mahali pabaya. Ni pale alipokuwa anazindua kikundi cha ulinzi shirikishi wa wananchi na polisi katika kijiji cha Kitenga. Je, kwa kauli hiyo alitaka kusema kuwa hata uzinduzi wa ulinzi aliokuwa anafanya haukuwa wa maana yoyote?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya DC iligongana na kauli ya Polisi Jamii wa Mkoa Maalum wa Tarime-Rorya aliyesema ndani ya polisi kuna askari “wachache” wanaosaidiana na wezi wa mifugo. Alitaka wafichuliwe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe tatizo siyo mifugo. Tatizo siyo wafugaji. Tatizo ni wizi. Wizi ni uhalifu endelevu unaoweza kukabiliwa na njia endelevu. Kama hakuna njia hizo endelevu, basi akili za watawala zitakwama; watalia, watalalamika na kujawa ghadhabu; watashindwa kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kauli ya DC, ambayo ni kauli ya serikali, wizi wa ng’ombe ukiendelea, serikali “itafuta” ufugaji huo. Wizi wa mbuzi ukianza na kupanuka, serikali itafuta ufugaji wa mbuzi. Wizi wa kondoo ukianza na kuenea, serikali itafuta ufugaji wa kondoo; na wizi wa kuku ukishamiri, serikali itafuta ufugaji wa kuku!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Fanya mwendelezo hapa. Kila kinachoshindikana kipigwe marufuku. Watu wakiibiana mno nguo, serikali ifute uvaaji nguo. Wakiibiana mno chakula, serikali ifute kilimo cha mazao ya chakula. Wakiibiana mno fedha, serikali izuie watu kuwa na fedha!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ndiyo dhana ya “Uhahulism” inayotokana na fikra za Uhahula wa Tarime. Huku ndiko kukiri kushindwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uhahula anapendekeza kufuta mifugo. Maana yake ni kwamba hajui uhusiano kati ya wananchi na mifugo yao. Inaonekana hajajitahidi kujifunza mazingira ya watu aliokabidhiwa kuongoza na hana ujuzi na maarifa ya kutawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mifugo ni uhai wa wafugaji. Mifugo ni mali. Mifugo ni fedha. Mifugo ni benki. Mingi au michache kama ilivyo, mifugo ndio utajiri wa pili kwa wafugaji. Kwanza ni watu – ndugu na marafiki ulionao; na pli ni mifugo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo kutenganisha wafugaji na mifugo ni kuwaondolea uhai – chakula – lishe ya nyama na maziwa. Ni kuwaondolea usalama wa maisha – watakosa kinga na kimbilio pale watakapokuwa na matatizo ya kiuchumi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuta mifugo ni kupora mali za wafugaji; ni kuwaibia fedha; ni kubomoa mabenki yao; ni kuua udugu, urafiki na uwezo wa jamii wa kujilisha, kujitunza na kuweka misingi kwa jamii zao za baadaye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili ndilo linadhihirisha hatari iliyopo pale viongozi wanapokuwa hawakutokana na mkondo wa ngazi za utawala; wanapokuwa wa kuotesha tu, na hasa wanapokuwa wanaamini kuwa kila kitu huenda kwa amri na siyo fikra na ushawishi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachosikitisha zaidi ni kwamba mkutano alikohutubia DC haukuwa wa wezi wa ng’ombe. Ulikuwa wa wafugaji na wananchi wengine, hata kama ndani yake kulikuwa na watuhumiwa wawili au watatu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo vitisho vya DC, kama vililenga wezi, basi havikuwafikia au viliwachochea. Kilichofika kwa wengi ni hatua za uonevu ambazo serikali wilayani ilikuwa inaahidi kwa watu na mali zao. Huu siyo uongozi. Siyo utawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna haja ya kurudia kuuliza: Serikali ikishindwa kazi ya ulinzi wa watu na mali zao, na ikakiri hivyo, wananchi wafanyeje? Labda wananchi na viongozi wao wa kweli wanajua. Tuwasikilize.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii imechapishwa katika gazeti la&lt;/span&gt; &lt;span style="font-style:italic;"&gt;Tanzania Daima Jumapili&lt;/span&gt;, &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;toleo ya 13 Septemba 2009)&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-743653637318984916?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/743653637318984916/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=743653637318984916' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/743653637318984916'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/743653637318984916'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/09/dc-akishindwa-serikali-imeshindwa.html' title='DC AKISHINDWA SERIKALI IMESHINDWA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-3687803491220326017</id><published>2009-09-05T02:38:00.004-07:00</published><updated>2009-09-05T03:07:37.321-07:00</updated><title type='text'>UJANGILI ULIORUHUSIWA NA SERIKALI</title><content type='html'>&lt;strong&gt;Uwindaji wa leseni ni ‘ujangili’ pia&lt;/strong&gt;   &lt;br /&gt;• Maliasili ya Tanzania, dunia itaisha&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;WAFUGAJI wanaofukuzwa kwenye makazi yao katika mbuga wana mengi ya kusema. Wengi hawana elimu ya darasani lakini ni wajuzi wa mazingira yao na wepesi wa kutambua mabadiliko. Hapa wanasema wanachoona ambacho serikali inaweza kufuatilia ili kuokoa maliasili wanyamapori.&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;WAMECHOMEWA makazi. Wakapigwa na wengine kuswekwa rumande kwa madai kuwa wamekaidi amri ya kuhama mbuga ambamo wameishi kwa miaka nendarudi. Lakini bado wana uchungu na nchi yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wana uchungu na maliasili za Tanzania. Wanapendekeza kuwa uwindaji katika mbuga ungesimamishwa ili kuruhusu wanyamapori kuongezeka na kurejesha utajiri mkubwa wa taifa na dunia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafugaji wa ng’ombe, mbuzi na kondoo ambao wameishi kwa kuingiliana sana na wanyamapori, wanasema serikali ingeweka sheria kali, kama hazipo, au kusimamia zilizopo ili kuokoa maisha ya wanyamapori.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Sisi ndio walinzi wa wanyama hawa, usione wanatufukuza. Tungewabughudhi wasingekuwa hapa. Wala hatuwali. Sisi tunakula mifugo yetu. Lakini kwa mtindo wa sasa, wanyama watatoweka,” anaeleza mkazi wa kijiji cha Ololosokwan.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna masimulizi mengi na marefu juu ya wanyamapori wanavyouawa kwa wingi. Mwanaume wa umri wa kati kijijini hapa anasema, “Kwa mfano, simba ni simba tu. Hawana mbadala. Kama simba watamalizika, hakuna tunachoweza kuona katika nafasi yake kiitwacho simba.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Tumeona mengi humu Loliondo. Hata wenzetu kutoka mbali wamekuja na kusimulia kuwa hali ni hiyohiyo. Wawindaji kutoka nje ya nchi wanaua hata watoto wa simba,” anaeleza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kijana wa umri upatao miaka 25 wa kijiji cha Magaiduru-Lorien anadakia na kusema, “Nimewahi kuona watalii wamebeba watoto wa simba na puma ndani ya gari lao.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kijana mwingine anaingilia kati, “Unasema simba tu? Mwaka jana wanamgambo wanaohudumia jumba la mfalme wa Umoja wa Nchi za Kiarabu (UAE) pale kilimani, walipita wakitangaza kuwa atakayepata chatu akiwa hai atalipwa shilingi milioni moja (1,000,000/=).” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Kwa hiyo na wewe uliingia vichakani kuwinda chatu?&lt;br /&gt;Jibu: Hapana. Mimi nina shughuli zangu. Angalia ng’ombe wote hawa (kama 1,200).&lt;br /&gt;Swali: Si ungemwambia mdogo wako akachangamkia hilo?&lt;br /&gt;Jibu: Tuliacha wengine wanaohitaji fedha za haraka watafute.&lt;br /&gt;Swali: Sasa chatu alipatikana?&lt;br /&gt;Jibu: Alipatikana. Tulisikia walipatikana sita, wakubwa kwa wadogo. Waliwachukua wakiwa hai.&lt;br /&gt;Swali: Kwani wewe umewahi kuona wanyama wakisafirishwa wakiwa hai?&lt;br /&gt;Jibu: Si unaona uwanja wa ndege ule pale (ndani ya Loliondo)? Madege makubwa yanatua hapo hata yenye uwezo wa kubeba magari makubwa. Nendeni ukaulize maeneo yale utapewa taarifa. Hata simba na chui wachanga wanasemekana kuchukuliwa…lakini usinifanye shahidi wako.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni madai makubwa na mazito. Yanahitaji kuthibitishwa. Wafugaji wanasema walichoona. Huenda wanyama wanaodaiwa kuchukuliwa kutoka mbugani wakiwa hai ndio tunawakuta katika “hifadhi za wanyama” mijini (mazuu) katika baadhi ya nchi za nje.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Maelezo ya aina hii yanafanya wafugaji wakazi wa mbuga za Loliondo wachukiwe na watu kutoka nje ambao walipewa mbuga kufanyia biashara ya utalii na bila shaka baadhi ya maofisa wa maliasili wanaoshirikiana nao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbuga za Loliondo ziko chini ya kampuni ya Ortelo Business Corporation (OBC) ya Umoja wa Falme za Kiarabu ambayo imekuwa ikiendesha biashara ya utalii wa uwindaji wanyama na upigaji picha kwa karibu miaka 17 sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafugaji wanachukiwa kwa kuwa “wanasema uongo.” Kusema uongo, katika hali hii ni kusema ulichoona; kwamba wanaoitwa watalii wanafanya zaidi ya kile walichotarajiwa kufanya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna masimulizi kuwa “watalii” – ambao wananchi hapa wanapenda kuwaita “majangili wenye leseni” – wanaua hata wanyamapori ambao hawapo kwenye orodha ya kuwindwa na kuchukua hata wanyama hai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Uwongo” wa aina hii ni aghali. Vijana wengi wanasema wakijulikana kuwa wametoa taarifa kwa watu wa nje, huenda wakakamatwa na “kuwekwa ndani.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Kweli, mfano tukijulikana kuwa tuliongea nanyi kuhusu mambo haya, wanaweza kutupoteza au kututupa rumande kwa muda mrefu mpaka tukakuta mifugo yetu yote (ng’ombe 210, mbuzi 90 na kondoo 45) vimeibwa,” anaeleza kijana akitupa macho huku na kule. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Sisi tunawajua wanyamapori. Wakiongezeka tunajua; wakipungua tunajua,” anasema Mzee Ngirimba mwenye umri wa miaka 59 kutoka kijiji cha Arash ambaye alikutwa Ololosokwan.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali kama ambavyo hakuna mbadala wa simba, vivyo hivyo hakuna mbadala wa swala, tembo wala digidigi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mfano, taarifa kuhusu idadi ya wanyamapori zinaeleza kuwa swala-twiga wamepungua sana katika mbuga nyingi nchini. Tandala wadogo na tandala wakubwa – wote wamepungua kwa kiasi kikubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanyama wengine ambao wakazi wa mbugani na baadhi ya maofisa wanyamapori wanakiri wamepungua ni digidigi wadogo ambao hutembea wawili-wawili na palahala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini wazee sita waliohojiwa juu ya wingi wa simba katika maeneo yao, walisema hata simba, chui, duma na mbwamwitu wamepungua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Hatuna elimu juu ya taratibu za wanyamapori na uwindaji, lakini tunajua kuwa siyo wanyama wote wanaowindwa. Lakini huku kwetu huwa tunaona wanapiga tu kila mnyama,” ameeleza mmoja wa wazee wa Olorien.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Kwa mfano tumeona walioua twiga na siku zote tunaambiwa kuwa twiga siyo mnyama wa kuwinda,” anaeleza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anasema amesikia kuwa hata simba, duma na chui hawastahili kuwindwa lakini wameona wawindaji wa kitalii wakiburuta mizoga ya wanyama hao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Masimulizi juu ya uwindaji shelabela – unaoua wanyama wakubwa na “watoto wao;” ukamataji wanyama hai na usafirishaji wake nchi za nje, ni mambo ambayo wafugaji katika mbuga wanasimulia kwa uwazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wauaji wakuu wa maliasili wanyamapori ni wale wenye leseni za kuwinda. Wanadaiwa kuua wanyama wengi kuliko idadi ya waliopangiwa na wanaua hata wale wasio kwenye orodha ya kuwindwa, wenye mimba na wachanga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wawindaji wa aina hii basi, hata kama wana leseni, ni wahujumu ambao tunaweza kukubaliana na wananchi wa eneo hili wanaowaita “majangili wenye leseni.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uwindaji wa aina hii unateketeza wanyamapori; unaua vizazi vya maliasili hii adimu duniani. Walinzi wa mbuga na wanyama waliomo wana mapendekezo, kama anavyosema mmojawao katikamahojiano:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali: Kwa hiyo unaona afadhali utalii wa kuwinda wanyamapori upigwe marufuku?&lt;br /&gt;Jibu: Wewe! Nani atakubali hilo? Hawa wazungu na waarabu wanaokuja wanataka kujiburudisha na serikali yetu inataka fedha. Unadhani nani atakubali hilo?&lt;br /&gt;Swali: Kwa hiyo waendelee kuwinda?&lt;br /&gt;Jibu: Hapana. Sisi tunaona wakisimamisha uwindaji kwa miaka kumi (10) wanyama watazaana na kuongezeka. Kuanzia hapo uwekwe utaratibu wa kuzuia kuangamiza wanyamapori.&lt;br /&gt;Swali: Unadhani uuaji wanyama bila kujali nani ana mimba, nani ana umri mdogo na nani hastahili kuwindwa unatokana na nini?&lt;br /&gt;Jibu: Sisi hayo hatuyajui. Hatuna majibu. Tunaona ni ukatili tu. Labda pia hawana mtu wa kuwaongoza ili kuwaambia ‘huyu msiue.’ Lakini tunaambiwa kuna masharti wanayopewa kabla ya kuingia kwenye mbuga kuwinda.&lt;br /&gt;Swali: Na hili la kubeba wanyamya hai?&lt;br /&gt;Jibu: Kwanza hilo hatukulikubali haraka. Tulidhani vijana wanasema hovyo. Jinsi siku zinavyokwenda ndipo tukapata ukweli. Inaonekana hakuna usimamizi. Hilo halipo hapa Loliondo peke yake. Tunasikia hata Serengeti katika eneo la Gumeti (Grumet).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzee huyu anasema hawajui iwapo wawindaji wa kitalii wanaruhusiwa kubeba nyama na kupeleka kwao&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafugaji ndio wamekuwa walinzi wa mbuga. Wanyama wote waliomo wamekusanyika, kuzaana na kuishi bila bughudha kwa kuwa wafugaji hawakuwawinda.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Dunia nzima inayokusanyika katika mbuga za Tanzania inakuja kushuhudia, bahati mbaya bila kujua, utashi, ujasiri na mapenzi ya wafugaji kwa wanyamapori. Bali leo hii wafugaji na mifugo yao wanaswagwa nje ya makazi yao na mali zao kuharibiwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Laiti wanyama wangekuwa na uwezo wa kutambua kuwa marafiki wao wa karibu, wa miaka mingi, wanatendewa ukatili. Wangepinga kwa maandamano na kauli kali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tetesi hizi ni muhimu kwa serikali na dunia nzima. Wanaopenda wanyama na mapato kutokana na wanyamapori, sharti wachukue baadhi ya hatua zifuatazo:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, kufanya uchunguzi juu ya madai ya walinzi wa miaka mingi wa wanyamapori. Hawa ni wafugaji ambao wamekuwa karibu na wanyama kiasi cha kujua hata tabia zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, uchunguzi uongoze katika kuchukua hatua madhubuti za kusimamisha uwindaji wa kiharamia katika mbuga zote nchini. Hii ni kuzuia uteketezaji maliasili ya dunia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua hizi zitazuia pia ukamataji na usafirishaji wanyama hai nchi za nje, kama utakuwa umegundulika na kuthibitika; na au kusitisha uwindaji kwa kipindi kirefu ili kuruhusu wanyamapori kuongezeka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu, kuangalia jinsi ya kusimamisha uwindaji wa aina fulani ya wanyamapori na kuweka usimamizi wa kutosha wa mamlaka ya wanyamapori katika hatua  zote za uwindaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nne, kubadili masharti ya miliki au ukodishaji wa mbuga ili kuondoa ukiritimba wa wamilikishwaji au wenye leseni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wamiliki au wenye leseni za kukodi wanapokuwa na mamlaka kama yale ya nchi, waweza kufanya wapendalo ikiwa ni pamoja na kuua kishelabela na hata kuhamishia wanyama nchi za nje.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tano, kuacha kuchoma makazi ya wafugaji na kusitisha hatua za sasa za kuwafukuza, wao na mifugo yao, kutoka kwenye mbuga. Badala yake watengewe maeneo ya kilimo na mifugo pale walipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mashamba madogo ya mahindi ya wafugaji, chini ya kilima ambacho kilele chake ndiko liliko “kasri” la mfalme wa UAE, yanaonyesha mabadiliko muwafaka katika maisha ya wafugaji. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafugaji hawa, wanaoanza kuwa wakulima pia, wanaendelea kuwa walinzi wa wanyamapori na chanzo cha taarifa muhimu za kunusuru maliasili ya Tanzania na dunia. Huu nao ni ulinzi wa aina yake. Serikali yaweza kuanzia hapa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wako wapi akina Luteni mstaafu, mfugaji na mkulima, Lepillal ole Molloimet, ili wajiunge na jumuia ya kimataifa katika kusemea wasio na sauti na kupigania maliasili za taifa na dunia? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com &lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com  &lt;br /&gt;&lt;strong&gt;&lt;br /&gt;(MAKALA HII ILICHAPISHWA KATIKA GAZETI LA MwanaHALISI TOLEO LA 19 AGOSTI 2009)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-3687803491220326017?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/3687803491220326017/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=3687803491220326017' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3687803491220326017'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3687803491220326017'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/09/ujangili-ulioruhusiwa-na-serikali.html' title='&lt;strong&gt;UJANGILI ULIORUHUSIWA NA SERIKALI&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-8129516451706573636</id><published>2009-09-05T01:46:00.000-07:00</published><updated>2009-09-05T02:03:45.784-07:00</updated><title type='text'>ASKOFU KAKOBE ATAMANI UDIKITETA</title><content type='html'>&lt;a href="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SqIpSDNFupI/AAAAAAAAAFs/wG_y39zXWh4/s1600-h/Kakobe.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 91px; height: 110px;" src="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SqIpSDNFupI/AAAAAAAAAFs/wG_y39zXWh4/s200/Kakobe.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5377906295108385426" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;                &lt;br /&gt;&lt;strong&gt;KUZIMA MAWAZO KWAWEZA KULETA VURUGU; &lt;br /&gt;KUKUBALI YATOKE KWAWEZA KUZIEPUSHA &lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI Askofu Zakaria Kakobe wa kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) ajiingize katika mjadala ambao hauwezi na hautaleta manufaa kwa kanisa wala waumini wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapema wiki iliyopita alinukuliwa akiwaambia waandishi wa habari kuwa Rais Jakaya Kikwete amezidi kwa upole kwa vile hajakemea kanisa Katoliki kwa kutoa “Waraka” wa elimu ya uraia kwa wananchi kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kakobe alisema pia rais amekuwa mpole mno kwa kutokemea Shura ya Maimamu kwa kutoa “Muongozo” wa waislamu ambao maimamu wanasema unalenga kumwelimisha mwislamu juu ya nafasi yake katika siasa za nchi hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Askofu wa kanisa la FGBF anasema maandishi haya yanaweza kuleta utata mkubwa na hata mifarakano katika jamii. Alimpongeza Kingunge Ngombale-Mwiru, mbunge mteule wa rais, kwa kukemea Waraka na kufikia hatua ya kusema “wauondoe” na kwamba Ngombale-Mwiru “aliona mbali.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini ukali wa rais unahitajika kwa lipi hapa? Katoliki wanasihi wananchi kujadili aina ya viongozi wanaowahitaji na ndio hao wawapigie kura. Wametoa andishi la kusaidia kuendesha mijadala miongoni mwa waamini na jamii kwa jumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Shura ya Maimamu imetoa andishi la kukumbushia lawama zao kwa utawala; malalamiko kuhusu kubaguliwa; nafasi ya mwislamu katika siasa za awali katika kutafuta uhuru na kuhimiza waislamu kuwachagua waislamu au wale wanaoona wataendeleza maslahi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, tujadili ukali wa rais. Huyu ni mtawala mkuu wa nchi. Ametokana na mfumo wa utawala ambao analazimika kuulinda, kuutetea na kuuendeleza. Ni mfumo huo ambao unatoa viongozi wanaolalamikiwa kwa kutokuwa makini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais awe na ukali upi zaidi; wa kiasi gani kuliko huu alionao sasa; anaoutumia na kuusimamia na unaosababisha kupatikana kwa viongozi wanaolalamikiwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Askofu Kakobe anasema Rais Kikwete anatembeza tabasamu tu. Lakini tabasamu la rais ni ishara ya utulivu wake moyoni; kwamba hana presha; kila kitu kinakwenda kama anavyotaka na kwa mujibu wa mfumo anaosimamia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Laiti Kakombe angejua kuwa mfumo wa jana na leo, ambao rais anasimamia, ni wa kibaguzi; unanyima fursa ya kuwa kiongozi  wa siasa mpaka uwe mwanachama wa chama cha siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni mfumo katili unaokufungia katika “mahabusu” ya chama hichochicho kiasi kwamba ukihama unakuwa umejifukuza kazi uliyopewa na umma kwa njia ya sanduku la kura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vilevile ukiwa na maoni tofauti, hata yanayolenga kuimarisha chama chako, kama yanaelemea baadhi ya wazito ndani ya vikao vya juu vya chama hicho kilichoko ikulu, basi utakuwa unajipalia mkaa; tena wa moto. Utawindwa. Unaweza kuuawa kisiasa. Huo ndio mfumo ambao rais anasimamia huku akiwa anatabasamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mfumo huu ndimo aliyeiba mabilioni ya shilingi anasamehewa kwa kurejesha kiasi, lakini aliyeiba chungwa anafungwa miaka mitatu. Ubaguzi mzito.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni humuhumu ambamo kuna makubwa ya kukamua utajiri wa taifa hili. Mikataba ya kinyonyaji; wizi wa waziwazi kabisa wa fedha za umma; uporaji raslimali hata wanyama, magogo na mchanga. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yote haya, hata kama hayakuanzishwa na viongozi wa utawala wa sasa, yako chini ya utawala wa rais anayeambiwa na Kakobe kuwa anunie barua ya kanisa kwa waamini na malalamiko ya waslamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, katika mfumo huu ndimo kuna waandishi wa Waraka na Muongozo. Machapisho haya yanaeleza ama jinsi ya kujikwamua kutoka katika mazingira tuliyomo kwa kuwa na viongozi wakweli na thabiti; au yanawasilisha maoni ya makundi na watu binafsi katika mustakabali wa siasa za nchi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa Kakobe anataka rais awe mkali katika kuzuia maoni ya makundi, asasi na taasisi za wananchi? Akifanya hivyo atajuaje maoni yao? Atajuaje kuwa anapingwa katika hatua hii au ile? Atajuaje malalamiko na lawama ambazo serikali yake inabebeshwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Askofu Kakobe atakuwa ameona kuwa  baadhi ya madhehebu duniani yameingia katika mageuzi ya fikra. Yanakiri kuwa hayawezi kuhudumia “roho za waamini na na waumini bila kufikiria hali zao kidunia.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Roho za wafuasi wa madhehebu hayo zinakaa katika makasha yaitwayo “miili.” Kama miili itakuwa imedhoofika kwa njaa, maradhi na ujinga, hata kile wanachohubiriwa ili kukidhi matakwa ya roho hakitaingia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kunahitajika maandalizi ya roho. Haya yanaanza kwa kutambua kuwa kuna mwili. Kwamba mtu yupo; tunamwona na anashikika; siyo wa kufikirika. Kwamba ana mahitaji ambayo sharti ayapate ili aweze kuwa na uwezo wa kupokea mahubiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maandishi makuu kwamba binadamu haishi kwa mkate (chakula) peke yake yana makali ya pili; kwamba binadamu haishi kwa kuhubiriwa tu, bali kwa chakula pia na mahitaji mengine ya mwili. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukamilifu wa mwili unahitajika ili kupata ukamilifu wa roho. Mbingu siyo kwa watu masikini na hohehahe peke yao, bali hata matajiri kwa njia ya halali ambao wamepondeka mitima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ndiyo maana hata kama rais hataki Waraka au Muongozo, sharti ajitahidi kuvisoma, kupata maoni ya wengine, kuyachambua na hata kuyatumia kutekeleza yale ambayo maandishi yanasema hata kulalamikia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali kuna tabia ya serikali kuhusudu ukimya wa watu, ujinga na umasikini wao. Hii ni mitaji mikubwa ya serikali nyingi duniani. Vilevile ni mitaji mikuu ya baadhi ya madhehebu ambayo yanataka “kupakia” wananchi mahubiri kama anayepakia gunia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanaohubiriwa ni watu wenye akili timamu na wana uwezo wa kufikiri. Wakipata fursa ya kujadili na kufanya maamuzi, wanaitumia vilivyo kuliko kutaka rais awanunie, awazibe mdomo na hivyo kuziba akili zao ili wasifikiri. Hapa Kakobe  amekwama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Fikra za Kakobe zinafanana na za serikali ya Zanzibar ambayo juzi ilitangaza kupiga marufuku Waraka na Muongozo. Bali hii siyo mara ya kwanza kwa serikali ya Zanzibar kufanya viroja.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna wakati ilizuia ufundishaji wa historia (na fasihi?) mashuleni kwa madai kuwa historia inaibua chuki na uhasama. Haya ni maamuzi ya woga, ya kidikiteta; yenye shababa ya kudhibiti akili za watu na utashi wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbona nchi hii inahitaji nyaraka nyingi tu zenye maoni mbalimbali, tena ya mirengo tofauti. Zinaweka wazi maoni ya waandishi na wananchi. Zinasaidia watawala kuona  walikofika au walikoshindwa kufika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuziba maoni ni kujifungia katika kiza cha ujinga na ubabe wa kidikiteta. Ni kuhalalisha juhudi za wananchi, kupitia asasi mbalimbali, kuandaa mikakati halali ya kuondoa watawala madarakani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata katika ukimya wa uzao wa udikiteta, mawasiliano hupenya na mikakati huundwa. Kipi bora: Kupata maoni ya wananchi au kusubiri hasira zao zijae vifuani na utokee mlipuko?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;(Makala hii itachapishwa katika safu ya SITAKI ya gazeti la &lt;strong&gt;Tanzania Daima Jumapili &lt;/strong&gt;toleo la 6 Septemba 2009)&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-8129516451706573636?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/8129516451706573636/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=8129516451706573636' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8129516451706573636'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8129516451706573636'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/09/askofu-kakobe-atamani-udikiteta.html' title='ASKOFU KAKOBE ATAMANI UDIKITETA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SqIpSDNFupI/AAAAAAAAAFs/wG_y39zXWh4/s72-c/Kakobe.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-1896749645478990858</id><published>2009-08-22T03:21:00.000-07:00</published><updated>2009-08-22T03:28:58.151-07:00</updated><title type='text'>MAANDALIZI YA VURUGU UNGUJA NA PEMBA</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/So_IGGx5j2I/AAAAAAAAAFk/13SRZxzyAxM/s1600-h/Amani+Karume.gif"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 158px; height: 200px;" src="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/So_IGGx5j2I/AAAAAAAAAFk/13SRZxzyAxM/s200/Amani+Karume.gif" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5372732887700967266" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;              &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Mategemeo, subira bila mafao Pemba&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI mtu mzima, nyumbani kwake na familia yake, aambiwe na mgeni jinsi ya kuvaa vizuri, kulea watoto, kuweka nyumba yake katika hali ya usafi, kutafuna polepole na kutoacha mdomo wazi wakati anapopiga miayo.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtu mzima atang’aka na kuuliza iwapo ni wewe umekuwa ukimwelekeza kwa miaka yote hadi kufikia umri huu wa miaka 50. Atakushangaa. Aweza kukujibu kwa hamaki na hasira.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndivyo ilivyokuwa mwishoni mwa wiki. Marafiki wa serikali za Muungano wa Tanzania na Baraza la Mapinduzi Zanzibar (BMZ), waliona serikali hizi zinataka kupiga miayo bila kuweka kiganja mdomoni. Wakazibonyeza: Tahadhari!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mabalozi wa nchi za Jumuiya ya Ulaya, Marekani, Japan na Canada wamezitaka serikali za Muungano na BMZ kuwa makini na demokrasi. Hii inafuatia hatua ya kusimamisha zoezi la kuhakiki daftari la wapigakura kisiwani Pemba, wiki mbili zilizopita, baada ya milipuko miwili ya mabomu katika makazi ya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katiba ya Zanzibar inazingatia kuwa kila raia ana haki ya kupiga na kupigiwa kura. Vigezo vya raia vipo. Lakini sheria ya uchaguzi inaongeza matakwa mengine, kuwa kila anayetaka kujiandikisha kupiga kura sharti awe na hati ya ukazi Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa wiki mbili sasa kumekuwepo migongano kisiwani Pemba. Siyo kwamba wote wanapinga kuwepo matakwa ya hati ya ukazi, bali hata wenye hati wanadai kuwa wamekuwa hawaandikishwi au kuhakikiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukazi umekuwa ukazi. Hivi kitambulisho kuwa ulipiga kura uchaguzi uliopita hakitoshi? Hivi kuwa na kitambulisho cha uraia kwa misingi ya ulipozaliwa, kukulia na bado unaishi hapo hakutoshi? Hivi ilikuwa lazima vitambulisho vya ukazi vitakiwe hivi sasa wakati wa uhakiki wa daftari; kwa nini kazi hiyo haikufanywa mapema?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tayari kuna madai ya wananchi kwamba wamekwenda kwenye vituo wakiwa na hati ya ukazi, hati ya kupigia kura uchaguzi uliopita na vyeti vya kuzaliwa, lakini wakakataliwa kuhakikiwa. Hapa ndipo penye utata.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Madai mengine ni kwamba kuna waliokwenda vituoni, bila hati ya ukazi, bila hati ya kuzaliwa, bila hati ya kupiga kura katika uchaguzi wowote uliopita, lakini wakapokewa na kuhakikiwa. Wananchi wanajiuliza: Huu ni mradi maalum wa serikali, upendeleo maalum na wa makusudi au ngekewa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, kabla serikali haijasimamisha uhakiki katika daftari la kupiga kura, tayari kulikuwa na makundi hapa na pale; yakijadili hali hii. Utata unazidi inapokuwa Pemba ni ngome ya chama kikuu cha upinzani Visiwani – Chama cha Wananchi (CUF).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuzingatia ushindi wa asilimia 100 wa CUF katika uchaguzi mkuu uliopita kisiwani Pemba, kila sehemu ya kisiwa hicho ni ngome ya chama hicho. Hatua yoyote ile basi, ya kuweka taratibu ngumu au zenye utata katika kuhakiki majina ya wapigakura, itafikiriwa kuwa inalenga kuhujumu CUF.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira ambamo hakuna maelezo ya serikali yanayoeleweka juu ya chanzo cha milipuko ya mabomu; na kutokana na milipuko hiyo kuwa ndani ya ngome ya chama cha upinzani, tayari kuna madai kuwa milipuko ililenga kutishia wapigakura wa upande wa upinzani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuwa milipuko ya mabomu imefanya watu watawanyike na kukimbilia mafichoni; yawezekana wengi wasirudi kujiandikisha kupiga kura. Inawezekana wengine wakaja wakati wa kujiandikisha umeisha au wakachukia na kukata tamaa kwa kuwa siasa imeingiliwa na tishio kwa maisha yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yote haya yakifanyika, haitakuwa kwa manufaa ya chama kikuu cha upinzani au hata vyama vidogo. Yaweza kuwa faida kuu kwa chama kilichoko ikulu ya Zanzibar. Kwa ufupi, inaweza kueleweka kuwa kura za wananchi tayari zimepigwa mabomu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katikati ya hali hii mabalozi wa Ulaya, Marekani, Canada na Japan wamesema kuwa hawafurahishwwi na hali kama ilivyo Kisiwani Pemba. Hilo tu, kwamba “Ndugu yangu, ziba kidogo mdomo wakati wa kupiga miayo.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya mabalozi tayari imeleta kizaazaa. Serikali ya Muungano imejibu kwa kusema iliishawaonya mabalozi wasiingilie mambo ya ndani ya nchi; huku Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ikisema mabalozi wamevuka mpaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UV-CCM) nao umekuja juu, mwenyekiti wake Hamad Masauni Yusuf Masauni akisema kuwa Tanzania iliishatoka kwenye ukoloni na kwamba  “mabalozi wafanye kazi zilizowaleta nchini.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kauli kali zisizojibu hoja ya mikingamo katika uhakiki wa daftari la wapigakura kisiwani Pemba. Ni kali lakini ambazo sharti zitolewe ili kujikakamua ingawa wote waliosema wanajua kuwa mataifa hayo ni wabia wa serikali, tena kwa muda mrefu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyovyote itakavyokuwa, tayari zoezi la kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu  na uchaguzi mkuu mwaka kesho, limeingia doa. Kwa mtindo huu, inawezekana madoa mengi yataingia hata kabla siku ya kudondosha karatasi katika sanduku la kura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali jambo moja ni muhimu hapa. Serikali, pamoja na ukali wake na kauli nyingine ambazo zinaweza kuwa zinakiuka itifaki, zinaelewana vema na wafadhili. Ukiangalia kwa undani utaona vema kwamba wanasikika kupingana lakini hawatupani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachofanyika ni kutaka kuonekana kuwa waliona jambo likifanyika; walihisi siyo sahihi; walilitolea kauli kwamba hawakufurahishwa; lakini mambo yanakwenda kama wanaoyafanya wanavyopenda. Hiyo ndiyo “itifaki.” Hakuna malumbano zaidi wala kukabana shingo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna aliyetegemea kauli za mabalozi kutikisa lolote katika mazingira ya sasa Pemba na huenda Unguja na Bara, anashauriwa avute pumzi. Kile ambacho mataifa haya wabia wa serikali wanaonekana wanaweza kufanya, huwa hakifanywi au kinafanywa kwa njia isiyofikia kubadilisha maamuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani ni mataifa haya ambayo utasikia yamekwishaahidi au tayari yametoa mabilioni ya shilingi kwa ajili ya shughuli za uchaguzi nchini – katika hali yoyote ile ambamo utakuwa umeandaliwa na watawala. Hatimaye watatangaza uchaguzi kuwa huru na wa haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Imekuwa hivyo siku zote. Itakuwa hivyo mwaka huu na mwaka kesho. Anayetaka mabadiliko katika msimamo wa mataifa ya nje kuhusu suala hili, atasubiri sana. Na kunakucha, kunakuchwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sharti nguvu ya mabadiliko itoke kwa wanaoumia pindi wanapoweka mguu chini. Kuna mwiba. Kama unachoma, basi uondoe. Wanaoona unachechemea huenda wakadhani siku hizi una mikogo. Chukua hatua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii ilichapishwa katika&lt;/span&gt; &lt;span style="font-style:italic;"&gt;Tanzania Daima Jumapili,&lt;/span&gt; &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;toleo la 16 Agosti 2009)&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-1896749645478990858?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/1896749645478990858/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=1896749645478990858' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1896749645478990858'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/1896749645478990858'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/08/maandalizi-ya-vurugu-unguja-napemba.html' title='MAANDALIZI YA VURUGU UNGUJA NA PEMBA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/So_IGGx5j2I/AAAAAAAAAFk/13SRZxzyAxM/s72-c/Amani+Karume.gif' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-6794139850061428945</id><published>2009-08-22T03:10:00.000-07:00</published><updated>2009-08-22T03:30:14.062-07:00</updated><title type='text'>UDIKITEA MBAYA SASA WAJA</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/So_GLdaSvmI/AAAAAAAAAFc/qFQufttWaMQ/s1600-h/SPIKA+SITTA.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 195px; height: 200px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/So_GLdaSvmI/AAAAAAAAAFc/qFQufttWaMQ/s200/SPIKA+SITTA.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5372730780652060258" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;CCM na ukandamizaji wa fikra&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;                    &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;   Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiwe nguzo ya nne ya dola. Nilitarajia kikae uwani, kijirembe kwa vipodozi na mavazi ya kila aina, kisubiri harusi, lakini kisikoromee nguzo yoyote ya dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jijini Dodoma, kupitia kwa mjumbe wa NEC ambaye pia ni spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano, CCM ilitoa onyo kwa wawakilishi wa wananchi kwamba wamepanua mno midomo yao; wamekijeruhi chama na serikali; sasa wachunge sauti na kauli zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wabunge wameambiwa, kupitia kwa Spika Samwel Sitta kuwa wasijadili masuala yahusuyo “ufisadi” ndani ya bunge bali ndani ya vikao vya chama, kikiwemo kikao cha wabunge wa CCM. Wameamriwa. Kutofanya hivyo ni “kukiumiza” chama na serikali na kuneemesha upinzani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Amri hizo kutoka Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, hakika zinakwenda kinyume cha matarajio. Kinyume cha utaratibu. Kinyume cha mwenendo wa “klabu” za kisiasa. Kinyume cha Katiba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo CCM inakaripia spika wa bunge; eti ametoa mwanya mkubwa kwa wabunge kuisakama serikali. Eti ameruhusu serikali idhalilishwe. Eti ameacha mwanya mkubwa unaotumiwa na baadhi ya wabunge kukaripia viongozi wa chama, serikali na hata viongozi wastaafu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CCM inataka spika wa bunge awanyamazishe wabunge. Awakemee na kuwakoromea pindi wanapokuwa wakali kwa serikali. Kwani sasa inadaiwa wabunge “wamekuwa huru kupita kiasi” na kwamba wanastahili kudhibitiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua ya CCM inalenga kufanya bunge kuwa kamati ya chama. Inalenga kufanya spika kuwa mhamasishaji wa shughuli za chama na serikali ndani ya bunge. Inalenga kugeuza bunge – kutoka msimamizi na mshauri wa serikali – kuwa sekretarieti ya chama na serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiyo ndiyo maana ya kukemea spika kwa madai kuwa “ameruhusu uhuru zaidi.” CCM inataka bunge lililopigwa pasi; lile la “Chama Kushika Hatamu” – magereza ya siasa yaliyoandaliwa na Pius Msekwa kutukuza mfumo wa chama kimoja. Watawala wanataka bunge liimbalo sifa na utukufu wa chama kimoja na kiongozi mmoja mwenye fikra ngumu na “zinazodumu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupitia kwa spika aliyenyamazishwa, wabunge wanyamaze. Kupitia kwa wabunge walionyamaza, wananchi nao “wafyate mkia.” Kuwepo na sauti moja, kauli moja – ile ya klabu moja siasa – CCM na serikali yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa ndipo panakuza ukinzani. Wananchi hawakuchagua wabunge ili wabunge waitetee serikali. Mbona serikali ina watetezi wengi bungeni? Dhana ya uwakilishi ina maana ya jicho, sikio na mdomo wa nyongeza wa wananchi; vilivyopewa jukumu la kusimamia na kushauri serikali na kutetea maslahi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa chama na serikali kutafuta kunyamazisha wananchi kupitia vijembe, vitisho na tuhuma dhidi ya spika, ni kutaka kuwa na taifa la mazezeta; linalosikia bila kuelewa; lisilofikiri na lisiloongea kwa kuwa limekatwa ulimi; lisilotoa hata mgumio wala mguno kwa kuwa limetumbukizwa katika woga usiomithilika.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kesho CCM yaweza kukemea Jaji Mkuu kwa madai kuwa hukumu zake zinakuwa kali kwa viongozi wa chama, serikali na viongozi wastaafu. Jaji mkuu aweza kusutwa kwa kutoa uhuru zaidi kwa mahakimu na majaji wenzake na kwamba uhuru huo “unadhoofisha serikali.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikifikia hapo, siyo tu uhuru wa kufikiri utakuwa umeingiliwa sana na hata kunyongwa; uhuru wa watu wa kuishi utakuwa mashakani. Hii ndiyo hatari kubwa zaidi. Kwa chama kilichoko ikulu kutamani taifa lililokimya, ni sawa na kutamani kutawala miti, mawe na wanyamapori. Siyo watu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja kuu inayowagawa wabunge hivi sasa na ambayo CCM na serikali hawataki kusikia wabunge wakiijadili hadharani, ni juu ya “ufisadi.” Chama hiki na serikali yake vinataka hoja hii ijadiliwe kimyakimya kwenye vikao na siyo kweupe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni hoja inayoeleweka kwa urahisi. Inayopenya katika vichwa vya wengi. Inayojadilika. Inayoweza kuhusishwa na maisha ya kila mmoja popote alipo. Inayofanya watu wafikiri, waulize maswali na watake majibu. Inahusu uhai wao – kufa au kupona.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wa watawala, hoja hii ni mbaya. Inaingiza watu wengi kwenye mjadala ambao serikali haiwezi kudhibiti. Ni mjadala huu mpana unaoweza kuathiri maamuzi ya wananchi wakati wa uchaguzi wa viongozi. Unaleta vidonda mwilini mwa serikali na CCM na unatonesha daima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mjadala huu ungehusu vyama vya upinzani, usingetafutiwa mbinu za kuuzima. Ungekuwa kipenzi cha watawala na ungekuzwa na kuenezwa nchini kote ili penye uoza paonekane. Yote yangefanywa “kwa jina la demokrasi na uhuru wa maoni.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali mjadala unapolalia watawala, basi hakuna suala la demokrasi wala haki na uhuru wa maoni. Unakuwa mchungu. Unatishia walioko kileleni. Unatishia uhalali wa utawala wa serikali. Matokeo yake, serikali inatafuta kuuzima kwa njia yoyote ile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vitisho vilivyoelekezwa kwa spika vinakwenda mithili ya hadhithi ya Karumakenge – maji yanatishia kuzima moto; moto unatishia kuchoma fimbo; fimbo inatishia kupiga Karumakenge; na Karumakenga anakubali kwenda shule. Bali hii ni hadithi ya kimaendeleo na endelevu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa NEC ya CCM inatishia kufukuza Spika Sitta; Sitta atishie kuadhibu wabunge; wabunge watishie kugomea wananchi wanaowatuma; na wananchi wanyamaze – kama maiti. Kunahitajika ukimya ambamo kishindo cha mende kitasikika kama tsunami. Hii si hadithi; ni hali halisi inayopingana na maendeleo. Ni ujima mchafu.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukame wa fikra na mijadala ambao CCM inataka utawale bunge na jamii kwa ujumla, ni msiba mkubwa kwa taifa. Hii ni sababu ya kutosha kupinga kuendelea kuwepo utawala wa serikali ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CCM, kama vilivyo vyama vingine, ni klabu ya kisiasa – moja ya asasi za kijamii za kuragbishia raia kushiriki katika siasa na utawala wa nchi zao. Kama klabu hii imeshindwa kutambua umuhimu wa uhuru na haki ya kuwa na maoni; na inatafuta njia za kuvihujumu; basi heri klabu ife kuliko uhuru wa watu na watu wenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahooo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii itachapishwa katika gazeti la&lt;/span&gt; &lt;span style="font-style:italic;"&gt;Tanzania Daima Jumapili,&lt;/span&gt; &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;toleo la Jumapili tarehe 23 Agosti 2009)  &lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-6794139850061428945?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/6794139850061428945/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=6794139850061428945' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6794139850061428945'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6794139850061428945'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/08/udikitea-mbaya-sasa-waja.html' title='UDIKITEA MBAYA SASA WAJA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/So_GLdaSvmI/AAAAAAAAAFc/qFQufttWaMQ/s72-c/SPIKA+SITTA.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-9215617881186884718</id><published>2009-08-11T02:41:00.000-07:00</published><updated>2009-08-11T02:48:22.445-07:00</updated><title type='text'>WAFUGAJI 'WAKIRUDI KWAO' ITAKUWAJE?</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SoE-UtyUENI/AAAAAAAAAFU/KPn5hH_PXtg/s1600-h/Ng%27ombe.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 200px; height: 129px;" src="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SoE-UtyUENI/AAAAAAAAAFU/KPn5hH_PXtg/s200/Ng%27ombe.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5368640756411273426" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Yatatokea maafa makubwa ya kuangamiza mali na maisha&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;br /&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SERIKALI haiwezi kukimbia wajibu wake wa kurejesha amani kwa jamii za wafugaji nchini, kusitisha uvamizi na uporaji ardhi yao ambao umewafanya wakose mahali pa kuishi na kulishia mifugo yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho serikali inatakiwa kufanya sasa, ni kupanga na kutangaza maeneo maalum ya makazi ya wafugaji na maeneo ya kufugia na kuchungia mifugo yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbukumbu zinaonyesha uzoefu wa serikali kutangaza mbuga za wanyama; mbuga za kuwindia kwa kuua wanyama au kuwinda kwa kutumia kamera (kupiga picha). Ni nadra kusikia serikali ikipanga, kutenga na kutangaza maeneo ya wafugaji na mifugo yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani kinachoendelea hivi sasa, katika mbuga za Loliondo, wilayani Ngorongoro, katika mkoa wa Arusha, ni mwendelezo wa ukatili usiomithilika unaoendeshwa kwa baraka na mipango ya serikali, kuwang’oa wafugaji kama magugu na kuwaacha juani wakauke.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya miaka mingi ya uporaji, uliopangwa, kutekelezwa na kuratibiwa na serikali – ya kikoloni na ile ya uhuru – au matendo ya watu binafsi ambayo hayakukemewa na mamlaka, watawala sasa wanageuza kibao na kusema wafugaji ni wavamizi. Wanasema warudi walikotoka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mfano wa Kilimanjaro Magharibi (West Kilimanjaro). Wakazi wa maeneo haya, wengi wao wakiwa Wamasai, walifukuzwa katika maeneo ya Enduimet na kuswagwa hadi chini ya mlima Kilimanjaro.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Madai yalikuwa kwamba wafugaji wanaharibu mazingira kwa “kuchezea vyanzo vya mito ya asili.” Baada ya wafugaji kuondolewa, wakulima wa kizungu na baadhi ya Waafrika walivamia maeneo ya mlimani na kuharibu vyanzo vya maji ambavyo wafugaji walitunza kwa miaka nendarudi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii, vyanzo vya maji vya Olmorog, Lelanwa, Kamwanga na Engare-Nairobi, vimepungukiwa maji na vingine kukauka kabisa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hali hii, nani ameharibu mazingira: Wafugaji walioyalinda miaka yote au wavamizi, wakiwemo wazungu wa Kiholanzi waliodai kuyalinda lakini wakayakausha kwa kilimo na ukosefu wa mipango endelevu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Madai hayohayo yalitumiwa kufukuza wafugaji kutoka eneo lote la Monduli. Wananchi katika eneo lenye rutuba la Lorkisalie waliswagwa nje kwa madai kuwa wazungu wanataka kuanzisha kilimo cha mbegu za maharage.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kilimo hakikudumu. Ardhi ikawa tayari imechafuliwa kwa wingi wa mbolea za kisasa na kupoteza uasili wake. Wafugaji wakawa wemeswagwa kama mifugo, kwenda “kokote kule” bila kutengewa sehemu maalum iliyopangwa na serikali kwa ajili ya kuishi na machungio.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naberera katika Simanjiro, lilikuwa eneo zuri la wafugaji. Ardhi nzuri iliyokuwa ikinawirisha watu na mifugo yao ilinyakuliwa na wazungu na Waafrika, wakiwemo viongozi wa siasa na serikali. Wafugaji wakatupwa nje.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Twende Kiteto. Sehemu kubwa ya ardhi iliyokuwa makazi ya wafugaji na malisho ya mifugo, ilivamiwa na baadhi ya viongozi wa siasa, serikali na matajiri wengine. Wafugaji wengi wakaswagwa nje na wakuja wakaanzisha kilimo cha mahindi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika eneo hili, wakulima wamefanya kufuru. Wameparamia hata vilima vya kijani vilivyotunzwa na wafugaji. Wameingilia vyanzo vya maji vilivyoneemesha mifugo. Sikiliza sauti ya mfugaji:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Sisi wachache tuliokuwa timesalia, tukawa kama ulimi katikati ya meno,” anaeleza mmoja wa wafugaji wa Kiteto. Wafungwa. Huu ukawa mwanzo wa mapigano kati ya wakulima na wafugaji katika eneo hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uporaji ardhi ya wafugaji ulienea na bado unaendelea katika maeneo mbalimbali. Angalia Serengeti ambako wafugaji wengi waliswagwa kama mifugo yao, nje ya makazi yao na malisho ya mifugo, kwa madai ya kuhifadhi wanyamapori.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serengeti ambayo imekuwa makazi ya wanyamapori ainaaina; kutambuliwa na kutangazwa dunia nzima kuwa kivutio cha aina ya pekee kwa watalii na labda “boma” la mwisho la viumbe wa porini, imelindwa na kuhifadhiwa na wafugaji ambao mifugo yao ilifanya urafiki na wanyamapori.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Njama za kutawanya, kutelekeza na labda hata kuteketeza wafugaji katika Serengeti ni njama za ngazi ya kimataifa. Vimeandikwa vitabu vingi juu ya maajabu ya Serengeti lakini nafasi ya mfugaji kama mhifadhi wa wanyama hao haijazingatiwa. Itaonekana picha ya mfugaji kwenye jalada tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii, ndani ya mbuga za Serengeti, ambamo wafugaji waliishi, kufugia ng’ombe, mbuzi na kondoo na kuchunga mbuga na wanyamapori, ndimo kumejaa wanaoitwa wawekezaji. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wawekezaji hawa hawataki hata kuona mtoto wa mfugaji akikatiza, wala ng’ombe akinusa maji ya mto ambao wafugaji wametunza kwa maisha yao yote. Kutoka ng’ambo moja ya mto hadi nyingine limekuwa kosa kubwa la kusababisha vifungo kwa walinzi wa Serengeti na watoto wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwekezaji ndani ya Serengeti hataki kuona mwananchi; anataka kuona watalii kutoka nje. Anataka kuona shilingi tu itokanayo na wanyamapori ambao wananchi wametunza na kuhifadhi kwa kipindi chote cha maisha yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa pia wafugaji waliswagwa nje ya maeneo yao walikoishi, kufuga na kulinda wanyamapori. Wafugaji walilinda wanyamapori kwa kuwa hawawali; wao hula mifugo yao tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi sasa wafugaji waliobaki Serengeti wanaishi kwa mfano uleule wa “ulimi katikati ya meno.” Wamefungwa. Wamebanwa mithili ya watumwa; katika nchi yao iliyopata uhuru wa kisiasa yapata miaka 50 iliyopita. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yaliyotokea West Kilimanjaro, Monduli, Simanjiro, Kiteto na Serengeti, ndiyo hayohayo yaliyotokea Ngorongoro: Kuvamiwa kwa ardhi na kufukuzwa kwa wakazi wa miaka yote ili kuanzisha “Jamuhuri za Wanyamapori.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maeneo yote tuliyojadili yamekuwa yakiitwa Masailand – kuanzia Kilimanjaro Magharibi hadi Lobo – kwenye mpaka wa Kenya. Haya ndiyo yalikuwa makazi ya Wamasai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Historia inasema Wamasai ni taifa linalotembea. Linalohamahama. Lina mifugo na linafuata maji na malisho. Lakini ukweli ni kwamba taifa hili lilikuwa limetua na kuridhika katika maeneo yaliyojadiliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama ambavyo hakuna mwenye asili ya mahali alipo, kwamba vizazi vilivyotangulia viliumbiwa hapo (imani) au viligeukia hapo kutoka nyani wangurumao (sayansi), Wanilotiki kutoka milima ya Golani sasa walikuwa wametua na “ardhi” yao kupewa jina na wakoloni kuwa Masailand.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jirani na Wamasai walikuwa Wabarbaig ambao pia katika miaka ya hivi karibuni walitendewa unyama huohuo wa kuporwa ardhi na kufukuzwa kwenye makazi yao na kuanza kutangantanga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mradi wa Basotu, Arusha wa kilimo kikubwa kilichoitwa “mashamba ya ngano ya Basotu” yaliyoendeshwa na Wakanada, uliwaacha Wabarbaig bila makazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hii hakuna mashamba. Kilimo kimeshindikana. Yalikuwa mazingaombwe. Ardhi imechoka. Limebaki vumbi tupu. Wabarbaig waliishatupwa nje; wanatangatanga na mifugo yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mtindo huu, jamii za wafugaji zimefanywa za wakimbizi wasiotakiwa popote pale ndani ya nchi yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Soma majina haya: Lomnyak Siololo, Kayiok Leitura, Ngiliyayi Ndoinyo, Ngirimba Ndoinyo, Sepekita Kaura na Tokore Siololo. Hawa ni miongoni mwa waathirika wakuu wa mipango ya serikali iliyofukarisha wananchi na kuneemesha watu kutoka nje ya nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi hawa, kutoka kijiji cha Ololosokwan, wamechomewa nyumba, mazizi ya ng’ombe na wanaswagwa, wao na ng’ombe wao, kutoka walikoishi kwenda kusikojulikana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kutokana na mfumo huu wa uvamizi na uporaji makazi, wafugaji wametafuta makazi na malisho katika maeneo mengine ya nchi hii. Ni nchi yao. Ni kwao kama kulivyo kwa wengine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatizo hapa ni kwamba serikali, iliyoshiriki kuwafanya wafugaji kuwa watu wa kutangatanga kuliko asili yao, ndiyo inatangaza kuwa wafugaji “warudi kwao.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa wafugaji wanauliza” “Kwetu ni wapi?” Swali kubwa hapa ni hili: Wafugaji wakirudi kwao, itakuwaje?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jibu: Vitatokea vita vikubwa vya kuangamiza watu na mali zao; kile kilichoimbwa kwa miaka mingi kuwa ni amani na utulivu wa nchi, kitatoweka kama ukungu wa asubuhi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutatokea vita kwa kuwa maeneo walikofukuzwa wafugaji sasa ni mbuga za wanyama zilizomo mikononi mwa waporaji wakubwa wa maliasili wanaopewa upendeleo kwa kuitwa “wawekezaji.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unawekeza nini katika mbuga yenye wanyama waliolindwa na kuhifadhiwa na wafugaji kwa karne na karne? Hapana. Hapa unachuma usipopanda. Vita vya wafugaji kujaribu kurudi walikotoka vitakuwa vikubwa na huenda endelevu na kwa gharama kubwa ya maisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wafugaji wakirudi walikotoka – Kilimanjaro Mashariki, Lorkisalie, Simanjiro, Kiteto na Basotu (Barbaig), kutakuwa na vita ambavyo vitaharibu mashamba ya “wakubwa,” majumba ya kifahari, mifumo ya maisha ambayo tayari imejengwa na kuangamiza uhai wa watu na viumbe vingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali amani pia haiwezi kuwepo kwa kuendelea kuwa na watu wanaofukuzwa kila waendapo kwa kuambiwa “rudi kwenu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati umefika kwa serikali kufanya mambo yafuatayo, yakiwa hatua za haraka na za mwanzo ili kusitisha uonevu na udhalilishaji wa wafugaji na kuepusha migongano na hata vita:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, kusimamisha na kuacha kabisa mipango ya kufukuza wafugaji kutoka makazi yao ya sasa. Hili litahusisha kuacha kuchoma moto makazi yao. Nchi hii ni yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, kurejesha wafugaji mahali pao katika sehemu ambako walifukuzwa hivi karibuni na kupanga, kuunda na kutangaza makazi ya wafugaji na malisho ya mifugo yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu, serikali isitishe na izuie uchochezi wa wanasiasa na baadhi ya watendaji wake kwa wafugaji waliohamishwa zamani, kwa kuwaambia kurejea walikotoka, kwani hilo litazua vita ya maangamizi makubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nne, wafugaji wakaribishwe pale walipo; waelezwe kuwa safari yao imefika mwisho; watengewe ardhi kwa makazi na malisho bila kujali walikotoka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tano, maeneo yaliyopangwa kwa ajili ya ufugaji yatengwe rasmi kwa alama zinazoonekana. Wafugaji wenye mifungo mingi, washirikishwe katika kugharimia  miundombinu muwafaka katika mpangilio mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sita, serikali ijenge mahusiano mapya kati yake na wakulima badala ya kuwakemea na kuwalaani kwa madai dhaifu kuwa mifugo mingi “inaharibu mazingira.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Saba, serikali iondokane na dharau na kutojali; badala yake itambue kuwa mifugo – mamilioni ya ng’ombe, mbuzi na kondoo wa wafugaji wanaotangatanga katika nchi yao – ni mali na kwamba kwa kuweka mazingira bora, itakuwa ya manufaa zaidi kwa wafugaji na taifa kwa jumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nane, wafugaji washawishiwe na asasi za kijamii na serikali, “kusimama” na kubaki walipo sasa na kufanya makazi hayo kuwa ya kudumu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tisa, wafugaji washirikishwe katika kuandaa makazi, malisho na miundombinu. Kwa mfano, malisho yawe ya maeneo makubwa ambamo mifugo itahama kutoka sehemu moja kwenda nyingine, ndani ya eneo husika, ili kuruhusu upatikanaji wa chakula katika maeneo walikochungiwa kwanza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umuhimu wa kushirikisha wafugaji katika kuandaa miundombinu unatokana na kuwepo kwa baadhi yao wenye uwezo kifedha kutokana na kuwa na mifugo mingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni hao ambao wana uwezo wa kuchangia ujenzi wa mipaka ya kutenganisha makazi na malisho, kujenga mabwawa wakati serikali inasaidia katika ujenzi wa miundombinu mingine kama ile ya maji, elimu, barabara na afya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumi, ndani ya mipaka ya maeneo ya malisho, na wafugaji wakiwa sehemu ya jamii ya wakulima katika maeneo husika, ndimo inaweza kuendeshwa elimu juu ya upunguzaji wa mifugo kwa ufugaji wa kisasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua hii itakayoendana na wafugaji kukataa kuendelea kusukumwa nje ya mahali walipo, itajenga mshikamano mkubwa kati ya wakulima na wafugaji na kufanya uhasama kuwa historia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipata fursa ya kuongea na Luteni mstaafu Lepilall ole Molloimet (60) kuhusu suala hili. Aliwahi kuwa mbunge kwa miaka tisa, mkuu wa wilaya kwa miaka 12 katika wilaya za Kiteto, Babati, Korogwe, Musona na Rombo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Molloimet ambaye sasa ni mfanyabiashara, anasema wakati umefika kwa Wamasai na wafugaji wengine kukataa kuhama kutoka walipo sasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anasema, “Wamasai wabaki pale walipo. Wakatae kuondoka. Washiriki elimu lakini wabaki na mila na desturi zao nzuri; wachague viongozi wao wazuri, wajiamini, wawe jasiri na wakatae kuonewa; wawe tayari kukosoa na kukosolewa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Molloimet anasema anawashangaa wabunge katika maeneo ambako wananchi wanaswagwa kama mifugo kutoka kwenye makazi yao ya miaka mingi. Anasema wabunge hao, kwa kukaa kimya, ina maana wanaunga mkono unyama ambao wananchi wanatendewa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Kwa ufupi, wabunge hawa wanastahili kujiuzulu maana wameshindwa kazi ya kuwakilisha na kutetea waliowachagua,” anasema Molloimet.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akiongea kwa sauti ya uchungu, Molloimet anaungana na baadhi ya wananchi wa Olorien, Soitsambu na Magaiduru-Lorien huko Ngorongoro.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Amasema, “Dunia haituelewi. Tunafukuza Wamasai katika maeneo yao; lakini tunakaribisha Wazungu na Waarabu! Nani atatuelewa. Mimi nasema tu kwamba wafugaji wanataka amani.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa zinasema juzi Jumatatu, ulifanyika mkutano juu ya hali ya wafugaji na hifadhi ya Loliondo. Miongoni mwa waliohudhuria mkutano huo katika kijiji cha Ololosokwan ni wawakilishi wa Chama cha Wanasheria wa Mazingira (LEAT).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengine ni asasi ya kimataifa ya utetezi wa wafugaji tawi la Tanzania (PINGOs), maofisa wa Idara ya Wanyamapori, Ortelo Business Corporation Limited ya Nchi za Falme za Kiarabu (OBC) walioshikilia eneo kubwa ya mbuga ya Loliondo na wajumbe wa kijiji cha Ololosokwan.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haijafahamika waliongelea nini. Lakini taarifa zinasema watakuwa walijadili hatua ya serikali ya kuchoma makazi na maboma ya mifugo wakilazimisha wananchi kutoka kwenye makazi yao na katika vijiji vilivyoandikishwa kisheria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii itachapishwa katika gazeti la&lt;/span&gt; &lt;span style="font-style:italic;"&gt;MwanaHALISI&lt;/span&gt; &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;toleo la 12 Agosti 2009)&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-9215617881186884718?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/9215617881186884718/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=9215617881186884718' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/9215617881186884718'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/9215617881186884718'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/08/wafugaji-wakirudi-kwao-itakuwaje.html' title='WAFUGAJI &apos;WAKIRUDI KWAO&apos; ITAKUWAJE?'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SoE-UtyUENI/AAAAAAAAAFU/KPn5hH_PXtg/s72-c/Ng%27ombe.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-5185995047130394961</id><published>2009-08-01T03:10:00.000-07:00</published><updated>2009-08-01T03:28:00.100-07:00</updated><title type='text'>KUSAJILI SIMU ZA MKONONI NI UHALIFU</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQYS2wd_PI/AAAAAAAAAFM/jqivWCiSkpU/s1600-h/iphone_1.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 190px; height: 200px;" src="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQYS2wd_PI/AAAAAAAAAFM/jqivWCiSkpU/s200/iphone_1.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5364939768320621810" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;BADALA YA KUVUMBUA WANADIDIMIZA TEKNOLOJIA&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;        &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;   Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI mpango wa kusajili wamiliki wa simu za mkononi na namba zao kama serikali inavyotaka na kama inavyoshinikiza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni kwa kuwa sababu zilizotolewa na serikali; na kusisitizwa na Mamlaka ya Udhibiti ya Mawasiliano Tanzania (TCRA); zile ambazo zinatumiwa kuhalalisha usajili; siyo za msingi na hazina mashiko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali ina maoni kuwa simu za mkononi zinatumiwa vibaya. Inadai zinatumiwa kufanya uhalifu. Kwamba zinarahisisha mawasiliano ya wale wanaopanga uhalifu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uhalifu unaotajwa ni pamoja na kutukana, kupanga wizi na, au hujuma; kutoa vitisho kwa watu mbalimbali; kutoa taarifa za upotoshaji na wakati wote huo bila muhusika kufahamika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inadaiwa kuwa namba na wamiliki wakisajiliwa, itakuwa rahisi kujua nani ametoa taarifa, uzushi, vitisho; na kupitia namba ipi ya simu. Serikali inafikiri kwa njia hii, kazi yake ya “ulinzi wa amani” itakuwa imerahisishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ina maana kwamba serikali na wenye makampuni ya kutoa huduma za simu za mkononi, wamekula njama. Wamekubaliana kuingilia mawasiliano ya wananchi na labda wamekuwa wakifanya hivyo, tena kwa kiwango kikubwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uhalifu hauletwi na simu. Uhalifu hauletwi na siri katika mawasiliano. Vyombo vya mawasiliano ni mifereji ya kupitishia taarifa. Unahitaji mawasiliano mapana kukabili uhalifu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira ambamo waliopewa jukumu la kuzuia uhalifu ndio wenyewe wanaofanya uhalifu; unahitaji vyanzo vya siri vya kuibua uhalifu. Pale penye uhalifu unaofanywa na watawala na wateule wao, unahitaji mifereji isiyo bayana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira ambamo aliyeibua uhalifu anatendewa kama mhalifu; na wakati mwingine jina lake kuwekwa wazi kwa wahalifu – wawe wakwapuzi wa mabilioni benki, wauza dawa za kulevya au majambazi yaliyokubuhu – unahitaji mifereji ya mawasiliano isiyo bayana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tujenge hoja kuwa mtu asiyejulikana, ambaye amekupelekea simu ya vitisho kupitia namba ya simu isiyojulikana ya nani, basi ameshindwa kutekeleza anachotaka. Tumuone kama anayetishia tu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali inawezekana akawa anatishia kweli. Hapo atakuwa ametoa onyo; amekupa muda wa kujipekua na kujiandaa. Simu hiyo pia yaweza kukupa fursa ya kuacha kile ulichokuwa ukifanya na ambacho tayari wengine wameona hakifai au kinawadhuru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira ya Tanzania, taarifa juu ya kifo cha mahabusu ambaye maofisa wa magereza hawataki kijulikane, inapatikana kwa mfereji wa siri wa mawasiliano – simu isiyoweza kutambulika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Orodha za wahalifu walioko serikalini, karibu sana na watawala wakuu, inafikia vyombo vya habari kwa njia ya simu ya siri. Maagizo ya siri ya kuumba au kuua, yanapatikana kwa njia ya namba ya simu isiyosajiliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kilio cha wananchi wakazi wa Kilosa, mkoani Morogoro na Ololosakwani, mkoani Arusha juu ya unyama wanaotendewa, kinafikia vyombo vya habari, watawala na dunia nje ya nchi, kwa njia ya simu isiyopekuliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dereva wa mbunge ambaye hajalipwa mshahara wake kwa miezi sita, anatumia namba isiyosajiliwa kuwasiliana na vyombo vya habari na hata spika wa bunge ili angalau kilio chake kiweze kusikika na       yeye apate kushughulikiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hayo ndiyo matakwa ya mazingira ya sasa. Dereva akijulikana kuwa analalamika, basi anafukuzwa kazi. Karani akifahamika kuwa “amevujisha” majina ya wezi idarani, anafukuzwa kazi palepale.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ofisa Utumishi akijulikana kuwa hakushirikishwa katika ajira ya watoto wa bosi wake, siyo tu atafukuzwa kazi; aweza kuundiwa kosa kubwa hata la kufikishwa mahakamani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfugaji wa Kilosa na Ololosakwani akijulikana kuwa ni yeye aliyepeleka taarifa za askari wa FFU kuchoma nyumba zao na kutesa wananchi, huenda “akapotezwa” katika mazingira ya kutatanisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tetesi nyingi kwa vyombo vya habari, watumishi makini na waaminifu ndani ya serikali, taasisi zake na hata makampuni na mashirika binafsi; zinapatikana kwa mifereji ya siri, kwa kuwa “uwazi” limekuwa neno tupu la wanasiasa na halimo katika utendaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tetesi hizi zimekuwa muhimu kwa hatua za kwanza za uchunguzi. Wakati aliye karibu aweza kukuona na kuongea nawe, aliye mbali anapata fursa ya kukupa taarifa bila wasiwasi wa kuchukuliwa hatua na wale wanaodaiwa kutenda uhalifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, wakati baadhi ya waandishi wa habari wamesahau au wamedharau msingi muhimu wa “kutunza chanzo cha taarifa,” baadhi wametaja majina ya waliowapa taarifa na kuwaweka hatarini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Simu ambazo haziwezi kuingiliwa ni nyenzo kuu ya wananchi na wafanyakazi waliomo katika karakati za kupigania uhuru na haki zao. Watapanga jinsi ya kukutana hadi jinsi ya kufanya walichopanga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Asasi za kijamii zilizomo katika ushawishi ainaaina, huweza kutumia njia hii ya simu isiyo wazi ili taarifa zisivuje, hadi hatua ya mwisho iliyolengwa na kufanya hoja zao kuibuka kwa kishindo na labda kupatikana kwa mafanikio yaliyotarajiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uhalifu hauletwi na simu za mkononi ambazo namba zake na wamiliki hawajulikani kwa watawala. Nyenzo hii ya mawasiliano ya teknolojia ya kisasa inaweza kutumiwa na mkweli au mwongo; mtiifu au mwasi; mwaminifu au mkora, “mungu” au “shetani.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliwahi kusema Karl Marx, kuwa uhalifu ni tasnia pana inayoajiri kuanzia mtu wa kada ya chini kabisa kama mesenja hadi profesa wa masuala ya jinai. Hapa kuna hoja ya “uendelevu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kadri jamii zinavyopita katika nyakati tofauti za maendeleo na kuingia na kutoka katika ustaarabu tofauti, ndivyo zinavyokumbana na matatizo mapya na changamoto mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mlango wa kusumumiza hautoshi kuziua mwizi. Chomeko siyo tena chombo cha ulinzi. Kofuli haifai tena kulinda nyumba. Magrili yanatawanywa kwa moto wa gesi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kukua kwa maarifa ya kuhudumia jamii kunaenda sambamba na uvumbuzi katika tasnia ya uhalifu. Huwezi kuzuia hili. Lakini serikali inakwenda mbali. Inafikiri kuwa simu ambazo haijui ni za nani, zinaleta au zinachochea uhalifu(!?) Huu ni udhaifu mbaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Badala ya kutafuta mbinu za kisasa za kukabiliana na kile wanachoona ni tatizo, serikali na makampuni ya simu wanatafuta kufanya teknolojia na matumizi yake kuwa butu. Huu ni mkasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali inaziba mifereji ya taarifa za siri kuhusu utendaji wake. Hasa kuziba kasi ya kuenea kwa taarifa juu ya mambo inayofanya lakini hayakustahili kufanywa na waliopewa madaraka ya utawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa serikali imeingilia uhuru wa mawasiliano wa mtu binafsi. Inakana maendeleo ya teknolojia. Inaziba upenyo wa kupitishia kilio na tetesi. Serikali inatenda uhalifu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii iichapishwa katika gazeti la Tanzania daima Jumapili, toleo la 22 Julai 2009) &lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-5185995047130394961?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/5185995047130394961/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=5185995047130394961' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5185995047130394961'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5185995047130394961'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/08/kusajili-simu-za-mkononi-ni-uhalifu.html' title='KUSAJILI SIMU ZA MKONONI NI UHALIFU'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQYS2wd_PI/AAAAAAAAAFM/jqivWCiSkpU/s72-c/iphone_1.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-3268758266580545289</id><published>2009-08-01T02:31:00.000-07:00</published><updated>2009-08-01T02:44:28.355-07:00</updated><title type='text'>KASHFA YA MEREMETA  YAWEZA KUZAMISHA SERIKALI</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQOHT7wpqI/AAAAAAAAAE8/ocra2LIR9FE/s1600-h/askari.bmp"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 200px; height: 138px;" src="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQOHT7wpqI/AAAAAAAAAE8/ocra2LIR9FE/s200/askari.bmp" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5364928574877902498" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;MAWE YAKISEMA, SERIKALI ITAUMBUKA&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;            Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI waziri Jeremiah Sumari achokoze Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kwa kutumwa au kwa sababu zake binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majeshi ni mawe makubwa. Majabali. Miamba. Majeshi ni wagumba. Majeshi yakitaka kuzaa sharti yakubali kufa polepole; kwa maana kwamba atokee wa kuyapasua ili yatoke mengi kwenye mawe makubwa au miamba. Hapo hayabaki mojamoja na imara tena.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na kawaida majeshi ya nchi hayachokozwi na mtu wa ndani wala wa nje. Wachokozi huchokoza nchi na watawala wa nchi zilizochokozwa huagiza majeshi yake kwenda mstari wa mbele na kukunja uchokozi kama jamvi la wageni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini uchokozi uliofanywa na waziri Sumari ni wa ndani na unaweza kufanya mawe makubwa, miamba kutamani kutoa sauti na kusema hayataki kupasuliwa; yaachwe kama yalivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akijibu swali la Dk. Willibrod Slaa juu ya ufisadi ndani ya mradi wa Meremeta, Sumari alitoa majibu ya vitisho. Alimwambia mwakilishi wa Karatu (CHADEMA) aachane na hoja ya ufisadi ndani ya Meremeta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiasi kinachodaiwa kupitia Meremeta kwenda mifuko isiyojulikana si haba. Ni zaidi ya Sh. 155 bilioni. Waziri anamwambia mbunge aachane na hoja ya Meremeta kwa madai kuwa mradi huo ulikuwa wa jeshi; kwamba ni suala nyeti na labda ni kuingilia suala la usalama wa taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri anataka kulazimisha mawe kusema. Mawe yatabaki kimya juu ya ahadi zao; juu ya mipango yao na silaha zao; juu ya mikakati ya sasa na baadaye; juu ya mbinu mpya walizopata katika medani ya vita; juu ya wanachopanga kufanya hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukimya huu ni kama jua, mvua na upepo vipigapo kwenye mwamba na mwamba ukavumilia. Zaidi ya hapo, miamba husema. Miamba mingi imeota juu ya mizimu ya kale iongeayo wakati wa jua kali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inawezekana, siku moja unapita karibu na miamba hiyo, wakati wa jua kali, ukasikia mtu akikuita kwa sauti ya juu sana – mara mbili au mara tatu – na usimwone.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wale dhaifu wa moyo huweza kuanguka chini na kuzimia; wengine humudu kukimbia hadi nyumbani kwao, wakitweta na kulowa jasho mwili mzima huku wakiishiwa na kauli. Mawe, majabali, miamba imeamua kusema!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati huo hujawahi kuichokoza. Hujailalamikia wala kuituhumu. Hujaisingizia wala kuihusisha katika miradi bubu ya watawala. Inasema tu. Inabubujika. Sembuse utakapoihusisha na wizi, uporaji, ukwapuaji, au kwa ujumla – ufisadi!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikae kimya? Sitaki waziri Sumari achokoze miamba na yenyewe iseme kwamba haijui Meremeta ni nini na ya nani. Kwamba haijawahi kunufaika na kampuni hiyo. Kwamba mafao yaliyotokana na Meremeta hayafahamiki jeshini. Kwamba hayakuingia jeshini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki waziri achokoze miamba ianze kukohoa na kunong’ona na hatimaye kulipuka. Miamba hii inajua kuwa fedha za kuendesha jeshi hutoka kwenye bajeti ya serikali inayosomwa na kupitishwa bungeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miamba hii inaelewa vema kwamba wakati Meremeta wanaanzisha mradi walihamisha wananchi kutoka makazi yao. Walihamisha hata kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa na kutawanya askari katika vijiji kwa kutumia mikokoteni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si wananchi – raia, wala askari walionufaika na mafao ya Maremeta baada ya kuanza kuvuna kutokana na mgodi. Shule na zahanati vilivyong’olewa havijarudishwa. Bwawa kubwa la maji lililokuwa sehemu ya uhai wa watu na viumbe anuwai, halijarejeshewa hadhi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki watawala jeshini wajitokeze na kuiumbua serikali juu ya matumizi haya. Sitaki wapatikane watumishi wa Wizara ya Ulinzi na kuthibitisha kuwa hawajawahi kupanga fedha za Meremeta au sehemu yake katika matumizi ya wizara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki maofisa wa ngazi za kati jeshi waanze kufurukuta na kusema hawataki kusingiziwa katika suala la ukwapuaji na hivyo kujitokeza na ukweli utakaoangamniza hadhi ndogo ya watawala iliyosalia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki askari wa vyeo vya chini ambao wanajua vema kilichokuwa kinaendelea waanze kujitokeza na kusema walichoona na nani hasa walikuwa wavunaji wakuu wa Meremeta na siyo jeshi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wala sitaki askari wakumbushe serikali kwamba Tume ya Jaji Bomani iliishasema kuwa Meremeta si mali ya serikali bali ni ya binafsi. Labda likisemwa na wao ndipo serikali itasikia na waziri Sumari ataelewa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani anataka azibuliwe masikio kuliko alivyofanya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Aliiambia Kamati ya Bunge kuwa Meremeta haimo katika orodha ya mashirika ya umma na kwamba ofisi yake haijawahi kuikagua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mei mwaka jana tulipeleka baruapepe kwa benki ya Nedcor Trade Services ya Afrika Kusini kuhusiana na suala hili. Hatukujibiwa. Tuliwaandikia Deutsche Bank AG ya Uingereza. Hawakujibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini kwa kufuatilia kinachoendelea ni kwamba serikali haifanyi lolote. Imetafuta mahali pa kuegesha na kusahau hoja za wananchi wanaotaka kujua huyu Meremeta ni nani na fedha alizochota alizitumia wapi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matumizi ya visingizio vya jeshi, kama anavyosema Sumari, hayana uzito tena. Hayamtishi yeyote. Wananchi, wachunguzi na wengine wanaotafuta ukweli wangestuka na hata kuogopa kama wangekuwa wameingilia undani wa shughuli za jeshi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini hili la kikampuni cha Meremeta halimtishi mtu. Badala yake linaweza kuiweka serikali pabaya, kwani inaendelea kujichanganya; kuficha ukweli na hatimaye kusema uwongo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatari kubwa inaweza kuzuka pale mawe, majabali na miamba itakaoamua kuvunja kimya; siyo lazima kwa mikutano ya hadhara bali kwa mn’ong’ono tu ambao hatimaye utavuma kama upepo wa kimbunga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na askari – hiyo miamba – ni watoto wa watu masikini na wao ni masikini pia. Hawana cha kupoteza kwa kusema ukweli wanaoujua. Hapo ndipo serikali itaumbuka zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani anaweza kuiondolea aibu serikali kwa kusema ukweli na kuijengea heshima na uhalali? Kama siyo mawaziri wake, nani hasa? Tusubiri majabali yaite wakati wa jua kali na kwa mzizimo wahusika wazimie?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uwezekano wa aliyezimia kupitiliza hadi dunia nyingine ni mkubwa kuliko aliyesimama. Kwa nini serikali ijiingize kwenye majaribu tata? Ukimya unaidhalilisha serikali na kuiondolewa uhalali. Itoboe kilichomo ndani ya Meremeta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii ilichapishwa katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili Juni 2009) &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-3268758266580545289?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/3268758266580545289/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=3268758266580545289' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3268758266580545289'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3268758266580545289'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/08/kashfa-ya-meremeta-yaweza-kuzamisha.html' title='KASHFA YA MEREMETA  YAWEZA KUZAMISHA SERIKALI'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQOHT7wpqI/AAAAAAAAAE8/ocra2LIR9FE/s72-c/askari.bmp' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-2397409154223415297</id><published>2009-08-01T02:15:00.000-07:00</published><updated>2009-08-01T02:30:25.849-07:00</updated><title type='text'>WOGA WA SERIKALI SASA WAPINDUKIA</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQLIPYZ9TI/AAAAAAAAAE0/tSiOuXyDWJ0/s1600-h/Jakaya-Mrisho-Kikwete.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 100px; height: 140px;" src="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQLIPYZ9TI/AAAAAAAAAE0/tSiOuXyDWJ0/s200/Jakaya-Mrisho-Kikwete.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5364925292300858674" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;br /&gt;Serikali inapotishia uhuru wa mijadala&lt;/span&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;     Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI watawala wakatae Waraka wa Kanisa Katoliki ambao hasa ni elimu ya uraia ambayo ni mhimu kwa maisha ya kiroho, kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa wananchi na taifa lao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wa watawala, kukataa elimu kunaweza kuonekana kuwa jambo la kawaida; kwani kwao, elimu ambayo haikutolewa na watawala, siku zote huonekana ama yenye kasoro au isiyofaa kabisa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitu kibaya zaidi ni kwa watawala kutaka kuzuia raia kusambaza elimu ya uraia kwa jamii kupitia asasi zao. Ni kama inavyodhihirika sasa kwa baadhi ya walioko kwenye utawala kupinga Waraka wa madhehebu ya Katoliki unaochokoza mawazo tu juu ya kupata viongozi bora nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimesoma waraka husika. Maudhui ni yaleyale ambayo tumezoea kuyasikia kanisani, misikitini na katika maoni ya watu wanaojali maslahi ya taifa. Lakini mara hii yameandikwa. Yamewekwa kwenye hali ya kudumu kwa muda mrefu na yataweza kufanyiwa rejea. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ufupi waraka ni wito kwa wananchi kukaa chini, kujadili na kuamua nani wanastahili kuchaguliwa kuwaongoza; wawe watu wa mwenendo na tabia gani. Sikuona zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waraka unafanya jambo moja kubwa ambalo watawala hawataki kusikia. Unawapa wananchi fursa, uwezo na ujasiri wa kujadili na kuamua nani wawachague kuwa viongozi wao. Basi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waraka unahimiza utekelezaji wa haki ya kila raia katika kupata uongozi; unahimiza wajibu wa kushiriki katika kuchagua viongozi na uongozi, kuanzia ngazi ya chini kabisa hadi ya taifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni waraka huu unaohimiza njia ya kukaa pamoja, kufanya uchambuzi na ikiwezekana kukubaliana juu ya vigezo vya kijamii mahali husika katika kupata viongozi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini hata baada ya majadiliano ya pamoja, bado kila raia ana uwezo na haki ya kupima nani, kati ya wagombea, anazidi wengine na anaweza kuwa kiongozi bora. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waraka unasaidia kuchokoza mbongo za washiriki katika mjadala kwa kueleza kiongozi bora ni nani. Huu ni uchokozi tu. Katika mjadala, wahusika waweza kutanua wigo wa waraka na kugusa hata hoja ambazo hazijafukuliwa na kuweka vigezo vyao. Hawafungwi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupatikana kwa mwafaka wa vikundi, makundi au jumuia pana juu ya nani wanafaa kuongoza, kunawatwisha wapigakura wajibu wa kipekee wa kufuatilia viongozi na utendaji wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Labda ni hapa ambapo watawala wanapata shida kuelewa au wanaelewa lakini wanaogopa. Wanafikiri kuwa zinaweza kupatikana kura za makundi na wao kuenguliwa kwa njia ya sanduku la kura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali ni ukweli usiopingika kuwa ujinga na umasikini ni mitaji mikubwa ya watawala. Kadri raia wengi wanavyobaki katika ujinga ndindindi, ndivyo watawala wanavyozidi kujichimbia ikulu mwaka baada ya mwaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna kitu kinaitwa elimu ya uraia ambayo hutolewa na watawala, basi ni ile ya kueleza uwezo wa serikali, majukumu yake, mafanikio yake, utii na heshima ya raia kwa mamlaka. Ni vitisho vitupu vinavyopora ujasiri wa wananchi na kuzidisha upofu na ujinga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Woga mkubwa wa serikali ni kwamba wananchi wakijua kinachoendelea ndani ya utawala, wataasi kimyakimya au watalipuka na kudai mabadiliko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hali hii, ikipatikana elimu ya kufanya watu wafikiri, wajadili kwa pamoja hoja kuu zinazowahusu; zinazohusu uhusiano wao na watawala na jinsi ya kufanya maamuzi;  basi serikali hujawa na woga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujasiri uliolengwa kupatikana kwa njia ya waraka wa kanisa unatishia “elimu” ya watawala; unabomoa kuta za siri, unaandaa jamii kuachana na ujinga na kuasisi mabadiliko ya fikra, bila kujali rangi, mahali mtu alipozaliwa wala imani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kanisa lisipofanya haya, na hasa leo, litabaki asasi kama asasi nyingine zisizo na uhai. Asasi zote, yakiwemo madhehebu, hazina budi kutambua kuwa haziwezi kuhudumia kiroho wale ambao ni dhaifu kimwili. Sharti zisimame nao na kuwapa ujasiri wa kufikiri na kutenda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mahali pengine, kuhubiri dini kwa watu masikini kumeongeza ukandamizaji. Wakati watawala wameishi katika uhondo, wametumia ghiliba ya kisiasa na mahubiri ya dini kufanya raia wawe butu zaidi na kulazimishwa kukiri kuwa hali waliyomo ndio matakwa ya Mwenyezi Mungu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua ya baadhi ya madhehebu kufundisha umuhimu wa kuwa na jamii inayofikiri, inayoelewa kinachotendwa na watawala, inayodai haki na inayojadili jinsi ya kuwa na viongozi na uongozi bora, ni ya kukaribisha na siyo kusuta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Walioingia katika uongozi kwa njia ya wizi, ghiliba, upendeleo na hujuma kwa wengine, ndio wanaweza kutilia mashaka fursa mwanana ya wapigakura kukaa pamoja na kujadili jinsi ya kupata viongozi bora.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna swali: Kila madhehebu yakitoa waraka wa uchaguzi itakuwaje? Jibu: Kwa kuzingatia maudhui ya waraka wa kanisa Katoliki, madhehebu mengine yatasema mambo hayohayo lakini kwa maneno tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja ya kuwa na kiongozi bora haina sura ya madhehebu. Hoja ya kukaa chini na kujadili nani katika jamii yenu anaweza kuwa kiongozi, haina hata harufu ya madhehebu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja ya uongozi bora ina misingi katika utu wa mtu na haki ya kila raia bila kulalia  imani za dini – za asili na za kuja – isipokuwa pale imani hizo zinapokuwa zinakiri kwelikweli kile tunachotaka: Haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, katika mazingira ya uhuru wa maoni, siyo madhehebu tu yenye haki ya kutoa elimu ya uraia kwa kutumia waraka; bali mashirika na asasi zote za kiraia na watu binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachohitajika siyo madhehebu au imani ya mtu au asasi, bali hoja ya kiongozi bora kutoka katika jamii na bila kujali ni wa madhehebu yapi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Elimu ya uraia inayopendekezwa na waraka wa sasa, haifuti wala kudhoofisha sifa za mgombea uongozi au mpiga kura ambazo zinatajwa na Katiba ya nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo ndivyo zinaweza kuwa nyaraka nyingine za madhehebu mengine, asasi nyingine, mashirika mengine na watu binafsi. Zitakuwa zinaimarisha sifa na misingi ya Katiba kwa kuwezesha raia kushiriki vya kutosha na kutumia utashi wao kupata viongozi bora. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waraka uwe mwanzo tu. Tunatamani pamoja na viongozi wa dini kuombea amani na utulivu, waanze kufikiria kuacha kuombea watawala na kuwafanya sehemu ya utukufu wa Mungu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni maombi ya viongozi wa madhehebu mbalimbali ambayo yamesimika madikiteta; kuwadumisha kwenye tawala na kuwaaminisha wananchi kuwa mamlaka waliyonayo (madikiteta) inatoka kwa Mungu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sharti wanaoogopa waraka wa kanisa Katoliki waanze kuogopa kutoombewa na kubarikiwa. Labda huu ndio utakuwa mwisho wa mwanzo wa kutenda mema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii itachapishwa katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili toleo la 2 Julai 2009)&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-2397409154223415297?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/2397409154223415297/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=2397409154223415297' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2397409154223415297'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2397409154223415297'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/08/woga-wa-serikali-sasa-wapindukia.html' title='WOGA WA SERIKALI SASA WAPINDUKIA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQLIPYZ9TI/AAAAAAAAAE0/tSiOuXyDWJ0/s72-c/Jakaya-Mrisho-Kikwete.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-3569762822940535897</id><published>2009-07-31T02:42:00.001-07:00</published><updated>2009-08-01T02:46:30.846-07:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>&lt;a href="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnK9BR8FC1I/AAAAAAAAAEs/xga8UoPzGXs/s1600-h/scan0022.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 200px; height: 140px;" src="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnK9BR8FC1I/AAAAAAAAAEs/xga8UoPzGXs/s200/scan0022.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5364557935844592466" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimewahi kula chakula kilichopikwa na kuandaliwa na walioko kwenye picha hii. Wanaitwa ANITA CATERERS. Inawezekana hata wewe umewahi kuonja mapishi yao. Bali nina uhakika kuna ambao hawajawahi. Wakati ndio huu. Ni rahisi kuwapata: Anita: Simu 0713 505312 na 0783063400 au S.L.P. 71775 Dar es Salaam, Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ofisa mmoja wa ubalozi wa nchi za nje aliyeonja chakula hicho alisema:"Najisikia kuwa Afrika na kuwa nyumbani mbali na nyumbani. Ni chakula ambacho kila mtu angependa kula na kukumbuka utamu wake siku hadi siku...Ni chakula chenye sura ya mataifa yote..."&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-3569762822940535897?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/3569762822940535897/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=3569762822940535897' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3569762822940535897'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3569762822940535897'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/07/nimewahi-kula-chakula-kilichopikwa-na.html' title=''/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnK9BR8FC1I/AAAAAAAAAEs/xga8UoPzGXs/s72-c/scan0022.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-2336792166335092211</id><published>2009-07-31T02:21:00.000-07:00</published><updated>2009-08-01T03:08:30.206-07:00</updated><title type='text'>CHAKULA CHENYE LADHA YA KARIBU NA MBINGUNI</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQUFL0jJOI/AAAAAAAAAFE/MmwmFXTLTR8/s1600-h/scan0022.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 200px; height: 140px;" src="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQUFL0jJOI/AAAAAAAAAFE/MmwmFXTLTR8/s200/scan0022.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5364935135410201826" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimewahi kula chakula kilichopikwa na kuandaliwa na walioko kwenye picha hii. Inawezekana hata wewe umewahi kuonja mapishi yao. Bali nina uhakika kuna ambao hawajawahi. Wanaitwa ANITA CATERERS. Wakati ndio huu. Ni rahisi kuwapata: Anita: Simu 0713 505312 na 0783063400 au S.L.P. 71775 Dar es Salaam, Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ofisa mmoja wa ubalozi wa nchi za nje aliyeonja chakula hicho alisema:"Najisikia kuwa Afrika na kuwa nyumbani mbali na nyumbani. Ni chakula ambacho kila mtu angependa kula na kukumbuka utamu wake siku hadi siku...Ni chakula chenye sura ya mataifa yote..."&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-2336792166335092211?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/2336792166335092211/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=2336792166335092211' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2336792166335092211'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2336792166335092211'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/07/chakula-chenye-ladha-ya-karibu-na.html' title='CHAKULA CHENYE LADHA YA KARIBU NA MBINGUNI'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SnQUFL0jJOI/AAAAAAAAAFE/MmwmFXTLTR8/s72-c/scan0022.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-7210682510119237911</id><published>2009-07-31T02:08:00.000-07:00</published><updated>2009-08-11T02:36:33.259-07:00</updated><title type='text'>WAFUGAJI WAFANYIWA UNYAMA WA KUTISHA</title><content type='html'>&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Ni katika &lt;/span&gt;Mbuga ya ‘Loliondo ya Mwarabu’&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;WAMEPOTEZA tabasamu. Nyuso zimekunjamana. Macho yanabubujikwa machozi. Hawana hamu na mgeni. Wewe waweza kuwa “haramia” anayerudi kumalizia uhai wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wanaume, wanawake na watoto ambao nyumba zao zimechomwa moto. Hawana pa kulala. Baadhi ya watoto hawajapatikana tangu walipokimbia milio ya mpasuko wa risasi na moto mkubwa uliotafuna nyumba zao kwa kasi isiyomithilika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiyo ni sura unayokumbana nayo katika eneo la Loliondo, mkoani Arusha, lililoko zaidi ya kilometa 400 Kaskazini Magharibi mwa mji wa Arusha. Hapa wafugaji wanalazimishwa kuhama ili kupisha “utalii wa uwindaji.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Njia ambayo wahamishaji wameamua kutumia ni ile ya kuchoma moto nyumba, maghala ya vyakula na maboma ya mifugo – ng’ombe, mbuzi na kondoo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkazi wa kitongoji cha Kirtalo-Karkarmoru katika kijiji cha Soitsambu anasema askari “waliovaa sare ya FFU” wakiwa na magari matatu ya aina ya Land Rover, moja likiwa na bendera nyekundu, ndio waliteketeza makazi kitongojini hapo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anasema walifika na kufyatua risasi angani huku wakiamuru wafugaji waondoke na ng’ombe wao. “Kufumba na kufumbua, askari wakaanza  kuchoma moto nyumba zetu (pote hapa, anaonyesha) na maboma ya ng’ombe.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unaonyeshwa lundo la majivu: Hapa ilikuwa nyumba ya baba. Hapa ya sisi watoto wake. Hapa lilikuwa ghala la chakula…Ndivyo ilivyo kote ambako moto umetumika kushinikiza wafugaji kuhama makazi yao. Ni msiba mkubwa.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzee Orkoskos Yiele anasema ana umri wa miaka 100. “Kaburi la baba yangu liko hapa. Kaburi la mama yangu liko hapa. Niondoke niende wapi?” anauliza huku machozi yakimdondoka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ana familia ya zaidi ya watu 60. Wote hawana mahali pa kulala. Wanakoka moto. Wanapika  kilichopatikana. Wanakula. Wanalala hapohapo nje wamezunguka meko – watoto kwa wakubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wiki mbili kabla ya kuchomewa nyumba, Mzee Orkoskos alikuwa na ugeni. Mmoja wa wageni alikuwa mwandishi Mussa Juma wa gazeti la Mwananchi aliyeko Arusha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mussa anakumbuka, “Hapa (akionyesha lundo la majivu), kulikuwa na nyumba nzuri tu kwa viwango vya huku. Tulikaribishwa na mzee Orkoskos, akatupa maziwa tukanywa na kuongea kwa muda mrefu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hakuna nyumba. Hakuna maziwa. Hakuna maboma ya ng’ombe, mbuzi wala kondoo. Hakuna furaha na vicheko. Ni kiza kisichobanduka nyusoni na ndani ya mitima ya wanakaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Orkoskos aliyeonekana kusononeka sana anasema, “Sijapotelewa fahamu; nimejawa hasira. Sina hamu ya kula. Wazazi wa watoto waliochoma mali zangu ni kama wajukuu zangu ambao hawana mahali pa kulala, mh…” (anashusha pumzi).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anaeleza kuwa mtoto wake wa kike alikuwa mjamzito wa miezi minane au tisa. Wakati anakimbia moto na risasi, mimba ilitoka na kichanga ambacho kilikuwa cha kiume kimefariki. “Nani anajua kingekuwa nani katika jamii yetu au nchi nzima?” anauliza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kati ya ng’ombe 1,000 wa mzee Orkoskos, 100 wamepotea (hadi Jumatano iliyopita). Alikuwa anaendelea kuthibitisha mifugo iliyopotea kati ya mbuzi 800 na kondoo 700 aliokuwa nao awali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Moto haukuchoma nyumba na mazizi peke yake. Ulichoma pia imani na utamaduni wa Wamasai. Mahali pa kufanyia tambiko, ambako ni moja ya sehemu muhimu kwa imani za jamii hii, napo palibakizwa majivu matupu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kitongoji cha Karkarmoru, Masambe Nguya anasema askari mmoja alipoona anatetemeka kwa woga, akammwagia mafuta ya petroli na “kunisukuma kwenye moto. Nilianguka chini kabla ya kuingia motoni; kutoka hapo nilikimbia bila kutazama nyuma.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anasema pamoja na mali nyingine, mbuzi wake wawili na mbwa wachanga wanne waliungulia kwenye nyumba yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hadi mwishoni mwa wiki, taarifa zilisema zaidi ya maboma 160 yalikuwa yameteketezwa katika eneo lote la Loliondo linaloitwa “Loliondo Game Controlled Area.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isidory Shirima anasema wafugaji wanatakiwa kuondoka kwenye maeneo hayo na “kurudi walikotoka.” Anasema walipewa miezi mitano ya kuondoka lakini wamekaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anawaonya waandishi kutoandika habari zinazolenga kuwachochea wafugaji na kwamba yeye ana jukumu la “kulinda na kutekeleza sheria iliyopo hadi itakapofutwa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Laiti Shirima angekutana na mzee Orkoskos  aliyekuwa analea makaburi ya wazazi wake ambao inaaminika walikufa wakiwa na umri mkubwa; na kujua kuwa kaya hiyo ina karibu karne mbili pale wanapoifukuza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukoo huu na koo zingine, umekuwa katika eneo hili hata kabla wakoloni wa Kiingereza hawajalitangaza kuwa mbuga ya wanyama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kawaida Wamasai hawali nyama ya pori. Hivyo wamekuwa walinzi wa wanyama ambao dunia inakuja kuona, kupiga picha na kuwinda. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Loliondo Game Controlled Area” ni eneo la ukubwa wa kilometa za mraba zipatazo 4,660. Hivi sasa eneo liko chini ya kampuni ya Ortelo Business Corporation (OBC) Limited ya Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu (UAE) ambayo mmiliki wake ametajwa kuwa Brigedia Mohamed Abdulrahim Al-Ali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama mkoloni wa Kiingereza, kama mwekezaji Ortelo Business Corporation Limited. Walichotaka na wanachoendelea kuhitaji ni wanyama tu. Siyo binadamu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Eneo la hifadhi, ambalo lina baadhi ya makazi yaliyoandikishwa kisheria kama vijiji, ni kubwa mno. Hata makao makuu ya wilaya, polisi, magereza, halmashauri, mji mdogo wa Wasso, vyote vimo katika eneo hili. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mujibu wa “miliki” hii, mtawala wa Ortelo anaweza kuchukua kijiko na kung’oa makao makuu ya wilaya au polisi, au hata kuyachoma moto kama askari walivyochoma makazi ya wafugaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jeuri hiyo inajidhihirisha kwa tangazo linaloingia moja kwa moja katika simu yako ya mkononi ya kampuni ya zain, pale unapoingia kwenye eneo hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ghafla unasikia ujumbe wa simu unaingia na          ukifungua unakuta yafuatayo kwa lugha ya Kiingereza: “Karibu Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu (UAE). Furahia kuwa kwako hapa kwa kutumia mtandao wa zain…” Hakika ni UAE ndani ya Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kuwepo kwa kampuni hii ya Arabuni ambako kunafanya wafugaji wawe na maoni makali dhidi ya Ortelo na serikali. Kila kitongoji unakokwenda, wahanga wanalaumu “Mwarabu” kuwa ndiye anashinikiza wahame.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leina Koipa wa kitongoji cha Olorien katika kijiji cha Ololosokwan anasema mtoto wake wa miaka minne, Meirish Koipa, alimaliza siku mbili vichakani akiwa amekimbia moto baada ya kuona makazi yao yanachomwa na askari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Huyu Mwarabu ndiye chanzo cha matatizo yetu. Hii ni mara ya pili ninachomewa nyumba. Wanachoma hapa nasogea pale. Sasa angalia nimeishaanza kujenga hapa. Itakuwa hivi mpaka watuue sote...” anaeleza Koipa kwa sauti ya uchungu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Julius Yiele (28) anasema, “Yote haya ni Mwarabu. Amehonga serikali na serikali sasa inatufukuza.” Nilipomwambia kuwa kauli hiyo ni kali na yenye madai makubwa, alijibu haraka, “Ndivyo ilivyo. Sisi ni wakazi wa hapa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naye Ormeron Narikai wa kitongoji cha Olorien anakumbuka kuwa alikuwa na Sh. 1,150,500 nyumbani. “Ziliungulia humo pamoja na sanduku langu jipya. Acha Waarabu watuue tubaki historia, lakini hatuhami,” anasema. Hapa unagundua uchungu uliokithiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali kivumbi cha kauli kilikuwa katika kijiji cha Ololosokwan, kwenye mkutano wa hadhara ambako wanakijiji walijadili uchomaji moto nyumba zao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzee Yohana Sinyiu (60), baada ya kuambiwa kuwa kuna waandishi wa habari, alianza kwa kuuliza iwapo wana uwezo wa kuandika ukweli ili taarifa zifike kwa watawala na nje ya nchi. Nilitakiwa kujibu swali hilo. Nilisema, “Uwezo tunao.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzee Sinyiu alisema, “Tanzania ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa. Imeridhia mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu. Ina Katiba. CCM ina ilani yake ya uchaguzi. Vipi serikali itutendee unyama jinsi hii?”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sauti ya ukali alisema, “Andikeni. Ishawishini serikali itutendee haki; itupe usalama kama ilivyokuwa. Sisi hapa ni CCM tangu wakati wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa na sasa Kikwete,” akitaja jina mojamoja la marais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama anayekaribia kudondokwa machozi, mzee Sinyiu anasema, “Hatujawahi kukaribisha upinzani hapa… Tunashangaa CCM kututendea hivi…”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkasa katika eneo hili unaelezwa vema katika ripoti ya kijiji yenye kichwa kisemacho, “Uharibifu uliofanywa na Operesheni ya OBC  na FFU dhidi ya wanakijiji cha Ololosokwan, tarehe 4 Julai 2009 saa 1 asubuhi hadi saa 4 asubuhi.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ripoti inataja majina ya waathirika wa operesheni: mkuu wa kaya na wote katika kaya husika. Jumla ya kaya 44 zilikumbwa na kimbunga hicho na watu 137 ama wamepoteza vifaa, vyakula, fedha, dawa za mifugo au mifugo. Ni hasara ya mamilioni ya shilingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mjadala wa ripoti hii ulikuwa mzito kutokana na kauli za wanakijiji. Babu Olonyo alisema, “Tunashangaa kuona mtu anatoka Arabuni anapewa ardhi, sisi hatuna mahali pa kuchimba choo, kupumzikia na hata kuzikana.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Sasa andika haya: Tumechoka kuishi… Mwambie mkuu wa wilaya na rais watupige bomu tufe tuishe,” alisema Olonyo akichuruzika chozi kutoka jicho la kushoto.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kanyo Ndoinyo (74) alisema, “Walikuja watawala wa Kiarabu, Kijerumani na Kiingereza. Wakatoka. Tukapata uhuru. Sasa ukoloni umerudi. Uhuru wetu umekwenda wapi?”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ephraim Kaula (54) anauliza, “Kumetokea nini katika awamu ya nne ya utawala,” na kuongeza “Tumekosa nini? Tumekaidi nini? Tuitwe wahanga wa nani… Sasa tutaendelea kulima. Tutajenga bila kujali kama tutakufa au tutapona.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msembi Ndoinye alisema, “Wanyama ambao Wazungu na Waarabu wanakuja kuona, kuwinda na hata kubeba na kupeleka kwao, tumewatunza sisi, lakini sasa shukrani ni kufukuzwa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nasha Leitura aliwakomalia waandishi wa vituo vya televisheni vya Channel Ten na Star TV watangaze kuwa kitendo cha kuwachomea nyumba na mali kimewafadhaisha; ni ukatili mkubwa na uvunjaji wa haki za binadamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Wewe mama (akimweleza mwandishi wa Channel Ten), usitangaze kidogokidogo. Toa yote kama ulivyoyaona na kuyasikia,” alisisitiza Leitura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naye Koya Timan alisema serikali imeanza kuzungumzia suala la fidia kwa waliopoteza mali. Mwanamke huyo aliuliza, “Fidia ni kitu gani? Watuache na ardhi yetu ili watoto hawa na watakaozaliwa wapate mahali pa kuishi. Inatosha tu kubakiwa na ardhi yetu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Mwambie rais arudishe Waarabu wake huko alikowatoa. Fikisha maneno haya kwamba sisi wanawake tumekutuma,” alisema Timan.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya Mwalimu Lukuine ilikuwa kavu na kali. “Serikali inatupeleka kama nyani; inaturudisha katika umasikini…hatuna imani na serikali hii.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwenyekiti wa kijiji cha Ololokwosan, Julius Kaura anasema, “Utaratibu wote wa ardhi umefuatwa. Kijiji kipo kisheria. Sisi tumezoea kufuata sheria. Lakini sasa serikali ndiyo haifuati sheria. Hii siyo sahihi,” alisema Kaura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiki ndicho kijiji pekee wilayani Ngorogoro ambacho kinajivunia wahitimu wawili wa chuo kikuu na ambacho kimetumia mapato yake yapatayo Sh. 146 milioni kusomesha wanafunzi 128 katika miaka minne iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Eneo lililo chini ya Ortelo lina uwanja wa ndege kwenye eneo linaloitwa Mumbarashani. Kuna madai kuwa ndege huingia na kutoka bila kukaguliwa hasa wakati wa msimu wa kuwinda. Lakini mkuu wa mkoa anasema kama hilo lina mashaka “basi wizara husika italiangalia.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mbuga hizo, kwenye kilima cha Masiendilo, ndiko kuna jumba kubwa la mfalme wa UAE ambako huwa anakaa wakati amekuja kuwinda. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mbuga hizi pia kuna kambi kubwa ya kufikia wageni wa mfalme na wengine wanaokuja kuwinda, pamoja na karakana kubwa ya magari katika eneo la Limawani ili kukamilisha madoido yanayohitajika kumhudumia mfalme wa UAE na wageni wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tangu mwaka 1992, mfame kutoka UAE na wageni wake, wamepata uhondo katika Loliondo, huku wafugaji wakipata kibano cha ama kusogezwa au kufukuzwa kabisa katika maeneo haya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msukumo wa sasa wa kufukuza wafugaji, hadi kuchoma moto makazi yao, unatokana na sheria mpya ya wanyamapori ya kutaka kutenganisha mbuga na makazi ya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hili, bila shaka Ortelo watapenda lifanyike haraka kabla sheria haijaanza kutumika ili eneo la kuwindia libaki pana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna taarifa kuwa Rais Jakaya Kikwete aliishafika kwenye kilima cha Masiendilo yaliko makazi ya mfalme, jambo ambalo linaweza kuongeza ugumu au kuleta wepesi wa kushughulikia maisha, mali na makazi ya wafugaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sasa mbuga ya wanyama ya Loliondo inabaki sehemu ya UAE kama tangazo la zain linavyosema. Maana yake ni kwamba Wamasai wafugaji na raia hawana chao; kwenye ardhi yao na ndani ya nchi yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali kuna haja ya kuchukua hatua, hata kufuta sheria na mikataba – vyote vya kilafi na kifisadi – vinayoharamisha makazi ya wazawa na kutukuza fedha za mwekezaji. Shabaha iwe kuheshimu na kulinda haki za wananchi wafugaji na wakazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais Kikwete ana uwezo mkubwa wa kuelewa hili; labda kama hataki na bila sababu yoyote. Kilio cha wananchi kilichorekodiwa hapa ni maarifa tosha kwa mwenye nia ya kuona haki inatendeka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahooo.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii ilichapishwa kwanza katika gazeti la MwanaHALISI toleo la Jumatano, 29 Julai 2009)&lt;/span&gt;&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-7210682510119237911?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/7210682510119237911/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=7210682510119237911' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/7210682510119237911'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/7210682510119237911'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/07/wafugaji-wafanyiwa-unyama-wa-kutisha.html' title='WAFUGAJI WAFANYIWA UNYAMA WA KUTISHA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-122998521034634887</id><published>2009-07-10T05:08:00.001-07:00</published><updated>2009-07-10T05:15:35.140-07:00</updated><title type='text'>TAKUKURU YAWEZA KUWA CHUO BADALA YA KOROKORONI</title><content type='html'>CHUO KITATOA ELIMU KWA WENGI&lt;br /&gt;   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI jengo kubwa la thamani ya Sh. 4.1 bilioni lililosimikwa jijini Dar es Salaam na kufunguliwa rasmi na Rais Jakaya Kikwete wiki iliyopita, litumike kufuatilia tu wala rushwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wala sitaki rais aagize tu uchunguzi wa rushwa na kuchukuliwa kwa hatua dhidiya wala rushwa katika vyama vya siasa na wakati wa uchaguzi wa Oktoba (serikali za mitaa) na uchaguzi mkuu 2010.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani jengo hili lingefanya makubwa zaidi. Hii ni kwa kuwa sitaki Taasisi ya Kuzia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) iwe taasisi ya kudumu (Samahani sana Dk. Edward Hoseah!).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa vyovyote vile TAKUKURU itakavyokuwa imeshonwa kisheria, taasisi hii haipaswi kuwa chombo cha kudumu. Yawezekana walioiunda ili idumu kadri rushwa inavyodumu, walikuwa na nia ya kuongeza ajira. Kwa maana hiyo, hawanabudi kuchunguzwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa usijali iwapo waliopendekeza “kuzuia na kupambana na rushwa” walikuwa rais, baraza la mawaziri au kwamba sheria ilitungwa na bunge. Kila mtu ana nafasi ya kupitiwa, kupotoka na kupotoshwa, kutojua, kusahau au kudharau; na daima kuna fursa ya kufanya mabadiliko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna awezaye kutabiri lini rushwa itaisha. Wala lugha ya kijeshi ya “kupambana” haina uwezo wa kumaliza rushwa. Rushwa yaweza kukua na kushamiri kutegemea mazingira ya utawala na watawala walioko madarakani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali rushwa huendana na vishawishi. Mahali ambako taratibu, kanuni na sheria vimeacha mwanya wa kutoa na kupokea rushwa, lazima rushwa itashamiri, bila kujali iwapo kuna taasisi tano 10 au 20 za “kuzuia na kupambana” na rushwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama madhara ya kutoa au kupokea rushwa ni madogo kuliko mafao ambayo mtoaji au mpokeaji atapata, basi rushwa itatolewa na itapokelewa. Kule kutokuwepo kizibo madhubuti ndiko kunatoa fursa na ndiko kishawishi na motisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuunda taasisi ambayo inafanya uchunguzi kwa “miaka yote,” inakamata, inasweka mahakamani watuhumiwa, tena kwa miaka yote, kuna uwezekano wa kufanya taasisi hiyo kuwa sehemu ya “porojo” za rushwa na hata kufanya baadhi ya viongozi wake kulenga na kulengwa na rushwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kazi za taasisi ya kuzua rushwa zinaweza kupimwa kwa tuhuma zilizoibuliwa na wafuatiliaji wake, zilizopokelewa kutoka kwa wananchi au kuelekezwa na viongozi, zilizochunguzwa, zilizothibitishwa, zilizofikishwa mahakamani na zilizoisha, kwa maana ya matokeo ya kesi mahakamani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kazi nyingine za taasisi zinapimwa kwa kuangalia upanuzi wa uelewa wa wananchi juu ya kazi zake na nafasi yao katika kusaidia kuibua wala rushwa. Hii ni eneo la elimu kwa umma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Eneo hilo la pili linalenga kufanya kazi ya kueleza na kufafanua maana ya rushwa, aina za rushwa, madhara ya rushwa na jinsi kila mwananchi anavyoweza kukabiliana na rushwa au kusaidia kutoa taarifa zenye lengo la kukabiliana nayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua mifano hiyo miwili kama kazi kuu za taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa. Ukiziagalia kwa mtizamo wa ukiritimba utaona taasisi ina jukumu kubwa, nene, zito lisiloisha na wakati mwingine, ambalo haiwezi kulikamilisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali ukiziangalia kazi hizo kuwa zinafanywa na taasisi, asasi na maeneo mengine katika jamii, utaona kuwa jengo kubwa lililofunguliwa Dar es Salaam halitakuwa na kazi ya kutosha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Karibu kila ofisi ya serikali inashughulikia suala la “kuzuia na kupambana na rushwa.” Asasi mbalimbali za kijamii zimelenga, hata bila kutamka, kuondoa rushwa ili shughuli zake ziende sawasawa na kwa mujibu wa matakwa ya jamii. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hatua hii, kuna haja ya kuwa na TAKUKURU inayofanya kazi za kupeleleza – kazi ambazo zinafanywa na polisi? Hivi polisi hawana uwezo wa kupelekewa vitonyo wakafanya uchunguzi wa jinai ya rushwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inalazimu kufanya mgeuko hata kama sheria ya TAKUKURU bado mbichi. Kwa jina tofauti lakini lenye maana ileile, taasisi hii iwe chuo maalum cha utawala kinachogusa nyanja zote za menejimenti – ndani ya serikali na sekta binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chuo hiki kinaweza kushirikisha taasisi nyingine, kama Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na kutoa elimu juu ya utawala, taratibu, kanuni na sheria zinazohusika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanafunzi wa chuo hiki ni wote waliomo serikalini, makampuni na mashirika yake, ofisi za makampuni na mashirika binafsi, wakufunzi kutoka vyuo mbalimbali ambao wanafundisha masomo katika eneo hili; asasi za kijamii zilizomo katika mapambano dhidi ya rushwa, wamiliki na waandishi wa vyombo vya habari; watumishi katika vyama vya siasa; wabunge na wanasiasa wengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ina maana kwamba kazi ya kuelimisha jamii juu ya rushwa, madhara yake, kuchochea wananchi  kuchukia na kupambana na vitendo vya rushwa, inaachwa mikononi mwa asasi zisizokuwa za kiserikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni asasi hizi, zilizo karibu zaidi na wananchi; zenye jukumu la kushawishi wananchi kukataa kutoa, kupokea rushwa na hata kuripoti vitendo vya rushwa; zisizo na maslahi katika rushwa kubwa au ndogo, ambazo zinaweza kukabiliana na rushwa maisha yote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfumo huu waweza kuondoa mashaka ya wengi kwamba taasisi kubwa ya kupambana na rushwa, iliyoundwa na serikali, inalipwa na serikali na kiongozi wake mkuu anateuliwa na rais, inaweza kuhongwa pia au kunyamazishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ina maana kwamba majengo yaliyofunguliwa jijini Dar es Salaam sasa yanakuwa chuo maalum kwa masomo ya utawala, huku rushwa likiwa moja ya masomo hayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maana kuu ni kwamba “TAKUKURU” kama taasisi kinakuwa chuo cha kutoa elimu ya kudumu na siyo taasisi ya kudumu. Elimu hii inadumu katika jamii kupitia asasi zake na vita vinaoenekana kupiganwa, majeruhi kuonekana na wafu kuhesabika, badala ya kusikika tu kupitia chombo cha serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa basi wafanyakazi wa kudumu wa TAKUKURU ama wanatafuta kazi mahali pengine; hasa katika asasi za kijamii au wanaomba kuajiriwa na chuo. Inawezekana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;(Makala hii itachapishwa katika toleo la Tanzania Daima Jumapili, 12 Julai 2009 katika safu ya SITAKI)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;&lt;/strong&gt;&lt;strong&gt;&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-122998521034634887?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/122998521034634887/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=122998521034634887' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/122998521034634887'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/122998521034634887'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/07/takukuru-yaweza-kuwa-chuo-badala-ya.html' title='TAKUKURU YAWEZA KUWA CHUO BADALA YA KOROKORONI'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-8373939920967194373</id><published>2009-06-30T05:57:00.001-07:00</published><updated>2009-06-30T06:19:50.075-07:00</updated><title type='text'>TUNAFIKIRI VIZURI NA KWA WEPESI KATIKA LUGHA TUNAYOJUA VIZURI ZAIDI</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SkoN9w3of0I/AAAAAAAAAEk/AcO8XGf-vX0/s1600-h/Profesa+Amandima+Lihamba.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 150px; height: 200px;" src="http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SkoN9w3of0I/AAAAAAAAAEk/AcO8XGf-vX0/s200/Profesa+Amandima+Lihamba.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5353106461824679746" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Serikali inavyoua lugha za asili Tanzania&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-style:italic;"&gt;•Sera zake zina sura ya ‘ndumia kuwili’ &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SERIKALI ina tabia ya “ndumila kuwili” kuhusu nafasi ya lugha za asili. Inaonekana ina utashi wa kuua lugha hizo kwa madai ya kukuza Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika Sera ya Utamaduni ya mwaka 1997 serikali inasema, “Jamii zetu zitaendelea kutumia na kujivunia lugha zake za asili kwa kuwa ndio hazina kuu ya utamaduni na maarifa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini katika Sera ya Habari ya mwaka 2003, serikali hiyohiyo inasema, “Lugha zitakazotumiwa na vyombo vya habari hapa nchini ni Kiswahili na Kiingereza.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika sera moja serikali inatambua kuwepo utamaduni na maarifa katika lugha za asili; katika sera nyingine serikali inasema hizo lugha zilizosheheni maarifa, zisitumiwe kwenye vyombo vya habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ni mpango wa kunyonga lugha za asili kwa kuzinyima pumzi – zisijitokeza kwenye vyombo vya kisasa vya mawasiliano mapana na hivyo kuteketeza hazina kuu ya utamaduni na maarifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Utamaduni na maarifa ni mazao ya akili. Ni matunda ya watu wanaofikiri na kutenda. Kinachoitwa hazina ya utamaduni ni mkusanyiko wa fikra na matendo ya watu katika jamii; katika kipindi maalum cha maisha yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika maana yake halisi, maarifa ni sehemu ya utamaduni pale tunapoainisha utamaduni kuwa ujumla wa maisha ya watu na mazingira yao katika jamii husika. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa kwa nini maisha ya watu wengi, walioko katika mila, desturi na maarifa yao, yawekwe kando katika matumizi ya vyombo vya habari? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ni ubaguzi wa aina yake, wenye sura ya unyanyapaa kwa mamilioni ya watu wasiozungumza Kiswahili wala Kiingereza.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kuzuia matumizi ya lugha za asili kwenye mikutano na katika vyombo vya habari, ni ubaguzi wenye madhara yafuatayo:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, ni kutaka kuua lugha husika. Ni kuua utamaduni na maarifa yaliyomo ambayo yalipatikana na yanaendelea kupatikana kupitia lugha hizo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maarifa hayo, ama yanaendelea kuundwa, yapo na yalikuwa hayajafahamika kwa mapana na, au hayakuwa yamesambazwa wala kuhifadhiwa katika lugha nyingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, kunyang’anya wanaotumia lugha za asili uwezo wa kuelewa, kubaini na kushiriki maongezi na mijadala inayowahusu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu, kupandikiza utatanishi, woga na kutojiamini miongoni mwa wanaotumia lugha za asili. Hali hii inaletwa na shinikizo la kila mmoja kutumia lugha ya shuruti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nne, kuondoa mfumo na mtiririko wa kufikiri ambao watumiaji wa lugha za asili walikuwa wamezoea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tano, kupunguza, kuzuia au kufuta kabisa, mawasiliano mapana, kwa njia ya lugha na vitendo na hivyo kudumaza au kufisha maarifa katika jamii husika kwa kupunguza au kuondoa uwezo wa kuzalisha mawazo mapya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sita, kupunguza wepesi wa kufikiri na kuelewa na kuondoa mshikamano wa jamii zinazotumia lugha za asili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Saba, kuvunja haki za binadamu kwa kuingilia, kutibua, kudhibiti, kukandamiza na kuzima lugha za asili – ambazo ni chombo cha fikra na maarifa kwa jamii husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uvujaji huu wa haki za binadamu umechukua sura ya kuhujumu:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, uhuru wa “kuwa wewe” na kuwa sehemu ya jamii yako kwanza kabla ya kuwa sehemu ya jamii pana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, uhuru wa kufikiri; tena kufikiri kwa wepesi na mtiririko. Tatu, uhuru wa kuwa na mawazo na kutoa na kupokea mawazo ya wengine. Nne, uhuru wa kutofautiana na mwenzako au yeyote; hata kama ni mtawala. Tano, uhuru wa kurithishana utamaduni na maarifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini watawala, ambao pia ni watunga sera zinazogongana, wamekuwa wakidai kuwa lugha za asili zinawagawa Watanzania. Wanataka Kiswahili na Kiingereza tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inabidi uwe mwendawazimu wa kiwango fulani ili uweze kuwasomea Wasukuma au Wamasai, wasiojua Kiswahili au Kiingereza, taarifa za habari za vijijini mwao, taifa au za kimataifa na kudai kuwa kwa njia hiyo unaunganisha taifa! &lt;br /&gt;Nimepata fursa ya kuhudhuria warsha ya 10 ya Mradi wa Lugha za Tanzania (19 -20 Juni 2009), juu ya “Nafasi ya lugha za asili katika jamii ya Tanzania,” ukumbi wa hoteli ya Beachcomber nje ya jijini la Dar es Salaam. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wachunguzi walikuwa wakionyesha, pamoja na mambo mengine, kazi walizochapisha juu ya lugha za watu wa jamii mbalimbali na kudhihirisha kuwa lugha ya kwanza kwa wananchi wengi, siyo Kiswahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja hii inakuja kufuatia matokeo ya tafiti nyingi duniani kuwa watoto wakifundishwa katika lugha yao ya kwanza ambayo walimu wao wanaijua vema, angalau kwa madarasa ya awali, hupata uwezo wa kuelewa haraka na hata kupata msingi wa kushika lugha na masomo mengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama ada, takwimu za aina hiyo lazima zilete mgongano kati ya watetetezi wa lugha za asili na wale wanaopenda Kiswahili na Kiingereza hata kwa mgongo wa kifo cha lugha za asili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna wasomi waliosema lugha za asili hazina maana na kwamba hakuna maarifa yoyote ya kuchota kutoka kwa watumiaji wa lugha hizo (!)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kwamba wenye kutumia lugha za asili ni wengi na bado wanafikiri na kutenda katika lugha hizo kuliko Kiswahili na Kiingereza; kuna waliosema lugha hizo zimepitwa na wakati; zinyofolewe baadhi ya misamiati na istilahi na kuachwa zife. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali hoja kuu inabaki bila kujibiwa: Mbona kuna kasi, mabavu ya sera za serikali na mpogoko wa hoja za baadhi ya wasomi katika kuhujumu lugha za asili?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatizo basi siyo kwamba lugha za asili zinawagawa Watanzania. Tatizo ni kwamba wananchi wakiendelea kuwasiliana katika lugha zao, ambamo wanaelewana vizuri na kutenda kwa muwafaka, yafuatayo yatadhihiri:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, watafikiri, tena kwa wepesi na kuelewana vizuri. Pili, wataungana zaidi na kuwa na mshikamano zaidi. Tatu, watasimamia utashi na kauli zao na hata kuvunja mikatale iliyowafunga miaka nendarudi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa msingi huu, malalamiko ya watawala kuwa lugha za asili zinagawa wananchi, na kuchochea ukabila, yanalenga kuhujumu uwezo huo wa kufikiri na kutenda kwa uhuru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Suala la ukabila bado limo katika vichwa vya wasomi wengi wenye vyeti vya hadhi ya juu katika taaluma mbalimbali. Huu nao ni msiba. Bado kuna wanaofikiri kuwa kuongea Luhaya au lugha yoyote ile ya asili, ni kuwa na ukabila.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawa hawajui au wamesahahu au wanakataa kukubali kuwa mtu anafikiri haraka katika lugha yake ya karibu zaidi; mifano yake inakuja haraka kupitia lugha hiyo; anakuwa mwepesi kuwasilisha na kutoa majibu katika lugha yake na hasa anapokuwa anaongea na wanaofahamu lugha yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata baadhi ya wasomi vyuoni bado wana matatizo na Kiswahili na Kiingereza. Sharti wafikiri kwanza, kwa mfano kwa Luhaya, ndipo waweke kwenye Kiswahili na baadaye watoe sauti kwa Kiingereza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu hufikiri vizuri na kwa usahihi zaidi katika lugha zao na hii ni haki yao kama walivyo na haki ya kuishi. Bali watawala na wengine waliomezwa na mkengeuko wameng’ang’ania dhana dhaifu kuwa lugha za asili zinaligawa taifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, tumekuwa na makabila au nchi au mataifa madogo? Twende Bukoba. Tarehe 8 Julai 1931, Omwami Rwagugira alikabidhiwa nishani aliyopewa na King George wa Uingereza (usijali sababu).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hotuba yake ya kukabidhi nishani, Bwana PC (mtawala wa jimbo – Provincial Commissioner) alisema, “Mwami Rwamugira amepewa nishani kwa uhodari wake na kazi alizofanya toka sisi tumeingia katika nchi hii ya Bukoba…”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tarehe 28 Mei 1933, Omukama wa Ihangiro alikaribisha masultani kutoka Dar es Salaam kwa kusema, “…Sina budi kutoa shukrani kwa watemi hawa waliofika katika mji wangu wa Rubungo na nchi yangu ya Ihangiro…” (Kutoka:Kitabu ya barua kakobi, 1931).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ufupi, hapa kulikuwa na watu. Wana utawala wao na lugha yao katika taifa lao. Waliongea, kufikiri na kutenda katika lugha yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wageni, kama Bw. PC na masultani walipata wakalimani na kumbukumbu ziliwekwa; tofauti kabisa na ubwege wa sasa ambako mzungu mmoja anafanya warsha ya wananchi 60 kuendeshwa kwa lugha ya Kiingereza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli hizi za Bakama kuhusu “nchi zao” hazikuja na ukoloni wa Uingereza. Wakoloni walizikuta na hali yake halisi. Kumbuka hiyo ni miaka 47 tangu Afrika ikatwe vipande kama keki ya harusi (1884).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Historia imejaa kumbukumbu, siyo tu za Tanganyika, ambako walitangulia Wajerumani na kabla ya hapo Waarabu, bali Afrika nzima inaonyesha kuwepo kwa tawala imara, zikiwa mataifa kamili, hata kama hazikuwa na silaha kama za wavamizi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vita vya kupambana na wavamizi Afrika viliendeshwa na viongozi wa mataifa ya Afrika yaliyokuwa yameimarika katika tawala zake. Ujio wa teknolojia mpya hauondoi ukweli wa utaifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Historia imejaa orodha ya watawala na viongozi wa vita walionyongwa au waliojiua kuliko kuchukuliwa mateka na wavamizi. Mapambano yote hayo yaliendeshwa katika lugha za asili zilizolingana na maendeleo ya teknolojia ya wakati huo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitu kikubwa kiliwashinda wavamizi wote katika historia. Walishindwa kuua lugha walizozikuta. Ukinzani kati ya makundi mawili ya “kigaidi” – wamisionari na wakoloni – ulizaa mbegu moja ambayo haikuwa imekusudiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wamisionari walishikilia baadhi ya lugha za asili na kuandika na kutafsiri vitabu vya dini katika lugha za wenyeji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawa walijua “neno halitapenya” kwa lugha ya mbali. Halitazungumzwa baada ya mahubiri. Halitakaa moyoni kama halina mfano wa karibu. Halitakumbukwa kama halikuwekwa katika mvumo unaoeleweka na uliozoeleka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna kitu kimoja tunachoweza kujivunia kwa kushinda uvamizi uliofanywa Afrika, ni kubakiwa na lugha za asili zilizosheheni maarifa ya jamii mbalimbali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndani yake kumefunikwa upendo na mshikamano wa jamii; chuki na hasira dhidi ya wavamizi; mbinu za kujikinga na kuendelea kuishi; ujasiri wa kukabiliana na adui; hekima ya kufanyia maamuzi; maarifa ya kuendeleza jamii na fursa za kuingizia maarifa mapya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, hapa kulikuwa na tawala, siyo makabila wala vikabila. Kulikuwa na lugha za mataifa zilizohudumia jamii anuwai katika kila nyanja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndani ya kitabu cha nyimbo za Luhaya za Kanisa la Kilutheri cha hadi miaka ya 1950 kulikuwa na wimbo uliotungwa kwa msingi wa kizalendo na kwa mantiki zote ulikuwa wimbo wa taifa:&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;  &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Mukama Katonda linda&lt;br /&gt;  Eihanga lya Buhaya&lt;br /&gt;  Abantu n’eitunga lyamwo&lt;br /&gt;  Ensi ogihe omugisha&lt;br /&gt;  Linda amaju n’ebibanja&lt;br /&gt;  Endimilo ozezege&lt;br /&gt;  Nabo abantu bakusiime &lt;br /&gt;  Bakuhulile wenka &lt;/span&gt;&lt;br /&gt;     &lt;br /&gt;&lt;span style="font-style:italic;"&gt;Tafsiri ya karibu ni:&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;  &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Ee Baba Muumba &lt;br /&gt;  Dumisha taifa la Buhaya&lt;br /&gt;  Watu na mali zao&lt;br /&gt;  Nchi uipe neema&lt;br /&gt;  Linda kaya na mashamba&lt;br /&gt;  Mavuno yawe teletele&lt;br /&gt;  Ndipo watu wakuhimidi&lt;br /&gt;  Na kukutii wewe tu&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;      &lt;br /&gt;Kanisa lilitambua utaifa wa mataifa mengi lakini katika lugha zao. Angalia jinsi ubeti wa wimbo uleule ulivyobadilishwa kukidhi maendeleo ya kisiasa (chapisho jipya): &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Mukama Katonda linda&lt;br /&gt;Ensi ya Tanzania &lt;br /&gt;Naichwe abantu otulinde&lt;br /&gt;Ensi ogihe omugisha  &lt;br /&gt;Kandi abemiluka yoona&lt;br /&gt;Obahe obwesigwa&lt;br /&gt;Singa waitu otubele &lt;br /&gt;Chwena tukuhulile&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;(Kutoka: Empoya, Northwestern Publishers, 1992) &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-style:italic;"&gt;Tafsiri ya karibu:&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;  &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Ee Baba Muumba&lt;br /&gt;  Dumisha taifa la Tanzania&lt;br /&gt;  Nasi watu utukinge&lt;br /&gt;  Nchi uipe neema&lt;br /&gt;  Na wote wenye majukumu&lt;br /&gt;  Uwape uadilifu&lt;br /&gt;  Eee Mungu utuwezeshe&lt;br /&gt;  Sote tukutii wewe&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na mabadiliko kutoka taifa la Buhaya kwenda taifa la Tanzania, bado nafasi ya lugha ya asili ni muhimu kuelezea kilichotokea ili kieleweke vema kwa wengi, kijadiliwe, kizame na watumiaji wa lugha hiyo waweze kufuatilia na kupima mabadiliko.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, kuzima lugha za asili kunalenga kuweka kando wananchi waliopevuka ndani ya lugha zao na kufanya jamii zenye uelewa mpana kupitia lugha za asili, kuwa kama misukule ya kuswagwa bila utashi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuhujumu lugha za asili ni kueneza ujinga. Watu hawatajua jinsi serikali ilivyoshindwa kutekeleza ahadi zake za kuondoa ujinga, umasikini, rushwa, magendo na ufisadi. Hivyo hawatachukua hatua. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani watawala wana tabia ya kupakata umasikini na ujinga. Umasikini hufanya wengi kubaki hohehahe, tegemezi na hata ombaomba. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujinga hufanya wasijue na hasa  mara hii wanapokuwa wanaelezwa kwa lugha ngeni, ngumu ambazo hawajui vema au hawajui kabisa na hawawezi kuzitumia kung’amua kinachoendelea. Kwa hiyo, ujinga na umasikini ni mtaji na ngao kuu za watawala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine, matumizi ya lugha za asili katika vyombo vya habari yangewezesha jamii pana kuelewa kinachojadiliwa; kuchangia na kukuza hoja na hata kuunga mkono au kukataa hoja. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani atashindwa kufarijika kwa kuona wenye ujuzi wa lugha za asili wakiajiriwa katika vyombo vya habari na serikali ikijitahidi kujua kilichomo kwa kuajiri wakalimani. Ajira.&lt;br /&gt;Mbona umoja wa watu wenye lugha anuai na wanaoelewa umuhimu na shabaha yao, unaweza kuwa imara kuliko umoja wa kushinikiza kupitia lugha moja au na nyingine ya kigeni? &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Bado Kiswahili kinaweza kuendelea kutumika na kukuzwa, kama kuna juhudi za kufanya hivyo. Bali kuwepo kwa lugha za asili, nyingi kama zilivyo, siyo &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;tishio,&lt;/span&gt; ni &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;fursa.&lt;/span&gt; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii itachapishwa katika gazeti la&lt;/span&gt; &lt;span style="font-style:italic;"&gt;MwanaHALISI,&lt;/span&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;toleo la Jumatano, 1 Julai 2009)&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-8373939920967194373?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/8373939920967194373/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=8373939920967194373' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8373939920967194373'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8373939920967194373'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/06/tunafikiri-katika-lugha-tunayojua.html' title='TUNAFIKIRI VIZURI NA KWA WEPESI KATIKA LUGHA TUNAYOJUA VIZURI ZAIDI'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SkoN9w3of0I/AAAAAAAAAEk/AcO8XGf-vX0/s72-c/Profesa+Amandima+Lihamba.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-5637264460833467895</id><published>2009-06-30T05:31:00.000-07:00</published><updated>2009-06-30T05:53:30.267-07:00</updated><title type='text'>SERIKALI IOMBE ASKARI WAKAE KIMYA</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SkoKsIQudqI/AAAAAAAAAEc/VbInWP4Wyzg/s1600-h/mKUU+WA+mAJESHI.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 200px; height: 137px;" src="http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SkoKsIQudqI/AAAAAAAAAEc/VbInWP4Wyzg/s200/mKUU+WA+mAJESHI.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5353102860331415202" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Mawe yakisema, serikali itaumbuka&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;SITAKI waziri Jeremiah Sumari achokoze Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kwa kutumwa au kwa sababu zake binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majeshi ni mawe makubwa. Majabali. Miamba. Majeshi ni wagumba. Majeshi yakitaka kuzaa sharti yakubali kufa polepole; kwa maana kwamba atokee wa kuyapasua ili yatoke mengi kwenye mawe makubwa au miamba. Hapo hayabaki mojamoja na imara tena.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na kawaida majeshi ya nchi hayachokozwi na mtu wa ndani wala wa nje. Wachokozi huchokoza nchi na watawala wa nchi zilizochokozwa huagiza majeshi yake kwenda mstari wa mbele na kukunja uchokozi kama jamvi la wageni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini uchokozi uliofanywa na waziri Sumari ni wa ndani na unaweza kufanya mawe makubwa, miamba kutamani kutoa sauti na kusema hayataki kupasuliwa; yaachwe kama yalivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akijibu swali la Dk. Willibrod Slaa juu ya ufisadi ndani ya mradi wa Meremeta, Sumari alitoa majibu ya vitisho. Alimwambia mwakilishi wa Karatu (CHADEMA) aachane na hoja ya ufisadi ndani ya Meremeta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiasi kinachodaiwa kupitia Meremeta kwenda mifuko isiyojulikana si haba. Ni zaidi ya Sh. 155 bilioni. Waziri anamwambia mbunge aachane na hoja ya Meremeta kwa madai kuwa mradi huo ulikuwa wa jeshi; kwamba ni suala nyeti na labda ni kuingilia suala la usalama wa taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri anataka kulazimisha mawe kusema. Mawe yatabaki kimya juu ya ahadi zao; juu ya mipango yao na silaha zao; juu ya mikakati ya sasa na baadaye; juu ya mbinu mpya walizopata katika medani ya vita; juu ya wanachopanga kufanya hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukimya huu ni kama jua, mvua na upepo vipigapo kwenye mwamba na mwamba ukavumilia. Zaidi ya hapo, miamba husema. Miamba mingi imeota juu ya mizimu ya kale iongeayo wakati wa jua kali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inawezekana, siku moja unapita karibu na miamba hiyo, wakati wa jua kali, ukasikia mtu akikuita kwa sauti ya juu sana – mara mbili au mara tatu – na usimwone.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wale dhaifu wa moyo huweza kuanguka chini na kuzimia; wengine humudu kukimbia hadi nyumbani kwao, wakitweta na kulowa jasho mwili mzima huku wakiishiwa na kauli. Mawe, majabali, miamba imeamua kusema!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati huo hujawahi kuichokoza. Hujailalamikia wala kuituhumu. Hujaisingizia wala kuihusisha katika miradi bubu ya watawala. Inasema tu. Inabubujika. Sembuse utakapoihusisha na wizi, uporaji, ukwapuaji, au kwa ujumla – ufisadi!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikae kimya? Sitaki waziri Sumari achokoze miamba na yenyewe iseme kwamba haijui Meremeta ni nini na ya nani. Kwamba haijawahi kunufaika na kampuni hiyo. Kwamba mafao yaliyotokana na Meremeta hayafahamiki jeshini. Kwamba hayakuingia jeshini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki waziri achokoze miamba ianze kukohoa na kunong’ona na hatimaye kulipuka. Miamba hii inajua kuwa fedha za kuendesha jeshi hutoka kwenye bajeti ya serikali inayosomwa na kupitishwa bungeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miamba hii inaelewa vema kwamba wakati Meremeta wanaanzisha mradi walihamisha wananchi kutoka makazi yao. Walihamisha hata kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa na kutawanya askari katika vijiji kwa kutumia mikokoteni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si wananchi – raia, wala askari walionufaika na mafao ya Maremeta baada ya kuanza kuvuna kutokana na mgodi. Shule na zahanati vilivyong’olewa havijarudishwa. Bwawa kubwa la maji lililokuwa sehemu ya uhai wa watu na viumbe anuwai, halijarejeshewa hadhi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki watawala jeshini wajitokeze na kuiumbua serikali juu ya matumizi haya. Sitaki wapatikane watumishi wa Wizara ya Ulinzi na kuthibitisha kuwa hawajawahi kupanga fedha za Meremeta au sehemu yake katika matumizi ya wizara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki maofisa wa ngazi za kati jeshi waanze kufurukuta na kusema hawataki kusingiziwa katika suala la ukwapuaji na hivyo kujitokeza na ukweli utakaoangamniza hadhi ndogo ya watawala iliyosalia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sitaki askari wa vyeo vya chini ambao wanajua vema kilichokuwa kinaendelea waanze kujitokeza na kusema walichoona na nani hasa walikuwa wavunaji wakuu wa Meremeta na siyo jeshi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wala sitaki askari wakumbushe serikali kwamba Tume ya Jaji Bomani iliishasema kuwa Meremeta si mali ya serikali bali ni ya binafsi. Labda likisemwa na wao ndipo serikali itasikia na waziri Sumari ataelewa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani anataka azibuliwe masikio kuliko alivyofanya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Aliiambia Kamati ya Bunge kuwa Meremeta haimo katika orodha ya mashirika ya umma na kwamba ofisi yake haijawahi kuikagua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mei mwaka jana tulipeleka baruapepe kwa benki ya Nedcor Trade Services ya Afrika Kusini kuhusiana na suala hili. Hatukujibiwa. Tuliwaandikia Deutsche Bank AG ya Uingereza. Hawakujibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini kwa kufuatilia kinachoendelea ni kwamba serikali haifanyi lolote. Imetafuta mahali pa kuegesha na kusahau hoja za wananchi wanaotaka kujua huyu Meremeta ni nani na fedha alizochota alizitumia wapi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matumizi ya visingizio vya jeshi, kama anavyosema Sumari, hayana uzito tena. Hayamtishi yeyote. Wananchi, wachunguzi na wengine wanaotafuta ukweli wangestuka na hata kuogopa kama wangekuwa wameingilia undani wa shughuli za jeshi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini hili la kikampuni cha Meremeta halimtishi mtu. Badala yake linaweza kuiweka serikali pabaya, kwani inaendelea kujichanganya; kuficha ukweli na hatimaye kusema uwongo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatari kubwa inaweza kuzuka pale mawe, majabali na miamba itakaoamua kuvunja kimya; siyo lazima kwa mikutano ya hadhara bali kwa mn’ong’ono tu ambao hatimaye utavuma kama upepo wa kimbunga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na askari – hiyo miamba – ni watoto wa watu masikini na wao ni masikini pia. Hawana cha kupoteza kwa kusema ukweli wanaoujua. Hapo ndipo serikali itaumbuka zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nani anaweza kuiondolea aibu serikali kwa kusema ukweli na kuijengea heshima na uhalali? Kama siyo mawaziri wake, nani hasa? Tusubiri majabali yaite wakati wa jua kali na kwa mzizimo wahusika wazimie?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uwezekano wa aliyezimia kupitiliza hadi dunia nyingine ni mkubwa kuliko aliyesimama. Kwa nini serikali ijiingize kwenye majaribu tata? Ukimya unaidhalilisha serikali na kuiondolewa uhalali. Itoboe kilichomo ndani ya Meremeta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;br /&gt;(Makala hi ilichapishwa katika toleo la Jumapili, 28 Juni 2009 la&lt;/span&gt; &lt;span style="font-style:italic;"&gt;Tanzania Daima Jumapili)&lt;br /&gt;&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-5637264460833467895?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/5637264460833467895/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=5637264460833467895' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5637264460833467895'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/5637264460833467895'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/06/serikali-iombe-askari-wakae-kimya.html' title='SERIKALI IOMBE ASKARI WAKAE KIMYA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SkoKsIQudqI/AAAAAAAAAEc/VbInWP4Wyzg/s72-c/mKUU+WA+mAJESHI.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-4981406611842138780</id><published>2009-06-17T05:00:00.000-07:00</published><updated>2009-06-17T05:11:18.861-07:00</updated><title type='text'>BAJETI INAYOPIGA MIAYO</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/Sjjc1baGCpI/AAAAAAAAAEU/Af_ZfqSjq_c/s1600-h/Mkulo.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 136px; height: 98px;" src="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/Sjjc1baGCpI/AAAAAAAAAEU/Af_ZfqSjq_c/s200/Mkulo.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5348267367950846610" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;MJADALA WA BAJETI ULIOJAA VISINGIZIO&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI mjadala juu ya bajeti ya mwaka 2009/10 kwa kuwa tayari umezaa visingizio. Kwani iwapo bajeti itashindwa kukidhi matarajio, serikali itajitetea kwa kusema, “kulikuwa na hali mbaya ya uchumi duniani.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini bajeti hii ina somo kuu kwa walioko serikalini na maeneo mengine yanayohusiana na utawala kisiasa na kifedha. Kuna kila sababu kwa wahusika kuanza twisheni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku moja kabla waziri wa Fedha na Uchumi kusoma bajeti bungeni, Rais Jakaya Kikwete alihutubia taifa. Alisema hali ya taifa si nzuri kiuchumi kutokana na msukosuko wa kiuchumi duniani. Akasema serikali imetenga Sh. 1.7 trilioni katika bajeti ya sasa kukabiliana na hali hiyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini wananchi wanakumbuka kuwa, wakati taarifa zimeenea dunia nzima kuhusu kuanguka kwa uchumi wa mabepari-viongozi duniani, Gavana wa Benki Kuu (BoT) na mawaziri katika serikali ya Kikwete walinukuliwa wakisema “Tanzania haitaathirika” kutokana na hali hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo tunaambiwa Tanzania imeathirika na rais analazimika kuandika dibaji ya bajeti ya taifa, ikiwa njia ya kujenga hoja ya kuweka kibano katika kukusanya kodi ili kupata fedha za kujinusuru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, gavana na mawaziri walipata wapi kauli hizo? Je, wana uelewa wa aina gani kuhusu mifumo ya fedha duniani? Je, wanajua mahusiano ya fedha za madola makubwa duniani na fedha za nchi hii? Maswali ni mengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inawezekana watawala wa siasa na fedha hawakujifunza hili shuleni na vyuoni? Inawezekana walisoma zamani na sasa wamesahau na hivyo wanahitaji kukumbushwa kwa njia ya twisheni? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Labda watawala wa siasa na fedha walitaka kuficha kinachobisha hodi. Wahaya husema katika methali, “Ekyaizile mabele” – huwezi kuficha matiti ya msichana yaliyoanza kuchomoza. Yataonekana tu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuficha kumekuwa tabia ya viongozi. Hakuna mvua. Kuna ukame mkubwa na mazao yamekauka. Viongozi watasema, “Hakuna njaa na hakuna atakayekufa kwa njaa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu wanakabwa na kunyang’anywa walichonacho. Nyumba zinabomolewa usiku na mchana na vitu mbalimbali vinaibwa. Watoto wa kike wanabakwa, albino wanakatwa viungo vya mwili na wengine kuuawa. Wengi wanashinda na kulala njaa. Viongozi watasema nchi ni shwari na kuna amani na utulivu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa huu ni ugonjwa; na ukificha ugonjwa kifo kitakuumbua. Kile ambacho gavana wa BoT na mawaziri walikuwa wakidai hakipo, ndicho kinaingizwa kwenye bajeti. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rais ambaye hakuwakemea wateule wake wakati wanatoa kauli zisizoweza kuthaminika katika medani ya uchumi wala siasa, leo analazimika kuwaambia wananchi kuwa na “uvumilivu” wakati wa utekelezaji wa bajeti ya kujikwamua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uchumi wa Tanzania utakosaje kuathirika kwa mafua ya uchumi wa nchi za kibeberu wakati ni sehemu yake? Uchumi tegemezi utakosaje kuathirika wakati anayetegemewa kayumba?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uchumi usiokuwa na viwanda wala kilimo – zile injini kubwa; na ambao hata umeshindwa kunadi vivutio vya asili kwa njia ya utalii – tunajua nchi zinaoishi kwa utalii tu – utakosaje kuyumba na hata kuanguka?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Gavana na waziri wanaweza kushindwa vipi kuona kuwa kushuka kwa mapato katika nchi za kibeberu; kufilisika kwa viwanda, kuongezeka kwa idadi ya wasio na kazi na kupungua au kukosekana kwa huduma za jamii kwa wasio na kazi, vinaweza kuathiri uchumi wa Tanzania?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani walipa kodi wakubwa katika serikali zinazotoa mikopo na misaada wakiishiwa, wakafilisika au hata wakilegalega, kwa nini serikali zao ziendelee kufikiria Tanzania? Watapunguza au watasitisha mikopo au misaada. Lazima nchi itaathirika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kauli za kutoathirika zilikuwa zinatolewa na wahusika ili kuficha janga na ili kuepusha “kuogopesha wananchi,” basi huu ni utoto wa ukubwani katika siasa na uchumi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania wengi sasa wanajua kuwa wanaishi kwa mashaka kutokana na sababu nyingi. Watawala wake wameshindwa hata kukusanya na kuweka akiba ya chakula. Likitokea janga pana la miezi mitatu, tayari serikali itaanza kuhaha kutafuta chakula kutoka nje ya nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa twende kwa mfano mmoja tu wa pamba. Serikali ilikuwa inaendesha karibu viwanda 20 vya nguo. Ikashindwa kuviendesha. Vikafa. Sasa  tunauza pamba nchi za nje. Viwanda vya nje vinavyotumia pamba vikikwama, basi pamba haitanunuliwa na iliyokusanywa itaozea ilipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkulima wa pamba asipouza pamba, hatalima tena. Asilipolima pamba na hana zao jingine, atafukarika zaidi, yeye na familia yake. Atakufa polepole. Kifo ndiyo hatima ya mahusiano kati ya Mtanzania na ubeberu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili linaweza kuonekana vema zaidi katika mazingira ya sasa; na hii ndiyo hali halisi katika nchi zote zinazojiita “changa” hata baada ya nusu karne ya kutoka kwenye ukoloni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nchi zote ambazo zimebaki kuwa shamba la bibi, ambamo wenye viwanda wanachota malighafi – mazao na madini – kama wanavyotaka, lazima zikose usingizi hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, kwa jinsi mfumo wa sasa wa uchumi wa nchi hii ulivyoshonwa kwenye mfumo wa uchumi wa kibeberu, siyo rahisi kukwepa mstuko, msukosuko na hata kuanguka kabisa kwa uchumi na kuangamia kwa watu wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Labda baada ya hili kutakuwa na funzo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii ilichapishwa katika toleo la Jumapili, 14 Juni 2007 la gazeti la Tanzania Daima Jumapili chini ya safu ya SITAKI)&lt;span style="font-style:italic;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-4981406611842138780?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/4981406611842138780/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=4981406611842138780' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/4981406611842138780'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/4981406611842138780'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/06/bajeti-inayopiga-miayo.html' title='BAJETI INAYOPIGA MIAYO'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/Sjjc1baGCpI/AAAAAAAAAEU/Af_ZfqSjq_c/s72-c/Mkulo.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-8465548514090916743</id><published>2009-06-17T04:40:00.000-07:00</published><updated>2009-06-17T04:56:16.754-07:00</updated><title type='text'>MAMILIONI ZAIDI WATAKUFA KWA MALARIA</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SjjYoLCKfNI/AAAAAAAAAEM/ok2tsM59_E8/s1600-h/Artemisia_kubwa.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 200px; height: 150px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SjjYoLCKfNI/AAAAAAAAAEM/ok2tsM59_E8/s200/Artemisia_kubwa.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5348262742170696914" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Ubeberu wanona kwa mgongo wa malaria&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;       Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;UHAI wa wananchi katika nchi za joto (tropiki), Tanzania ikiwemo, uko hatarini kutokana na ugonjwa wa malaria unaoua kwa wingi na kwa kasi kuliko ukimwi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nchi hizi, hasa watawala wake, wamejisahau. Badala ya kuchochea matumizi ya tiba asilia zilizoko kwenye makazi ya watu; na kuweka mazingira ya kujenga viwanda vyake, wameendelea kutegemea dawa kutoka viwanda vikubwa vya nje.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya uzembe huu wa kujisahau ni makubwa na mabaya. Watafiti wanaotoka nchi zenye viwanda vya dawa, wataendelea kupendekeza ni dawa ipi “bora” wamegundua itumike kutibu malaria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati huo wenye viwanda vya kutengeneza dawa na wafanyabiashara katika tasnia hii, wataendelea kutoa na kusimamia bei ya bidhaa hiyo bila kujali nani tajiri na nani masikini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, kutokuwepo matumizi mapana ya dawa asilia; kutokuwepo utafiti na ujenzi wa viwanda vya ndani vya kutengeneza dawa; na kutokuwepo ruzuku kwenye dawa zinazotoka nje ili zipatikane bure au kwa bei inayowezekana, basi watu wengi watakufa kwa malaria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa serikali ya Tanzania imekiri kuwa bei ya dawa ya kutibu ugonjwa wa malaria, ambayo imeiidhinisha itumike, ni kubwa mno na wananchi hawawezi kuimudu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi cha karibu miaka kumi, serikali imesema klorokwini (CQ) haifai, iachwe. Ikaachwa. Ikaleta SP (Sulphadoxine-pyrimethamine). Baadaye ikasema hata hiyo haifai, iachwe. Ikaachwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali imekuja na dawa inayoitwa “mseto,” kwa ufupi wa ALU. Kabla hii haijaenea nchini, sasa inakiri kwamba imeleta kinyamkera. Dawa hii ni ghali sana. Dozi moja ni kati ya Sh. 13,000 na Sh. 15,000.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii maana yake ni nini? Ni kwamba Tanzania inashirikishwa, kwa kujua au kutojua, katika mchezo unaoangamiza maisha ya mamilioni ya wananchi na wakazi wengine katika nchi za tropiki, ambako ugonjwa wa malaria unaua bila simile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uchunguzi unaonyesha kuwa karibu watu milioni tatu hufa kwa malaria kila mwaka katika nchi za tropiki. Kati ya idadi hiyo, milioni moja ni watoto; ambayo maana yake ni kuwa mtoto mmoja hufa duniani kila baada ya sekunde 30.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haya ni maafa makubwa na mbu aina ya Anofelesi, ambaye hueneza malaria, tayari amepewa na watafiti na walio katika mapambano dhidi ya malaria, jina la “gaidi mkubwa kuliko wote duniani.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Gaidi huyu amenufaisha wenye viwanda vya kutengeneza dawa za kupambana na malaria na wote walio katika mkondo wa biashara ya dawa hizi, kiasi kwamba wagonjwa katika nchi masikini watakosa tiba. Watakufa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkurugenzi wa Roche, kampuni kubwa ya kutengeneza dawa aliyeko Korea Kusini amenukuliwa akisema, “…Hatuko katika biashara ya kuokoa maisha ya watu, bali kupata fedha; uokoaji maisha siyo jukumu letu…” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alikuwa akijibu ombi kwa kampuni yake kupunguza bei ya dawa za kukabiliana na ukimwi. Inatarajiwa atakuwa na kauli ileile au kali zaidi akiombwa kupunguza bei ya dawa za malaria kwa watu wanaoishi kwenye tropiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hatua nyingine, mkondo mwingine wa viwanda, katika kasi isiyo ya kawaida, umetengeneza dawa bandia. Kwa hiyo, wakati dawa halisi haikamatiki kwa bei, dawa bandia haitibu au ni sumu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri wa Afya, Profesa David Mwakyusa alikiri jijini Dar es Salaam wiki iliyopita kuwa dawa ya malaria ambayo imependekezwa na wataalam, hainunuliki. Ni ghali sana. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alirejea kilio cha mataifa masikini na wanaowaunga mkono, kuwa uundwe mfuko wa kimataifa (Global Fund) ambamo wenye fedha watachangia, ili fedha hizo zipelekwe kwa wenye viwanda vya dawa kupunguza gharama za uzalishaji na hivyo kupunguza bei ya dawa husika kwa watumiaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ina maana “watu wema” wamchangie fedha tajiri mwenye viwanda vya kutengeneza dawa, ili apunguze gharama za uzalishaji na ili bei ya dawa ipungue. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nchi masikini za tropiki zimeshindwa kupata mwelekeo katika kuzuia na kutibu malaria. Kwanza, zimeshindwa kuua mbu Anofelesi anayeeneza ugonjwa huu. Pili, zimeshindwa kupata tiba inayopatikana kwa gharama nafuu, kwa wepesi na karibu na makazi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachofanyika hivi sasa ni watawala kubabaika; kutapatapa na kuburuzwa na makampuni yanayotengeneza dawa za kutibu malaria. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inawezekana hakuna kuburuzwa, bali watawala na makampuni kadhaa katika nchi hizi, wanashiriki biashara haramu ya “kuzalisha fedha” na siyo “kuokoa maisha” ya watu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, likija pendekezo kuwa baada ya miaka 50 sasa “klorokwini” haimudu tena kutibu malaria, basi watawala na wataalam wa nchi hizi masikini, ama huchekea kiganjani kwa mtindo wa “kufa kufaana;” au huanza kuweweseka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rafiki yangu, Leonard Mutakyahwa, aishiye Dar es Salaam na Morogoro, hukumbwa na malaria kila baada ya miaka mitatu na nusu au minne. Lakini hadi hivi karibuni alikuwa akiendelea kutumia vidonge vya klorokwini kutibu malaria. Ilikuwa haijamkataa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mutakyahwa anaishi mjini. Lakini Mzee Flaviani Byeyombo wa kijiji cha Bushumba, Muleba ambako nilizaliwa na kukulia, hajawahi kumeza kidonge cha klorokwini au chochote kile cha kutibu malaria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzee huyu hutumia mitishamba. “Kila nipatwapo na homa – mwili kukanyanyaa na kulegea, nikaumwa kichwa na wakati mwingine kuanza kuona kizunguzungu, macho kutoona vizuri na wakati mwingine kuwa na kichefuchefu, basi najua ndiyo hiyo mnayoita malaria imenitembelea,” anaeleza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maelezo ya Byeyombo hayaonyeshi dalili ya malaria peke yake. Dalili hizo zaweza kuwa za magonjwa mengine mengi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo dawa anayotumia mzee huyu, familia yake na wenzake kijijini, ni mseto wa majani ya miti mingi unaoitwa omubazi g’womushana kwa kutibu malaria na magonjwa mengi mengine na hata kuwa kirutubisho. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata Wahaya na wakazi wa muda mrefu wa Bukoba (Buhaya) ambao sasa wanaishi Dar es Salaam na miji mingine, na ambao wameendeleza mila na desturi za vyakula vyao na tiba, bado wanatumia mseto huu kwa tiba nyingi.&lt;br /&gt;   &lt;br /&gt;Unaweza kupendekeza bila woga, kwamba bila mitishamba, watu waishio katika nchi za tropiki wangekuwa wameteketea wote; kwani wanaofikiwa na vidonge vya kuzuia au kutibu malaria ni idadi ndogo – hasa Afrika. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haya ndiyo maisha ya mamilioni ya watu waishio mijini. Kidonge au kijiko cha dawa ya kunywa kutuliza kikohozi, kuondoa mwasho mwilini, kuongeza damu; kukomesha kuhara au kutibu malaria, hakifiki mbali. Mitishamba ndiyo imekuwa ngao na tiba kuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukitaka waweza kusema kuwa wakazi wa nchi za tropiki waishio nje ya miji, wamejilinda, kujikinga na kujitibu kuliko tawala ambazo zinaweza kuwa zinakimbilia hongo ya asilimia 10 kwenye gharama ya dawa za viwandani; na nyingine zikiwa feki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kule ambako kidonge kama klorokwini kilipenya, matumizi yake hayakuwa sahihi. Kutokuwepo elimu ya kutosha juu ya matumizi, ama kulisababisha vifo au usugu wa malaria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakumbuka Mama Zulfa, kijijini Bushumba, Muleba aliyenieleza mwaka 1996, “Nimechukua hivyo hapo (vidonge vya klorokwini); juzi nilimeza viwili, hivyo vingine viwili nitameza tena huko mbele iwapo nitajisikia homa tena.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kijiji cha Mwamihanza, Shinyanga, mwaka 1985, tukiwa kwenye ziara ya Mwalimu Julius Nyerere, mama mmoja aliniambia alivyonunua vidonge vinne vya klorokwini na kuwagawia watoto wake wanne – kila mmoja kidonge kimoja. “Naona sasa wanaendelea vizuri,” alieleza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, klorokwini, SP na hata ALU, ni baadhi ya dawa ambazo zimekuwa zikibambikizwa kwa jamii hata bila maelezo ya kutosha kuhusu matumizi bora. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupungua kwa kinga dhidi ya malaria na usugu wa ugonjwa huo, haviwezi kamwe kuwa kwa viwango sawa kwa sehemu zote katika nchi moja au katika nchi zote za tropiki. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali hakuna anayetaka kujua ni sehemu gani ya nchi ilikuwa haijafikiwa na dawa za viwandani; mwingiliano wake na wenye malaria uko vipi; idadi gani ya watu wanatumia dawa zipi na waliokuwa hawatumii dawa hizo walikuwa wanatumia nini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa njia hiyo, king’ora kikilia Ulaya, kwamba sampuli ya mji mdogo kama Kongwa (Dodoma), na siyo vijijini, inaonyesha usugu wa malaria – na sehemu nyingine kama hizo katika nchi nyingine – basi inatosha kuharamisha dawa na kuingiza mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja ya mtanuko wa eneo la maambukizi, inakubalika; lakini kuna hoja kinzani kwamba walioambukizwa malaria ambako vidonge havikufika wamepona. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo kuna njia nyingine isiyo rasmi ya kutibu ugonjwa huo na nchi za tropiki hazistahili kuendelea kuwa “panya wa maabara” – wa kufanyia majaribio ya dawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hadi hapa tunaona ni kwa kiasi gani nchi za tropiki zilivyoendelea kucheza na mauti ndani ya nyumba wakati mkombozi yuko mlangoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tafiti za dawa za asili za kutibu malaria zimekwenda goigoi sana katika Tanzania na nchi za tropiki, hasa Afrika wakati watafiti walikuwa na mahali pa kuanzia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waliougua malaria wapo. Dawa zilizotumika kuwatibu zipo. Waliotibiwa kwa mitishamba hadi wakapona wapo – ni mamilioni. Ugumu umekuwa wapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata wakati nchi za tropiki zikiendelea na utafiti na “ombaomba,” uko wapi mkakati wa kuhimiza wananchi kutumia dawa za asili?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Misitu na vichaka vya nchi za tropiki ni mali, ni dawa, ni baraka. Majani na mizizi kutoka nchi hizi, na hasa Afrika, vimetumika kutengeneza dawa ambazo zinaletwa nchini na kuuzwa aghali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mchungaji Emmanuel Mwakalinga wa Tukuyu, mkoani Mbeya pamoja na kazi zake za kuhubiri neno la Mungu, anatoa dawa aina mbalimbali kwa magonjwa kadha wa kadhaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa Mwakalinga ndiko chimbuko jingine la    dawa za kutibu malaria, homa ya matumbo na magonjwa mengine yaliyoshindikana. Ni dawa za mitishamba. Wako wengi wa aina hii nchi nzima na katika nchi za tropiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Swali kuu ni wataalam wa nchi hizi wamefanya nini, kwa miaka 50, kutumia ujuzi wa waendesha tiba kwa kutumia dawa asilia? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali za nchi hizi zimefanya nini katika kujenga mazingira na kuchochea elimu katika medani hii ili kukabiliana na mbu na malaria?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata pale serikali ziliposhindwa kufanya haya, zimechukua hatua gani kuhimiza wananchi kutumia mitishamba iliyoko karibu nao, kwa maelekezo madogo tu ya wenye ujuzi, ili kukabili malaria?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninafahamu nyumba moja jijini Dar es Salaam ambayo mazingira yake yamepandwa miti shamba kwa ajili ya matibabu ya malaria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mjini Morogoro, kuna eneo moja karibu na viwanda, Kihonda ambako mtu mmoja amepanda miche ya mitishamba aina ya Artemisia annua. Mmea huu wenye asili ya China umekuwa ukitumiwa kwa kutibu malaria na magonjwa mengine kwa zaidi ya miaka 2000.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na uchunguzi unaoendelea kwa ngazi ya maabara mbalimbali duniani, baadhi ya nchi za tropiki zimeanza kupanda, kuvuna na kutumia mmea huu, wenye aina zaidi ya 50, kwa tiba ya mafanikio.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majirani wa Tanzania – Kenya na Uganda, wana bustani za mmea huu. Kenya inakadiriwa kuwa na wakulima zaidi ya 4,000 ambao wameanza kuvuna fedha kutokana na kuuza majani ya artimesia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Asasi ya kijamii ya Natural Uwemba System for Health (NUSAG) kaskazini mwa Tanzania imekuwa ikishirikiana na asasi nyingine katika Afrika Mashariki kutafuta tiba ya malaria kwa bei nafuu na mmea huu umekuwa moja ya vyanzo vya tiba ya uhakika na isiyokuwa na athari mbaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mazingira ya dawa ya sasa ya kutibu malaria ni kwamba kutokana na ughali wake, wanaofikiwa na dawa hiyo watakufa wakiitazama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna ubaya gani kwa wataalam nchini, hata kama hawajakamilisha uchunguzi wa dawa nyingi nchini zinazotibu malaria, kupiga mbiu ya matumizi ya mitishamba ambayo imelinda uhai wa mamilioni ya wananchi kwa miaka yote?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna ubaya gani kufanya hoja ya kuokoa maisha ya wananchi, kwa njia ya tiba za asili, kuwa ajenda muhimu ya wataalam wa tiba na watawala?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna ubaya gani kuhimiza kilimo, kikubwa na kidogo, cha Artemisia annu, hata kama sehemu ya bustani kwa kila kaya, ili watu wajiponye, angalau kwa sasa, huku wakisubiri tiba za kisasa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umuhimu wa kufanya haya haraka unatokana na takwimu: Mtoto mmoja hufa duniani kila baada ya sekunde 30; na kwa jumla watu milioni tatu hufa kila mwaka kutokana na malaria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kila kabila au jamii ina omubazi g’womushana kwa jina tofauti. Kwenye dawa hizo ongeza Artemisia annu; na nyingine na nyingine za mitishamba. Watu wapone; hata kama ni kuahirisha kifo tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tuogope kutangaza tiba kwa kuwa haijafanyiwa “uchunguzi wa kisasa” au tumihimize matumizi kuokoa maisha ya watu wengi? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa Mutakyahwa anatumia mitishamba kutibu malaria na ana bustani ya Artemisia annu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii imechapishwa katika toleo la Jumatano, 17 Juni 2009 la gazeti la MwanaHALISI)&lt;span style="font-style:italic;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-8465548514090916743?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/8465548514090916743/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=8465548514090916743' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8465548514090916743'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8465548514090916743'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/06/mamilioni-zaidi-watakufa-kwa-malaria.html' title='MAMILIONI ZAIDI WATAKUFA KWA MALARIA'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SjjYoLCKfNI/AAAAAAAAAEM/ok2tsM59_E8/s72-c/Artemisia_kubwa.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-2832658187806636489</id><published>2009-05-22T10:02:00.000-07:00</published><updated>2009-05-22T10:06:23.513-07:00</updated><title type='text'>JINSI SERIKALI INAVYOTAKA KUUA UHURU WA MAONI</title><content type='html'>&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Serikali inavyotaka kuua uhuru wetu&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI serikali iwe kipofu au ifanywe kipofu. Kuwa kipofu ni tofauti na kutoona. Wakati kutoona ni kuondokewa na uwezo wa kuona, kuwa kipofu ni kupoteza fahamu na akili, na mara nyingi kwa kudanganywa au kwa utashi binafsi unaotokana na tamaa na, au ujinga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mapendekezo mapya katika Sera ya Habari na Utangazaji, kwamba mtu mmoja ataruhusiwa “kumiliki aina moja tu ya chombo cha habari, kama ni magazeti, au redio au televisheni, na siyo vyote kwa wakati mmoja,” basi serikali imejitia upofu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kujitia upofu ni kukataa kufikiri. Ni kukata tamaa. Ni kujisalimisha kwa vihoja na viroja. Ni kushindwa kujitazama na kujitathmini. Ni kutafuta visingizio vya kuziba penye udhaifu. Ni kukoleza kulala na kusinzia kwa mishipa ya fahamu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kinachokoleza upofu katika mapendekezo ya marekebisho ya Sera ya Habari na Utangazaji ni maelezo ya nyongeza. Inatajwa kuwa mmiliki aliye na vyombo vyote hivyo, “apewe muda wa miaka mitano kuuza hisa za vyombo vyake vingine.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mujibu wa muundo, kanuni na taratibu nchini, vinavyoitwa vyombo vya umma, hakika ni vyombo vya serikali. Uanzishwaji, uendeshaji, uwajibikaji na hata ugharimiaji wake, vyote ni kwa mfumo wa kumilikiwa na serikali na siyo “umma.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mateka wa kwanza basi sharti awe serikali ambayo kwa jina la “umma” inamiliki redio, televisheni na magazeti. Huu ndio mgongano wa kwanza wa maslahi katika utekelezaji kwa upande wa serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa takribani miaka 24 sasa, baadhi yetu tumetaka serikali iachie vyombo vya habari inavyomiliki ili iandikwe na kutangazwa kama inavyoonekana na siyo kwa kurembwa, kuonewa haya au inavyotaka. Serikali imekataa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumependekeza serikali ijiondoe katika umiliki wa vyombo vya habari ndipo itapata hadhi na uhalali wa kuvisema na kuvikosoa, badala ya mtindo wa sasa ambapo serikali ni mshindani kama wengine lakini inatumia nafasi yake kukandamiza mshindani mwenzake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali imekataa yote hayo. Imebaki mmiliki wa vyombo vya habari; msajili wa vyombo vingine vya habari, mtunga sera, msimamizi wa sera, mdhibiti wa vyombo vya habari na bado mshindani miongoni mwa wenye vyombo vya habari. Mgongano wa maslahi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali kwa uzoefu wa ukaidi wa serikali, hatutaona ikiuza redio, televisheni au magazeti yake. Tutashuhudia shinikizo kwa wenye vyombo kuuza vyombo vyao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapendekezo ya sera ndiyo huzaa sera na hatimaye kuelekeza mfumo wa sheria. Marekebisho yanayopendekezwa kwenye sera ya mwaka 2003 yanaonekana yamelenga mtu mmoja au wawili wenye kumiliki aina nne za vyombo vya habari – redio, televisheni, magazeti na shirika la habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, katika haraka ya serikali ya kudhibiti iliowalenga, haitaji Shirika la Habari kuwa aina nyingine ya chombo cha habari katika kifungu 2.3.2 kinachosomeka, “Maelekezo ya Sera.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenye aina tatu za vyombo vya habari ambao serikali inaweza kuwa imelenga, ni Reginald Mengi, Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP na Media Solutions anayemiliki redio, televisheni na msululu wa magazeti, baadhi yakiwa na msimamo mkali wa kukosoa na kuibua taarifa za rushwa na ufisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwingine mwenye aina tatu za vyombo vya habari ni Anthony Diallo, mmiliki na Mtendaji Mkuu wa Sahara Communications yenye redio, televisheni na gazeti moja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika siku za hivi karibuni ni Reginald Mengi ambaye amelalamikiwa na serikali kwa kuipa nguvu hoja ya ufisadi nchini. Ameibuka na majina ya watu watano aliowaita “mafisadi papa.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja ya Mengi ilipojibiwa na mmoja wa waliotuhumiwa, Rostam Aziz, naye Waziri wa Habari George Mkuchika akaibuka na kudai kufunga mjadala huo kwa madai kuwa unataka “kuligawa taifa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyombo vya habari vya IPP na Media Solutions, hasa magazeti – This Day, KuliKoni na Nipashe – vimejizolea tuzo katika ushindani wa kuandika habari za uchunguzi katika rushwa na utawala bora. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, ni vyombo vya IPP, hasa televisheni, ambayo imemulika hata kelele za chinichini na mikwaruzo kati na baina ya wabunge na kutoa mwanya kwa wengi kujieleza, ambao bila chombo hicho, wangepotea kimyakimya kutoka jukwaa la siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapendekezo ya serikali basi, yanalenga kuzima nguvu ya vyombo hivyo; mvumo na mfumo wake ratibishi na hatimaye kurejesha taifa katika usiku wa giza nene la upungufu na hata ukosefu wa taarifa ambazo, bila vyombo hivyo zisingepatikana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali inalenga kuua stadi na uwezo wa viwango ainaaina wa watumishi katika vyombo hivi; kwani pamoja na kupendekeza kuwa wenye aina zote tatu wauze hisa za aina nyingine mbili za vyombo vya habari, hakuna mwenye hakika ya vyombo vilivyouzwa kuendelea kukua, kushamiri na kutumika kwa malengo na manufaa yaliyotarajiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa kuna mkakati wa kuua ajira ya mamia, kama siyo maelfu ya wafanyakazi wanaotegemea vyombo hivi na wengi wanaotegemea mafao yatokanayo na mishahara ya watumishi katika vyombo hivi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapendekezo ya serikali katika sera yanalenga kuzima ujasiri katika uandishi wa habari za uchunguzi; ujasiri uliopatikana baada ya muda mrefu wa mafunzo darasani na kwa njia ya vitendo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haya ni mapendekezo maalum ya kuzima ushindani wa kibiashara kati ya vyombo vya habari vya serikali na vyombo binafsi na kurejesha wananchi katika mazingira ya kutokuwa na utashi juu ya chombo gani wanataka kiwape habari na taarifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapendekezo yanalenga kukatisha tamaa na kuogofya wale ambao tayari walikuwa wamehamasika na wanataka kuanzisha vyombo vingine vya habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua ya serikali kupitia mapendekezo, inalenga kupunguza kiwango cha taarifa zilizokuwa zinawafikia wananchi. Hii ina maana ya kujenga mazingira ya uficho zaidi kwa serikali na watendaji wake. Uko wapi uwazi bila vyombo vingi vya kuuweka wazi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatari kubwa ipo kwenye uhuru wa maoni. Hapo ndipo kuna janga. Kuwepo kwa vyombo vingi vya habari kunaweka mazingira ya wananchi wengi kutoa na kupata habari na taarifa; kubadilishana mawazo, kuelimishwa na kuelimishana na kuwa na maoni yao juu ya mambo mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sauti nyingi za wananchi juu ya wanavyoona utawala na wanavyotaka uwe; juu ya furaha, huzuni, pongezi, malalamiko, vilio, shangwe na maafa, huweza kufika kwa wenzao na watawala kama kuna vyombo vingi vya habari. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupunguza idadi ya vyombo vya habari katika mazingira ya sasa, ni kutaka kuziba mifereji ya fikra na elimu; ni kutoa mwanya kwa uvumi na ujinga; ni kutaka wananchi wasikilize sauti moja kutoka kileleni; ni kuzika wananchi wakiwa hai katika mazingira ambamo hawatasikika wakipambana au wakilia na kuomba msaada.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Turudi darasani kidogo na kwenye uzoefu. Uhuru wa maoni kwa maana ya uhuru wa kujieleza, haukamiliki mpaka mtu aseme maoni yake – kwa kauli au vitendo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni mpaka maoni yake yasikike kwa mwenzake, kundi au halaiki; au yachapishwe kwenye gazeti, au yatangazwe kwenye redio au televisheni. Vyombo vya habari ndivyo husaidia kukamilika kwa takwa la uhuru wa maoni na ndio maana vyombo hivyo ni sehemu ya uhuru wa kujieleza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa serikali inapendekeza wenye vyombo waviuze. Labda wanao wanunuzi. Wamuuzie nani ambaye ataviendesha kama vilivyokuwa vinaendeshwa. Mapendekezo haya ndiyo yanatarajiwa kuwa katika sheria mpya ya uhuru wa habari na uhuru wa kupata habari. Hii ni hatari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama pendekezo la serikali litapitishwa na wadau, au litashinikizwa, sheria itakayotokana na sera hii itakuwa moja ya sheria za kishetani ambazo wadau wa habari wamepinga tangu 1985.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali kuna masomo mawili yanayopatikana hapa. Kwanza, pendekezo la serikali, ikiwa mdau katika huduma na biashara ya habari, linadhihirisha kuwa imeshindwa mbinu za ushindani na sasa imeamua kutumia mabavu kwa njia ya sera na sheria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, serikali imejipanga kuingilia uhuru wa wananchi wa kupata habari na kuwa na maoni. Itafanya hivyo kwa kuviondoa vyombo vya habari ambavyo tayari vilikuwa vimepenya jamii na vinakimbiliwa na wengi ili kutoa taarifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapendekezo ya serikali hayakubaliki na kila mwenye nia njema kwa taifa hili anaitaka serikali iyatupilie mbali. Inabidi hata walioyaleta wajue kuwa wao siyo wapangaji wa kudumu serikalini. Zimwi wanalojaribu kuumba watalikuta nje ya lango pindi wakiachishwa, wakifukuzwa kazi au wakistaafu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali ingejizolea heshima kwa kuhimiza watu binafsi na asasi mbambali kuanzisha magazeti mengi na vituo vingi vya redio na televisheni, bila kujali nani ana vyombo vya aina zipi. Kinachohitajika ni taifa linaloongea; na siyo la watu walionyang’anywa uwezo wa kuwa na maoni na vyombo vya kutolea maoni hayo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi kwa nini mtu akatae kujiandalia mazingira mazuri ya uhuru uliotamalaki na badala yake  ajiandalie mahabusi akingali madarakani? Tusikubali vipofu wajinyonge. Tuwanyang’anye kitanzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt; &lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii itachapishwa katika gazeti la&lt;/span&gt; &lt;span style="font-style:italic;"&gt;Tanzania Daima Jumapili&lt;/span&gt;, &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;toleo la 24 Mei 2009)&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-2832658187806636489?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/2832658187806636489/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=2832658187806636489' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2832658187806636489'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2832658187806636489'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/05/jinsi-serikali-inavyotaka-kuua-uhuru-wa.html' title='JINSI SERIKALI INAVYOTAKA KUUA UHURU WA MAONI'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-2565830552413974994</id><published>2009-05-16T02:01:00.000-07:00</published><updated>2009-05-16T02:19:16.107-07:00</updated><title type='text'>SERIKALI IKITENDA JINAI, WANANCHI WAFANYEJE?</title><content type='html'>&lt;a href="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/Sg6EGxPWZnI/AAAAAAAAAEE/l9hRcCta7Mg/s1600-h/mkuchika.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 88px; height: 107px;" src="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/Sg6EGxPWZnI/AAAAAAAAAEE/l9hRcCta7Mg/s200/mkuchika.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5336347860312417906" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;WAZIRI MKUCHIKA (pichani juu) ATAKA KUNYAMAZISHA WANANCHI&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SERIKALI imeficha ukweli. Katika hatua hii, serikali inaweza kutuhumiwa kusema uwongo; na kusema uwongo ni kutenda jinai. Je, serikali ikitenda jinai itakuwaje?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika taarifa yake, serikali imepiga marufuku kile ilichoita “malumbano” kati ya Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz kwa maelezo kuwa “yanaweza kutumbukiza taifa katika uvunjaji amani.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa ya Waziri wa Habari, George Mkuchika kwa vyombo vya habari juzi Jumatatu imesema serikali “haitakubali kusikia malumbano” hayo na “haitavumilia kuona vyombo vya habari vikichangia kuligawa taifa katika makundi na kudumaza maendeleo.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa ndipo penye mgogoro. Wasomaji wa magazeti, wasikilizaji redio na watazamaji wa televisheni hawajawahi kuona kile serikali inachokiita “malumbano.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mengi ametuhumu watu kuwa “mafisadi.” Mmoja wao ni Rostam. Naye Rostam amejibu, tena kwa kutumia chombo cha umma – Televisheni ya Taifa (TBC1).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa akili ya kawaida, kilichotendeka ni kuibua hoja zilizokuwa zikienda chinichini. Kilichoanikwa ni matendo ya watu binafsi yanayohusu uchumi na maisha ya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kile ambacho serikali inaita “malumbano” ni eneo la “soko huria” la mawazo ambamo, kwa miaka miwili sasa, wananchi wamekuwa wakichangia kwa njia ya kulalama kwamba keki ya taifa inaliwa na wachache.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa serikali inasema “haitakubali kusikia” na wala “haitavumilia” kuona vyombo vya habari na waandishi wakichangia kugawa taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ndio udikiteta mchafu. Kwanza, serikali inatafuta nini katika “malumbano?” Kama ni malumbano kweli, si iwaache walumbanao wafanye wafanyavyo? Malumbano si huisha hoja zikiisha?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, serikali inajikoroga. Upande mmoja inasema kuna malumbano kati ya watu wawili; na upande mwingine inasema wananchi wameanza kugawanyika; hawa wakiunga mkono Mengi na wale wakiunga mkono Rostam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Basi haya siyo malumbano. Huu ni mjadala wa hoja za kina. Ni mdahalo wa gonga nikugonge wa kuibua mazito na machungu yanayohusu jamii. Ni uwanja wa kumwaga taarifa kwa wenye macho kuona na wenye masikio kusikia. Ni kitanzi pia cha wasema uwongo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini serikali inasema sasa basi! Nyamaza! Huu ni ukatili. Ni udikiteta. Kuna hasara gani kwa wananchi kuwa upande wanaotaka, wanaoelewa, wanaothamini na waliotayari kutetea?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu, serikali haisemi ukweli pale inapodai kuwa nchi itaingia katika “uvunjaji” amani. Watu huru wanapojadili yanayowahusu wao na jamii yao, haitazamiwi serikali ijenge visingizio vya kupotea kwa amani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu wakiona mabaya yanatendeka; wakakaa kimya au wakanyamazishwa, wakajenga chuki kimyakimya, wakafura kwa hasira; basi linalofuata ni mlipuko mkubwa kuliko mabomu ya Mbagala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mlipuko huu ni hatari zaidi, hata na hasa kwa watawala, kuliko mdahalo juu ya nani “anakula nini.” Bali sasa ni wazi kwamba kwa hatua ya serikali ya kuzima mjadala, lazima “kuna jambo.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nne, serikali makini ingefurahia mdahalo. Ingepata vyanzo vizuri na sahihi vya taarifa mwanana za kufanyia kazi iwapo ina nia kweli ya kufanya kazi. Lakini inaonekana imechoka haraka na mapema. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa siyo tu serikali haitaki kusikia, bali pia haitaki wananchi wasikie na washiriki mjadala. Huu ni udikteta mchafu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtu angetarajia “mapapa” watajwe na “fisadi nyangumi” watajwe ili wananchi waone tofauti kati ya papa na nyangumi. Waone nani anaamsha hisia zao ili waone na kupigania haki na maisha yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakika, mmoja wa samaki hawa wakubwa aweza kuwa mwandani wa wananchi. Panahitajika uibuaji taarifa. Upembuzi. Uchokonozi wa kina na ushiriki wa wananchi katika mjadala. Kuzima hili ni ukatili wa kidikteta. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tano, serikali inatumia vitisho kuzima mjadala. Inanukuu na kujivunia sheria katili zenye harufu ya kifashisti kama hii Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 na nyingine yenye chembechembe za kibedui – Sheria ya Utangazaji ya mwaka 2003.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katikati ya majigambo ya utawala bora, ukiona bado kuna watawala wanaojivunia sheria zinazopingana hata na katiba zao, na uhuru na haki za wananchi, basi ujue udikteta umeota mvi. Wanaua uhuru na haki ili watawale misukule na siyo watu wanaofikiri na wenye utashi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sita, kwa serikali “kutahadharisha” wahariri na waandishi, ina maana ya kuwafunga midomo na mikono. Wasifikiri. Wasitende. Wasubiri serikali iamue andika hili, andika lile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Saba, kuna upandikizaji woga. Waziri anasema sheria “zinakataza mtu, watu kuzungumzia au kujadili suala ambalo tayari liko mahakamani.” Hakuna sheria ya aina hiyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chukua maneno ya waziri kama yalivyonukuliwa hapo juu. Ama waziri hakuelewa sheria inasemaje au ameinukuu nje kabisa ya muktadha. Sheria aina hiyo itakuwa za kishetani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Magwiji wa sheria waliishafundisha kuwa waamuzi wa kesi mahakamani siyo hakimu au jaji peke yake. Kuna wakili wa pande mbili na kuna wananchi wanaofuatilia kesi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kila fungu litatoa hukumu yake; na hilo ndilo hufanya hakimu au jaji awe makini akijua siyo mwamuzi pekee, hata kama waamuzi wengine hawakuketi mbele ya mahakama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo suala la kutojadili kilichoko mahakamani ni uzushi unaolenga kutisha na kunyamazisha wananchi. Hata kuibuliwa kwa madai ya nyongeza, nje ya yale ambayo mtuhumiwa tayari amesomewa mahakamani, siyo kosa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kweli kabisa maoni nje ya mahakama yaweza kusaidia kuweka wazi zaidi kinachoendelea mahakamani. Hiyo ni kama mawakili watakuwa wamepata taarifa zaidi za kunoa stadi kuchokonolea kile ambacho walikuwa hawakukiona na kukiwasilisha kwa ustadi zaidi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini mjadala nje ya mahakama hauwezi, hata kidogo, kuharibu kinachoendelea mahakamani. Vitisho kama vile vya Mkuchika ndivyo vinaweza kuharibu mbongo za watu na kuwapokonya uhuru wa maoni. Naomba kuwasilisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo, serikali imetumia mabavu kujaribu kuzima mjadala ambao ungeisadia. Sasa kuna madai kuwa imefanya hivyo kwa kuogopa itaguswa pale – kati ya papa na nyangumi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna kila sababu ya kupinga udhalimu huu katika nyakati tulizomo. Tukinyamaza watawala watashindilia watu kwenye magunia kama dagaa na kututupa mwaloni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuvunjika kwa amani ni visingizio. Kutumia visingizio kukwepa ukweli ni kuficha ukweli hadi kufikia viwango vya kusema uwongo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kusema uwongo kuwa mjadala utaleta maangamizi kitaifa ni kutenda jinai.&lt;br /&gt;Serikali ikitenda jinai wananchi wafanyeje?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614871&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii ilichapishwa katika gazeti la&lt;/strong&gt; &lt;em&gt;MwanaHALISI&lt;/em&gt; &lt;strong&gt;toleo la 13 Mei 2009)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-2565830552413974994?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/2565830552413974994/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=2565830552413974994' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2565830552413974994'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2565830552413974994'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/05/serikali-ikitenda-jinai-wananchi.html' title='&lt;strong&gt;SERIKALI IKITENDA JINAI, WANANCHI WAFANYEJE?&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/Sg6EGxPWZnI/AAAAAAAAAEE/l9hRcCta7Mg/s72-c/mkuchika.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-383825528618654401</id><published>2009-05-16T01:49:00.000-07:00</published><updated>2009-05-16T01:53:49.075-07:00</updated><title type='text'>WANAGAPI WATAPIMWA AKILI TANZANIA?</title><content type='html'>&lt;strong&gt;Vimbwanga vya Ikulu, BoT na walinzi&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                         &lt;strong&gt; Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI kupuuza vimbwaga. Vina maana yake katika mazingira maalum ya utawala uliopo. Ilitokea katika historia ya nchi hii, moto ukaunguza Benki Kuu ya Tanzania (BoT). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi walistuka. Wengine walishangaa. Wengi walihisi kulikuwa na njama za kuficha wizi au kuharibu ushahidi kwa kuchoma nyaraka. Ndani ya benki maofisa walikanuliana macho na kauli za “sihusiki” zikawa salaam za kila siku.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kilichostua wengi wakati huo na hadi sasa ni aliyeshitakiwa. Alikuwa mlinzi – korokoroni. Kesi ilinguruma. Ulijengwa ushahidi wa kushindilia na kuokoa. Hukumu hii hapa. Ni mbele ya jaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jaji anachukua hukumu iliyoandikwa.  Anageuzageuza kurasa. Anateremsha miwani yake ambayo inagota kwenye pua. Anawaangalia waliofurika mahakama kwa kupitia juu ya miwani yake. Anawaangalia washitakiwa. Anaanza kusoma hukumu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni maneno mengi. Ni sentensi nyingi. Ni aya nyingi kwenye karatasi nyingi. Mahakama imetulia, tuli! Anasoma. Anahoji na kujijibu. Anatulia kwa sekunde kadhaa na kuvuta pumzi huku waliojaa mahakama wakisubiri “hukumu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kauli zisizo na usumbufu wa maneno marefu, magumu na ya mchanganyiko wa Kiingereza na Kilatini, ambayo hutumiwa na wanasheria wengi, jaji anasema kuwa, kila anapoangalia pale mahakamani, haoni waliotenda jinai ya kuchoma benki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alikuwa na maana kwamba wahusika hawakuwa mahakamani. Hawakushitakiwa. Aliyekuwa kizimbani, kwa maoni yake, uelewa na kwa mujibu wa sheria, hakuwa na hatia. Alimwachia. Mlinzi hakuelewa. Wasikilizaji walipigwa na mshangao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waliochoma benki hawajawahi kufikishwa mahakamani hadi leo. Hata hivyo, mabenki hayaungui kwa moto wa sigara za wapita njia na hakuna joto la kukamata watuhumiwa wengine. Labda moto huo ulikuwa mwanzo wa kindumbwendumbwe kilichoko BoT leo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sikiliza ya Ikulu, Dar es Salaam. Ni alfajiri au asubuhi. Ikulu kunawaka moto. Nani kaunguza makao ya rais (mara hii yumo Benjamin Mkapa)? Wengi wanastuka. Wengine wanashangaa. Wengi wanahisi kuna kilichounguzwa ili kuharibu ushahidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Magari ya kuzima moto ikulu hayapo. Wanaowahi kufika ikulu ni kampuni binafsi ya ulinzi na zimamoto. Lazima walinzi wa langoni wajiulize iwapo zimamoto ya “moto wa binafsi” inaweza kuzima moto wa “ofisi ya umma.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Subiri kidogo. Wakawasubirisha. Moto haukusubiri. Hadi uamuzi unafanywa, kwamba kampuni binafsi  yaweza kuzima “moto wa umma,” moto uliishatafuna vipande vya ikulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa hakuna kesi. Wataalam wanaeleza chanzo na hakuna wa kukamata. Lakini ikulu imeungua na ikulu haziungui kwa moto wa sigara za mpitanjia. Ni vimbwanga vya Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wiki iliyopita mwanaume mmoja aliingia ikulu bila kubisha hodi. Akaenda hadi maeneo ya ofisi. Bila shaka akakagua au akashangaa mandhari ya ofisi kuu ya taifa. Kwani wale ndege kishingo – tausi, wanaoranda bustanini humo kila siku hulipa kiingilio? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya utalii huu wa muda mfupi, mwanaume huyo alichuma ua bustanini ikulu; labda kwa shabaha ya kutaka  kuwaonyesha wenzake kuwa alikuwa ndani ya ikulu bila kukaribishwa na rais wala ofisa yeyote. Akaanza kutoka kupitia lango kuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tofauti na vimbwanga vya BoT na moto wa ikulu, hiki kina manjonjo ya aina yake: Kabwela asiye na kitanda kaingia ikulu bila kikwazo. Walinzi walikuwa wapi? Mtoto wa watu kajiingilia ikulu na analo la kusimulia, nyumbani au kijiweni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bahati – yoyote ile – mbaya au nzuri, mwanaume huyo akadakwa langoni akiwa anatoka. “Unatoka wapi wewe? Kwanza uliingiaje mpaka kule?” Ni maswali lakini hayana uzito bali mwanaume huyo hafanyi mikwara. Anajieleza. Huko ndiko wanaita kumatwa. Sasa kuna taarifa kuwa mtu huyo apelekwe hospitali kupimwa akili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hali yakawaida, nani anastahili kupimwa? Hapa kuna kijana aliyeingia ikulu bila kelele wala mikwaruzo na alikuwa anatoka bila kubughudhi yeyote isipokuwa akiwa amebeba ua alilochuma. Huyu apimwe nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pale ikulu anakaa rais wake. Wanakaa watumishi wa umma. Wapo askari wa kulinda amani na amani ni amani yake na wakaao ikulu na wengine wanaoingia. Apimwe nini? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si angepimwa asiyejua kuwa ikulu inapaswa kuwa eneo la utalii wa watu wa nje na ndani ya nchi na kwamba ni moja ya vivutio na sehemu ya elimu kwa jamii?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kati ya walinzi na mwanaume aliyeingia ikulu bila hodi, nani apimwe akili? Wale ambao hawakuona mtu anaingia na aliyeingia na kutoka bila kufanya baya lolote, nani hasa apimwe akili?&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kwanza ikulu imekuwa moja ya “vijiwe” maarufu. Imezungukwa na watafuta kivuli wakati wa jua kali; wauza maji, karanga na kahawa. Hivi karibuni, baada ya wakazi wakuu wa ikulu kufoka ndipo askari wakazizunguka na kufanya kamatakamata ya zimamoto.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini Makamu wa Rais Mohammed Shein amestuka zaidi hivi karibuni. Anasema ofisi zimegeuzwa soko. Ni biashara “mtindo mmoja.” Wauzaji wanaingia na kutoka, utadhani kazi za serikali zimehamishiwa kwingine; kilichochukua nafasi hiyo ni uuzaji na ununuzi wa sidiria, suruali, chupi, t-sheti, blausi, mashati, vipodozi na nywele za watu wa kale!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wangapi watapimwa akili? Yule tu aliyeingia ikulu au na walinzi wa ikulu, watumishi wote wa ikulu, wakuu wa ikulu, wafanyabiashara – wa kuuza na kununua – wa ikulu? Nani atasalia katika kupimwa akili? Wauza karanga getini?  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukimaliza vituko vya ikulu na BoT, njoo kwenye vituko vya kupotea kwa vilaputopu. Kwa maana ya sasa, “laptop” ni kompyuta ndogo ya mkononi au mezani. Inatumika kama kompyuta yoyote ile bali ni rahisi kubeba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa sikiliza vimbwanga vya laputopu. Leo laputopu ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) imepotea. Wanasema imeibwa “kiaina.” Huyu ndiye amekabidhiwa mamlaka ya kuamua nani ashitakiwe nani asishitakiwe. Kalaputopu kage kanaweza kuwa na nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo hiihii laputopu ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeibwa. Wanasema imeibwa “kiaina.” Huyu ndiye mkuu wa idara ya vipimo nyeti anayekimbiliwa wa mwisho kutoa uthibitisho wa lolote linalohitajika kupimwa kikemia. Kalaputopu kake kanaweza kuwa na nini? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kaa chini utunge matukio haya kama shanga: Moto wa BoT, moto wa ikulu, mwanaume anayetokea lango kuu la ikulu akiwa na ua mkononi na kupotea kwa laputopu za watumishi wa ngazi ya juu serikalini. Kizaazaa! Nani apimwe akili? Watapimwa wangapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com &lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii itachapishwa katika gazeti la&lt;/strong&gt; &lt;em&gt;Tanzania Daima Jumapili&lt;/em&gt; &lt;strong&gt;toleo la 17 Mei 2009)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-383825528618654401?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/383825528618654401/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=383825528618654401' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/383825528618654401'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/383825528618654401'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/05/wanagapi-watapimwa-akili-tanzania.html' title='WANAGAPI WATAPIMWA AKILI TANZANIA?'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-3771302895500602491</id><published>2009-04-28T05:02:00.000-07:00</published><updated>2009-04-28T05:18:18.075-07:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SfbzvBSEuII/AAAAAAAAAD8/xtAxhuS4DUY/s1600-h/Venance+Muliki+W%27ialango.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 146px; height: 200px;" src="http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SfbzvBSEuII/AAAAAAAAAD8/xtAxhuS4DUY/s200/Venance+Muliki+W%27ialango.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5329715198163204226" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mr.Venance Muliki W'ialango (picture), has been appointed Secretary General of Mouvement National de Congo - Lumumba (MNC-L)with effect from February 2009. Mr. W'ialango has been secretary general of the youth movememnt of the party of Lumumba for over 12 years now and his recent elevetion talks a lot about his industriousness and capability to handle current issues in a party whose most leaders have been living in exile.Mr. W'ialango has told reporters in Dar es Salaam, Tanzania that he will be going to his home constituency - Fizi in South Kivu where he says elders have asked him to become their member parliament.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dr. Albert Onawelho, the president of MNC-L lives in London and is expected to run for the presidency in the general elections coming April 2010.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-3771302895500602491?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/3771302895500602491/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=3771302895500602491' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3771302895500602491'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3771302895500602491'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/04/mr.html' title=''/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SfbzvBSEuII/AAAAAAAAAD8/xtAxhuS4DUY/s72-c/Venance+Muliki+W%27ialango.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-8490619062688471795</id><published>2009-04-25T02:35:00.000-07:00</published><updated>2009-04-25T02:41:00.957-07:00</updated><title type='text'>WAZIRI GHASIA ANATETEA SIRI ZIPI?</title><content type='html'>&lt;strong&gt;Waziri Ghasia anayeleta ghasia&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI Hawa Ghasia kwa kuwa analeta ghasia katika mjadala kuhusu siri na hasa kile kinachoitwa “nyaraka za siri za serikali.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya waziri huyu wa Utumishi bungeni wiki hii, inaonyesha kuwa yeye binafsi, na huenda siyo serikali, anataka wananchi watembee wamebana pumzi kwa kuogopa kuwa kila walichonacho mkononi ni siri ya serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ameonya kwamba yeyote atakayekutwa na nyaraka za siri za serikali, “hata kama ni mbunge,” atachukuliwa hatua za kisheria. Ni onyo kali kutoka kwa Waziri wa Utumishi katika Ofisi ya Rais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja ya siri imejadiliwa mara nyingi. Nilidhani wahusika serikalini walielewa. Kumbe tulipoifikisha kileleni wengine walikuwa hawajaingia serikalini. Ndio sasa wanajaribu kuitoa kileleni na kuirudisha sakafuni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kila serikali duniani ina siri. Siri hizi hupangwa kwa viwango maalum – ndogo, kubwa kidogo, kubwa, kubwa sana, kubwa kabambe, kubwa na nene, kubwa na nzito, kubwa kuliko…&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtanuo huu wa ukubwa hutegemea mfumo wa utawala na tabia ya wachache walioko madarakani ambao hutunga sheria za kulinda kile wanachoona ni siri za serikali. Wakati mwingine, katika ukorokoroni wa nyaraka, watawala hujikuta wanaona kila kitu ni siri na hakuna viwango tena. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Upele mgongoni mwa serikali huitwa siri. Mba shingoni mwa serikali huitwa siri. Jipu makalioni mwa serikali huitwa siri. Kikohozi cha muda mrefu huitwa siri. Tatizo hapa ni kwamba hufikia wakati hata mkubwa kwenda haja kubwa hadharani huitwa siri!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni katika hatua hii, watu huangalia pembeni; hutema kwa kinyaa, huku wakibinua midomo kama waliolamba tone la shubiri na kunong’ona, “Ee, kila kitu siri, siri.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siri ya serikali inabidi iwe siri kwa manufaa ya nchi. Haiwezi kuwa kwa manufaa ya watawala au kundi la watawala peke yao. Lakini ainisho hili huleta mgogoro kati ya watawala na watawaliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ununuzi wa ndege za kijeshi huitwa siri. Ukodishaji ndege za jeshi kwa watu binafsi huitwa siri. Uuzaji ardhi, mikataba ya kuchimbaji madini, mikataba ya uzalishaji na ugavi wa nishati ya umeme, vyote huitwa siri. Vivyo hivyo uuzaji wa raslimali nyingine za taifa nje ya nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siri hupanuka hadi kuhusisha shughuli za rais nje ya shughuli kuu ya utawala. Mikataba ya ununuzi wa rada na manunuzi mengine panapotumika fedha za umma hufanywa siri pia. Siri za aina hii hufikia wakati zikawakwama kooni wale waliopewa jukumu la kuzilinda, nao wakaamua kuzitoa; siyo kama siri bali kama makabrasha tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa ndipo yanapotokea maasi. Ni hapa ambapo serikali inashindwa kuthibitishia hata mlinzi kuwa kile anacholinda ni siri. Ni hapa ambapo mlinzi anaamua kusema, “Potelea mbali. Hata kama nitapoteza kibarua, lakini sharti hili lifahamike kwa wengi.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna anayenunua vikaratasi vyenye mikataba na viapo vya wahusika katika mikataba hiyo iliyofanywa siri. Hayupo. Mengi ambayo serikali inaita nyaraka za siri yanatolewa kwa hisani tu na hata bila juhudi za uchunguzi wa kina.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanaodaiwa kuwa walinzi wa siri hawajatoa taarifa zozote za kuibiwa kwa nyaraka wala kuvunjwa kwa sefu za nyaraka na kukwapuliwa kwa siri. Taarifa hizo hazipo. Raia wema waliochoka kuona “siri” zisizo siri ndio wanawapelekea “makaratasi” wabunge na waandishi wa habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukitumia viwango sahihi, na kwa kuzingatia misingi ya uandishi wa habari za uchunguzi, utaona kuwa sehemu kubwa ya kile ambacho wengi wanaita “uchunguzi,” hasa siyo uchunguzi kwa maana halisi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa nyingi zinapatikana kwa njia ya nyaraka zilizotolewa kwa hisani – na mara nyingi bila ufundi wala ubunifu – na wakati mwingine bila juhudi za mwandishi au mbunge. Hii waweza kuita “chakupewa.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, kwa kutumia ustadi na ufuatiliaji wa kiwango cha “kuku wa kujitafutia,” taarifa hizo zimetoa mwanga wa kile kinachoendelea na wakati mwingine kupanua wigo wa kidogo kilichopatikana kuwa mkubwa zaidi na kuhusisha wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyovyote ilivyo, serikali inapaswa kulinda kile ambacho inaita nyaraka zake za siri. Hakuna mwenye uwezo wala mamlaka ya kulinda siri za serikali isipokuwa serikali yenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni serikali itakayobuni na kuweka njia “bora” za kulinda siri zake – ziwe siri kweli au viinimacho. Ni serikali inayostahili kujua nani mwenye uwezo wa kulindia siri na uwezo huo hunawirishwaje, huongezwaje na hulindwaje.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mpaka hapa ni muhimu basi kukubaliana kuwa kama serikali ina siri, basi ilinde siri zake. Serikali ikishindwa kulinda siri zake; na siri hizo zikatoka, haina sababu ya kulalamikia yeyote – awe mbunge au mwandishi wa habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maswali ambayo huulizwa mara nyingi ni: Kama serikali imeshindwa kulinda siri zake, walioko nje ya serikali watazilinda vipi? Watawajibikaje kuzilinda? Watajuaje kuwa ni siri na kama ni siri za serikali?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini hata wakijua, kwa maelezo rasmi kuwa ni siri, kwanza watajuaje kuwa hazijachoka na ndiyo maana zimeachiwa kuranda mitaani? Pili, watashindwaje kuzitumia katika hoja iwapo wanaona kuwa zina chembechembe za kuinua uelewa wa jamii juu ya mwenendo wa serikali yao?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu, hata wabunge na waandishi wakizisaka kwa mbinu, ufundi na ujanja wao, kwa lengo la kuneemesha jamii na kukuza mwamko na uelewa, bado hilo haliwezi kuwa kosa machoni mwa wananchi ambao walifichwa ukweli husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali kuna haja ya kuzingatia jambo moja. Mjadala juu ya wizi au matumizi ya nyaraka za siri za serikali unarudi wakati wadau wa utawala bora, wakiwemo waandishi wa habari, wanasheria, wabunge, wanaharakati wengine wanasubiri serikali kuwasilisha bungeni muswada wa Uhuru wa Habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuzingatia mwelekeo uliotolewa na wadau nje ya serikali, kuhusu umuhimu na njia za “kukomboa habari,” mapendekezo hayo yakizingatiwa katika sheria ya Uhuru wa Habari, yatamaliza malalamiko ya Ghasia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwani hadi sasa, kila kilichosemwa bungeni na kuandikwa na kutangazwa na vyombo vya habari – kile ambacho serikali ilikuwa haijakitoa rasmi – hakina madhara kwa serikali adilifu wala jamii kwa ujumla. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama serikali iko makini na inajiandaa kuwatendea haki wananchi wake kwa kutambua uhuru wao wa kupata taarifa na habari, na kusimamia utekelezaji wa uhuru huo, basi Ghasia hana budi kuanza mazoezi ya kuishi nje ya mipaka bandia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii itachapishwa katika safu ya SITAKI ya gazeti la &lt;/strong&gt;&lt;em&gt;Tanzania Daima Jumapili &lt;/em&gt;&lt;strong&gt;la 26 Aprili 2009)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-8490619062688471795?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/8490619062688471795/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=8490619062688471795' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8490619062688471795'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8490619062688471795'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/04/waziri-ghasia-anatetea-siri-zipi.html' title='&lt;strong&gt;WAZIRI GHASIA ANATETEA SIRI ZIPI?&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-8210628400681060266</id><published>2009-04-24T05:23:00.000-07:00</published><updated>2009-04-24T05:28:29.547-07:00</updated><title type='text'>UNYANG'ANYI UNAOSIMAMIWA NA SERIKALI</title><content type='html'>&lt;strong&gt;Wananchi wanapoitwa ‘wavamizi’ Kilosa&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NI vilio vitupu. Baadhi ya wananchi wenye mifugo – Wamasai, Wairaqw, Wabarbaig na Wasukuma wanawindwa kama swala.  Wanaambiwa waondoke wilayani Kilosa. Eti warudi makwao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Je, kila Mtanzania angeambiwa arudi kwao, nani angebaki alipo? Nani siyo uzao wa mzunguko wa mataifa madogo? Nani mtu wa asili Tanzania?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini makabila haya yanawindwa na kufanyiwa ukatili kwa kuwa yana mifugo. Wilayani Kilosa serikali inaendesha kile wanachoita “operesheni” ya kupunguza mifugo na kufukuza wenye mifugo wasiokuwa “wenyeji” wa wilaya hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wamasai wanasema ni “presheni ya kupilisi” – operesheni ya kufilisi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wa Kata, wakiandamana na polisi na mgambo, wanavamia eneo la mwenye mifugo, ndani au nje ya mipaka yake. Wanaswaga mifugo hadi wanakodai ni “zizi la serikali.” Kuwagomboa sharti ulipe Sh. 30,000 kwa kila kichwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Wanatwambia tuuze mifugo yetu palepale; au tuisombe kwa malori hadi kwenye mnada, Pugu, Dar es Salaam, au tuhamie mkoani Lindi ambako wanasema wametenga ardhi kwa ajili ya wafugaji,” anaeleza mfugaji Kalaita Parkuris huku machozi yakimlengalenga machoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kalaita ni mwathirika wa operesheni. Polisi wenye silaha na mgambo waliingia kwake na kukomba mazizi – ng’ombe 340 na mbuzi 120 katikati ya eneo la eka zipatazo 70 ambako ameishi tangu 1963. &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;“Presheni nini hii? Nini hii kama siyo taka kutupilisi,” alihoji Kalaita alipoongea wiki iliyopita na waandishi wa habari, chini ya mti, nje ya nyumba yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kalaita anasema alikataa kugomboa mifugo yake na kuacha ichukuliwe chini ya ulinzi wa polisi. Anaulizwa kama angekutana na Rais Jakaya Kikwete angemwambia nini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anajibu, “Ningesema awachukue watoto awalishe. Watakufa hawa,” huku akionyesha watoto wapatao 30 walioketi nyuma yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndugu yake anadakia, “Kuwachukua ni kama kuwapoteza. Ni kama wamekufa, maana hawapo.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapo ni kijijini Mkundi, Kata ya Dumila. Lakini ndivyo ilivyo katika maeneo mengi wilayani Kilosa. Haishangazi basi kukuta akina mama wa kitongoji cha Ngaiti wakiimba mbele ya waandishi wa habari:&lt;br /&gt;Maisha bora&lt;br /&gt;kwa mwekezaji &lt;br /&gt;Maisha bora &lt;br /&gt;kwa mafisadi &lt;br /&gt;Maisha duni &lt;br /&gt;Kwa mfugaji &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanawake hawa ni sehemu ya jamii ambayo shughuli yake kuu, kwa miaka yote, ni ufugaji wa asili. Kuwaondolea njia yao ya maisha, kwa kasi ya kuwafilisi, hakika ni kuvunja haki za binadamu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupora mifugo ambayo ni ajira, uchumi na egemeo la uhai wa wananchi, kuna athari nyingi na kubwa kwa maisha yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watakosa chakula – nyama na maziwa. &lt;br /&gt;Watakufa kiuchumi na kupoteza uhai kabla ya wakati wao. Watoto wao watashindwa kwenda shule au kubaki hai wakichunga mifugo ya kaya zao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unyang’anyi huu kwa njia ya “operesheni ya kupunguza mifugo na kuondoa wahamiaji Kilosa,” tayari umezaa mifarakano. Sasa utazaa vita vikubwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bibi Yasoi Kadege, mwenye umri wa miaka 97, wa kitongoji cha Ndagani kijijini Mabwegere, amechoka, amekata tamaa, anatamani ujana wake umrejee mara moja. Hauji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa unasimuliwa jinsi polisi na mgambo, walivyokomba ng’ombe 385 wa kaya hii wakiacha nyuma ndama wachanga 21. Hadi wiki iliyopita ni ndama watatu waliokuwa wamebakia; wakiwa taabani. Watakufa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sikiliza kikongwe Yasoi akijadiliana na mmoja wa waliofika nyumbani kwake:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yasoi: Huko kwenu peresheni hii imefika?&lt;br /&gt;Mgeni: Ipo. Wamechukua mifugo mingi tu.&lt;br /&gt;Yasoi: Sasa wewe kaa hapa; ungana na mwanangu ili mwende Morogoro; piganeni vita mkomboe mali zenu.&lt;br /&gt;Mgeni: (Kicheko cha kugegema) Sawa bibi, ni kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yasoi hana nguvu tena. Alibebwa na watu watatu kutoka ndani ya banda lake. Hata pale nje alipokaa, alihitajika mtu wa kuegemea na mwingine kuzuia asiangukie mbele.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hana amani. Hana chakula. Chakula chake ni maziwa na “maziwa yote” yalichukuliwa na serikali. Maziwa ya kopo ambayo amepelekewa na wajukuu wake yanamletea kiungulia na sasa hataki hata kuyaona. Atakufa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mita 200 kutoka kwa Yasoi ni kwa Tisini Madamanya, mwenyekiti wa kitongoji cha Madagani, kijijini Mabwegere ambaye anasema askari walikomba mbuzi wake wapatao 250. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tisini ana wake tisa na zaidi ya watoto 40 (jirani yake anasema ana watoto zaidi ya 70), watakufa njaa kama hawakupata msaada wa haraka. Mtoto mwenye umri mdogo hapa ana siku 14.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kijiji cha Mabwegere ni cha wafugaji. Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilosa, Ephrem W. Kalimalwendo anadai kuwa halmashauri haijawahi kufanya operesheni kijijini humo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anapoelezwa unyang’anyi katika sehemu mbalimbali ambako waandishi wamefika na kusimuliwa uporaji, anakana kuhusika kwa serikali yake ya wilaya. Sasa nani amefanya uhalifu huo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kalimalwendo anakataa pia kuwa watu wanaporwa mifugo; anadai kuwa wanauza wenyewe au wanaondoka nayo kwa kuwa hawana “vibali” vya kuishi Kilosa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anapoulizwa iwapo kuna wanaoweza kuwa wanafanya “operesheni” nje ya operesheni maalum ya wilaya, anajibu kuwa hajui; ghafla anasema hawapo; baadaye anasema, ninyi (waandishi) mnaadika kwa kupendelea wafugaji. Kigeugeu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bali Mkurugenzi Kalimalwendo anasema wenye mifugo kutoka bonde la Ihefu mkoani Mbeya ambako walifukuzwa na wengine kutoka mikoa kadhaa nchini, “wamevamia Kilosa” na kupunguza uwezo wake wa kuhimili mifugo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anasema wilaya ina eneo la hekta 530,000 kwa kilimo na hekta 430,000 kwa kufuga na kwamba kwa eneo hilo la wafugaji, wilaya inahitaji ufugaji wa kisasa wa ng’ombe 150,000 tu (wastani wa ng’ombe watatu kwa kila hekta).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hadi sasa halmashauri imefanikiwa kuondoa wilayani humo zaidi ya ng’ombe 18,000, anasema mkurugenzi na kusisitiza kuwa wasiokuwa wenyeji wa Kilosa “lazima waondoke.”&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kalimalwendo siyo mwenyeji wa Kilosa lakini tayari anamiliki ardhi ipatayo eka 10 katika kijiji cha Malangali ambamo wenye mifugo wametimuliwa na inadaiwa ardhi itamilikishwa kwa wawekezaji kutoka nje ya nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuhusu kwa nini mkurugenzi amiliki ardhi katika wilaya ambayo anadai ina ardhi haba, Kalimalwendo anang’aka, “Hilo haliwahusu. Haliwahusu kabisa. Yaani mtu kununua eka 10 tu…nasema haliwahusu.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi sasa Kilosa ni kilio na kusaga meno kwa wenye mifugo. Mifugo inakamatwa. Kama mfugaji hana fedha za kuigomboa, inauzwa kwa “bei ya bure.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mfano, ng’ombe ameuzwa kwa Sh. 120,000 hata 80,000 badala ya Sh. 450,000 au 500,000 na wanunuzi wanakuwa tayari wameandaliwa na madalali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Wanatuvamia. Wanaamuru twende Lindi au tuuze mifugo papo hapo huku tumeshikiwa bunduki. Huu siyo ubinadamu,” anaeleza mkulima na mfugaji wa Mabwegere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Utaratibu wa serikali wilayani umezaa ubaguzi, unyanyapaa kwa wafugaji na hasa Wamasai ambao wana mifugo mingi na umetoa mwanya kwa uporaji kwa kisingizio cha operesheni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna tatizo Kilosa. Panahitajika mpango mpana, wa kistaarabu, wa muda mrefu wa kugawa ardhi, kwa kushirikiana na mikoa mbalimbali ili wenye mifugo wapate maeneo ya kufugia na kulishia bila manyanyaso.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;(&lt;strong&gt;Makala hii ilichapishwa katika gazeti la &lt;/strong&gt;&lt;em&gt;MwanaHALISI&lt;/em&gt; &lt;strong&gt;toleo la Jumatano15 Aprili 2009)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-8210628400681060266?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/8210628400681060266/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=8210628400681060266' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8210628400681060266'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8210628400681060266'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/04/unyanganyi-unaosimamiwa-na-serikali.html' title='&lt;strong&gt;UNYANG&apos;ANYI UNAOSIMAMIWA NA SERIKALI&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-2701144041234944344</id><published>2009-04-24T05:16:00.000-07:00</published><updated>2009-04-24T05:19:18.494-07:00</updated><title type='text'>UVUNJAJI HAKI ZA BINADAMU + +</title><content type='html'>&lt;strong&gt;Viongozi waoga, katili wa Bukombe&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SITAKI viongozi wa wilaya ambao uwezo wao wa kufikiri ni mdogo na ambao wana haraka na uchu wa kutenda makosa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wa aina hiyo ni kama aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Bukombe, mkoani Shinyanga, Magesa S. Mulongo na kamati ya ulizi na usalama ya wilaya hiyo ambao wanalalamikiwa kwa kuwafukuza baadhi ya waandishi wa habari kutoka wilayani humo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Madai ya mkuu wa wilaya na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama yametajwa kuwa “waandishi wa habari kukiuka maadili ya kazi zao.” Hapa ndipo penye mnofu wa mjadala na uchambuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi nani hasa anapaswa kujua maadili ya kazi au taaluma fulani? Naomba kujibu haraka. Ni yule mwenye taaluma au kazi husika. Kwamba muhusika anaweza kutenda kinyume, haina maana kwamba hajui maadili. Anaweza kuwa ananufaika binafsi kwa kutofuata maadili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna mwingine ambaye anaweza kuwa anajua maadili ya kazi au taaluma yoyote, ni yule anayefanya utafiti na anayejali kufuatilia misingi na utekelezaji wa kazi inayohusika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Najenga mashaka juu ya uwezo wa mkuu wa wilaya ya Bokombe kujua kinachoitwa “maadili ya waandishi wa habari.” Najenga mashaka pia juu ya uwezo wa wajumbe wa kamati ya ulizi na usalama wa wilaya ya Bokombe kujua nini hasa kinaitwa uandishi wa habari, unavyofanywa na maadili yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa nini? Kwa sababu viongozi wa ngazi hii wameumbwa kwa woga. Ni katope wa tuhuma, shutuma na hata malalamiko. Wanayeyuka kwa sentensi moja ambayo mwandishi amenukuu kutoka mdomoni mwa mwananchi mmoja mwenye malalamiko halali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Najenga mashaka, juu ya tabia ya viongozi wa wilaya, ya kuogopa hata kishindo cha paka, inavyoweza kujua kazi na maadili ya waandishi wa habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naharakisha kusema, tena kwa uhakika, kwamba hakuna hata mmoja kati ya walioshiriki uamuzi wa kufukuzwa waandishi wa habari kutoka wilayani Bukombe, ambaye anajua hata msingi mmoja na muhimu – ule wa kuandika au kutangaza ukweli – wa taaluma ya habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanasiasa hawa wa ngazi ya wilaya, kama baadhi ya wale wa ngazi ya kitaifa, na hasa tunapojadili suala la habari, uhuru wa habari na haki na uhuru wa kupashana habari, siyo watu wa kutumainiwa kutoa maamuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watu waliotengenezwa ama kwa hariri au mabonge ya barafu, ni watu hatari sana. Watachanika kwa upepo mdogo au watayeyule kwa joto la mpakato tu. Kwa hiyo sharti waishi kwa mashaka na woga, wakidhani kila mmoja anataka kuwachana au kuwayeyusha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanasiasa wa Bukombe wanawatilia mashaka waandishi wa habari. Wanawaona, wanaamini, na ni kweli, kwamba hata waandishi wanawaona viongozi hao. Lakini viongozi wanataka sura zao, matendo yao na hata fikra zao, viishie Bukombe ambako wamewafungia wananchi katika giza la taarifa na kuwaaminisha kuwa wanafikiri kwa niaba yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yeyote anayeweza au anayejaribu kuonyesha sura halisi ya wanasiasa hao; jinsi wanavyotenda na wasivyotenda; jinsi walivyoshindwa au wasivyoweza kutenda, lazima ataonekana mbaya, mchafu, mfitini, mchochezi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niliwahi kufukuzwa mkoani Ruvuma. Ilikuwa katika miaka ya 1970. Mkuu wa mkoa Athumani Kabongo, akikaa na kamati yake, alinilazimisha kuhudhuria kikao ndani ya ofisi ya TANU na kudai mbele ya wajumbe kuwa nimeandika uwongo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alichukua hatua baada ya siku tatu za kuzungukia kata mbalimbali, ikiwemo kata ya Kilagano kujionea mwenyewe na wajumbe wake kwamba mahindi yalikuwa yanaoza wakati taifa likikabiliwa na njaa kubwa. Nilikuwa nimeandika taarifa hizo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Amri ya mkuu wa mkoa ilitolewa saa mbili tu baada ya mkoa kuunda kile ulichoita Operesheni Okoa Mazao ikisimamiwa na mkuu wa polisi mkoani. Angalia unafiki huu wa kiwango cha juu!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini niliwaambia viongozi kuwa sifukuziki. Badala ya kuondoka mkoani, nilichukua usafiri wa lori na kujichimbia wilayani Mbinga ambako niliibua makali zaidi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakumbuka mwandishi wa Radio Tanzania wakati huo, Abysai Stephen alinikuta Mbinga na kunieleza kuwa ameagizwa na mkuu wa mkoa anambie kuwa niondoke mkoani vinginevyo wangenikamata na kunifunga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna somo hapa. Nilikataa kuondoka mkoani. Niliendelea kuandika. Viongozi na polisi waliendelea kunisaka. Mkurugenzi wa wilaya aliona umuhimu wa kazi yangu. Akanipa gari la kwenda hadi Lipalamba na Mitomoni, kwenye mpaka wa Tanzania na Msumbiji. Niliibua mengi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ukaidi huu na kwa kazi iliyojaa usahihi wa aina ya kipekee, umma ulinufaika na serikali ilijua nani alikuwa anasema uwongo. Kilichofuatia ni viongozi wengi kuhamishwa, akiwemo mkuu wa mkoa, Athumani Kabongo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanasiasa wa ngazi ya kijiji, kata, wilaya, mkoa, taifa, hata kokote walipo, hawana uwezo wala mamlaka ya kuamua juu ya taaluma ya habari isipokuwa kwa sheria kandamizi ambazo wamezitunga. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawana uelewa katika taaluma hii. Hawana nia njema kwa uandishi na waandishi. Lakini hakuna anayewazuia kuwa na maoni. Acha wawe hivyo, nasi tuwashangae. Lakini wakitaka kuchukua hatua yoyote ya kuzuia waandishi kufanya kazi yao, sharti wafikirie kwanza uhuru wa wengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwenye uwezo wa kutoa uamuzi juu ya malalamiko yao ni mahakama. Waende huko. Washindwe. Warudi kwenye vigoda vyao na kupiga miayo; kwani katika mazingira haya, hakuna mahakama yenye uwezo wa kutoa hukumu ya kuzuia, kuzima wala kunyang’anya uhuru wa habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini sharti waandishi wa habari nao wakatae kufukuzwa. Ukondoo haulipi. Afadhali mwandishi akakamatwa, kuswekwa lupango na kuondolewa kesho kwa amri ya mahakama, kuliko kubaki huru mitaani lakini kichwa chini kama kondoo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapo ndipo somo litakolea. Tujifunze kusema: Hapana. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(IMECHAPISHWA KATIKA GAZETI LA&lt;/strong&gt; &lt;em&gt;TANZANIA DAIMA JUMAPILI&lt;/em&gt;)&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-2701144041234944344?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/2701144041234944344/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=2701144041234944344' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2701144041234944344'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/2701144041234944344'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/04/uvunjaji-haki-za-binadamu.html' title='&lt;strong&gt;UVUNJAJI HAKI ZA BINADAMU + +&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-3304308427808792358</id><published>2009-03-21T08:36:00.001-07:00</published><updated>2009-03-21T08:41:23.241-07:00</updated><title type='text'>'WAUMINI' WANAOANGAMIA KIMYAKIMYA</title><content type='html'>&lt;strong&gt;Serikali isiyojali maisha ya ‘Masalia’  &lt;/strong&gt;          &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                  &lt;strong&gt;  Na Ndimara Tegambwage&lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;SITAKI serikali ichukue nafasi ya mtazamaji tu pale maisha ya watu yanapokuwa hatarini; hata kwa madai kuwa huo ni utashi wa waliomo hatarini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili linahusu wale wanaojiita Wasabato Masalia. Hii ni klabu ya wanaojiita waumini katika imani fulani wanayoona inaweza kuwafikisha kwa Mungu au kuwaweka katika njia ielekeayo kwake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waumini hawa wanajiita “masalia.” Kwa jina hilo tu, utaona kuwa wao ni “mabaki.” Yaweza kuwa mabaki baada ya wenzao kuangamia au kupotea. Yaweza kuwa mabaki baada ya kuchekecha na wao kubaki makapi. Yaweza kuwa mabaki kwa uamuzi wao kuwa watabaki walivyo na hawataki kubadilishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hali ya kawaida, masalia ni masazo; yale yaliyoachwa, siyo kwa utashi wa masazo bali kwa utashi wa waliokuwa na uamuzi. Hatua ya kijiita masalia au masazo ni hatua ya kukata tamaa. Hatua ya kuwekwa pembeni na hata kutengwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wasabato Masalia walitoka mikoa mbalimbali nchini na kwenda Dar es Salam kwa shabaha moja: Kutumia uwanja wa ndege wa kimataifa – Julius Nyerere Airport (JNA) kwenda sehemu mbalimbali za dunia kuhubiri “Neno la Bwana.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kilichowakwamisha hakina uhusiano na masuala ya jinsia; kwamba walitaka kuhubiri “Neno la Bwana” bila kuhubiri “Neno la Bibi.” Walikwamishwa na sheria, kanuni na taratibu za safari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Walitaka kukaa uwanja wa ndege JNA, hadi hapo “Bwana” atakapoamua kuwachukua, tena kwa ndege, bila wao kuwa na pasipoti; bila vibali vya kusafiria kwenda nchi za nje (viza) na bila tiketi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiyo ni miezi tisa iliyopita. Walikuwa 52; sasa wamebaki 30. Kuna madai kuwa hao  pungufu (12) wameachana na imani isiyotekelezeka. Hilo laweza kuwa kweli au si kweli. Bali hao 30 bado wanakaa Tabata-Segerea, kwenye viunga vya Dar es Salaam wakisubiri “meli ya angani” iwapeleke kuhubiri nchi za nje.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kipindi chote, serikali imekaa kimya, ikiangalia mabaki ya wasabato yakilazimisha pumzi kutoka ndani ya miili yao, lakini bila mafanikio. Na kwa kuwa wameachwa bila ukaguzi, uangalizi na ufuatiliaji wa karibu, yawezekana hata hao 20 wanaosemekena kukana imani, siyo kwamba wamehama kambi, bali wamekufa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Usiri uliowaweka pamoja katika kuamini kisichoaminika wala kuaminiwa; ni usiri huohuo unaoweza kuwafanya wasitoe taarifa juu ya wagonjwa na waliokufa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kushindikana kwa utekelezaji wa mpango wao; au tuseme ile hatua ya Mungu ya kukataa kuwapelekea ndege isiyodai pasipoti, nauli na tiketi wala viza; mawili haya yanawafanya waone aibu na hivyo kushindwa kurejea kwenye jamii za awali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ving’ang’anizi au masalia waliosalia kati ya 50 wa awali, waweza kuitwa wenye “imani kali.” Maana ya imani kali (entuhi), ni ukaidi usio na mipaka; usiojali hoja, fikra wala hekima. Katika hili mambo kadhaa yaweza kujitokeza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanza, masalia waweza kuendelea kuishi Segerea; wakiugua na hata kufa mmojammoja na kimyakimya, hadi pasiwepo na masalia wa masalia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, masalia waliosalia au watakaokuwa wamesalia hapo baadaye, waweza kuamua kutorudi makwao; wakatawanyika miongoni mwa jamii wanamoishi na kuwa mzigo kwa jamii hiyo ambako watakuwa ombaomba hadi mwisho wa uhai wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu, masalia wa masalia waweza, hasa baada ya kuona Mungu amekataa au amedharau au ameshindwa kuwapelekea ndege, kuamua kuondoa maisha yao, tena kwa pamoja, ili kukwepa kimbunga cha aibu na hasira ya wanafamilia wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nne, masalia wa masalia waweza kuanzisha ushawishi mpya; tena kwa nguvu zaidi; kupata wafuasi wengine wanaojifikiria kuwa wameachwa na kwa pamoja kuunda jamii ya waliosazwa – wasiolima, wasiochuuza wala kufanya kazi yoyote, bali kuwa waumini wa kisichoaminiwa na kubaki ombaomba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tano, masalia wa masalia wanaendelea kujamiiana na kuzaa watoto masalia wa masalia wa masalia. Kizazi hiki ni bomu kubwa na hatari kwa maisha yao wenyewe na taifa kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sita, masalia waliofikia hatua ya kujiaminisha kuwa Mungu atawapelekea ndege ili wasafiri bwerere kwenda watakako duniani kote, tayati ni watu hatari kwao wenyewe na jamii wanamoishi. Mbegu yao yaweza kuzaa gugu lenye uwezo wa kuangamiza bustani za fikra na hekima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini serikali imekaa kimya juu ya maisha ya hatari ya wasabato masalia. Na hapa hatuongelei imani. Hakuna imani hapa! Kuna kuemewa kwa akili ambako kuna msingi katika mambo mengi yakiwemo, umasikini uliokithiri na ujinga uliowazonga na kuwafanya kujifungia na kufanya kazi moja tu maishani: Kuomba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alikuwa Mama Theresa wa Calcutta (mzaliwa wa Albania); mtumishi wa watu aliyejizolea heshima na utukufu kwa njia ya kutumikia watu. Siku moja alikuta masista aliokuwa akifanya nao kazi wametoka kwenda “kusali.” Aliwashangaa sana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katikati ya kitongoji cha Calcutta; jiji linalochukuliwa kuwa chafu zaidi na lililojaa masikini wa viwango vya kufa nchini India, Mama Theresa alikemea mtindo wa kusali, kusali, kusali!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aliwaambia masista, walipokuwa wamerejea kutoka kusali, kwamba kamwe wasithubutu tena kuweka muda maalum wa kusali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alisema, kwa kila tendo jema wanalofanya – iwe kuosha vidonda vya masikini, vya waliopata ajali, kulisha walio taabani na hata kusikiliza matatizo ya wanyonge – wanakuwa wamesali. Kusali kwa njia ya vitendo. Kusali kwa njia ya utumishi. Kusali na kutukuza Mungu kwa njia ya kutumikia wengine na kujitumikia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo, katika viunga vya jiji la Dar es Salaam, wasabato masalia wanajiua polepole – kwa kukaa na kuomba; kusubiri kisichopo; kutokuwa hata na kazi ndogo ya kujilisha, wao na familia zao; wanatenda jinai ya kujaribu kuondoa uhai wao kwa kisingizio cha kuomba Mungu na kusubiri maajabu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna mwenye busara ambaye atapendekeza serikali itumie nguvu kukamata na kuondosha masalia. Wala hakuna mwenye busara atakayependekeza serikali iache masalia wafe kwa kisingizio cha “demokrasi na uhuru wa kuabudu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuwaacha wafe mmojammoja au hata kwa makundi, ni kukiri kushindwa wajibu wa kulinda watu/raia na mali zao – jukumu kuu la serikali. Na masalia hawajaisha kabisa. Bado wana uhai na walichonacho ndiyo mali iliyosalia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali inayojali yaweza kuokoa maisha ya Wasabato Masalia. Na itende.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;(Makala hii itachapishwa katika Toleo la&lt;/strong&gt; &lt;em&gt;Tanzania Daima Jumapili&lt;/em&gt; &lt;strong&gt;la 22 Machi 2009 katika safu ya SITAKI)&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-3304308427808792358?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/3304308427808792358/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=3304308427808792358' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3304308427808792358'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/3304308427808792358'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/03/waumini-wanaoangamia-kimyakimya.html' title='&lt;strong&gt;&apos;WAUMINI&apos; WANAOANGAMIA KIMYAKIMYA&lt;/strong&gt;'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-8679671775619626776</id><published>2009-03-06T08:55:00.000-08:00</published><updated>2009-03-06T09:03:03.602-08:00</updated><title type='text'>Uwongo wa Butiku, Kitine na Warioba</title><content type='html'>Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Uwongo wa Butiku, Kitine na Warioba&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;SITAKI kusikia vilio vya wasioambilika. Hapa Joseph Butiku. Kule Joseph Warioba. Huku Hassy Kitine. Sitaki!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa imekuwa nongwa. Tumsikilize nani? Mara Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimepoteza dira. Mara nchi inaendeshwa kienyeji. Mara CCM inatapatapa. Tumsikilize nani na nani hasa mkweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wewe ni mwanachama wa chama kikongwe. Kilichokupa madaraka hadi ukayachoka au hadi kikakunyang’anya. Bado umo tu – CCM ndiyo baba, CCM ndiyo mama! Halafu unalalama kila kukicha: CCM mbaya! Hawana uongozi. Hawana dira.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi nani hasa atakuamini? Unatafuta nini wewe mwenye dira mahali ambako hakuna dira? Nani kakushikia huko? Utamu upi usioweza kuutema?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Imetokea vipi ukawa na dira katikati ya wasio na dira? Au dira ipo na wewe umeanza kushindwa kuisoma. Au dira imepotea kweli na wewe unasema, “potelea mbali” tutakufa wengi huko anga za mbali au maji marefu. Hutaki kuachana na chombo ingawa una mwavuli; ingawa una chombo cha kuelea. Unataka kuponea humohumo au kufia humohumo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Eh! Hata baada ya kujua kuwa chombo chako hakina dira; waongozaji wanatapatapa na chombo chenyewe kinaendeshwa kienyeji; bado hutoki? Hivi wewe ukoje? Ni kauli za dhati au za kufurahisha baraza?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi ni kweli dira ya CCM imetoweka au wajanja wameipoteza, kwa hiyo haipo? Nani alikuwa ameishikilia mara ya mwisho? Ameiweka wapi? Yeye anasemaje? Amehojiwa? Au dira ipo lakini “wazee” hawa hawawezi tena kusoma; hawawezi tena kuelewa hata wakisoma?&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Sikiliza. Kitine anasema hali iliyopo inahatarisha “usalama wa taifa.” Anasema nchi inaendeshwa kienyeji; uchumi na maliasili za taifa vimeshikwa na wageni wakati wazalendo wakifangia barabara na kufanya kazi za uboi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anajua hayo yanafanyika chini ya utawala wa CCM. Bado ni mwanachama wa CCM na bado hataki kutoka katika chama hicho. Anataka kulalama, kusikika na kurudi ukimyani. Basi. Huyu mkweli, mwongo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Anayotaja Kitine yameanza kuwa hivyo tangu lini? Si yalikuwepo alipokuwa mkuu wa mashushushu nchini? Si yalishamiri wakati akiwa waziri, Ofisi ya rais, anayeshughulikia “Utawala bora?” Je, wakati huo hayakuonekana katika dira ya chama chake?&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Butiku na Warioba wamekuwa wakilalamikia CCM na serikali kukosa mwelekeo katika mambo mbalimbali. Niliwahi kushikana mashati na Warioba katika safu hii hadi akanipigia simu na kuniuliza, “Wewe…ulikuwa umelewa wakati unaandika makala hii?” Tulicheka. Yaliisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara hii Butiku anatumia mkutano wa uchaguzi wa Chama cha Wananchi (CUF) kupeleka ujumbe kuwa chama chake “kinatapatapa” na kwamba hakina uongozi thabiti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Joseph Butiku ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere. Alikuwa msaidizi maalum wa Mwalimu kwa zaidi ya miaka ishirini. Warioba alikuwa Waziri Mkuu, Waziri na sasa wakili; lakini mtu mwenye uzito wa aina yake katika jamii na kauli yake inasikika na kuheshimika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukitaka kuwatendea haki Butiku, Kitine na Warioba, sharti kwanza ukubali kuwa ni watu, raia wa Tanzania , wenye haki ya kuwa na maoni juu ya mambo yanayowahusu wao na nchi yao . Wana haki ya kuona kama wanavyoona.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, sharti ukubali kuwa wana haki ya kushawishi wengine kuona kama wenyewe wanavyoona. Hili hasa ndilo linafanya watoe kauli zao hadharani; bila woga wala kificho. Sasa tatizo liko wapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatizo liko katika kulalamika. Tuanze hivi: Kulalamika kunatokana na kutokubaliana jinsi mambo yanavyoendeshwa – utawala, miliki ya raslimali za taifa na mengine. Kunatokana na wao kutokuwa kwenye nafasi ya kuweza kuleta mabadiliko wanayoona ni muwafaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa nyakati tofauti, hawa walikuwa kwenye nafasi za madaraka. Hawakulalamika. Labda hawakuona au waliona lakini wakazidiwa nguvu; au waliona ni mambo ya kawaida. Jana na leo ni tofauti; kila siku inayokuja na kupita, ni mwalimu na wakati huohuo ni maarifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini siku zimepita nyingi. Walimu, tena walimu bora, wamekuwa wengi na maarifa yanapaswa kuwa yameongezeka. Bahati mbaya kwa Butiku, Warioba na Kitine, maarifa hayaongezeki na wingi wa walimu bora si hoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inafikia wakati unalazimika kufikiri kuwa watu hawa ni waongo; tena waongo sana . Kuna tatizo; wanasema linawauma na kuwasumbua. Linawakera. Wanaelewa kiini chake. Lakini mbona hawachukii, na badala yake wanabakia kulalamika tu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siyo hoja mpya, kwamba ukichukia unachukua hatua. Hakika hatua haiwezi kuwa malalamiko katika vyombo vya habari au mikutanoni. Kuchukia siyo kuendelea kujiviringisha kwenye tope; kulialia huku ukiendelea kujizamisha miongoni mwa unaolalamikia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mazingira ya sasa nchini, kuchukia siyo tena kuendelea kuimba wimbo uleule wa kusubiri Mwenyezi Mungu alete fikra mpya na kupitia kwa kiongozi mkuu wa chama au serikali. Hapana!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli usiopingika kuwa Warioba, Butiku na Kitine wamepoteza muda mwingi kupiga porojo badala ya kuwaelekeza Watanzania nini kifanyike ili kuondoa kile ambacho wanaona hakifai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naye aliyeko madarakani, chukua mfano wa Rais Jakaya Kikwete, ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM, wala hana papara. Amewapa kamba ndefu ili kila mmoja ajinyonge kwa wakati wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ijumaa wiki hii aliwaambia waliostaafu uongozi wakae kimya kama Mzee Rashid Mfaume Kawawa na siyo kuwa “kilomolomo” wakati wao walishindwa yao walipokuwa kwenye uongozi. Amewachoka!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama Butiku, Kitine na Warioba wamesikia hayo na wangekuwa makini, wasingebakia CCM na kulalama kila kukicha. Kwa mfano, jinsi Butiku na Kitine walivyoongelea utawala na CCM, hawana sababu ya kubaki kwenye chama hicho “hatari.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wana kila sababu, pamoja na Warioba na wengine, kuhama chama hatari wanachosema kinatapatapa, kinauza nchi, kinaongoza kwa njia ya ubabaishaji; na kuanzisha chama kipya au kujiunga na kilichopo kwa ajili ya kuleta mabadiliko wanayotaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutofanya hivyo na badala yake kubakia kulalama, ni kupoteza muda na fursa mwanana ya kufanya jambo la maana katika maisha yao na maisha ya taifa lao. Ukichukia sharti uchukue hatua na hatua sahihi ni kuhama na kuelekeza umma wapi pa kuweka nguvu ili kukamilisha matumaini yao .&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hadi hapa, ningeombwa kutaja mafanikio ya CCM, nisingeacha kutaja “uwezo” wake wa kufyonza nguvu za mwili, roho na akili za viongozi na wanachama wake wengi, kiasi kwamba hata wanapokuwa hawakubaliani nacho, hubaki makasha yasiyoweza kufanya maasi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hiyo nayo ni sababu tosha ya kukataa mikatale ya CCM. Warioba, Butiku na Kitine, mpooo? Kuendelea kulalamikia CCM na utawala wake, na wakati huohuo kubaki kwapani mwake, ni kudhihirisha udhaifu, uwongo na unafiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;br /&gt;(Makala hii ilichapishwa katika safu ya SITAKI katika toleo la&lt;/span&gt; &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Tanzania Daima Jumapili&lt;/span&gt; l&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;a 1 Machi 2009)&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-8679671775619626776?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/8679671775619626776/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=8679671775619626776' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8679671775619626776'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/8679671775619626776'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/03/uwongo-wa-butiku-kitine-na-warioba.html' title='Uwongo wa Butiku, Kitine na Warioba'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-6771147471168788066</id><published>2009-03-06T08:45:00.000-08:00</published><updated>2009-03-06T08:50:28.470-08:00</updated><title type='text'>SERIKALI IONJESHWE UANDISHI WENYEWE</title><content type='html'>WAANDISHI WA HABARI WASIOHITIMU&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;span style="font-style:italic;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                            Na Ndimara Tegambwage&lt;br /&gt;SITAKI waandishi wa habari wafundishwe jinsi ya kuandika habari kwa muda wote wa maisha yao. Ifike mahali wajue kuandika na waanze kuwafundisha wenzao wanaoingia katika kazi hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kasheshe iliyozuka wiki hii kati ya ikulu na gazeti la Mwananchi inatokana na kutokomaa kwa waandishi katika taaluma yao. Hili linawahusu waandishi walioko kwenye magazeti, redio, televisheni, mashirika ya umma, makampuni binafsi na hata ikulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwananchi waliandika kichwa cha habari (3 Machi 2008), “Kikwete ajitosa sakata la umeme.” Maelezo yakasema Kikwete amesema Sheria ya Manunuzi ya Umma “isiwe kikwazo” katika miradi mikubwa ya umeme. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Gazeti likaongeza kuwa hilo limetokea wakati “suala la ununuzi wa mitambo ya ufuaji umeme wa dharura ya Dowans Tanzania Limited limekuwa gumzo kubwa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kesho yake, Mkurugenzi wa mawasiliano ikulu, Salva Rweyemamu akasema gazeti hilo limeonyesha “Rais Kikwete amejiingiza kwenye suala la ununuzi wa mitambo ya umeme ya Dowans.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa idhini yenu wasomaji, naomba turudi darasani. Tutumie vifungu sita vya taarifa ya ikulu (a, b, c, d, e na f). Shabaha iwe kuonyesha kwanza, jinsi ikulu isivyokuwa na sababu ya kulalamika; na pili jinsi Mwananchi lilivyowanyima wananchi uhondo wote katika taarifa ya ikulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu (a):  “Kwamba sekta ya madini isimamiwe kikamilifu kwa kuhakikisha kuwa wenye leseni za kutafuta na kuchimba mafuta wanazitumia kwa masharti yaliyoombewa na kuwa wasiozitumia leseni hizo kwa kuzingatia masharti ya leseni hizo wanyang’anywe leseni hizo badala ya kuzitumia kuendesha ulanguzi tu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe gazeti lingeandika kwamba mkutano wa tathmini ya utendaji wa serikali umegundua kuwa:&lt;br /&gt;(i) Sekta ya madini haisimamiwi kikamilifu&lt;br /&gt;(ii) Wenye leseni za kutafuta na kuchimba madini wanazitumia kuendesha ulanguzi tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujumla wa yote haya ni kwamba waziri muhusika na watendaji hawafanyi kazi yao na kwa hiyo hawastahili kuwepo. Rais aliyekuwa kwenye kikao ni shahidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu (b): “Kwamba zichukuliwe hatua za haraka kukomesha kabisa wizi wa mafuta ya transfoma ambao umesababisha hasara kubwa kwa taifa na kuvuruga mtandao wa kusambaza umeme kwa wananchi.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe gazeti lingeandika kuwa tathmini ya utendaji wa serikali imegundua kuwa: &lt;br /&gt;(i) Wizara na polisi wameshindwa kudhibiti wizi wa mafuta ya transfoma, tena kwa muda mrefu&lt;br /&gt;(ii) Uzembe huo umesababishia hasara kubwa kwa taifa (hapa wangetafuta takwimu)&lt;br /&gt;(iii) Uzembe huo au kutotenda kumevuruga mtandao wa kusambaza umeme nchini nzima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujumla wa yote haya ni kwamba waziri muhusika na watendaji hawafanyi kazi yao na kwa hiyo hawastahili kuwa kwenye nafasi hizo. Rais aliyekuwa kwenye kikao ni shahidi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu (c): “Kwamba Kamishna wa Madini Nchini, kwa kutumia madaraka na mamlaka yake kisheria, achukue hatua mara moja kukomesha uchimbaji wa kokoto katika maeneo yasiyostahili, na hasa katika eneo la Kunduchi/Tegeta, Dar es Salaam ambako serikali ilikwishakupiga marufuku uchimbaji wa kokoto, lakini baadhi ya wachimbaji wamerudi katika eneo hilo kuendesha uchimbaji.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe gazeti lingeandika kuwa tathmini ya utendaji wa serikali imegundua kuwa: &lt;br /&gt;(i) Kamishna wa Madini hajui au ameshindwa kutumia madaraka yake kisheria na hivyo ameshindwa kazi&lt;br /&gt;(ii) Amri ya serikali haina uzito au inapuuzwa katika eneo la kuchimba kokoto la Kunduchi/Tegeta&lt;br /&gt;(iii) Au amri inapindwa na baadhi ya watendaji serikalini kwa manufaa binafsi.&lt;br /&gt;Ujumla wa yote haya ni kwamba watendaji wizarani wameshindwa kazi, kwa hiyo waondolewe; au serikali imekosa nguvu, hivyo iweje? Rais aliyekuwa kwenye kikao ni shahidi.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kifungu (d): “Kwamba ziongezwe juhudi katika uzalishaji wa umeme nchini kwa sababu programu ya taifa ya uzalishaji umeme bado iko nyuma na liko pengo kubwa kati ya mahitaji halisi ya umeme nchini na umeme unaozalishwa kwa sasa.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe gazeti lingeandika kuwa tathmini ya utendaji wa serikali imegundua kuwa: &lt;br /&gt;(i) Watawala hawakuwa na taarifa, hadi wiki hii, kuwa programu ya taifa ya uzalishaji umeme bado iko nyuma&lt;br /&gt;(ii) Wizara na serikali kwa ujumla haikujua, hadi leo, kuwa kuna pengo kubwa kati ya mahitaji halisi ya umeme na umeme unaozalishwa&lt;br /&gt;(iii) Wahusika katika kufanya utafiti/kutoa taarifa watakuwa wamezembea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujumla wa yote haya ni kwamba watawala na watendaji, kwa miaka yote, wanafanya wasichojua; kwamba hawastahili kuwa madarakani. Rais aliyekuwa kwenye kikao ni shahidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu (e): “Kwamba dhana ya tenda na Sheria ya Manunuzi isiruhusiwe kuwa kikwazo katika miradi mikubwa mikubwa ya miundombinu ya nishati hasa ile ambako wawekezaji wamejitokeza katika maeneo ambako taifa linahitaji uwekezaji mkubwa na wa haraka na ambako nchi inaonekana ilichelewa kuwekeza.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe gazeti lingeandika kuwa tathmini ya utendaji wa serikali imegundua kuwa:  &lt;br /&gt;(i) Serikali imedhamiria kuvunja sheria za nchi kwa maslahi ya wawekezaji&lt;br /&gt;(ii) Utaratibu mzima wa kuitisha tenda sasa ni upuuzi mtupu pale wawekezaji watakapokuwa wamejitokeza&lt;br /&gt;(iii) Sasa ni mwendo holela kwa wawekezaji – wakiishajitokeza na kuwa nchini, basi sheria ya manunuzi iende likizo&lt;br /&gt;(iv) Nchi sasa itavamiwa na kuwa “uwanja wa fujo”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujumla wa yote haya ni kwamba Sheria ya Manunuzi ya Umma haina maana tena na kwamba kitakachotumika ni “ujanja kuwahi” kwa upande wa wenye miradi mikubwa na hasa ya umeme. Aidha, huu waweza kuwa mwanzo wa “uwanja wa fujo” katika kila sekta ya uwekezaji. Rais aliyekuwa kwenye kikao ni shahidi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu (e): “Kwamba kasi iongezwe katika kuhakikisha kuwa maeneo yaliyoahidiwa umeme yanapatiwa umeme bila ucheleweshaji usiokuwa na sababu.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kumbe gazeti lingeandika kuwa tathmini ya utendaji wa serikali imegundua kuwa: &lt;br /&gt;(i) Wizara husika imeshindwa kwenda kwa kasi inayohitajika katika kusambaza umeme&lt;br /&gt;(ii) Maeneo yaliyoahidiwa umeme yanacheleweshwa kupata umeme&lt;br /&gt;(iii) Hakuna sababu zozote za msingi za kuchelewesha usambazaji umeme.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ujumla wa yote haya ni kwamba uzembe umekithiri; waliopewa madaraka wameshindwa kazi na kwamba wakati ukifika serikali itaumbuka kwa kushindwa kutekeleza ahadi zake. Rais aliyekuwa kwenye kikao ni shahidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa usahihi zaidi, gazeti lingeandika kuwa wajumbe wa mkutano wa tathmini, walijiumbua mbele ya Rais Jakaya Kikwete kwa kujadili mambo ambayo walipaswa kuwa wameyafanya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Au, rais atakuwa alishangazwa sana na kauli za wajumbe katika kikao cha kujadili utekelezaji katika Wizara ya Nishati na Madini ambako imedhihirika, kwa mujibu wa taarifa ya ikulu, “karibu hakuna kinachoendelea.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huo ndio ungekuwa uandishi wa kuhitimu. Hata kama gazeti lingekabwa koo, kungekuwa na sababu kuwa limefikisha ujumbe kwa wananchi. Kwamba siri ya uzembe ndani ya ofisi za serikali, sasa imefichuka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ndio uandishi wa aina ya “uchambuzi fafanuzi,” ambao ni muhimu sana katika vyombo vya habari ambavyo vinatumikia wananchi katika kada zao nyingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Walichofanya Mwananchi ni kuripoti moja kwa moja kilichosemwa kwa kuongeza kidogo tu, mazingira ambamo hayo yametendeka. Halijakosea. Hata hivyo, hii haitoshi kukomea ambapo gazeti hilo lilikomea – kwa gharama yoyote ile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nenda mbele. Nenda ndani zaidi. Chukua mifano ya fafanuzi zilizowekwa kwa kila kipengee cha ikulu. Ikulu na serikali kwa ujumla, watazoea. Wataheshimu. Watavumilia. Tuwazoeshe wao na waandishi wao. Tuhitimu nao. Inawezekana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;(Makala hii itachapishwa katika safu ya SITAKI  ya gazeti la&lt;/span&gt; &lt;span style="font-style:italic;"&gt;Tanzania Daima Jumapili&lt;/span&gt; &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;toleo la 8 Machi 2009)&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;0713 614872&lt;br /&gt;ndimara@yahoo.com&lt;br /&gt;www.ndimara.blogspot.com&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8943712461165130839-6771147471168788066?l=ndimara.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://ndimara.blogspot.com/feeds/6771147471168788066/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8943712461165130839&amp;postID=6771147471168788066' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6771147471168788066'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8943712461165130839/posts/default/6771147471168788066'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://ndimara.blogspot.com/2009/03/serikali-ionjeshwe-uandishi-wenyewe.html' title='SERIKALI IONJESHWE UANDISHI WENYEWE'/><author><name>ndimara tegambwage</name><uri>http://www.blogger.com/profile/05750977914976705256</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8943712461165130839.post-5044244870719410998</id><published>2009-02-21T06:37:00.000-08:00</published><updated>2009-02-21T06:54:35.401-08:00</updated><title type='text'>VITA DHIDI YA RUSHWA TANZANIA</title><content type='html'>&lt;a href="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SaAVaURCpLI/AAAAAAAAAD0/a6PpvmkcB8w/s1600-h/Mbunge+Ndesamburo.jpg"&gt;&lt;img style="float:left; margin:0 10px 10px 0;cursor:pointer; cursor:hand;width: 153px; height: 156px;" src="http://2.bp.blogspot.com/_M2dlJvBabWg/SaAVaURCpLI/AAAAAAAAAD0/a6PpvmkcB8w/s200/Mbunge+Ndesamburo.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5305263902903411890" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Ndesamburo: Taarifa ndiyo silaha dhidi ya rushwa &lt;/strong&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Mahojiano kati ya Mheshimiwa Philemon NDESAMBURO, Mbunge wa Moshi Mjini na mwandishi wa habari Ndimara Tegambwage, siku 10 baada ya Ndesamburo kujiuzulu kutoka Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka, hapo 10 Januari 2007. Ndesamburo alijiuzulu kutokana na madai kwamba wabunge wamehongwa katika suala la madai ya Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi dhidi ya Adam Kighoma Malima, Mbunge wa Mkuranga, Pwani. Sababu nyingine aliyotoa ni kwamba utawala (executive) unaingilia Bunge&lt;/strong&gt; &lt;em&gt;(Mahojiano haya yalihifadhiwa kwenye blogu ya Ansbert Ngurumo. Nayaweka kwenye blogu yangu kurahisisha upatikanaji wake. Asante Ansi kwa kuyahifadhi)&lt;/em&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Swali:&lt;/strong&gt; Wakati ukiongea na waandishi wa habari juu ya kujiuzulu kwako, ulisema kwamba una umri mkubwa, zaidi ya miaka 70. Je, kwa umri huu bado unaweza kushiriki mapambano dhidi ya rushwa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Jibu:&lt;/strong&gt; Nani amekwambia kuwa umri ni kikwazo? Niliwaambia waandishi wa habari kwamba hata nikifa, nimeishazidi miaka 70. Basi. Ni umri mkubwa lakini siyo kwamba sina uwezo wa kuchukua maamuzi; tena hapa ndipo nastahili kuwa jasiri zaidi katika kukataa rushwa au tendo lolote la kifisadi. Kupambana na rushwa, kwanza ni dhamira, na pili, ni hatua mahsusi za kukataa kutoa au kupokea rushwa; kukataa kuhusishwa na rushwa na kufanya kila unaloweza kuzuia kitendo cha rushwa. Hapa suala la umri linatoka wapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Swali:&lt;/strong&gt; Bado niko kwenye umri. Nasema ungeanza mapema harakati hizi. Siyo leo. Na kwa msingi huo hakutakuwepo wa kuziendeleza kwani umri wako sasa ni mkubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Jibu:&lt;/strong&gt; Kupambana kunahitaji kuanzia pale ulipo. Kuanzia pale ulipopata fursa. Nasema suala la uzee haliingii hapa. Wenye umri mkubwa watafanya kile wanachoweza kwa wakati wao. Wataachia wengine wanaowafuata na vizazi vingine.&lt;br /&gt;Hata hivyo, siyo mimi niliyeanzisha mapambano dhidi ya rushwa. Wananchi wengi hawataki rushwa. Kuna asasi mbalimbali ambazo zimekuwa zikipambana na rushwa. Zilianza zamani. Mimi sikuanzisha chochote. Nilisema kuna madai kwamba wabunge wamehongwa. Madai yenye shina katika ofisi kubwa ya serikali – Ofisi ya Waziri Mkuu.&lt;br /&gt;Kwa kuwa nami nilikuwa mmoja wa wanaoshughulikia shauri muhimu katika Kamati, nikasema sikupokea rushwa, na kwa msingi huo, hata kama wenzangu watakaa kimya, mimi siwezi kubaki kwenye Kamati na kuyapa nguvu madai ya rushwa. Nikajiuzulu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;strong&gt;Swal
