JAJI MKUU NA AJIRA YA VIBARUA
Na Ndimara Tegambwage
JAJI Mkuu Agustino Ramadhani ametonesha vidonda. Kitendo chake cha kukutana na madereva na kusikiliza dhiki zao, kimezua adha kwa baadhi ya walioongea sana kikaoni.
Vidonda vilivyomwagiwa chumvi nyingi ni vya madereva Hoseah Mahenge na Godlove Ngilangwa; wote watumishi wa Mahakama ya Kazi jijini Dar es Salaam. Mahusiano yao na waajiri wao yametajwa kuwa “yanatota.”
Madereva hawa wamo katika ajira ya mahakama kwa takriban miaka mitano sasa. Wanalipwa mshahara wa Sh. 48,000 kwa mwezi na kwa muda wote huo, wamebaki vibarua. Hawajaajiriwa (!?).
Kinacholeta uzito katika suala la vibarua hawa ni kwamba mahakama inayowaajiri ndiyo imeundwa maalum kwa kazi kuu ya kushughulikia mashauri ya waajiriwa na waajiri – Mahakama ya Kazi.
Swali linaloulizwa na wengi ni, vipi Mahakama ya Kazi, inayopaswa kusimamia haki miongoni mwa waajiri na waajiriwa, inaweza kuwa katika kinachoonekana kuwa mgogoro wa kazi?
Swali jingine ni, Mahakama ya Kazi itakuwaje mfano bora kwa waajiri wengine na watumishi inaopatanisha, iwapo yenyewe, kama mwajiri, nyendo zake zinagongana na misingi ya ajira?
Labda tuulize swali jingine hapa: Kama Mahakama ya Kazi inaweza kumweka mtumishi kwa miaka mitano akiwa kibarua, jambo ambalo halikutarajiwa, nani awe msuluhishi, au hata mwamuzi?
Kumbe Jaji Mkuu ameanzisha utaratibu wa kukutana na kada mbalimbali katika utumishi wa mahakama. Mara hii alitaka kukutana na madereva ili kujua mazingira ya kazi zao na matatizo yanayowakabili.
Ni hapo, mbele yake, vilipomwagwa vilio vya madereva.
Hiyo ni miezi minne iliyopita. Madereva wa mahakama walikaa chumba kimoja na jaji mkuu. Kila mmoja aliyejisikia kutoa dukuduku lake alifanya hivyo.
Turudi kwa Hoseah Mahenge na Godlove Ngilangwa. Ninayoandika ndiyo yanafahamika ofisini kwa madereva-vibarua hawa. Hoseah ameoa. Ana watoto wawili. Godlove ameoa. Ana watoto watatu. Sikujua jinsia ya watoto hao.
Wanalipwa mshahara wa Sh. 48,000 kila mmoja kila mwezi kutunza familia zao. Jinsi gani kiasi hicho kinaweza kukidhi mahitaji, ni swali la kujibiwa na wahusika hao.
Taarifa za kiofisi zinaonyesha Hoseah amemaliza Kidato cha Nne. Amepata mafunzo ya udereva. Ana leseni. Amehitimu mafunzo ya nyongeza Chuo cha Usafirishaji cha Ubungo, Dar es Salaam.
Aidha, amepata mafunzo mengine katika Mamlaka ya VETA na chuo kingine cha Kihonda, Morogoro ambacho kimeelezwa kuwa moja ya vyuo muhimu kwa madereva.
Naye Godlove Ngilangwa anaonyeshwa kuwa amemaliza shule ya msingi, lakini amehudhuria mafunzo ya udereva katika vyuo mbalimbali na anaimudu kazi yake vema kama afanyavyo Hoseah.
Madereva hawa wanaelezwa kuwa miongoni mwa walionyoosha kidole wakiomba kujieleza na walipopewa nafasi, walimwaga vilio vyao kwa Jaji Mkuu Ramadhani.
Kilio chao kikuu kilikuwa kutopewa ajira ya kudumu kwa takriban miaka mitano sasa; malalamiko yao kutosikilizwa kwa kipindi kirefu; kupewa uhamisho bila kulipwa gharama za usumbufu; na kutopewa hadhi wanayostahili kama madereva wenye ujuzi kamili.
Imefahamika kwamba baada ya kikao na jaji mkuu, kiongozi huyo wa mahakama aliwaambia madereva wote kuwa ameelewa. Walipotaka kujua lini waliyomweleza yatafanyiwa kazi, imeelezwa kuwa jaji aliwaambia kuwa atafuatilia.
Wakati Hoseah na Godlove wanapokea Sh. 48,000 kwa mwezi, madereva wengine wanapokea zaidi ya Sh. 85,000; wanapangiwa safari zenye marupurupu ya alawansi na wanapata mafao mengine kama waajiriwa wa kudumu.
Kinachouma zaidi kwa upande wa madereva hawa wawili ni kwamba, kuna wenzao ambao hawana ujuzi wala uzoefu wa kiwango chao, ambao wana mshahara mkubwa na marupurupu kedekede.
“Mimi siwezi kujitapa, kwa mfano, kwa Hoseah. Ni kama mwalimu wetu; anajua mengi. Lakini kwa nini wanamweka kibarua kwa miaka yote hii, ni jambo ambalo haliwezi kupata jibu la hekima,” ameeleza mmoja wa madereva wa Mahakama ya Kazi.
Dereva mwingine wa Mahakama Kuu alimwambia mwandishi huyu kwamba miaka minne na zaidi ni kipindi kirefu cha kumweka mtu akisubiri ajira ya kudumu, hasa katika taasisi inayoamua mashauri yanayohusu waajiri na waajiriwa.
“Sisi wengine hatuna hata viwango vya kuwazidi hawa, lakini tuna fursa ya kupata mikopo na marupurupu mengine ya kiofisi, wakati wao wanakodoa macho kama watoto wa mama wa kambo,” ameeleza.
Hapa ndipo Jaji Mkuu anapopata kazi ya nyongeza. Kwanza ameanzisha utaratibu mzuri wa kuongea na kada mbalimbali. Utamu wa utaratibu huu umejichimbia kwenye nia yake ya kujua kulikoni katika maisha ya wafanyakazi wa ngazi ya chini.
Leo hii, Mkuu wa Mahakama anagundua kuwa tawi jingine la ofisi yake, limeweka madereva vibarua kwa takriban miaka mitano. Bila shaka hili linamsononesha.
Anagundua kuwa vibarua hao wamelia kwa muda mrefu lakini hakuna aliyewasikiliza. Bila shaka atajiuliza, iwapo suala la ajira ya dereva linaweza kupuuzwa, kutelekezwa, kudharauliwa au kunyamaziwa tu, kuna mangapi katika safu za juu ambayo hayaendi sawa?
Katika kudadisi suala hili, zimepatikana taarifa kwamba miezi kadhaa iliyopita, hasa baada ya madereva kukutana na jaji, kulikuwa na uvumi kuwa Hoseah na Godlove wangeachishwa kazi
Pendekezo hilo liligonga ukuta pale wahusika walipong’amua kuwa watalazimika kulipa kiasi kikubwa cha fedha kwa madereva hao. Kilichofuatia hapo ni madai kwamba madereva hawana elimu inayostahili.
Lakini ukweli ni tofauti na madai hayo. Hoseah ana elimu ya sekondari; amehudhuria mafunzo; ana vyeti na ujuzi mkubwa. Naye Godlove, pale alipoajiriwa kama kibarua, hakukuwa na masharti ya elimu ya sekondari.
Bali ukweli unabaki palepale kwamba watumishi wote ambao hawajafikia viwango vya elimu hupewa muda wa kusoma, na kwamba muda huo ukiisha wanakuwa ama wamepata elimu hiyo au hujiondosha kwenye ajira.
Godlove hajapewa sharti hilo wala muda wa kufanya hivyo. Sababu pekee ni kwamba hakuwa kwenye ajira ya kudumu kwa zaidi ya miaka minne; akitumikia chombo ambacho kinashughulikia mashauri ya aina hiyo kuwa ni ukiukaji sheria na haki!
Hivi sasa ni Jaji Mkuu Agustino Ramadhani ambaye anaweza kumaliza tatizo la ajira la vibarua hawa na wengine waliomwaga vilio vyao mbele yake.
Inaweza kuonekana kuwa “aibu” kwa watendaji katika Mahakama ya Kazi, kuona Jaji Mkuu akiteremka hadi ngazi hiyo, kushughulikia ajira ya vibarua. Bali kwa shabaha ya kuonyesha mfano, itabidi afanye hivyo.
(Imeandikwa rasmi kwa ajili ya gazeti la MwanaHALISI, 2 - 9 Januari 2008)
Simu: 0713 614872
ndimara@yahoo.com
Sunday, December 30, 2007
Saturday, December 29, 2007
NDEGE YA JESHI KATIKA BIASHARA
SITAKI Na Ndimara Tegambwage
Serikali inapodharau wananchi
SITAKI wananchi wakubali kudharauliwa na serikali waliyoiweka madarakani. Sitaki serikali iwaone kama wapiga kelele tu, kwa mtindo wa “wacha waseme, usiku watalala.”
Ni wiki ya nne sasa tangu wananchi waitake serikali yao iwaeleze ilikuwaje helikopta ya Jeshi la Wananchi (JWTZ) ikabeba “raia” wa Marekani, Uingereza, Canada na Australia kwa safari za kibiashara nchini.
Maswali makuu ni iwapo jeshi sasa limeingia katika biashara, kwa kukodisha baadhi ya zana zake za kivita; iwapo linakodisha helikopta peke yake au hata silaha nyingine; na nani ananufaika na biashara ambayo inaweza kuteketeza usalama wa nchi.
Imethibitika sasa kwamba watu hao kutoka nje ya nchi hawakuwa watumishi wa serikali za nchi zao; wala hawakuwa wametumwa na serikali. Aidha, nchi hizo hazina mkataba wala ushirikiano wa aina hiyo na jeshi au serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Lakini serikali imeendelea kukaa kimya. Hakuna maelezo. Na moja ya njia kuu za serikali kuficha ukweli, kuzima hoja, kuua mjadala na hata kusema uwongo, ni kukataa kusema.
Kukataa kusema kuna maana ya kutokuwa na jibu sahihi; kupuuza kilio cha wananchi; kutojali; kudharau hoja iliyoko mezani; na kudharau wananchi kwa msingi kuwa “hata hivyo hawana la kufanya.”
Kwa mujibu wa sheria zinazotawala jeshi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ndio msemaji mkuu wa chombo hicho.
Waziri amepewa jukumu la kulinda na kutawala vitu viwili muhimu katika jeshi. Kwanza, akulie na kutawala askari; na pili, asimamie na kulinda silaha.
Kwa ufupi, na kwa maana halisi ya kiufundi, askari na silaha ni “vifaa” muhimu na maalum chini ya uangalizi wa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa; kwa sasa Profesa Kapuya.
Askari ni neno linalotumika kitofautisha mtu na kitu, lakini katika maana hali ya jeshi, askari ni silaha. Ni silaha inayopumua; inayoishi katika mabweni ya jeshi; tofauti na silaha nyingine inayotunziwa katika ghala.
Waziri anapaswa kujua askari amepelekwa wapi na kwa kazi ipi; lini na kwa kipindi gani. Anapaswa kujua kifaa au silaha hii au ile iko wapi, imesogezwa wapi, kwanini; inatumikaje huko ilikopelekwa; inatumiwa na nani, kwa muda gani na iwapo ni kwa manufaa ya jeshi na nchi.
Katika hili la hekikopta, Kapuya anapaswa kujua majina ya raia wa nchi za nje ambao walikutwa na ndege; walikuja nchini kwa shughuli gani; nani aliwapeleka kwake au kwa msaidizi wake kuomba helikopta.
Ni waziri huyohuyo ambaye anapaswa kujua iwapo “wageni” waliomba msaada wa helikopta au walilipa kiasi gani ili wapewe silaha muhimu ya jeshi.
Waziri ndiye anaweza kujua rubani wake wa silaha inayoruka amelipwa kiasi gani cha posho, ikiwa nyongeza kwa mshahara wake wa kila mwezi. Waziri Profesa Juma Kapuya.
Lakini ni Kapuya ambaye siku chache baada ya kutunukiwa uwaziri; wakati wa fungate ya ushindi wa Rais Jakaya Kikwete, alichukua ndege ya JWTZ kwenda jimboni kwake.
Vyombo vya habari vilipohoji matumizi ya ndege ya jeshi, ni Kapuya aliyejibu, kwa jeuri isiyomithilika na kwa kuuliza, “Nisipotumia ndege nitumie farasi?”
Mara hii, Kapuya hana hata jeuri ya kutoa jibu la kejeli au angalau kueleza kuwa anajua lolote juu ya helikopta. Alinukuliwa na waandishi wa habari akisema yuko jimboni hakuwa na lolote la kusema.
Inawezekana kweli, watu kutoka nje walikuwa wanapiga picha ambazo zingetumika kusaidia shughuli za utalii hapo baadaye, lakini Wizara ya Utalii ina bajeti na mipango yake ambayo haiingiliani na silaha za jeshi.
Hata kama watatokea wenye kisingizio kwamba Wizara ya Utalii ilikuwa inajua kuwepo kwa wapigapicha hao kutoka nchi za nje, helikopta ya jeshi inafanya nini katika biashara hii ya kitalii.
Matumizi ya vyombo vya jeshi katika shughuli za binafsi na za watu wa nje, ni ushahidi tosha kwamba jeshi limeingizwa kwenye biashara ya watu binafsi.
Katika kila biashara kuna ushindani. Katika ushindani kuna kupata na kupoteza. Katika mazingira ya ushindani kwa kutumia raslimali za watu wengi kuna wanaosikitika, wanaolalamika na wanaopinga matumizi ya zana za kazi kwa manufaa ya watu binafsi na wachache.
Silaha zinazopumua ambazo ndizo hutumia silaha bubu katika tasnia ya kijeshi, huweza kujenga hisia kutumiwa na watu binafsi na hivyo kugawanyika, hasa linapokuja suala la maslahi.
Huo unaweza kuwa mwanzo wa mgawanyiko ndani ya ngome ambazo hazikuwahi kufikiria kutumiwa kwa biashara, bali kwa ulinzi, na ulinzi pekee wa nchi hii.
Profesa Kapuya aseme anachojua juu ya helikopta ya jeshi. Kunyamaa kwake ni kuasisi maafa yatokanayo na ulegevu katika safu za ulinzi wa nchi.
(Mwandishi wa makala
hii anapatikana kwa simu:
0713 614872; imeili:
ndimara@yahoo.com
Serikali inapodharau wananchi
SITAKI wananchi wakubali kudharauliwa na serikali waliyoiweka madarakani. Sitaki serikali iwaone kama wapiga kelele tu, kwa mtindo wa “wacha waseme, usiku watalala.”
Ni wiki ya nne sasa tangu wananchi waitake serikali yao iwaeleze ilikuwaje helikopta ya Jeshi la Wananchi (JWTZ) ikabeba “raia” wa Marekani, Uingereza, Canada na Australia kwa safari za kibiashara nchini.
Maswali makuu ni iwapo jeshi sasa limeingia katika biashara, kwa kukodisha baadhi ya zana zake za kivita; iwapo linakodisha helikopta peke yake au hata silaha nyingine; na nani ananufaika na biashara ambayo inaweza kuteketeza usalama wa nchi.
Imethibitika sasa kwamba watu hao kutoka nje ya nchi hawakuwa watumishi wa serikali za nchi zao; wala hawakuwa wametumwa na serikali. Aidha, nchi hizo hazina mkataba wala ushirikiano wa aina hiyo na jeshi au serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Lakini serikali imeendelea kukaa kimya. Hakuna maelezo. Na moja ya njia kuu za serikali kuficha ukweli, kuzima hoja, kuua mjadala na hata kusema uwongo, ni kukataa kusema.
Kukataa kusema kuna maana ya kutokuwa na jibu sahihi; kupuuza kilio cha wananchi; kutojali; kudharau hoja iliyoko mezani; na kudharau wananchi kwa msingi kuwa “hata hivyo hawana la kufanya.”
Kwa mujibu wa sheria zinazotawala jeshi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ndio msemaji mkuu wa chombo hicho.
Waziri amepewa jukumu la kulinda na kutawala vitu viwili muhimu katika jeshi. Kwanza, akulie na kutawala askari; na pili, asimamie na kulinda silaha.
Kwa ufupi, na kwa maana halisi ya kiufundi, askari na silaha ni “vifaa” muhimu na maalum chini ya uangalizi wa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa; kwa sasa Profesa Kapuya.
Askari ni neno linalotumika kitofautisha mtu na kitu, lakini katika maana hali ya jeshi, askari ni silaha. Ni silaha inayopumua; inayoishi katika mabweni ya jeshi; tofauti na silaha nyingine inayotunziwa katika ghala.
Waziri anapaswa kujua askari amepelekwa wapi na kwa kazi ipi; lini na kwa kipindi gani. Anapaswa kujua kifaa au silaha hii au ile iko wapi, imesogezwa wapi, kwanini; inatumikaje huko ilikopelekwa; inatumiwa na nani, kwa muda gani na iwapo ni kwa manufaa ya jeshi na nchi.
Katika hili la hekikopta, Kapuya anapaswa kujua majina ya raia wa nchi za nje ambao walikutwa na ndege; walikuja nchini kwa shughuli gani; nani aliwapeleka kwake au kwa msaidizi wake kuomba helikopta.
Ni waziri huyohuyo ambaye anapaswa kujua iwapo “wageni” waliomba msaada wa helikopta au walilipa kiasi gani ili wapewe silaha muhimu ya jeshi.
Waziri ndiye anaweza kujua rubani wake wa silaha inayoruka amelipwa kiasi gani cha posho, ikiwa nyongeza kwa mshahara wake wa kila mwezi. Waziri Profesa Juma Kapuya.
Lakini ni Kapuya ambaye siku chache baada ya kutunukiwa uwaziri; wakati wa fungate ya ushindi wa Rais Jakaya Kikwete, alichukua ndege ya JWTZ kwenda jimboni kwake.
Vyombo vya habari vilipohoji matumizi ya ndege ya jeshi, ni Kapuya aliyejibu, kwa jeuri isiyomithilika na kwa kuuliza, “Nisipotumia ndege nitumie farasi?”
Mara hii, Kapuya hana hata jeuri ya kutoa jibu la kejeli au angalau kueleza kuwa anajua lolote juu ya helikopta. Alinukuliwa na waandishi wa habari akisema yuko jimboni hakuwa na lolote la kusema.
Inawezekana kweli, watu kutoka nje walikuwa wanapiga picha ambazo zingetumika kusaidia shughuli za utalii hapo baadaye, lakini Wizara ya Utalii ina bajeti na mipango yake ambayo haiingiliani na silaha za jeshi.
Hata kama watatokea wenye kisingizio kwamba Wizara ya Utalii ilikuwa inajua kuwepo kwa wapigapicha hao kutoka nchi za nje, helikopta ya jeshi inafanya nini katika biashara hii ya kitalii.
Matumizi ya vyombo vya jeshi katika shughuli za binafsi na za watu wa nje, ni ushahidi tosha kwamba jeshi limeingizwa kwenye biashara ya watu binafsi.
Katika kila biashara kuna ushindani. Katika ushindani kuna kupata na kupoteza. Katika mazingira ya ushindani kwa kutumia raslimali za watu wengi kuna wanaosikitika, wanaolalamika na wanaopinga matumizi ya zana za kazi kwa manufaa ya watu binafsi na wachache.
Silaha zinazopumua ambazo ndizo hutumia silaha bubu katika tasnia ya kijeshi, huweza kujenga hisia kutumiwa na watu binafsi na hivyo kugawanyika, hasa linapokuja suala la maslahi.
Huo unaweza kuwa mwanzo wa mgawanyiko ndani ya ngome ambazo hazikuwahi kufikiria kutumiwa kwa biashara, bali kwa ulinzi, na ulinzi pekee wa nchi hii.
Profesa Kapuya aseme anachojua juu ya helikopta ya jeshi. Kunyamaa kwake ni kuasisi maafa yatokanayo na ulegevu katika safu za ulinzi wa nchi.
(Mwandishi wa makala
hii anapatikana kwa simu:
0713 614872; imeili:
ndimara@yahoo.com
Saturday, December 22, 2007
HELIKOPTA YA JESHI NA UTALII
Likizo ya rais na usalama wa taifa
SITAKI Rais Jakaya Kikwete aende likizo wakati kuna “suala kubwa linaloshusu usalama wa nchi.”
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyememu aliviambia vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Ijumaa kuwa rais yuko likizo, lakini aweza kufanya kazi iwapo kuna suala kubwa linalohusu usalama wa nchi.
Ukweli ni kwamba rais asingekwenda likizo, kwani suala linalohusu usalama wa nchi lipo mezani kwake. Ni lile linalohusu usalama wa mipaka ya nchi na wananchi wake.
Ni suala la kuingia katika ghala la silaha za Jeshi la Wananchi (JWTZ), kuchukua helikopta ya jeshi na kuruka hadi Arusha, huku waliokuwemo, tena watu kutoka nchi za nje – Uingereza, Canada, Marekani na Australia, wakipiga picha.
Tutake tusitake, hili ni suala la usalama wa nchi. Linahusu usalama wa wananchi na mali zao. Linahusu maisha ya nchi na viumbe wake.
Katika safu hii wiki iliyopita, nililalamikia ukimya wa serikali kuhusu tukio hilo. Niliuliza maswali 42. Nilidhani wahusika wataelewa. Watakuwa wepesi wa kujibu. Wataona wanawajibika kutoa majibu. Wataonyesha uadilifu.
Leo hii, wiki tatu tangu kupatikana kwa taarifa za helikopta ya jeshi kutumiwa na watalii kupiga picha, hakuna taarifa yoyote ya serikali – kutoka kwa Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Juma Kapuya au Amiri Jeshi Mkuu, Jakaya Mrisho Kikwete.
Katika hali hii, sharti watu wenye uchungu na nchi hii; wale wanaojali usalama wa nchi na watu wake, waendelee kuuliza. Hii ni kutokana na uzito wa suala lenyewe; ni kubwa na “linahusu usalama wa nchi.”
Ingawa wanaoiuzia silaha Tanzania wanajua kuna aina gani, kiasi gani, kutoka wapi, kwa bei ipi, zinaweza kutumiwa vipi na zina uwezo gani; kuna mambo kadhaa hawajui. Kwa mfano, hawajui lini silaha hizo zinahitajika kufanyiwa kazi.
Lakini hatua ya watu kutoka nchi za nje, kukodi, au kupewa, au kuiba helikopta ya jeshi na kuitumia kwa kazi binafsi, inaonyesha kuwa: Jeshi limeingiliwa. Kuna wanaojua taratibu za kila siku jeshini, matumizi ya zana; zipi zinahitajika sasa, zipi zikodishwe na zipi zikae “stendibai.”
Hao ndio wanakwenda ama kuchukua, kukodi au kupewa helikopta za jeshi. Au kuna “Idara ya Masoko” jeshini inayotangaza na kufuatilia wateja wa kutumia hekikopta zake.
Aidha, hatua ya kupata helikopta ya jeshi kwa matumizi binafsi, inaonyesha ama ulinzi ndani ya jeshi umepungua au umelegezwa. Nani kapunguza au kalegeza ulinzi na kwa nini; ndilo swali kubwa hivi leo.
Nani amekataa kuweka suala hili mezani kwa Rais Kikwete, mpaka rais anakwenda likizo bila kulishughulikia? Au, nani amemshauri rais kuwa ni “jambo dogo” kwa hiyo alale na kusahau?
Au tafsiri ya “usalama wa nchi” ndiyo inagomba? Na hili linawezekana. Kuna wanaodhani usalama wa nchi ni usalama wa rais kutopinduliwa, kutopingwa au kutoseng’enywa. Huo ni ufinyu na upofu.
Nani anaweza kumuaga rais, na kumtakia likizo njema, wakati katika jeshi lake kuna biashara inayoweza kuzaa mtafaruku mkubwa wa kuweza kumeza amani nchini au kurudisha nyuma maendeleo madogo ya kidemokrasi yaliyopatikana?
Labda rais awe anajua kuwa kinachoendelea “ni kidogo kisicho na athari mbaya na kubwa;” au anaridhika kuwa kinachofanyika ni sahihi; au hana taarifa kamili juu ya kinachotendeka.
Vyovyote itakavyokuwa, hapo ndipo rais anapaswa kujenga mashaka juu ya chochote kinachotendeka; hasa chochote ambacho wananchi wametilia mashaka; na hasa kile ambacho wachambuzi wameonyesha kinaweza kuleta madhara kiulinzi, kisiasa na kiuchumi.
Ukimya wa serikali unaleta tafsiri nyingi. Kwamba wanaokataa kutoa kauli, wanajua kinachoendelea lakini wanashindwa kutoa majibu ambayo wanajua vema kwamba hayatazima kiu ya wananchi na wapenda nchi.
Kwamba wanaokataa kutoa kauli wanajua nani aliidhinisha matumizi ya helikopta nje ya utaratibu; wanajua kama ndio utaratibu na wanajua nani anachuma kutoka mradi huu ambao bila shaka unaingiza fedhi nyingi.
Na katika hili, tukizungumzia viongozi serikalini ambao wanapaswa kutoa kauli, tuna maana ya kwanza na moja kwa moja, Rais Kikwete, Waziri Mkuu Edward Lowassa, Waziri Kapuya, mteule wa rais, Jenerali Mwamunyange na Waziri wa Habari Mohamed Seif Khatib.
Kama wasemaji wanaona suala hili la kuvunja na kuingia kwenye ngome ya jeshi na kuchukua, kuiba au kupewa helikopta ni suala dogo, kwa nini hawatoi majibu yanayolingana na “udogo” huo?
Kama wanaona ni suala kubwa, tena la ulinzi na usalama wa nchi, kwa nini wanakaa kimya na kumwacha rais aende likizo wakati kuna suala kubwa la kumzuia kwenda kulala?
Mkuu wa Mawasiliano ikulu, Salva Rweyemamu, anasema likitokea jambo kubwa la usalama wa nchi, rais anaweza kufanya kazi akiwa likizoni.
Salva, mpelekee rais suala hili. Mfafanulie kwamba, kama ngome ya jeshi imepenywa, na watu kutoka nje wakachukua helikopta ya jeshi kwa raha binafsi, basi yeye na wananchi wake wote, wako uchi!
Mwambie avae na avalishe nchi yake. Lakini muhimu zaidi, mwambie ajibu maswali ya wananchi yaliyowasilishwa kupitia safu hii – wiki iliyopita na leo – ili wajue nafasi yake katika hili na hatua anazochukua.
(Makala hii imeandikwa kwa kuchapishwa katika safu ya SITAKI ya gazeti la Tanzania Daima, Jumapili, 23 Desemba 2007. Mwandishi anapatikana kwa simu: 0713 614872; imeili: ndimara@yahoo.com)
SITAKI Rais Jakaya Kikwete aende likizo wakati kuna “suala kubwa linaloshusu usalama wa nchi.”
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyememu aliviambia vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Ijumaa kuwa rais yuko likizo, lakini aweza kufanya kazi iwapo kuna suala kubwa linalohusu usalama wa nchi.
Ukweli ni kwamba rais asingekwenda likizo, kwani suala linalohusu usalama wa nchi lipo mezani kwake. Ni lile linalohusu usalama wa mipaka ya nchi na wananchi wake.
Ni suala la kuingia katika ghala la silaha za Jeshi la Wananchi (JWTZ), kuchukua helikopta ya jeshi na kuruka hadi Arusha, huku waliokuwemo, tena watu kutoka nchi za nje – Uingereza, Canada, Marekani na Australia, wakipiga picha.
Tutake tusitake, hili ni suala la usalama wa nchi. Linahusu usalama wa wananchi na mali zao. Linahusu maisha ya nchi na viumbe wake.
Katika safu hii wiki iliyopita, nililalamikia ukimya wa serikali kuhusu tukio hilo. Niliuliza maswali 42. Nilidhani wahusika wataelewa. Watakuwa wepesi wa kujibu. Wataona wanawajibika kutoa majibu. Wataonyesha uadilifu.
Leo hii, wiki tatu tangu kupatikana kwa taarifa za helikopta ya jeshi kutumiwa na watalii kupiga picha, hakuna taarifa yoyote ya serikali – kutoka kwa Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Juma Kapuya au Amiri Jeshi Mkuu, Jakaya Mrisho Kikwete.
Katika hali hii, sharti watu wenye uchungu na nchi hii; wale wanaojali usalama wa nchi na watu wake, waendelee kuuliza. Hii ni kutokana na uzito wa suala lenyewe; ni kubwa na “linahusu usalama wa nchi.”
Ingawa wanaoiuzia silaha Tanzania wanajua kuna aina gani, kiasi gani, kutoka wapi, kwa bei ipi, zinaweza kutumiwa vipi na zina uwezo gani; kuna mambo kadhaa hawajui. Kwa mfano, hawajui lini silaha hizo zinahitajika kufanyiwa kazi.
Lakini hatua ya watu kutoka nchi za nje, kukodi, au kupewa, au kuiba helikopta ya jeshi na kuitumia kwa kazi binafsi, inaonyesha kuwa: Jeshi limeingiliwa. Kuna wanaojua taratibu za kila siku jeshini, matumizi ya zana; zipi zinahitajika sasa, zipi zikodishwe na zipi zikae “stendibai.”
Hao ndio wanakwenda ama kuchukua, kukodi au kupewa helikopta za jeshi. Au kuna “Idara ya Masoko” jeshini inayotangaza na kufuatilia wateja wa kutumia hekikopta zake.
Aidha, hatua ya kupata helikopta ya jeshi kwa matumizi binafsi, inaonyesha ama ulinzi ndani ya jeshi umepungua au umelegezwa. Nani kapunguza au kalegeza ulinzi na kwa nini; ndilo swali kubwa hivi leo.
Nani amekataa kuweka suala hili mezani kwa Rais Kikwete, mpaka rais anakwenda likizo bila kulishughulikia? Au, nani amemshauri rais kuwa ni “jambo dogo” kwa hiyo alale na kusahau?
Au tafsiri ya “usalama wa nchi” ndiyo inagomba? Na hili linawezekana. Kuna wanaodhani usalama wa nchi ni usalama wa rais kutopinduliwa, kutopingwa au kutoseng’enywa. Huo ni ufinyu na upofu.
Nani anaweza kumuaga rais, na kumtakia likizo njema, wakati katika jeshi lake kuna biashara inayoweza kuzaa mtafaruku mkubwa wa kuweza kumeza amani nchini au kurudisha nyuma maendeleo madogo ya kidemokrasi yaliyopatikana?
Labda rais awe anajua kuwa kinachoendelea “ni kidogo kisicho na athari mbaya na kubwa;” au anaridhika kuwa kinachofanyika ni sahihi; au hana taarifa kamili juu ya kinachotendeka.
Vyovyote itakavyokuwa, hapo ndipo rais anapaswa kujenga mashaka juu ya chochote kinachotendeka; hasa chochote ambacho wananchi wametilia mashaka; na hasa kile ambacho wachambuzi wameonyesha kinaweza kuleta madhara kiulinzi, kisiasa na kiuchumi.
Ukimya wa serikali unaleta tafsiri nyingi. Kwamba wanaokataa kutoa kauli, wanajua kinachoendelea lakini wanashindwa kutoa majibu ambayo wanajua vema kwamba hayatazima kiu ya wananchi na wapenda nchi.
Kwamba wanaokataa kutoa kauli wanajua nani aliidhinisha matumizi ya helikopta nje ya utaratibu; wanajua kama ndio utaratibu na wanajua nani anachuma kutoka mradi huu ambao bila shaka unaingiza fedhi nyingi.
Na katika hili, tukizungumzia viongozi serikalini ambao wanapaswa kutoa kauli, tuna maana ya kwanza na moja kwa moja, Rais Kikwete, Waziri Mkuu Edward Lowassa, Waziri Kapuya, mteule wa rais, Jenerali Mwamunyange na Waziri wa Habari Mohamed Seif Khatib.
Kama wasemaji wanaona suala hili la kuvunja na kuingia kwenye ngome ya jeshi na kuchukua, kuiba au kupewa helikopta ni suala dogo, kwa nini hawatoi majibu yanayolingana na “udogo” huo?
Kama wanaona ni suala kubwa, tena la ulinzi na usalama wa nchi, kwa nini wanakaa kimya na kumwacha rais aende likizo wakati kuna suala kubwa la kumzuia kwenda kulala?
Mkuu wa Mawasiliano ikulu, Salva Rweyemamu, anasema likitokea jambo kubwa la usalama wa nchi, rais anaweza kufanya kazi akiwa likizoni.
Salva, mpelekee rais suala hili. Mfafanulie kwamba, kama ngome ya jeshi imepenywa, na watu kutoka nje wakachukua helikopta ya jeshi kwa raha binafsi, basi yeye na wananchi wake wote, wako uchi!
Mwambie avae na avalishe nchi yake. Lakini muhimu zaidi, mwambie ajibu maswali ya wananchi yaliyowasilishwa kupitia safu hii – wiki iliyopita na leo – ili wajue nafasi yake katika hili na hatua anazochukua.
(Makala hii imeandikwa kwa kuchapishwa katika safu ya SITAKI ya gazeti la Tanzania Daima, Jumapili, 23 Desemba 2007. Mwandishi anapatikana kwa simu: 0713 614872; imeili: ndimara@yahoo.com)
SALAAM ZA MWAKA MPYA
Centre for Democratic and Strategic Management
(IDEA works through its Five Units, namely: Socio-Political and Economic; Legal and Constitutional Affairs (Legal Aid); Human Rights and Good Governance; News Analysis, Media Research and Training; and Conflict Management. P.O. Box 71775, Dar es Salaam, Tanzania Tel: 0741 614 872, e-mail:ideacent@yahoo.com)
21 December 2007
IDEA wishes to share
with you
the joys and hopes of the
Seasonal Festivities and
look forward to a prosperous
New Year 2008.
Let’s keep holding together.
Ndimara Tegambwage
Executive Director
ideacent@yahoo.com
ndimara@yahoo.com
www.ndimara.blogspot.com
(IDEA works through its Five Units, namely: Socio-Political and Economic; Legal and Constitutional Affairs (Legal Aid); Human Rights and Good Governance; News Analysis, Media Research and Training; and Conflict Management. P.O. Box 71775, Dar es Salaam, Tanzania Tel: 0741 614 872, e-mail:ideacent@yahoo.com)
21 December 2007
IDEA wishes to share
with you
the joys and hopes of the
Seasonal Festivities and
look forward to a prosperous
New Year 2008.
Let’s keep holding together.
Ndimara Tegambwage
Executive Director
ideacent@yahoo.com
ndimara@yahoo.com
www.ndimara.blogspot.com
Saturday, December 15, 2007
JESHI LAINGIA BIASHARA YA UTALII?
JWTZ NA BIASHARA YA KITALII
Na Ndimara Tegambwage
SITAKI serikali ikae kimya kuhusu matumizi ya helikopta ya Jeshi la Wananchi (JWTZ) iliyoanguka mkoani Arusha siku 11 zilizopita. Sitaki!
Maelezo ya awali ni kwamba helikopta ya jeshi ilikuwa imebeba “watalii” kutoka Canada, Marekani, Uingereza na Australia na kwamba ilianguka na kuwaka moto.
Watalii na helikopta ya jeshi? Watalii kutoka nchi za nje, na siyo watalii wa ndani ya nchi, na helikopta ya jeshi? Watalii wasiokuwa na uwezo kifedha wa kukodisha ndege yao mpaka watumie helikopta ya jeshi?
Watalii kutoka nchi tajiri, Canada, Marekani na Uingereza, nchi washirika wakubwa katika maendeleo ya Tanzania kwa kutoa mikopo na misaada, hawana uwezo wa kukodi ndege kutoka kampuni binafsi? Mpaka watumie helikopta ya jeshi?
Eti watalii walikuwa wanapiga picha za Ziwa Natron na mlima Oldonyo wenye volcano hai! Kwamba ziwa na mlima haviwezi kuonekana vizuri kutoka ndege ya kiraia mpaka mpigapicha awe katika ndege ya jeshi?
Katika hili kwa nini serikali inakaa kimya? Inataka habari hii ife? Inataka wananchi waendelee kujiuliza maswali mengi bila kupata majibu sahihi? Au inataka baadaye, itoke na kauli kwamba mambo ya jeshi hayajadiliwi katika vyombo vya habari?
Hakika, hapa serikali isisubiri kuumbuliwa. Ni jana, Jumamosi, baadhi ya waandishi wa habari walikabidhiwa tuzo za uandishi wa uchunguzi nchini. Ukweli ni kwamba bado wanatambaa, lakini tuzo hizo ni motisha kubwa katika kuandika habari za uchokonozi.
Leo hii, hakuna habari nono kama hii. Rubani wa helikopta ni nani? Helikopta ilianzia wapi safari ya kwenda Natron na Oldonyo. Ilipita wapi na “watalii” walikuwa wakifanya nini kabla ya kukaribia maeneo waliyokuwa wakitaka kupiga picha?
Je, kuna kitengo cha utalii katika JW? Kama kipo, kina ndege na helikopta ngapi? Vifaa vyake vingine kwa shughuli hii ni vipi? Je, utalii ni moja ya miradi ya jeshi ya kuzalisha fedha za matumizi ya nyongeza? Je, jeshi linapungukiwa fedha kiasi cha kuanzisha miradi ya “kubangaiza?”
Je, helikopta iliyobeba watalii iliidhinishwa na nani kufanya kazi hiyo? Ilitoka ngome ipi ya jeshi? Kwa nini iliamuliwa kuwa hiyo ndiyo ilikuwa inafaa? Rubani wa helikopta ya jeshi alijuaje maeneo ya kupita ili watalii wapate picha nzuri waliozotaka?
Kuna maswali mengi. Wanaoitwa watalii walitoka wapi kabla ya kuingia Tanzania? Nani anaweza kuthibitisha kweli kwamba ni watalii? Viwanja vya ndege na, au mipaka ya nchi ina rekodi gani juu ya kuingia nchini kwa watalii hao?
Tayari helikopta imeanguka na kuungua. Watalii wamepona! Nani amethibitisha uraia wa watalii? Balozi za nchi watokako watalii hao, zilizoko Dar es Salaam, zinasemaje juu ya raia wake, kama kweli wanatoka huko?
Balozi ambazo nchi zao huning’iniza serikali za nchi nyingi zikizitaka kuwa adilifu, zinasema nini juu ya raia wake kutumia helikopta ya jeshi la ulinzi kwa raha na mafao ya binafsi?
Kuna uhusiano gani kati ya watalii wa Canada, Marekani, Australia na Uingereza kwa upande mmoja, na balozi na nchi watokako, kwa upande mwingine? Je, inawezekana “watalii” wametumwa kutoa mtihani wa uimara au ulegevu wa jeshi?
Nani alichora mpango wa watalii kutumia helikopta ya jeshi? Huyo lazima awe mtu muhimu katika mahusiano ya jeshi. Kwamba ndege ndogo za kibiashara zinagombea maegesho kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere, ni motisha gani watalii walipata kutumia ndege ya jeshi?
Hapa ni muhimu kujua iwapo rubani alikuwa askari wa JW au raia anayejua kuvurumisha kikata hewa hicho Je, rubani wa helikopta alikodishwa kwa kiasi gani au alikuwa wa kujitolea?
Je, helikopta ya jeshi ilichukuliwa kwa mkataba upi? Kuna malipo yoyote yaliyotolewa au ahadi ya kulipa? Kiasi gani cha malipo – fedha taslimu au asante kwa njia mbalimbali? Lini malipo hayo yatatolewa au yalitolewa?
Lakini muhimu pia ni kujua nani hasa anafaidika na malipo hayo – aliyeidhinisha matumizi ya helikopta, rubani na aliyemtuma, baadhi ya maofisa wakuu jeshini, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa au ikulu? Nani anapokea “mshiko?”
Muhimu pia ni kwamba Amiri Jeshi ni rais. Mara hii ni Jakaya Mrisho Kikwete ambaye wakati anaondoka wiki hii kwa ziara ya Marekani aliacha helikopta yake imetumiwa na “watalii” na imeanguka na kuungua.
Amiri Jeshi anasemaje juu ya matumizi ya helikopta “yake?” Helikopta za jeshi, kama zilivyo ndege na magari ya jeshi, ni sehemu ya zana za kazi; waweza kusema, zana za ulinzi wa taifa. Vimeundwa na vinapaswa kutumika na kusimamiwa kwa misingi ya ulizi.
Nafasi ya Amiri Jeshi ni ya kulinda maisha na mali za wananchi ndani ya mipaka ya nchi yao na dhidi ya uchokozi au uvamizi kutoka nje. Kwa maana pana, helikopta ni mali ya wananchi, waliyonunua kwa kodi wanazotozwa na inayopaswa kutumiwa kwa ulinzi wao.
Katika mazingira ambamo serikali imekataa kutoa taarifa juu ya helikopta ya jeshi kutumiwa na watalii kutoka nje kufanya shughuli binafsi, ni uandishi wa wa uchokonozi ambao pekee unaweza kusaidia kuleta nuru juu ya kilichotendeka.
Hadi hapo taarifa zitakapowekwa wazi, acha kila mwananchi awe na mawazo yake: Kwamba sasa jeshi linabangaiza kama machinga; au halina ulinzi kwani kila mmoja aweza kuingia na kujichukulia ndege anavyotaka; au ulinzi wa wananchi sasa mashakani; au wakubwa wameamua kutumia jeshi kufanya biashara ya anga; au amiri jeshi kaenda likizo.
(Makala hii imeandikwa kwa ajli ya safu ya SITAKI, gazeti la Tanzania Daima Jumapili, 16 Desemba 2007. Mwandishi anapatikana kwa simu: 0713 614872; imeili: ndimara@yahoo.com)
Na Ndimara Tegambwage
SITAKI serikali ikae kimya kuhusu matumizi ya helikopta ya Jeshi la Wananchi (JWTZ) iliyoanguka mkoani Arusha siku 11 zilizopita. Sitaki!
Maelezo ya awali ni kwamba helikopta ya jeshi ilikuwa imebeba “watalii” kutoka Canada, Marekani, Uingereza na Australia na kwamba ilianguka na kuwaka moto.
Watalii na helikopta ya jeshi? Watalii kutoka nchi za nje, na siyo watalii wa ndani ya nchi, na helikopta ya jeshi? Watalii wasiokuwa na uwezo kifedha wa kukodisha ndege yao mpaka watumie helikopta ya jeshi?
Watalii kutoka nchi tajiri, Canada, Marekani na Uingereza, nchi washirika wakubwa katika maendeleo ya Tanzania kwa kutoa mikopo na misaada, hawana uwezo wa kukodi ndege kutoka kampuni binafsi? Mpaka watumie helikopta ya jeshi?
Eti watalii walikuwa wanapiga picha za Ziwa Natron na mlima Oldonyo wenye volcano hai! Kwamba ziwa na mlima haviwezi kuonekana vizuri kutoka ndege ya kiraia mpaka mpigapicha awe katika ndege ya jeshi?
Katika hili kwa nini serikali inakaa kimya? Inataka habari hii ife? Inataka wananchi waendelee kujiuliza maswali mengi bila kupata majibu sahihi? Au inataka baadaye, itoke na kauli kwamba mambo ya jeshi hayajadiliwi katika vyombo vya habari?
Hakika, hapa serikali isisubiri kuumbuliwa. Ni jana, Jumamosi, baadhi ya waandishi wa habari walikabidhiwa tuzo za uandishi wa uchunguzi nchini. Ukweli ni kwamba bado wanatambaa, lakini tuzo hizo ni motisha kubwa katika kuandika habari za uchokonozi.
Leo hii, hakuna habari nono kama hii. Rubani wa helikopta ni nani? Helikopta ilianzia wapi safari ya kwenda Natron na Oldonyo. Ilipita wapi na “watalii” walikuwa wakifanya nini kabla ya kukaribia maeneo waliyokuwa wakitaka kupiga picha?
Je, kuna kitengo cha utalii katika JW? Kama kipo, kina ndege na helikopta ngapi? Vifaa vyake vingine kwa shughuli hii ni vipi? Je, utalii ni moja ya miradi ya jeshi ya kuzalisha fedha za matumizi ya nyongeza? Je, jeshi linapungukiwa fedha kiasi cha kuanzisha miradi ya “kubangaiza?”
Je, helikopta iliyobeba watalii iliidhinishwa na nani kufanya kazi hiyo? Ilitoka ngome ipi ya jeshi? Kwa nini iliamuliwa kuwa hiyo ndiyo ilikuwa inafaa? Rubani wa helikopta ya jeshi alijuaje maeneo ya kupita ili watalii wapate picha nzuri waliozotaka?
Kuna maswali mengi. Wanaoitwa watalii walitoka wapi kabla ya kuingia Tanzania? Nani anaweza kuthibitisha kweli kwamba ni watalii? Viwanja vya ndege na, au mipaka ya nchi ina rekodi gani juu ya kuingia nchini kwa watalii hao?
Tayari helikopta imeanguka na kuungua. Watalii wamepona! Nani amethibitisha uraia wa watalii? Balozi za nchi watokako watalii hao, zilizoko Dar es Salaam, zinasemaje juu ya raia wake, kama kweli wanatoka huko?
Balozi ambazo nchi zao huning’iniza serikali za nchi nyingi zikizitaka kuwa adilifu, zinasema nini juu ya raia wake kutumia helikopta ya jeshi la ulinzi kwa raha na mafao ya binafsi?
Kuna uhusiano gani kati ya watalii wa Canada, Marekani, Australia na Uingereza kwa upande mmoja, na balozi na nchi watokako, kwa upande mwingine? Je, inawezekana “watalii” wametumwa kutoa mtihani wa uimara au ulegevu wa jeshi?
Nani alichora mpango wa watalii kutumia helikopta ya jeshi? Huyo lazima awe mtu muhimu katika mahusiano ya jeshi. Kwamba ndege ndogo za kibiashara zinagombea maegesho kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere, ni motisha gani watalii walipata kutumia ndege ya jeshi?
Hapa ni muhimu kujua iwapo rubani alikuwa askari wa JW au raia anayejua kuvurumisha kikata hewa hicho Je, rubani wa helikopta alikodishwa kwa kiasi gani au alikuwa wa kujitolea?
Je, helikopta ya jeshi ilichukuliwa kwa mkataba upi? Kuna malipo yoyote yaliyotolewa au ahadi ya kulipa? Kiasi gani cha malipo – fedha taslimu au asante kwa njia mbalimbali? Lini malipo hayo yatatolewa au yalitolewa?
Lakini muhimu pia ni kujua nani hasa anafaidika na malipo hayo – aliyeidhinisha matumizi ya helikopta, rubani na aliyemtuma, baadhi ya maofisa wakuu jeshini, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa au ikulu? Nani anapokea “mshiko?”
Muhimu pia ni kwamba Amiri Jeshi ni rais. Mara hii ni Jakaya Mrisho Kikwete ambaye wakati anaondoka wiki hii kwa ziara ya Marekani aliacha helikopta yake imetumiwa na “watalii” na imeanguka na kuungua.
Amiri Jeshi anasemaje juu ya matumizi ya helikopta “yake?” Helikopta za jeshi, kama zilivyo ndege na magari ya jeshi, ni sehemu ya zana za kazi; waweza kusema, zana za ulinzi wa taifa. Vimeundwa na vinapaswa kutumika na kusimamiwa kwa misingi ya ulizi.
Nafasi ya Amiri Jeshi ni ya kulinda maisha na mali za wananchi ndani ya mipaka ya nchi yao na dhidi ya uchokozi au uvamizi kutoka nje. Kwa maana pana, helikopta ni mali ya wananchi, waliyonunua kwa kodi wanazotozwa na inayopaswa kutumiwa kwa ulinzi wao.
Katika mazingira ambamo serikali imekataa kutoa taarifa juu ya helikopta ya jeshi kutumiwa na watalii kutoka nje kufanya shughuli binafsi, ni uandishi wa wa uchokonozi ambao pekee unaweza kusaidia kuleta nuru juu ya kilichotendeka.
Hadi hapo taarifa zitakapowekwa wazi, acha kila mwananchi awe na mawazo yake: Kwamba sasa jeshi linabangaiza kama machinga; au halina ulinzi kwani kila mmoja aweza kuingia na kujichukulia ndege anavyotaka; au ulinzi wa wananchi sasa mashakani; au wakubwa wameamua kutumia jeshi kufanya biashara ya anga; au amiri jeshi kaenda likizo.
(Makala hii imeandikwa kwa ajli ya safu ya SITAKI, gazeti la Tanzania Daima Jumapili, 16 Desemba 2007. Mwandishi anapatikana kwa simu: 0713 614872; imeili: ndimara@yahoo.com)
Saturday, December 8, 2007
MIAKA 46 YA UHURU WA TANGANYIKA
Kilio kwenye sherehe za uhuru
SITAKI awepo wa kusema kwamba kwa umri wa miaka 46 ya uhuru wa kisiasa wa Tanganyika, “hakuna kilichofanyika.” Sitaki!
Atakuwa anakataa kuona mengi ambayo watawala wamesimamia au wamepuuza kusimamia. Kwani “kufanyika” ni pamoja na kupuuza, kusahau, kuzembea na kukataa kufanya kilichostahili kufanywa.
Acha wenye uwezo na sababu za kuimba nyimbo za wasifu kwa watawala kwa kile walichofanya, wafanye wapendavyo. Wenye dukuduku hapa na pale walitoe; nasi wenye uelewa kuwa kila walichofanya watawala ulikuwa wajibu wao, acha tulenge penye upogo.
Kwamba kwa miaka 46 ya uhuru wa kisiasa wa Tanganyika, Wabarbaig, taifa dogo kaskazini mwa nchi hii, bado wanaswagwa kama wanyama kutoka makazi yao ya miaka nendarudi. Sababu? Watawala wanataka kutoa eneo kwa “wenye fedha” kutoka nchi za nje.
Ni wimbo gani wataimba Wabarbaig hawa katika kuadhimisha miaka 46 ya uhuru? Nani malenga wa “magugu-watu” awezaye kupeperusha midomo yake kusifu kisichosifika. Hapa kuna malenga wa vilio.
Nani kasema ni Wabarbaig peke yao? Kuna kilio kutoka kila pembe ya nchi. Penye rutuba siyo tena mahali pa wananchi kuishi. Rutuba imeleta balaa. Mtanganyika anag’olewa kama gugu na mkoloni mpya anasimikwa kwa lugha ya “mwekezaji.”
Rutuba imekuwa balaa kama madini na vito vya thamani vilivyokuwa balaa. Sikiliza kilio cha wakazi wa Buhemba, mkoani Mara. Waliswagwa kutoka makazi yao ya miaka mingi; wakapoteza mashamba, shule, zahanati na uasili wao.
Waliowang’oa na kuwatupa pembeni, waliwaahidi maziwa na asali, pindi mgodi wa Buhemba, waliodai ni wa serikali, utakapoanza kufanya kazi.
Miaka sita ilipita. Wachimbaji wakachimba. Dhahabu wakabeba. Mgodi sasa umefungwa. Wachimbaji wamekimbia kwa madai ya kufilisika. Wananchi hawajapata chochote. Bado wanalia na kusaga meno.
Yuko wapi malenga wa Buhemba? Ataimba nini ili sauti yake ichanganyike na kurandana na sauti za wanaosifu watawala kwa miaka 46 ya uhuru. Ni madimbwi ya jasho; ni mito ya machozi. Haihitajiki kwenye sherehe.
Nenda kote kwenye machimbo ya dhahabu na almasi katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kagera na Mara. Ni masimulizo hayohayo ya kutia simanzi.
Waliopaswa kuwa walinzi wa mali na uhai wa Watanganyika “waliopata uhuru” miaka 46 iliyopita, ndio wamewatangulia matajiri; wakiwasha moto wa risasi kufukuza magugu-watu ili “waungwana” waitwao wawekezaji, waweze kuchota dhabu na almasi bila kelele wala mikwaruzo.
Watanganyika hawa, wanaoswagwa kwa moto wa risasi, wanashuhudia hata mchanga wa nchi yao ukipakiwa kwenye ndege ziyeyukiazo angani, huku zikiacha vumbi liletalo maradhi na umasikini wa kutaga mayai.
Ziko wapi ndimi za kusifia watawala? Ziko wapi koo za kupitishia sauti nyororo za kukumbukia kuondoka kwa Twaining, gavana wa mwisho wa Uingereza nchini hapa? Zitoke wapi nderemo na vifijo kwenye mwamba huu wa ufukara, vitisho na michirizi ya damu?
Nani atasimama na kusema watawala hawakufanya chochote katika miaka 46 ya uhuru? Hana macho? Hana masikio? Hafikiri? Anataka aambiwe kwamba anatumia “miwani ya mbao” – ule usemi wa rais mstaafu Benjamin Mkapa? Athubutu.
Waulize vijana waitwao wana-Apolo na wenzao wengine katika machimbo ya tanzanite. Kama ilivyo kwenye dhababu na almasi, uchimbaji wao mdogo, na kwa muda mrefu, ulibadili maisha yao.
Kuna waliojenga nyumba; tena nzuri. Wengi walisomesha watoto wao. Kuna walionunua magari na wengine kuweza kuwa na biashara kubwa baada ya mauzo na biashara hizo kunufaisha wananchi wengi katika mkoa wa Arusha (sasa Manyara) na mikoa ya jirani.
Leo hii, kutokana na tanzanite kuvamiwa na kampuni kubwa za nje, tena kwa muda mfupi, mapato ya mchimbaji mdogo yamepungua, mategemeo yake kwa muda mrefu yametoweka na utajiri kutokana na tanzanite umehamishiwa Afrika Kusini, nchi za Asia Mashariki na Ulaya.
Hizo ndizo hasara za uchimbaji wa kiwango kikubwa kwa kutumia kampuni kubwa za nje zilizoingia kwa mikataba ya kinyonyaji. Utajiri unafyonzwa. Nchi inaachiwa maandaki na ufukara usiomithilika.
Leo hii, wachimbaji wadogo waliodhihirisha utajiri wa nchi yao kwa kuinua maisha yao, sasa wanaendelea kufukarika kila kukicha. Na tayari wenye migodi mikubwa wametangaza kuwa zao hilo, linalopatikana Tanzania peke yake, limepungua sana. Linaisha.
Kwa wale ambao utajiri wao wa asili, tanzanite, umechimbwa mbele ya macho yao na kutokomezwa katika matumbo ya ubeberu na wao kubaki masikini kuliko walivyokuwa miaka 46 iliyopita, wana wimbo gani wa wasifu kwa watawala?
Nenda mikoa ya kanda ya Ziwa Viktoria. Wananchi wanaoishi kuzunguka ziwa hilo, kwa miaka nendarudi, wamenufaika na ziwa hilo. Wamevuna samaki kwa ajili ya chakula na biashara pia.
Uvuvi mdogo umewawezesha kupata kitoweo, kufanya biashara ndogo na kuweza kulinda maisha yao. Leo ni tofauti. Kwa miaka 15 sasa, wavuvi wadogo wameonekana kama wavuvi haramu. Waulize wao. Watakwambia ziwa liliuzwa tangu zamani. Ni kweli.
Wavuvi wakubwa, kwa kutumia ngazi za utawala katika vijiji, kata, tarafa na baadhi ya wilaya, wamedhibiti uvuvi mdogo kiasi kwamba wananchi wanaoishi kuzunguka ziwa wanakuwa na hamu ya kula samaki wa Viktoria kama walioko maili 2000 kutoka ziwa hilo!
Simulizi za kweli za waliopigwa kwa kukutwa na samaki; waliolemazwa kwa kipigo na waliokufa kutokana na hasira za kuazima kutoka kwa wenye makampuni ya uvuvi, zimeenea kanda nzima. Ni majuto.
Matokeo yake ni kwamba wenye biashara kubwa ya samaki ndio wameamua wenye ziwa (wananchi) wale nini. Wanavua kwa wingi. Wanachomoa minofu. Wanaisafirisha nchi za nje. Yale mabaki – mifupa – (mapanki), ndiyo wanawatupia wananchi.
Ni mapanki ambayo wananchi wanapigania na kung’oana meno wakitafuta kupata mnuko wa samaki wa ziwa lao.
Uko wapi mdomo uwezao kuimba wasifu wakati wa miaka 46 ya uhuru wa Tanganyika? Wamwimbie nani? Wamwimbie nini? Kwa lipi? Kwa kuwanyang’anya ziwa na samaki wao? Kwa kuwaunganisha na kunguru kugombea mapanki?
Kilio ni kikubwa. Kipo katika matumizi ya misitu na maliasili na raslimali nyingine za taifa hili. Sitaki kuamini kwamba wananchi waliomo katika mazingira yote haya wana chochote cha kusifia utawala.
Wanachojua wananchi wengi ambao hawako kwenye utawala ni kwamba wao ni tabala la mwisho. Tabaka la kwanza limejijengea mahekalu ambamo mume anaishi na mke wake, mtoto na mbwa mkubwa mweusi! Nani atasema watawala hawakutenda? Walitenda walichotaka.
Walichonacho wananchi wengi ambao hawako kwenye utawala, ni uhai na dhamira kwamba mapambano yanaendelea. Wingi wa miaka (46), wakati wanaendelea kuona kiza, ndio kichocheo kikubwa katika harakati hizo. Soma alama za nyakati.
(Makala hii imeandikwa kwa ajili ya toleo la Tanzania Daima Jumapili, 9 Desemba 2007 safu ya SITAKI. Mwandishi anapatikana kwa simu: 0713 614872, imeili: ndimara@yahoo.com)
SITAKI awepo wa kusema kwamba kwa umri wa miaka 46 ya uhuru wa kisiasa wa Tanganyika, “hakuna kilichofanyika.” Sitaki!
Atakuwa anakataa kuona mengi ambayo watawala wamesimamia au wamepuuza kusimamia. Kwani “kufanyika” ni pamoja na kupuuza, kusahau, kuzembea na kukataa kufanya kilichostahili kufanywa.
Acha wenye uwezo na sababu za kuimba nyimbo za wasifu kwa watawala kwa kile walichofanya, wafanye wapendavyo. Wenye dukuduku hapa na pale walitoe; nasi wenye uelewa kuwa kila walichofanya watawala ulikuwa wajibu wao, acha tulenge penye upogo.
Kwamba kwa miaka 46 ya uhuru wa kisiasa wa Tanganyika, Wabarbaig, taifa dogo kaskazini mwa nchi hii, bado wanaswagwa kama wanyama kutoka makazi yao ya miaka nendarudi. Sababu? Watawala wanataka kutoa eneo kwa “wenye fedha” kutoka nchi za nje.
Ni wimbo gani wataimba Wabarbaig hawa katika kuadhimisha miaka 46 ya uhuru? Nani malenga wa “magugu-watu” awezaye kupeperusha midomo yake kusifu kisichosifika. Hapa kuna malenga wa vilio.
Nani kasema ni Wabarbaig peke yao? Kuna kilio kutoka kila pembe ya nchi. Penye rutuba siyo tena mahali pa wananchi kuishi. Rutuba imeleta balaa. Mtanganyika anag’olewa kama gugu na mkoloni mpya anasimikwa kwa lugha ya “mwekezaji.”
Rutuba imekuwa balaa kama madini na vito vya thamani vilivyokuwa balaa. Sikiliza kilio cha wakazi wa Buhemba, mkoani Mara. Waliswagwa kutoka makazi yao ya miaka mingi; wakapoteza mashamba, shule, zahanati na uasili wao.
Waliowang’oa na kuwatupa pembeni, waliwaahidi maziwa na asali, pindi mgodi wa Buhemba, waliodai ni wa serikali, utakapoanza kufanya kazi.
Miaka sita ilipita. Wachimbaji wakachimba. Dhahabu wakabeba. Mgodi sasa umefungwa. Wachimbaji wamekimbia kwa madai ya kufilisika. Wananchi hawajapata chochote. Bado wanalia na kusaga meno.
Yuko wapi malenga wa Buhemba? Ataimba nini ili sauti yake ichanganyike na kurandana na sauti za wanaosifu watawala kwa miaka 46 ya uhuru. Ni madimbwi ya jasho; ni mito ya machozi. Haihitajiki kwenye sherehe.
Nenda kote kwenye machimbo ya dhahabu na almasi katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kagera na Mara. Ni masimulizo hayohayo ya kutia simanzi.
Waliopaswa kuwa walinzi wa mali na uhai wa Watanganyika “waliopata uhuru” miaka 46 iliyopita, ndio wamewatangulia matajiri; wakiwasha moto wa risasi kufukuza magugu-watu ili “waungwana” waitwao wawekezaji, waweze kuchota dhabu na almasi bila kelele wala mikwaruzo.
Watanganyika hawa, wanaoswagwa kwa moto wa risasi, wanashuhudia hata mchanga wa nchi yao ukipakiwa kwenye ndege ziyeyukiazo angani, huku zikiacha vumbi liletalo maradhi na umasikini wa kutaga mayai.
Ziko wapi ndimi za kusifia watawala? Ziko wapi koo za kupitishia sauti nyororo za kukumbukia kuondoka kwa Twaining, gavana wa mwisho wa Uingereza nchini hapa? Zitoke wapi nderemo na vifijo kwenye mwamba huu wa ufukara, vitisho na michirizi ya damu?
Nani atasimama na kusema watawala hawakufanya chochote katika miaka 46 ya uhuru? Hana macho? Hana masikio? Hafikiri? Anataka aambiwe kwamba anatumia “miwani ya mbao” – ule usemi wa rais mstaafu Benjamin Mkapa? Athubutu.
Waulize vijana waitwao wana-Apolo na wenzao wengine katika machimbo ya tanzanite. Kama ilivyo kwenye dhababu na almasi, uchimbaji wao mdogo, na kwa muda mrefu, ulibadili maisha yao.
Kuna waliojenga nyumba; tena nzuri. Wengi walisomesha watoto wao. Kuna walionunua magari na wengine kuweza kuwa na biashara kubwa baada ya mauzo na biashara hizo kunufaisha wananchi wengi katika mkoa wa Arusha (sasa Manyara) na mikoa ya jirani.
Leo hii, kutokana na tanzanite kuvamiwa na kampuni kubwa za nje, tena kwa muda mfupi, mapato ya mchimbaji mdogo yamepungua, mategemeo yake kwa muda mrefu yametoweka na utajiri kutokana na tanzanite umehamishiwa Afrika Kusini, nchi za Asia Mashariki na Ulaya.
Hizo ndizo hasara za uchimbaji wa kiwango kikubwa kwa kutumia kampuni kubwa za nje zilizoingia kwa mikataba ya kinyonyaji. Utajiri unafyonzwa. Nchi inaachiwa maandaki na ufukara usiomithilika.
Leo hii, wachimbaji wadogo waliodhihirisha utajiri wa nchi yao kwa kuinua maisha yao, sasa wanaendelea kufukarika kila kukicha. Na tayari wenye migodi mikubwa wametangaza kuwa zao hilo, linalopatikana Tanzania peke yake, limepungua sana. Linaisha.
Kwa wale ambao utajiri wao wa asili, tanzanite, umechimbwa mbele ya macho yao na kutokomezwa katika matumbo ya ubeberu na wao kubaki masikini kuliko walivyokuwa miaka 46 iliyopita, wana wimbo gani wa wasifu kwa watawala?
Nenda mikoa ya kanda ya Ziwa Viktoria. Wananchi wanaoishi kuzunguka ziwa hilo, kwa miaka nendarudi, wamenufaika na ziwa hilo. Wamevuna samaki kwa ajili ya chakula na biashara pia.
Uvuvi mdogo umewawezesha kupata kitoweo, kufanya biashara ndogo na kuweza kulinda maisha yao. Leo ni tofauti. Kwa miaka 15 sasa, wavuvi wadogo wameonekana kama wavuvi haramu. Waulize wao. Watakwambia ziwa liliuzwa tangu zamani. Ni kweli.
Wavuvi wakubwa, kwa kutumia ngazi za utawala katika vijiji, kata, tarafa na baadhi ya wilaya, wamedhibiti uvuvi mdogo kiasi kwamba wananchi wanaoishi kuzunguka ziwa wanakuwa na hamu ya kula samaki wa Viktoria kama walioko maili 2000 kutoka ziwa hilo!
Simulizi za kweli za waliopigwa kwa kukutwa na samaki; waliolemazwa kwa kipigo na waliokufa kutokana na hasira za kuazima kutoka kwa wenye makampuni ya uvuvi, zimeenea kanda nzima. Ni majuto.
Matokeo yake ni kwamba wenye biashara kubwa ya samaki ndio wameamua wenye ziwa (wananchi) wale nini. Wanavua kwa wingi. Wanachomoa minofu. Wanaisafirisha nchi za nje. Yale mabaki – mifupa – (mapanki), ndiyo wanawatupia wananchi.
Ni mapanki ambayo wananchi wanapigania na kung’oana meno wakitafuta kupata mnuko wa samaki wa ziwa lao.
Uko wapi mdomo uwezao kuimba wasifu wakati wa miaka 46 ya uhuru wa Tanganyika? Wamwimbie nani? Wamwimbie nini? Kwa lipi? Kwa kuwanyang’anya ziwa na samaki wao? Kwa kuwaunganisha na kunguru kugombea mapanki?
Kilio ni kikubwa. Kipo katika matumizi ya misitu na maliasili na raslimali nyingine za taifa hili. Sitaki kuamini kwamba wananchi waliomo katika mazingira yote haya wana chochote cha kusifia utawala.
Wanachojua wananchi wengi ambao hawako kwenye utawala ni kwamba wao ni tabala la mwisho. Tabaka la kwanza limejijengea mahekalu ambamo mume anaishi na mke wake, mtoto na mbwa mkubwa mweusi! Nani atasema watawala hawakutenda? Walitenda walichotaka.
Walichonacho wananchi wengi ambao hawako kwenye utawala, ni uhai na dhamira kwamba mapambano yanaendelea. Wingi wa miaka (46), wakati wanaendelea kuona kiza, ndio kichocheo kikubwa katika harakati hizo. Soma alama za nyakati.
(Makala hii imeandikwa kwa ajili ya toleo la Tanzania Daima Jumapili, 9 Desemba 2007 safu ya SITAKI. Mwandishi anapatikana kwa simu: 0713 614872, imeili: ndimara@yahoo.com)
Saturday, December 1, 2007
SIKU YA UKIMWI DUNIANI
Serikali inavyopakata UKIMWI
SITAKI wimbo wa UKIMWI. Una beti nyingi zisizokatika. Umetungwa kwa shinikizo. Waumini wa kweli ni wachache. Ambao wangeuimba hawaujui; wanalia na kusaga meno. Wanakufa haraka.
Ni jana. Desemba Mosi. Inaitwa “Siku ya Ukimwi Duniani” (SUD). Kwa waliomo vitani dhidi ya gonjwa hili lisilochanjo wala tiba, akili zimeshonwa kwenye meza za maabara na matokeo mapya ya tafiti katika kukabiliana na gonjwa hili.
Kwa waliopokea kampeni dhidi ya ukimwi kama wimbo usiokatika wa kuombea fedha za kutumbulia katika mahekelu yao mapya pembezoni mwa miji mikubwa, jana ilikuwa siku nyingine ya kuongeza ubeti mpya.
Jana ilikuwa siku nyingine ya kusambaza takwimu za vitisho vya maambukizi; mahitaji makubwa ya fedha za kampeni; umuhimu wa kuwa na tume nyingi za kupambana na ukimwi na asasi lukuki za “ombaomba” waneemekao kwenye mgongo wa ukimwi.
Hiyo ni jana. Ndivyo ilivyokuwa mwaka jana na mwaka juzi. Ndivyo itakavyokuwa mwaka kesho na keshokutwa. Wanaochuma kwenye mgongo wa ukimwi hawataki ukomo wa virushi vya ukimwi (VVU) wala ugonjwa wa ukimwi.
Ugonjwa unaoua, usio na chanjo wala tiba, unatengewa siku moja katika mwaka na dunia; “kuuadhimisha” au kuadhimisha juhudi za kukabiliana nao; au kukumbushana umuhimu wa mapambano dhidi yake.
Siku ya Ukimwi Duniani inatukumbusha mambo mengi. Kubwa kuliko yote ni kwamba watawala hawajawa makini katika vita dhidi ya ukimwi. Bado wanauchekea na kuupakata.
Kwanza, Tanzania ni moja ya nchi zinazoendelea ambako watawala walisukumwa na nchi wafadhili kuanza kujadili ukimwi hadharani na kuingiza mkakati wa kukabiliana nao katika mipango ya nchi.
Pili, ukimwi umeandamana na unyanyapaa. Unyanyapaa maana yake ni ubaguzi dhidi ya walio na VVU au wagonjwa wa ukimwi. Ubaguzi huu maana yake ni kutengwa, kukimbiwa, kuepukwa na ndugu, rafiki na jamii.
Lakini kwa nini wagonjwa wa ukimwi wananyanyapaliwa wakati wagonjwa wa kipindupindu hawafanyiwi hivyo? Kipindupindu kinatokana na “kula mavi” au uchafu. Ukimwi unatokana na mahusiano ya mtu na mtu.
Kwa hiyo basi kuna unyanyapaa pia katika kipindupindu lakini sharti uchimbe zaidi. Kipindupindu hupatikana vichochoroni, katika mazingira machafu; kule wanakoishi hohehahe; makazi yasiyo na mpaka kati ya mifereji ya maji safi na majitaka
Kipindupindi hupatikana katika mazingira ya wasio na sufuria ya pili ya kuchemshia maji; wasio na fedha za kununua maji salama; wasio na fedha za kununulia mkaa wa kuchemshia maji; wasio na fedha za kula sehemu zenye usafi; masikini walao kwenye jalala na wasio na uelewa (elimu) juu ya kujikinga.
Hawa walitengwa zamani kwa mpangilio wa jamii kitabaka. Waliishanyanyapaliwa zamani kutokana na hali zao dhoofu kiuchumi ambamo walisukumwa na mkondo wa uchumi unaotawala.
Leo hii, wenye VVU na ukimwi wananyanyapaliwa kwa madai kwamba mgonjwa wa ukimwi anakufa baada ya mateso makubwa – kuugua kwa muda mrefu, kudhoofu kupindukia, kuhara na kutapika na hatimaye kuwa “mzigo” kwa waangalizi wake.
Ukichanganya haya mawili, kipindupindu na ukimwi, utaona kwamba, kote kuna unyanyapaa. Ni masikini na asiye na elimu ambaye anakufa kwa mahangaiko, kukata taamaa na hata kujiua. Hajui, na hana uwezo kifedha wa kukabiliana na kipindupindu na ukimwi.
Wagonjwa wa ukimwi wenye elimu na mali wanajua kuwa kifo kutokana na ukimwi kinaweza kuahirishwa kwa kupambana na magonjwa virukizi, kwa kula chakula chenye viini muhimu na cha kutosha kuimarisha mwili.
Wenye VVU wamethibitika kuishi maisha yao yote na kufa katika umri mkubwa. Hii ni iwapo wamepewa elimu na wana uwezo wa kunawirisha maisha yao kwa chakula kinachotosha na chenye viini muhimu vya kulinda na kuimarisha miili yao.
Katika nchi ambamo hakufanyiki utafiti juu ya kinga wala tiba ya VVU na ukimwi, kama Tanzania, kwa nini kusiwe na mkakati mkubwa wa kulinda uhai wa watu kwa njia ya elimu na lishe?
Kuna watakaosema tayari kuna asasi za kimataifa, Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Mfuko wa Mkapa, asasi mbalimbali za kitaifa, asasi za mikoani na wilayani hadi kwenye kata.
Waandishi wa habari katika darasa langu la uchunguzi wa habari, katika wilaya za mikoa ya Kanda ya Ziwa Viktoria, wamegundua utitiri wa asasi za “kupambana” na ukimwi zilizoanzishwa na maofisa wilayani ili zipokee fedha na kuyeyuka.
Hii ina maana gani? Kwamba elimu iliyotarajiwa haipo; kama ipo haifikii walengwa. Fedha zilizolenga kueneza elimu na kuleta afueni kimaisha, haziwafikii walengwa. Kuna wizi. Lakini pia hakuna usimamizi wa kutosha.
Tanzania ina wizara 25 za serikali. Rais Kikwete anafikiria kupunguza baadhi ya wizara. Huenda zikabakia 15 au 18. Katika hizo 18, kwa nini kusiwemo Wizara ya Kupambana na Ukimwi (WIKUKI) inayoongozwa na wanaharakati wa afya za jamii na siyo lazima waliovaa nguo za kijani?
Ni kweli kuna wizara zilizoshindwa kufanya kazi zake barabara. Lakini hatua ya kuwa na wizara inaonyesha kuwa makini na inaahidi uhakika wa mipango ya elimu juu ya VVU na ukimwi; juu ya dawa za kuahirisha kifo; mipango mizuri ya usambazaji wa fedha na usimamizi na ufuatiliaji wenye tija.
Watawala wakifanya ajizi, wananchi wataendelea kupukutika, na wao kama watakuwa wamesalia, watatawala ardhi na nyasi peke yake, kwani maliasili nyingine kama wanyama, misitu na madini, wameishatoa kibali vihamishwe vyote.
(Makala hii itachapishwa katika safu ya SITAKI katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili, Desemba 2, 2007)Mwandishi anapatikana Simu: 0713 614872; imeili: ndimara@yahoo.com)
SITAKI wimbo wa UKIMWI. Una beti nyingi zisizokatika. Umetungwa kwa shinikizo. Waumini wa kweli ni wachache. Ambao wangeuimba hawaujui; wanalia na kusaga meno. Wanakufa haraka.
Ni jana. Desemba Mosi. Inaitwa “Siku ya Ukimwi Duniani” (SUD). Kwa waliomo vitani dhidi ya gonjwa hili lisilochanjo wala tiba, akili zimeshonwa kwenye meza za maabara na matokeo mapya ya tafiti katika kukabiliana na gonjwa hili.
Kwa waliopokea kampeni dhidi ya ukimwi kama wimbo usiokatika wa kuombea fedha za kutumbulia katika mahekelu yao mapya pembezoni mwa miji mikubwa, jana ilikuwa siku nyingine ya kuongeza ubeti mpya.
Jana ilikuwa siku nyingine ya kusambaza takwimu za vitisho vya maambukizi; mahitaji makubwa ya fedha za kampeni; umuhimu wa kuwa na tume nyingi za kupambana na ukimwi na asasi lukuki za “ombaomba” waneemekao kwenye mgongo wa ukimwi.
Hiyo ni jana. Ndivyo ilivyokuwa mwaka jana na mwaka juzi. Ndivyo itakavyokuwa mwaka kesho na keshokutwa. Wanaochuma kwenye mgongo wa ukimwi hawataki ukomo wa virushi vya ukimwi (VVU) wala ugonjwa wa ukimwi.
Ugonjwa unaoua, usio na chanjo wala tiba, unatengewa siku moja katika mwaka na dunia; “kuuadhimisha” au kuadhimisha juhudi za kukabiliana nao; au kukumbushana umuhimu wa mapambano dhidi yake.
Siku ya Ukimwi Duniani inatukumbusha mambo mengi. Kubwa kuliko yote ni kwamba watawala hawajawa makini katika vita dhidi ya ukimwi. Bado wanauchekea na kuupakata.
Kwanza, Tanzania ni moja ya nchi zinazoendelea ambako watawala walisukumwa na nchi wafadhili kuanza kujadili ukimwi hadharani na kuingiza mkakati wa kukabiliana nao katika mipango ya nchi.
Pili, ukimwi umeandamana na unyanyapaa. Unyanyapaa maana yake ni ubaguzi dhidi ya walio na VVU au wagonjwa wa ukimwi. Ubaguzi huu maana yake ni kutengwa, kukimbiwa, kuepukwa na ndugu, rafiki na jamii.
Lakini kwa nini wagonjwa wa ukimwi wananyanyapaliwa wakati wagonjwa wa kipindupindu hawafanyiwi hivyo? Kipindupindu kinatokana na “kula mavi” au uchafu. Ukimwi unatokana na mahusiano ya mtu na mtu.
Kwa hiyo basi kuna unyanyapaa pia katika kipindupindu lakini sharti uchimbe zaidi. Kipindupindu hupatikana vichochoroni, katika mazingira machafu; kule wanakoishi hohehahe; makazi yasiyo na mpaka kati ya mifereji ya maji safi na majitaka
Kipindupindi hupatikana katika mazingira ya wasio na sufuria ya pili ya kuchemshia maji; wasio na fedha za kununua maji salama; wasio na fedha za kununulia mkaa wa kuchemshia maji; wasio na fedha za kula sehemu zenye usafi; masikini walao kwenye jalala na wasio na uelewa (elimu) juu ya kujikinga.
Hawa walitengwa zamani kwa mpangilio wa jamii kitabaka. Waliishanyanyapaliwa zamani kutokana na hali zao dhoofu kiuchumi ambamo walisukumwa na mkondo wa uchumi unaotawala.
Leo hii, wenye VVU na ukimwi wananyanyapaliwa kwa madai kwamba mgonjwa wa ukimwi anakufa baada ya mateso makubwa – kuugua kwa muda mrefu, kudhoofu kupindukia, kuhara na kutapika na hatimaye kuwa “mzigo” kwa waangalizi wake.
Ukichanganya haya mawili, kipindupindu na ukimwi, utaona kwamba, kote kuna unyanyapaa. Ni masikini na asiye na elimu ambaye anakufa kwa mahangaiko, kukata taamaa na hata kujiua. Hajui, na hana uwezo kifedha wa kukabiliana na kipindupindu na ukimwi.
Wagonjwa wa ukimwi wenye elimu na mali wanajua kuwa kifo kutokana na ukimwi kinaweza kuahirishwa kwa kupambana na magonjwa virukizi, kwa kula chakula chenye viini muhimu na cha kutosha kuimarisha mwili.
Wenye VVU wamethibitika kuishi maisha yao yote na kufa katika umri mkubwa. Hii ni iwapo wamepewa elimu na wana uwezo wa kunawirisha maisha yao kwa chakula kinachotosha na chenye viini muhimu vya kulinda na kuimarisha miili yao.
Katika nchi ambamo hakufanyiki utafiti juu ya kinga wala tiba ya VVU na ukimwi, kama Tanzania, kwa nini kusiwe na mkakati mkubwa wa kulinda uhai wa watu kwa njia ya elimu na lishe?
Kuna watakaosema tayari kuna asasi za kimataifa, Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Mfuko wa Mkapa, asasi mbalimbali za kitaifa, asasi za mikoani na wilayani hadi kwenye kata.
Waandishi wa habari katika darasa langu la uchunguzi wa habari, katika wilaya za mikoa ya Kanda ya Ziwa Viktoria, wamegundua utitiri wa asasi za “kupambana” na ukimwi zilizoanzishwa na maofisa wilayani ili zipokee fedha na kuyeyuka.
Hii ina maana gani? Kwamba elimu iliyotarajiwa haipo; kama ipo haifikii walengwa. Fedha zilizolenga kueneza elimu na kuleta afueni kimaisha, haziwafikii walengwa. Kuna wizi. Lakini pia hakuna usimamizi wa kutosha.
Tanzania ina wizara 25 za serikali. Rais Kikwete anafikiria kupunguza baadhi ya wizara. Huenda zikabakia 15 au 18. Katika hizo 18, kwa nini kusiwemo Wizara ya Kupambana na Ukimwi (WIKUKI) inayoongozwa na wanaharakati wa afya za jamii na siyo lazima waliovaa nguo za kijani?
Ni kweli kuna wizara zilizoshindwa kufanya kazi zake barabara. Lakini hatua ya kuwa na wizara inaonyesha kuwa makini na inaahidi uhakika wa mipango ya elimu juu ya VVU na ukimwi; juu ya dawa za kuahirisha kifo; mipango mizuri ya usambazaji wa fedha na usimamizi na ufuatiliaji wenye tija.
Watawala wakifanya ajizi, wananchi wataendelea kupukutika, na wao kama watakuwa wamesalia, watatawala ardhi na nyasi peke yake, kwani maliasili nyingine kama wanyama, misitu na madini, wameishatoa kibali vihamishwe vyote.
(Makala hii itachapishwa katika safu ya SITAKI katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili, Desemba 2, 2007)Mwandishi anapatikana Simu: 0713 614872; imeili: ndimara@yahoo.com)